Waziri Innocent Bashungwa awakabidhi Wakuu wa Majeshi Wastaafu Land Cruiser LC300 mpya

Waziri Innocent Bashungwa awakabidhi Wakuu wa Majeshi Wastaafu Land Cruiser LC300 mpya

View attachment 2635275
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Innocent Bashungwa @innocentbash amewakabidhi magari mapya Wakuu wa Majeshi Wastaafu kwa maelekezo ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Wakuu wa Majeshi Wastaafu waliokabidhiwa magari ni CDF Mstaafu George Waitara na Robert Mboma na makabidhiano hayo yamefanyika katika Ofisi za Wizara ya Ulinzi Mtumba Jijini Dodoma

Akikabidhi Magari hayo, Waziri Bashungwa amesema kuwapatia Wastaafu hao magari ni sehemu ya maelekezo ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba wapatiwe magari mapya ambayo yanatengenezeka na spea zake zinapatikana kwa urahisi.

“Wakuu hawa wa Majeshi Wastaafu walifanya kazi kubwa na iliyotukuka kipindi cha utumishi wao kwa Nchi yetu, Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan imewapatia magari na kuwatakia kheri na maisha marefu Majenerali Wastaafu hawa”

AYO TV
kwani wastaafu wako wawili tu?
 
Wakuu wa wabrashi viatu wao haiwahusu? au ndo waliamua kujichangachanga wenyewe walau wakatoa ile Prado...
CDF ( Chief of Defence forces) ni Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama ( ikiwemo jeshi la Polisi)


wengi wanadhani akitajwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na usalama maana yake ni Mkuu wa Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) huyu ni Bosi wa Majeshi yote na ndio sababu wakuu wote wa Jeshi la Polisi, Magereza, Uhamiaji ni wasaidizi wake

jeshi la Polisi ni sehemu ya Defence forces

hivyo IGP kupewa gari sawa na Bosi wake si sawa
 
Kutaja miaka ni kosa, hapa una refer to kifungu gani? Kindly share hicho kifungu, au kushare hicho kifungu cha sheria nayo ni kosa?
kuweka hadharani circular za Serikali ni kosa kwa mujibu wa sheria

umesahau Mwananchi iliwahi kufungiwa kwa kuweka hadharani stahiki za mawaziri kwa mujibu wa sheria?

sikumbuki vifungu rasmi kwa kuwa si Mwanasheria na sijawahi kuvikariri
 
CDF ( Chief of Defence forces) ni Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama ( ikiwemo jeshi la Polisi)


wengi wanadhani akitajwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na usalama maana yake ni Mkuu wa Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) huyu ni Bosi wa Majeshi yote na ndio sababu wakuu wote wa Jeshi la Polisi, Magereza, Uhamiaji ni wasaidizi wake

jeshi la Polisi ni sehemu ya Defence forces

hivyo IGP kupewa gari sawa na Bosi wake si sawa

Hakuna mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama mkuu.

Kuna mkuu wa majeshi ya ulinzi tu.yaani ,ardhi,anga na maji.
Kiitifaki Yeye ni superior kwa wakuu wa vyombo vya mrengo huo yaani anakuwa senior kwa IGP,DGTISS,CGP,CGF,DGPCCB nk.
 
View attachment 2635275
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Innocent Bashungwa @innocentbash amewakabidhi magari mapya Wakuu wa Majeshi Wastaafu kwa maelekezo ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Wakuu wa Majeshi Wastaafu waliokabidhiwa magari ni CDF Mstaafu George Waitara na Robert Mboma na makabidhiano hayo yamefanyika katika Ofisi za Wizara ya Ulinzi Mtumba Jijini Dodoma

Akikabidhi Magari hayo, Waziri Bashungwa amesema kuwapatia Wastaafu hao magari ni sehemu ya maelekezo ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba wapatiwe magari mapya ambayo yanatengenezeka na spea zake zinapatikana kwa urahisi.

“Wakuu hawa wa Majeshi Wastaafu walifanya kazi kubwa na iliyotukuka kipindi cha utumishi wao kwa Nchi yetu, Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan imewapatia magari na kuwatakia kheri na maisha marefu Majenerali Wastaafu hawa”

AYO TV
Kwa kweli sisemi neno zaidi ya kusisitiza UZALENDO kwa Taifa maskini la Tanzania.

Wanajeshi tunapaswa kuwajali sana yes. Wana uzalendo wa kweli. Lakini tunapaswa pia kukumbuka kuwa nchi ipo kwenye mkongojo wa kouchumi.


Enewei nisiandike sana, mdomo koma!
 
Mwamunyange
Mabeyo

Hawa vipi? Wao hawahusiki au??

IMG_1454.jpg
 
Kwa kweli sisemi neno zaidi ya kusisitiza UZALENDO kwa Taifa maskini la Tanzania.

Wanajeshi tunapaswa kuwajali sana yes. Wana uzalendo wa kweli. Lakini tunapaswa pia kukumbuka kuwa nchi ipo kwenye mkongojo wa kouchumi.


Enewei nisiandike sana, mdomo koma!
Nimeona hata Bajeti ya Wizara ya ulinzi nimkubwa sana ,Til.3 za wazi Je ambazo hazitajwi ni kiasi gani?

Hii nayo sio sawa sana Kwa Nchi Maskini kama Tanzania
 
Akikabidhi Magari hayo, Waziri Bashungwa amesema kuwapatia Wastaafu hao magari ni sehemu ya maelekezo ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba wapatiwe magari mapya ambayo yanatengenezeka na spea zake zinapatikana kwa urahisi.
Bei ya spea za haya magari kwa wastaafu itakuwa rafiki kweli?!
 
Back
Top Bottom