Waziri Gwajima tengua uamuzi wako wa kuunga mkono sheria ya maadili Arusha, hili ni bomu unatengeneza

Waziri Gwajima tengua uamuzi wako wa kuunga mkono sheria ya maadili Arusha, hili ni bomu unatengeneza

Anataka iwe kama Zanzibar.

Lengo amfurahishe mteuzi wake
Simfurahishi mtu yoyote pasipo tija Bali natimiza wajibu wangu kuiongoza jamii kwenda mbele na maendeleo na ustawi pasipo kuathiri taratibu za kawaida za binadamu. Hii video hapa chini ndiyo msimamo wangu thabiti kwenye hii hoja, hayo mengine msimamo wako. Kila mmoja na msimamo wake, tusubiri matokeo ndugu. Jioni njema na Baraka.


Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Nimpongeze Mheshimiwa waziri kwa majibu mazuri na elimishi.
Kwa upande wangu, mporomoko wa maadili unaanzia kwenye uvaaji; akina dada nguo za kubana, vimini, mipasuo (inayoacha nje sehemu kubwa ya mapaja) na suruali(jeans) zenye chane na kwa kina kaka kuvaa mlegezo. Uvaaji huo unaweza kupelekea msisimko wa mwili hivyo kuvuta hisia na kuhamisha akili ya mtu mwingine na kumletea mawazo hasi. Mitindo ya nywele sina tatizo nayo kwani sidhani kama ina athari zozote. Hivyo basi, jamii ielimishwe katika eneo hilo la uvaaji wa mitindo
sisimuzi.
Kuhusu kukaa bila kazi nyakati za mchana, nina imani kila mtu ana kwao/ kwake eneo anapoishi. Na kuna viongozi wa mitaa, basi hao viongozi wahakikishe wanajua shughuli za kila mtu anayeishi eneo lake na sheria ndogo za kudhibiti vitendo viovu (pengine vya kuiga mitandaoni) zinatungwa na kusimamiwa ipasavyo.
Kwa sheria na adhabu nilizoziona kwenye hiyo jamii, Vijana wanaweza kutoroka taratibu na kulowea ktk miji isiyo na hizo sheria hasa miji mikubwa ambako wanaweza kuharibika zaidi.
Ahsante Sana kwa mchango mzuri wenye tija ya hoja. Na mm hapa kama waziri mwenye dhamana ya jamii, siwezi kuwakatisha tamaa jamii hasa ambayo imeona kuwa imiliki ajenda ya mabadiliko. Hatua ngumu kuliko zote kwenye uongozi ni kuwafanya Wanadamu wawe sehemu ya ufumbuzi wa changamoto zao. Sasa Hawa wamefika wenyewe kwenye hatua hiyo, letu sisi kuwa guide, regulate, train... Ili wapanue mawazo wafike salama safari yao na kwa tija. Video ya mwelekeo wangu hii hapa[emoji116]


Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Kwamba mtu akinyoa kiduku basi maadili yameporomoka.... halafu ukikutana na mmasai mwanaume kasuka na mapambo ya shanga utamtetea aendele na hilo sababu ni utamaduni/asili? Nguo fupi, mitindo ya nywele haijawahi kuwa chanzo cha kuporomoka kwa maadili.

Hakuna watu smart wenye wanaovaa vizuri lakini ukifatilia wameoza kitabia?
Acheni kuwa mashabiki wa ujinga watu wa aina hii ndio mmekuwa vichocheo vya ushoga na mmonyoko wa maadili Kwa nyanja mbalimbali.
 
Habari za mchana.

Kwanza ahsante kwa kufuatilia habari za jamii.

Halafu, mimi ningekuwa wewe nataka kutoa ushauri kwanza ningeanza hivi;

Nashukuru Mungu sasa jamii imeanza kutambua umuhimu wa kudhibiti mmomonyoko wa maadili jambo ambalo ni kilio kikubwa na walau wanakaa na kujadili hata kama mijadala yao inaweza ikawa labda ina changamoto. Hii ni hatua moja.

