Waziri Gwajima tengua uamuzi wako wa kuunga mkono sheria ya maadili Arusha, hili ni bomu unatengeneza

Habarini za asubuhi wote. Mm nimefuatilia humu hizi hoja naona kama wore tunataka kudhibiti mmomonyoko wa maadili ila Kila mtu ana njia yake. Ila nashukuru kwanza Kila mmoja anakiri kuna mmomonyoko wa maadili.

Sasa nirudi kwenye point moja: hivi mfano, kupanda kwa joto la mwili ni dalili tu ya tatizo fulani la kiafya. Na mara nyingi magonjwa mbalimbali husababisha kupanda kwa joto. Sasa twende tukamtibu mgonjwa Sasa mfano. Hivi dalili au tabia za huo ugonjwa ambazo ni labda joto kupanda, kuishiwa nguvu, kuishiwa maji mwilini maumivu nk tutazinyima dawa za kutuliza siyo hadi tusubiri huko maabara waje na majibu waseme nini hasa hiki? [emoji1]

Haya mjadala safi kabisa njooni tuelimishane kwa nn mara ingine wakati unasubiri C ni unajikuta unaanza na A na mwisho unafanya majumuisho.

Ila tunapochangia mawazo ya kila mmoja na yaheshimiwe tusiende na spirit ya I want to outshine someone.... [emoji3060]

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Huo "mpango" jamii ilishirikishwa lini? Au mlijikalia wenyewe mkadanganyana mkaja na mpango ambao jamii hawaujui?

Hivi wanachi wangapi Tanzania hii wanaoijuwa google?

Ndiyo yaleyale nilisema, sana utakuja na ubunifu wa porojo na ngonjera (thesis), hakuna utekelezaji.

Unatakiwa uwepo kwenye jamii na uelewe "rootcauses" za matatizo ni nini. Siyo kuandaa maandiko yaliyojaa matatizo ambayo yanajulikana bila kuwa na ubunifu unaoonekana unashughulikiwa na wizara uanayiongoza. Ungekuwa na mipango mizuri usingeenda huko ulikoenda ili uonekane kwenye vyombo vya habari kuwa umeenda.

Ngoja nikusaidie, naona huna ubunifu, unaanza kutaka kunibadilishia kibao mimi na wananchi. Kama mimi na wanachi ndiyo unatuona tuna matatizo, basi ume fail wewe kutufanya tusiwe matatizo.

!) List down matatizo yote uyajuayo kayiaka wizara yako, halafu yatengenishe ya kidara (Administation) na kiuutendaji (Operations) Halafu ueleweuyayafikisha vipi kwa wateja wao (jamii) na uawauzia vipi ufumbuzi (Sales and Marketing.


Bila kujiundia mipango inayeaendana kwa principle hizo za Adminisration, Operation, Salase and Marketing Utabaki zima moto (reactive) maisha yako.

Kwa kuanza na hizo principals utaoata kuwa na plan, plan yako iwe ya muda mfupi, wa kati na mrefu.

Ukisha kuwa na plan hapoapo utakuwa unaingia kwenye kuwa (proactive).

Ukihitaji msaada wa ku plan, nipo hapa, uliza tu, tutakusaidia.

Kingine kabla sijakisahau. Sahau kabisa kuwa wewe hiyo ya uwaziri ni kazi. Usiwe na metality ya kama mwajiriwa uliyoizowea maishani mwako. Kuwa na metality ya kuwa huo ni mtihani wa Muum a wako, utawatumikia vipi waja wake.

Nafahamu, ni vigumu sana kwako ku "learn to unlearn", simply empty your cup and start afresh.

Kila siku asubuhi ukimaliza ablution zako na sala zako, uwe unafikiri, jana nimekibuni kipya cha kuwatumikia Watanzania. Ukiona vy0ote ni vilevile vya siku zote, elewa kuwa you are simply a reactive minded person.

Na huo waraka ulonambia ni-u-"google" nafanya hivyo sasa hivi.

Uwe na amani.
 
Nimeupitia huo waraka uliotaka niutafute, kabla sijaenda mbali nimekuta kuwa matumizi yake yameshakwisha:

1.2 Muda wa Utekelezaji
Muda wa utekelezaji wa Mwongozo huu ni miaka mitano kuanzia 2017/18 hadi 2021/22. Hata hivyo, baadhi ya vipengele vya mwongozo vinaweza kubadilishwa kulingana na mazingira pamoja na mahitaji halisi ya jamii kwa wakati husika.


