Pre GE2025 Waziri Jafo: Zaidi ya Viwanda 28,000 Vimejengwa Ndani ya Miaka 4 ya Rais Samia.Ampongeza Kwa Kuleta Mageuzi Makubwa ya Uwekezaji

Pre GE2025 Waziri Jafo: Zaidi ya Viwanda 28,000 Vimejengwa Ndani ya Miaka 4 ya Rais Samia.Ampongeza Kwa Kuleta Mageuzi Makubwa ya Uwekezaji

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Jamani mbona mapambio yamezidi kuwa ni matusi sasa kwa Samia.

Kwamba mnataka kuwaaminisha watanzania (watanganyika) kuwa hii ndo mara ya kwanza kwa taifa kupata viwanda?

Viwanda 30,000?! Je viimezalisha ajira kiasi gani? Vimetoa ajira kwa vijana kiasi gani? Je hivi Viwanda ni vya Samia au Viwanda vya Watanzania?!

Kuanzia Nyerere, kwenda kwa Mwinyi, kisha Mkapa, na baadaye Kikwete pamoja na Hayati Magufuli, kulikuwa na viwanda kiasi gani mpaka viwanda hivi 30,000 vionekane kama ndo nuru ya ajabu kwenye hili taifa?! Ongeeni ukweli huyu Mama mnamtoa kwenye reli tayari kwa mapambio kana kwamba kila anachokifanya anatumia pesa zake binafsi yeye na Mzee Hafidh.

Samia ni mtumishi wa umma, hizi sifa na pongezi pelekeni kwa watanzania wanaotoa kodi kwa ajili ya taifa lao, Samia halipi kodi ya aina yoyote na anatumia pesa za watanzania na kutunzwa na watanzania. Sitaki kukuita chawa ila punguzeni mapambio mnatengeneza picha kuwa Samia anatufanyia hisani kwa pesa zake! UONGO KIWANGO CHA LAMI NA NYIE MNAFAHAMU HILO
 
Awamu ya Samia ndio imetafsiri maana halisi ya Tanzania ya viwanda na sio vi wonder kama kule tulikotoka. Pia soma Rais Samia anatafsiri Tanzania ya viwanda kwa vitendo

Nawakumbusha tuu kwamba sera ya Kufungua Nchi inalipa na imeleta majibu .👇👇

View: https://www.instagram.com/reel/DGlUKyzNpXW/?igsh=MXVpeW5odDltM3N5eg==

Vinazalisha energy, na visungura labda. Hivi viwanda 30,000 vinazalisha bidhaa gani au ni kauli ile ukiwa na cherehani 3 basi ni kiwanda
 
30,000 wewe huna hata kimoja!? Ukoo wako hauna hata kimoja, Familia yako haina

Wanyonge hawa
 
Magufuli hakujenga? Au ndiyo kumpa mama yenu sifa za kitoto ili awape ugali.
 
Jibu swali - Magufuli alijenga vingapi? Afu msivyo na aibu eti Bwawa la Nyerere, SGR, Daraja la Busisi mnasema juhudi za mama yenu...loooh
Kaulize mashabiki wa Magufuli unaniuliza Mimi kwani umewahi niona namkubali Mwendazake?
 
We don't need those tanks wenee an investoe who will build LNG Plant at Mtwara
Uko out of touch,Mama anajenga Lindi https://www.reuters.com/business/en...onclude-talks-lng-project-by-june-2025-02-11/
Screenshot_20250301-213555.jpg
 
Manufacturing plant, processing plant, production plant.

30,000 plants constructed in 4 years? In this very Tanzania?

Honestly speaking, we don’t need this crap here!

Hizi porojo duni ziishie kwenye majukwaa ya siasa na vikao vya machawa.
Ajabu Iko wapi Sasa?
 
Unajua maana ya viwanda 30,000 wewe?

Vingejengwa 500 tu usingesikia kelele za vijana wasio na ajira!

Acheni propaganda za kijinga!
Hata shughuli za mamantilie wanaopika vitumbua navyo ni viwanda. Hata shughuli za wale wanatengeneza keki za harusi, birthday, graduation and so on, navyo ni viwanda!
 
Back
Top Bottom