Halafu ningeshauri kuwa, sasa tafadhali, wataalamu wa Maendeleo na Ustawi na wengine mbalimbali waende wakae na jamii hii wawaongoze vema Ili Nia yao nzuri isiishie njiani hasa ukizingatia kwamba yako mambo mengi ya kutazama.

Hapo mm ningeona ushauri wako mzuri sana na wewe ungekuwa pengine mwanatimu hiyo, kama mwingine aliyetoa ushauri makini kwenye ukurasa wa BASATA jana sasa tunamtumia.

Hii habari ya WAKATI WOTE kuwa NEGATIVE tu na jamii na kuibua MABAYA TU mema hapana mimi binafsi nakataa na ndiyo kinachotuzamisha sisi nchi nyingi za bara letu. Lazima tujue kupokea, kushauri na kurekebisha kwa hekima na kutia moyo wengine.

Hakuna jambo gumu kama kuifanya jamii Ione wajibu wao, hivyo wanapouona ni HATUA MOJA na wanapohitaji technical support ni HATUA INGINE.

Kwa taarifa yako, sisi kupitia uzoefu huu sasa tunapeleka maelekezo kote wakae wafanye mipango chini ya wataalamu kupitia hatua hii ya kuwa, jamii IMEONA KIU ya kufanya mabadiliko.

Hata hivyo, AHSANTE SANA kwa mchango wako. Pongezi kwao SITATENGUA ila tunaenda na wataalamu huko ili twende nao kisayansi zaidi maana hii ni safari ya mabadiliko ya fikra za jamii.

Ubarikiwe.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Hongera sana, lakini hata hivyo wapenda mabadiriko tupo na wewe binafsi napenda viongozi wanaosaidia jamii kukua kimaadili.
Nchi yetu inapitia kipindi kigumu vijana wengi wame iga tabia za hovyo mitandaoni, na kuzileta mtaani wanaishi maisha ya hovyo kiukweli inasikitisha simama katika ukweli na daima ukweli utashinda.
 
Habari za mchana.

Kwanza ahsante kwa kufuatilia habari za jamii.

Halafu, mimi ningekuwa wewe nataka kutoa ushauri kwanza ningeanza hivi;

Nashukuru Mungu sasa jamii imeanza kutambua umuhimu wa kudhibiti mmomonyoko wa maadili jambo ambalo ni kilio kikubwa na walau wanakaa na kujadili hata kama mijadala yao inaweza ikawa labda ina changamoto. Hii ni hatua moja.

Halafu ningeshauri kuwa, sasa tafadhali, wataalamu wa Maendeleo na Ustawi na wengine mbalimbali waende wakae na jamii hii wawaongoze vema Ili Nia yao nzuri isiishie njiani hasa ukizingatia kwamba yako mambo mengi ya kutazama.

Hapo mm ningeona ushauri wako mzuri sana na wewe ungekuwa pengine mwanatimu hiyo, kama mwingine aliyetoa ushauri makini kwenye ukurasa wa BASATA jana sasa tunamtumia.

Hii habari ya WAKATI WOTE kuwa NEGATIVE tu na jamii na kuibua MABAYA TU mema hapana mimi binafsi nakataa na ndiyo kinachotuzamisha sisi nchi nyingi za bara letu. Lazima tujue kupokea, kushauri na kurekebisha kwa hekima na kutia moyo wengine.

Hakuna jambo gumu kama kuifanya jamii Ione wajibu wao, hivyo wanapouona ni HATUA MOJA na wanapohitaji technical support ni HATUA INGINE.

Kwa taarifa yako, sisi kupitia uzoefu huu sasa tunapeleka maelekezo kote wakae wafanye mipango chini ya wataalamu kupitia hatua hii ya kuwa, jamii IMEONA KIU ya kufanya mabadiliko.

Hata hivyo, AHSANTE SANA kwa mchango wako. Pongezi kwao SITATENGUA ila tunaenda na wataalamu huko ili twende nao kisayansi zaidi maana hii ni safari ya mabadiliko ya fikra za jamii.