Sasa Mheshimiwa uikuwa unanipiga porojo kama mnazopigana bungeni ili unitowe njiani tu?

Huo ndiyo ubunifu wako? Dah. Badilika.

"If such are the priests, then God bless the congregation". - Deedat.
 
Niliposoma majibu yako nikajisemea moyoni huu ndio uongozi wenye hekima na busara.

Uwanja wa mpira wakati wa mechi mara nyingine pass hupigwa kwa shuti kali lenye kasi lakini mpokeaji hutuliza kwa ustadi na kuupooza mpira ili baadae apige pass nzuri imfikie mchezaji mwingine katika eneo sahihi.

Wewe ni sawa na mchezaji anayetuliza mpira kwa ustadi licha ya kupewa pass mbovu ili atoe pass nzuri inayofika eneo husika. Kwa thread ilivyoandikwa mwingine angejibu kwa hasira. Majibu yako si ya kugutua siku zote hata Instagram. Uko very calm. Na unaendana na wizara yako yenye mambo ya socialisation ndani yake. Hongera mheshimiwa upewe maua yako.
 
Kwa uchache kabisa, yote hayo yapo, na yamefanyika. Nadhani pia, tunapowasilisha taarifa za utekelezaji mfano kwenye bajeti zetu, vema kupata muda wa kupitia.

Huko kwenye Google nimekupa ww hapo uliyehumu kwa urahisi kama mdau, wale wengine wasio humu wanayo mipango ofisini kwao.

Hii mipango yote unayosema mingine ipo ni utaratibu wa kawaida kabisa.

Labda niulize; hivi mfano umeweka ulinzi kwenye taasisi yako au nyumbani kwako Ili kuzuia wezi na vibaka; halafu ikatokea wamefanikiwa kupenya, ukaamka tajiri kuongeza nguvu na silaha yako, tutasema uko reactive siyo? Au limetokea tukio kunahitajika system support?

Nauliza tu[emoji28]

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Huna haja ya kutumia herufi kubwa, zinatufokea kwa kelele tu.
 
Kwanza nakushukuru kwa kuupitia. Pili niseme kuwa, nimebaini kuwa nawe unahitaji kufuatilia systematic kile tunafanya na matoleo ya taarifa zetu Ili utoe mchango wako Vizuri zaidi. Hivi umesahau kuwa juzi tumetoka kusema kuwa mpango huo umefanyiwa tathmini na wadau wote na Sasa tunakwenda toleo jipya kabisa? Mbona tumesema Sana, vikao na wadau wote tumefanya dodoma na taarifa zimetoka na kwenye hotuba ya Bajeti tumesema na maswali tumejibu bungeni mara kadhaa.

Na siku tukiuzindua hii novemba kuelekea siku 16 za kupinga ukatili nitauleta hapa ni ku tag.

Tupunguze basi jamani sijui chuki hizi au sijui nn... Mungu atusaidie Sana maana tunajenga nyumba moja na Kila talent inahitajika, active... reactive.. proactive... combination... zote ni karama tu kwa ajili ya matumizi nyakati tofauti tofauti [emoji1]

Asubuhi njema na baraka.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Nisome vizuri tu. kuna mada chungu nzima nimeanzisha za kuelimisha jamii kwenye mambo tofauti tofauti. Hilo usiwe na shaka nalo kabisa.

Hiyo ndiyo kazi yangu ya muhimu zaidi baada ya kustaafu na nashukuru siku hizi kuna hii mitandao ya mawasiliano, tunaweza kuyafikisha kwa wengi, tusije kuondoka nayo hata moja hatujalifikisha.
 
Nawatakia kazi njema.

Mimi hata bila mpango wenu nnaufikisha ujumbe kiaina yangu a kwa muono wangu kila siku, nipo "highly dynamic and proactive to the core". Hujanielewa tu.

Tegemea " tons of constructive criticism" kutokea kwangu. Naamini kuna japo moja itakuwa na maana.

Naendelea kuupitia ule mpango ulio "expire." nione kuna nini cha kushauri baada ya kuupitia.
 
Hbr za asubuhi. Mungu akubariki Sana.

