Waziri Jafo: Tanzania Bara kuingia Zanzibar kwa pasipoti ni kujirudisha nyuma

Waziri Jafo: Tanzania Bara kuingia Zanzibar kwa pasipoti ni kujirudisha nyuma

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Bunge limepitisha bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Waziri mwenye dhamana, Dkt Selemani Jafo akisema hoja ya kutaka kurejesha utaratibu wa watu wa Tanzania Bara kuingia Zanzibar kwa pasipoti ni kujirudisha nyuma.

Jafo amesema hayo jana Jumanne Aprili 23, 2024 akitoa majumuisho ya jumla kuhusu hoja za Wabunge zilizotokana na mjadala wa bajeti ya wizara hiyo.

“Kaka yangu pale alipozungumza kwamba, kwa nini watu wasiingie na pasipoti Zanzibar, nikasema aah! kaka wazo zuri lakini unataka kuturudisha nyuma.”

“Katika mchakato huu Serikali ya awamu ya pili chini ya hayati Mzee Mwinyi (Ali Hassan Mwinyi) wakati kule Serikali iliyokuwa chini ya Rais Dk Salmin Amour, kipindi kile walikuwa wanajadili, jambo hili lilitoka kipindi hicho likaonekana linaleta usumbufu,” amesema Dk Jafo.

“Hivi mtu leo mtani wangu Gwajima (mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima) atoke Kawe akienda kule Zanzibar atafute pasipoti, tutarudi nyuma sana, na hii si makusudio ya Muungano wetu,” amesema.

Hoja ya kurejesha pasipoti Zanzibar ilitolewa na mbunge wa Konde, Mohamed Said Issa aliyesema Rais wa kwanza hayati Mwalimu Julius Nyerere alikuwa ana akili sana na kwamba haamini kama alizidiwa maarifa na Rais Sheikh Abeid Amani Karume kwa kusema Zanzibar watu waingie kwa utaratibu.

=======================

Minister Dr. Selemani Jafo said that the proposal to reinstate the requirement for mainland Tanzanians to enter Zanzibar with a passport would be a step backward. He mentioned that during the second phase of the government, under the late President Ali Mwinyi, this issue was discussed and it was deemed to be troublesome. Jafo emphasized that this would cause significant setbacks and is not in line with the spirit of our Union.

Pia soma
 
Pongezi ziende Kwa Marehemu Mtikila aligoma kutii masharti kuwa chama Cha Sasa ili kisajiliwe kinatakiwa kuwa na wanachama pande zote mbili za muugano ikiwemo Zanzibar.Wakati huo kwenda Zanzibar ilikuwa watu wanaenda na passport.Akasema hiyo ni sawa na kwenda kusajili raia wa nchi nyingine kuwa wanachama wa chama Cha Sasa Cha nchi ingine.Akagoma kuwa siwezi beba passport kwenda nchi nyingine kutafuta wanachama na akatishia kuburuza Serikali mahakamani wafute Hilo sharti.Passporrt zikafutwa .Sharti la kuwa na wanachama pande zote likabaki
 
Pongezi ziende Kwa Marehemu Mtikila aligoma kutii masharti kuwa chama Cha Sasa ili kisajiliwe kinatakiwa kuwa na wanachama pande zote mbili za muumgano ikiwemo Zanzibar.Wakati huo kwenda Zanzibar ilikuwa watu wanaenda na passport.Akasema hiyo ni dawa na kwenda kusajili raia wa nchi nyingine kuwa wanachama wa chama Cha Sasa Cha nchi ingine.Akagoma kuwa siwezi beba passport kwenda nchi nyingine kutafuta wanachama na akatishia kuburuza Serikali mahakamani wafute Hilo sharti.Passporrt zikafutwa .Sharti la kuwa na wanachama pande zote likabaki
Mtikila alikuwa mwamba sana kwenye masuala ya katiba na muungano
 
Hii ishu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni sawa na mke na mume.., yaani mke chake ni chake lakini cha mme ni cha wote!! inashangaza sana.
Uko vizuri mkuu. Aina hii ya muungano haipo mahali popote duniani. Namkumbuka Mbunge Charles Kashemeza Kabuye (RIP) alipendekeza Zanzibar iwe mkoa wa 21(wakati Ile) na Dr. Salmon Amour awe mkuu wa mkoa. Namkumbuka wabunge wa Zanzibar walitaka kummeza!! Ipo siku akili ikitukaa sawa tutaukubali ushauri wake! Keep za muungano kuzimaliza ni ngumu. Au nasema uongo ndugu zangu!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Bunge limepitisha bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Waziri mwenye dhamana, Dkt Selemani Jafo akisema hoja ya kutaka kurejesha utaratibu wa watu wa Tanzania Bara kuingia Zanzibar kwa pasipoti ni kujirudisha nyuma.

Jafo amesema hayo jana Jumanne Aprili 23, 2024 akitoa majumuisho ya jumla kuhusu hoja za Wabunge zilizotokana na mjadala wa bajeti ya wizara hiyo.

“Kaka yangu pale alipozungumza kwamba, kwa nini watu wasiingie na pasipoti Zanzibar, nikasema aah! kaka wazo zuri lakini unataka kuturudisha nyuma.”

“Katika mchakato huu Serikali ya awamu ya pili chini ya hayati Mzee Mwinyi (Ali Hassan Mwinyi) wakati kule Serikali iliyokuwa chini ya Rais Dk Salmin Amour, kipindi kile walikuwa wanajadili, jambo hili lilitoka kipindi hicho likaonekana linaleta usumbufu,” amesema Dk Jafo.

“Hivi mtu leo mtani wangu Gwajima (mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima) atoke Kawe akienda kule Zanzibar atafute pasipoti, tutarudi nyuma sana, na hii si makusudio ya Muungano wetu,” amesema.

Hoja ya kurejesha pasipoti Zanzibar ilitolewa na mbunge wa Konde, Mohamed Said Issa aliyesema Rais wa kwanza hayati Mwalimu Julius Nyerere alikuwa ana akili sana na kwamba haamini kama alizidiwa maarifa na Rais Sheikh Abeid Amani Karume kwa kusema Zanzibar watu waingie kwa utaratibu.
Na wao wakiji huku kwa passport itakuaje?
 
Uko vizuri mkuu. Aina hii ya muungano haipo mahali popote duniani. Namkumbuka Mbunge Charles Kashemeza Kabuye (RIP) alipendekeza Zanzibar iwe mkoa wa 21(wakati Ile) na Dr. Salmon Amour awe mkuu wa mkoa. Namkumbuka wabunge wa Zanzibar walitaka kummeza!! Ipo siku akili ikitukaa sawa tutaukubali ushauri wake! Keep za muungano kuzimaliza ni ngumu. Au nasema uongo ndugu zangu!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Kuliwezesha hilo lazima kwanza uondoe status ya uzanzibar kwa wananchi ndani ya Zanzibar.

Watu wote wajione ni watanzania na siyo wazanzibar inawezekana lakini kwa miaka mingi sana.
 
Na wazanzibari kuingia bara eaingie na passport pia ,mbeleni huko wataishi juu ya maji wasipoacha huo ubinafsi ,waasisi wetu waliona mbali kufanya mungano huu ili Zanzibar ikijaa watu wapungue kuishi bara kama ilivyo sada
 
Back
Top Bottom