Ubarikiwe.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Kuja hapa na kushiriki huu mjadala tayar umeonyesha ww ni Kiongozi wa namna gani bila kujali utakachokiongea maana ulikuwa na uwezo wa kuipotezea hii mada na Kukaa zako kimya kama wafanyavyo viongozi wengine wa nchi, nakupongeza sana muheshimiwa tuko pamoja na wewe na kazi Yako inaonekana endelea na moyo huo huo na Mungu akutangulie katika majukumu Yako.

Uchaguzi ujao Chadema ikichukua nchi tunategemea uje kuwa wazir mkuu inshaallah!!
 
Mie naona wapo sahihi... na wanatakiwa waigwe.

Kuna vizazi vya watu wajinga wajinga sana wanakuja kutusumbua mitaani.
Juzi hapa kuna jamaa wa Arusha alikuwa analewa sana halafu anakuja kumuamsha mama yake usiku kwa matusi ili apewe chakula (mama yake ni mjane)....jamaa akaonywa mara ya 1, ya pili na ya tatu kwa muda wa wiki 3

Baada ya hapo jamii ya Waarusha wakambeba akiwa amelewa na kumpeleka porini... akachapwa viboko 70

Siku 3 nzima amelala ndani...na leo hagusi kabisa kilevi

Sasa hapo viboko havijasaidia?
 
Nimeshamjibu kwa kumshukuru na kumwelimisha, sijui kama atanielewa. Hebu na wewe soma uone kama naeleweka. Maana maana sasa nitoe mfano kuwa; mtu anapoanza hatua za mabadiliko anapita historia ndefu ya kuanza kutembea na kuanguka na kusimama. Sasa kama jamii yetu ndiyo inaanza jambo ambalo sijui wapi kwingine liliwahi fanyika, halafu anatoka mtu anasema halifai, maana yake tunazimisha hatua za jamii badala ya kwenda kushirikiana nao ku adjust Nia yao njema.

Hata hivyo niliamua kupongeza nikijua kabisa wako wengine wataangalia upande mmoja hasi waje waanze kuishusha chini ile jamii huku wao wenyewe wakiwa hawafanyi Chochote kwenye jamii zao waliko.

Mtihani sana ila tutashinda kwa ujasiri.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Mama Hongera sana, upo vizuri na endelea na juhudi hizo
 
Juzi hapa kuna jamaa wa Arusha alikuwa analewa sana halafu anakuja kumuamsha mama yake usiku kwa matusi ili apewe chakula (mama yake ni mjane)....jamaa akaonywa mara ya 1, ya pili na ya tatu kwa muda wa wiki 3

Baada ya hapo jamii ya Waarusha wakambeba akiwa amelewa na kumpeleka porini... akachapwa viboko 70

Siku 3 nzima amelala ndani...na leo hagusi kabisa kilevi

Sasa hapo viboko havijasaidia?
Waambie hao watandikaji.. waongeze tena 70 zingine ili wamrudishe kwenye Default settings kabisa. Hahah
 
Mimi nalia na wazazi wasio fundisha maadili watoto wao haya mambo hatutayaona kabisa. Lakini kuanza kukandamiza uhuru wa mtu binafsi ni ujinga tu.
 
Moja kwa moja kwenye mada,

Uongozi wa Kijiji Arumeru, Mkoa wa Arusha ulipitisha sheria ndogondogo za kukuza maadili baada ya matukio ya vijana kuuawa kwa makosa ya kuiba na mmomonyoko wa maadili ikiwemo kunyoa viduku na kuvaa vimini ndio sababu!

Waziri Dkt. Gwajima D uko serious kabisa ku endorse huu ujinga (respectfully)? Ni kweli kunyoa kidugu, kusuka nywele na kuvaa vimini ndio kunachangia mmonyoko wa maadili? Hili ni jambo ukaona uliunge mkono?