Kwa umri wangu huu, na majukumu yangu haya, na uzoefu nilioupata ikiwemo kuchambuliwa kama karanga na mitandao, ni kama chuma kilichopita kwenye moto wa gesi[emoji28][emoji28][emoji28]

Kwanza nawashukuru wachambuzi wote wote wote kwa aina zao. Wameniumbia kitu kipya moyoni mwangu ambacho najivunia saaaana... maana, ikiwa naijua kweli na wengine hawaijui maana wakati wa kweli kujidhihirisha haujafika au basi tu wengine wanapindisha tu kwa kusudi lao maana wakati haujafika wa kweli. Kwa, hivyo kuwachukia ni kukosa hekima na kujiudhi na kumuudhi Mungu.

Katika hali hiyo mishale ninayopigwa kwenye kweli naipokea na kukiri na ile pasipo kweli na haki huwa nashangaa inaji transform kuwa nguvu ya hekima inayonipa ari na furaha ya kuchati na watu mbalimbali na kupata maoni yao na kwa bashasha navaa uhalisia wao na kuzungumza nao kikawaida kabisa [emoji28]

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Andika vizur basi huo uandishi umefunzwa wapi KAZI ukaidi Tu hata Sheria za uandishi huna kisha kuja shindana na Dkt
Mkuu mimi kujadiliana na shangazi yangu Mama Gwajima mbona ni vitu vya kawaida,mama na mwanae tunateta hoja kwa hoja na tunaelewana.
Au una jingine zaidi ya hilo la uoga wa kuzungumza hoja kwa tuliowapa dhamana ya kutuongoza???
Sisi vijana wa miaka ya 80,s chama cha CCM kilitujenga katika katika,kutoa hoja na kuzungumza ukweli na watu tuliowapa dhamana ya kutuongoza.
 
Ahsante Sana FaizaFoxy, nami nakushukuru Sana kwa muda wako. Maana katika mjadala huu pia tumeweza kuamsha wengi hapa jukwaani na nje ya Jukwaa hili. Walau wamejua kuna mpango uliopita na unaokuja na kwamba ni mpango wa Serikali na Jamii. Hakika Mimi mwenzenu mkija nyie ambao mna critics Kali, huwa nawapenda na kuwaheshimu kabisa, maana faida ni kuwa, weeengi wakiona mjadala wa waziri na watu wakubwa wenye ajenda za nguvu kama wewe ndugu yangu, huwa wanakuja, na hapa nami ndiyo nafanya branding ya wizara na mambo yake na kuifikia jamii. Lakini pia tunafanya branding ya hekima kwa watoto wetu kuwa hata moto uje mkali namna gani, panapo Nia njema Mungu huupoza na kuugeuza Baraka.

Karibuni sana jamani mm nipo kupokea mishale yoooote kwani najua mwisho wa mishale ni Baraka za kwenda kujenga [emoji1241]jamii yetu [emoji1666][emoji123][emoji120][emoji106][emoji253]

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Hii video ina kila kitu na kinaeleweka . Na ulichofanya kuunga mkono agenda ya wanakijiji cha Olevolos ambacho kiko umbali wa karibu kilometa 10 kutoka Arusha mjini ni jambo jema sana. Na mara nyingi maeneo kama haya ya pembezoni mwa mji kwa nchi yetu huwa kwa asilimia kubwa yanakaliwa na wenyeji wenye asili ya mkoa huo au mji huo walio na mila na desturi zao. Kiasi kwamba mgeni akiingia eneo hilo lazima afuate utaratibu uliopo.

Labda tukumbushane kidogo kuhusu asili yetu.Wote ambao asili yetu ni vijijini mara zote tunapokwenda kusalimia ndugu wa ukoo vijijini nguo za mjini huwa tunaziacha mjini hukohuko. Kwa nini tunafanya hivyo? Bila shaka tunatambua mila na desturi za kila eneo husika. Na kujua mila na desturi za kila eneo ni kujua mavazi na mapambo ambayo yanakubalika kwenye jamii husika katika hicho kijiji. Na hii ipo kwenye vijiji vyote Tanzania. Maeno hayo huwezi kwenda na nguo fupi kama kimini au zile taiti transparent watakushangaa na utaonwa umeenda kuiharibu jamii yao . Na ndio maana akina mama wakiwa wanaenda vijijini huwa wananunua vitenge na kushona mavazi yenye staha na huwezi kuta vijijini uvaaji wa kata K umeshamiri.