Tanzania na Afrika kwa ujumla imepambwa na tamaduni nyingi za kupendeza na baadhi ya mambo ni mitindo mbalimbali ya nywele na mavazi. Kutoka na muingiliano wa watu vitu vingine vinaenda na kubadilika mengine yakiwa sehemu ya buruduni, kama vile Ronaldo alivyoteleta kisahani na kikabamba. Sasa hii ni sababu ya kumfanya mtu atoe fine?

Huwezi kumpangia mtu cha kuvaa au mtindo wa nywele kama havunji sheria yoyote, shughulika na mzizi wa tatizo sio mambo ambayo hayana maana.

Nguo fupi au viduku vingekua ni sababu mababu zetu ndio sasa ndio watakuwa watu washenzi na waliokosa ustaarabu kuliko wote, Watindinga na Wahadzabe na wote wenye kufanana nao watakuwa hawana maana kabisa.

Vipi mwanaume akivaa bukta fupi huyu nae anaenda kulipa fine? Akiwa anapiga kazi zake huko juani shati kaliweka kiunoni anatembea kifua wazi, hapa vipi, anakuwa kamomonyoa maadili ya kijiji kizima?

Kijana akiwa kijiweni bila shughuli ya kufanya nayo fine, kwa soko gani la ajira la kuzuia vijana kuranda hovyo? Waziri Dkt. Gwajima D kuwa serious bwana, badala ya kuunga mkono hili ilitakiwa kutafuta njia ya kumaliza mzizi wa tatizo.

Vijana wanajiingiza kwenye wizi, badala ya kuweka sheria ambazo hazina maana uundwe mradi wa kuwaghulisha au wapewe ujuzi utakaowawezesha kujiajiri na kuishia kwenye uhalifu. Wewe ni mmoja wa watu smart sana serikalini usifanye vitu vya kijinga kama hivi vikaharibu CV yako.
Yale ni miongoni mwa maamuzi ya kipumbavu kabisa kuwahi kuyaona
 
Kwenye mavazi na vyovyote vile kwa nje hakutafsiri undani wa mtu. Nje ya mtu yaweza kuwa njema sana inavutia ila ndani yake ikawa hatari sana. Ila Kila jamii inajua kuweka diagnosis yake kwa wakati wake. Na jamii hii imeanza mjadala huo hivyo, maana yake Sasa imeona tatizo, ina kiu ya kubadilika na IMEFUNGUA MLANGO WA MAJADILIANO.

Sisi sasa, ambao tunadhani tunajua Sana, tunatakiwa kutafuta BOND nao na kuzungumza Ili kufikia kile tunachodhani kuwa, hiki sasa ni community reconciliation point. Vinginevyo hata sisi tunaodhani tunajua Sana, tuna changamoto ambazo hata huko vitani kwenye kurekebisha hayo maadili hatumo.

Ahsanteni, tuendelee kujadiliana.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
WAZIRI NIKUTAKE RADHI WASWAHILI WANASEMA ASHUKUM SIO MATUSI ILA TANZANIA HAKUNA MAADILI KUANZIA KWA VIONGOZI MPAKA WATU BINAFSI NADHANI UMESHAELEWA NACHOMAANISHA.
MTU MZIMA AKIVULIWA NGUO UCHUTAMA UNAFIKI NI KITU KIBAYA SANA.UKWELI NI KWAMBA TANZANIA HAKUNA MAADILI KUANZIA KWA VIONGOZI WETU NA BABA ZETU NA MAMA ZETU NA VIONGOZI WETU WA KIIMANI
NA KAMA YUPO MTANZANIA AU KIONGOZI WA KITANZANIA MWENYE MAADILI YA KITANZANIA NITAJIE HATA MMOJA.
LABDA TUANZE NA WEWE DADANGU UNAYO MAADILI YA KUJIVUNIA MBELE YA JAMII YAKO NA WATANZANIA KWA UJUMLA?????
 
Nimeshamjibu kwa kumshukuru na kumwelimisha, sijui kama atanielewa. Hebu na wewe soma uone kama naeleweka. Maana maana sasa nitoe mfano kuwa; mtu anapoanza hatua za mabadiliko anapita historia ndefu ya kuanza kutembea na kuanguka na kusimama. Sasa kama jamii yetu ndiyo inaanza jambo ambalo sijui wapi kwingine liliwahi fanyika, halafu anatoka mtu anasema halifai, maana yake tunazimisha hatua za jamii badala ya kwenda kushirikiana nao ku adjust Nia yao njema.

Hata hivyo niliamua kupongeza nikijua kabisa wako wengine wataangalia upande mmoja hasi waje waanze kuishusha chini ile jamii huku wao wenyewe wakiwa hawafanyi Chochote kwenye jamii zao waliko.

Mtihani sana ila tutashinda kwa ujasiri.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Hakuna cha msingi ulichomjibu mtoa mada, ameongelea uhalisia na namna ya kukabiliana na hizo changamoto. Kilichofanywa na hao viongozi wa kijiji husika hakipaswi kuungwa mkono kamwe, na ni uvunjifu mkubwa wa haki za raia. Wajaribu kutatua chanzo na wewe hukupaswa kuliunga hilo mkono.
Hicho kijiji si kisiwa ni kama ambavyo nchi yetu si kisiwa, nikitoka mjini ambako hakuna hiyo sheria na kwenda huko kuwa salimia wazee na nimevaa suruali ya jinzi iliyotobolewa magotini nitachukuliwa kama muhalifu na kutozwa faini. Nchi ya ajabu sana hii.
Kuweni serious na masuala ya msingi kwa maendeleo ya nchi hii na si bla bla kila siku
 
Ukitaka kulipima jambo lolote kama ni baya au zuri lipime Kwa watu unao wapenda mfano unajisikiaje baba Yako au mama Yako wakinyoa viduku? Vipi mama yako au dada Yako akitembea uchi?
Lina koneksheni gani na uhalifu au mmomonyoko wa maadili. Hadi Karne iliyopita tulikuwa tukicheza ngoma za asili huku wadada chuchu zikiwa nje.
 
Hakuna cha msingi ulichomjibu mtoa mada, ameongelea uhalisia na namna ya kukabiliana na hizo changamoto. Kilichofanywa na hao viongozi wa kijiji husika hakipaswi kuungwa mkono kamwe, na ni uvunjifu mkubwa wa haki za raia. Wajaribu kutatua chanzo na wewe hukupaswa kuliunga hilo mkono.
Hicho kijiji si kisiwa ni kama ambavyo nchi yetu si kisiwa, nikitoka mjini ambako hakuna hiyo sheria na kwenda huko kuwa salimia wazee na nimevaa suruali ya jinzi iliyotobolewa magotini nitachukuliwa kama muhalifu na kutozwa faini. Nchi ya ajabu sana hii.
Kuweni serious na masuala ya msingi kwa maendeleo ya nchi hii na si bla bla kila siku
Ukiwa kiongozi unatakiwa ku regulate mambo ya jamii yaende mahala sahihi, siyo kuzimisha hatua za jamii kwamba wewe na mimo ndiyo tunajua zaidi. Sasa mm msimamo wangu ni ku regulate, kuwezesha jambo lenye Nia njema liende kwenye mstari sahihi. Sawa, kama kwenye maneno yangu hapa kwenye video. Naanza na wewe kukuelimisha kwanza maana na ww ni sehemu ya jamii vilevile.


Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
WAZIRI NIKUTAKE RADHI WASWAHILI WANASEMA ASHUKUM SIO MATUSI ILA TANZANIA HAKUNA MAADILI KUANZIA KWA VIONGOZI MPAKA WATU BINAFSI NADHANI UMESHAELEWA NACHOMAANISHA.
MTU MZIMA AKIVULIWA NGUO UCHUTAMA UNAFIKI NI KITU KIBAYA SANA.UKWELI NI KWAMBA TANZANIA HAKUNA MAADILI KUANZIA KWA VIONGOZI WETU NA BABA ZETU NA MAMA ZETU NA VIONGOZI WETU WA KIIMANI
NA KAMA YUPO MTANZANIA AU KIONGOZI WA KITANZANIA MWENYE MAADILI YA KITANZANIA NITAJIE HATA MMOJA.
LABDA TUANZE NA WEWE DADANGU UNAYO MAADILI YA KUJIVUNIA MBELE YA JAMII YAKO NA WATANZANIA KWA UJUMLA?????
Hongera Sana ww mtakatifu mwenye Nuru [emoji847][emoji847][emoji847]inuka sasa uangaze Nuru yako ikawe dawa kwenye janga hili la mmomonyoko wa maadili.... sisi tunasubiri Nuru yako ituangazie....