Agenda ya kijiji cha Olevolos ipewe heko na iwe mfano kwa vijiji vingine kuweka standards zao . Hizo nguo zikivaliwa bar huko hakuna atakayewafuata .
 
Safi sana![emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
Hapo unaendelea kunipiga porojo na ngonjera. Ulisema ipo ukanipa ni google, kwenda nakuta mipngo expired. Dah.


Hilo la tajiri na mlinzi mfano mfu huo. Hapo nikutafuta ku "score points" kijinga tu. "I am way ahead of that BS".

Hio habari za bajeti sijuwi ni nini, nazo ni kujitafutia "scapegoat" tu. Kuwa na ubunifu. Mbona jamii yetu matatizo yake mengi (siyo yote) najulikana na mnachoshindwa mpaka sasa ni kuwa wabunifu wa kuyapatia ufumbuzi wa kuyatatua tu. Yaani mnakuwa kama mzazi anaevuta sigara halafu anamwabia kijana wake "usivute sigara ni mbaya kwako", hivi yatamuingia kweli?.

Ndiyo hivyo, bora liende tu.

Yaani mmekaa kujibu kisiasa siasa (yaani uongo uongo tu )na kutowana njiani.

Tuonesheni plan zenu, siyo unanipa mpango wa ofisi ya waziri mkuu uliopitwa na wakati halafu unanambia bado unafanyiwa tathmini uletwe mpya. Ina maana hakuna mpango wowote hapo mnajiendea kimazowea tu. Badilika.

Majibu yako ni "highly contradictive". Tafadhali huku mitandaoni tusipigane porojo, porojo pelekeni bungeni huko. Hapa tunataka facts, kama yapo unasema hili na hili hili ndilo lipo, kama hauna plan, simple tu, sema hatuna plan, lakini tumekuelewa na tutaifanyia kazi, na ukitoa ahadi uifanye kweli.
 
Nashukuru sana uongozi wa kijiji kizima kwa kujaribu kujiwekea utaratibu mzuri sana ambao utawezesha Jamii husika kuishi katika maadili, sioni shida kabisa katika hilo, Ndugu Doroth Gwajima, Umefanya vema kuunga Mkono jitihada hizi kwani hii itakua chachu hata kwenye maeneo Mengine mengi, Nina ushahidi usio na shaka kuthibitisha kwamba Uvaaji wa nguo fupi , unyoaji wa viduku pamoja na kushinda vijiweni ni matokeo makubwa ya mmonyoko wa maadili kwani uchochea ukahaba, uvutaji bangi, wizi, pamoja na umaskini , Naombeni sana nifikishieni pongezi kwa Jamii husika kwa kutambua umuhimu wa vijana katika kuliendeleza Taifa.

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
Kwa hiyo una watetea hao wanao vaa vichupi na vitaiti na kutembea navyo barabarani 🤔 au na wewe ni mmoja wao🤔 Kwani kuna faida gani mtu ukivaa nasu uchi na kutembea hadharani 🤔 sio Kila kitu kwa sababu wazungu wanafanya basi na nyie huku uswahilini mfanye mnaonekana kama wendawazimu, kwani mkivaa kwa kujistili vizuri kuna madhara yoyote mnapata 🤔 kama unaona ni Sheria za kijinga hamia Marekani ambako hata ukitembea uchi wa mnyama hakuna atakae kuwaza

Tena waziri uangalie na mziki wa bongo flavor kwa jicho la tatu kwa sababu kuna wasanii ni chanzo kikubwa cha uvunjifu wa maadili, Kila siku kwenye nyimbo zao wana hamasisha kunywa pombe na kuvuta bangi bila kusahau ngono tena hadi ngono ya kinyume na maumbile, lakini cha ajabu kwenye mikutano yenu ya kiasa ndio mnawaita kutumbuiza na wanaimba hizo nyimbo zao ambazo kama una akili timamu huwezi kusikiliza ushenzi wanao tamka humo ndani, wanapaswa kushughulikiwa kabisa hao wapuuzi 😡😡
 
Jamii ya watu wa Arumeru imefanya vizuri,kujipanga na kutokomeza ujinga,hii ingetakiwa ifanyike nchi nzima,vijana wanaharibika

Tunawaunga mkono
 
Sio yeye tu hata sisi tunawaunga mkono wana Arumeru,wapo sahihi sana kupita maelezo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…