Uzuri hata Sauli kabla hajawa Mtume Paulo alitoka kwenye dhambi nyingi, akaja akageuka kuwasafisha wengine. Inuka tu uangaze sisi tuna shida na Nuru.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Hongera Sana ww mtakatifu mwenye Nuru [emoji847][emoji847][emoji847]inuka sasa uangaze Nuru yako ikawe dawa kwenye janga hili la mmomonyoko wa maadili.... sisi tunasubiri Nuru yako ituangazie....

Uzuri hata Sauli kabla hajawa Mtume Paulo alitoka kwenye dhambi nyingi, akaja akageuka kuwasafisha wengine. Inuka tu uangaze sisi tuna shida na Nuru.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
TATIZO MH UNALETA SIASA KWENYE MAISHA HALISI YA VIJANA WA KITANZANIA AMBAO TUNA UPEO WA KUELEWA MAMBO KIUELEDI.
VIONGOZI WETU HAWANA MAADILI NA NDIO VIOO VYA JAMII WANAOIGWA NA VIJANA .NA VIJANA WANAIGA YANAYOFANYWA NA VIONGOZI WETU AMBAO WANAOONGOZA KWA MMOMONYOKO WA MAADILI TENA WAZIWAZI BILA VIFICHO.
WA KULAUMIWA NI VIONGOZI WETU TULIOWAPA DHAMANA YA KUTUONGOZA WAMEKOSA MAADILI NA UKIWAKOSOA BASI WEWE NI JEURI NA HUNA NIDHAMU NA MHAINI UNASITAHILI KIFUNGO NA ADHABU KALI.
WATANZANIA WANAOGOPA KUSEMA NDIO MAANA WAPO KIMYA.
 
TATIZO MH UNALETA SIASA KWENYE MAISHA HALISI YA VIJANA WA KITANZANIA.
VIONGOZI WETU HAWANA MAADILI NA NDIO VIOO VYA JAMII WANAOIGWA NA VIJANA .NA VIJANA WANAIGA YANAYOFANYWA NA VIONGOZI WETU AMBAO WANAOONGOZA KWA MMOMONYOKO WA MAADILI TENA WAZIWAZI BILA VIFICHO.
WA KULAUMIWA NI VIONGOZI WETU TULIOWAPA DHAMANA YA KUTUONGOZA WAMEKOSA MAADILI NA UKIWAKOSOA BASI WEWE NI JEURI NA HUNA NIDHAMU NA MHAINI UNASITAHILI KIFUNGO NA ADHABU KALI.
WATANZANIA WANAOGOPA KUSEMA NDIO MAANA WAPO KIMYA.
Hata mm sijakudharau kabisa, tena wala sijakubeza. Ila nimekuongoza tu kwenye mstari wa hekima kuwa, ukipewa neema ya kuwa mwana wa Nuru, usianze kuhoji kwa nn huyu ni mwana wa Giza ila amestahili hili. Wewe inuka uangaze ufanye jambo la kuleta nafuu kwenye jamii, utaonekana na utainuliwa na Mungu utatumika kwa ajili ya jamii. Sasa na wewe tatizo lako ukielezwa lugha za hekima unaona umepuuzwa unaletewa siasa. Njoo Sasa huku tuna mitandao mingi ya Mashujaa wa kijamii uje tushirikiane, na karama yako ionekane. Vinginevyo kukaa humu na kushutumu na uko mbali uwanja wa vita mm naona na ww huna msaada na hatutoki tulipokwama.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom