Waziri Jerry Slaa: Mimi siyo Mtoto wa Maskini, baba yangu alikuwa Rubani. Nimekataa Rushwa ya Milioni 300

Waziri Jerry Slaa: Mimi siyo Mtoto wa Maskini, baba yangu alikuwa Rubani. Nimekataa Rushwa ya Milioni 300

Waziri wa Ardhi mh Jerry Slaa amesema kuna Wanasiasa wanaona Sifa kujiita Watoto wa Maskini Lakini yeye siyo Maskini baba yake alikuwa Rubani na hadi leo anakula hela ya Urithi.

Mh Slaa ametuma salamu kwa mafisadi wote kwamba yeye hana Njaa na hapokei Rushwa kwa sababu Biblia imesema mla Rushwa ni kipofu.

Waziri amekataa Rushwa ya tsh 300 milioni kutoka kwa tajiri Mmoja aliyejenga kituo cha Mafuta Kinyume cha utaratibu pale Mikocheni.

I wish you a Merry Christmas 😀
Usanii mtupu
 
HUYU WAZIRI KASEMA UKWELI
BABA YAKE NI MCHAGGA WA MACHAME NIMEFANYA NAYE KAZI AKIWA RUBANI NA MAMA
YAKE ALIKUWA AFISA WA NGAZI YA JUU WA JESHI LA POLISI.SASA FIKIRIA RUBANI WA SIKU NYINGI HALAFU MCHAGA. WAZIRI KASEMA UKWELI.
Tunao marubani wengi mtaani ambao wamestaafu toka kwenye complex aviation (military) ambako hakuna auditing (umewahi kusikia CAG ame-audit jeshi?); badala ya simple aviation (civil) na pia wamo wachaka (wachagga) lakini ni machokambaya hatari.
 
Waziri wa Ardhi mh Jerry Slaa amesema kuna Wanasiasa wanaona Sifa kujiita Watoto wa Maskini Lakini yeye siyo Maskini baba yake alikuwa Rubani na hadi leo anakula hela ya Urithi.

Mh Slaa ametuma salamu kwa mafisadi wote kwamba yeye hana Njaa na hapokei Rushwa kwa sababu Biblia imesema mla Rushwa ni kipofu.

Waziri amekataa Rushwa ya tsh 300 milioni kutoka kwa tajiri Mmoja aliyejenga kituo cha Mafuta Kinyume cha utaratibu pale Mikocheni.

I wish you a Merry Christmas 😀
Rushwa inatangazwa hivi? Job true true
 
Mimi kuna kitu sikuelewi

Huyo mwenye petrol station kosa lake nini hasa ? Kwa nini ashupaliwe hivyo?


Kama kujenga kituo labda maeneo ya makqzi uswahilini mbona viko vingi mno tena viko kwenye Mbanano wa wa makazi kote ikiwemo jimboni kwake
Mbona huo mfoko hatujauona akifoka kule wakati vituo kibao viko makazi ya watu?
Vya jimboni kwake huenda alivuta. Sasa Mikocheni amekutana na mamaa wa UN Habitat, patachimbika bila greda kama NEMC, EWURA na Manispaa walivuta na kutoa vibali. Kama wanataka kuujuwa muziki mnene wa Tibaijuka vizuri wafe wakamuulize Mugabe, Malkia Elizabeth na Mkapa kuhusu makazi Harare.
 
Inawezekana mnyororo wa thamani ulikuwa mrefu bwashee Mwekezaji katoa B 3 Waziri anapelekewa M 3 yaani 10%

Hata Wewe usingekubali Wahuni waondoke na 90%

Waziri Silaa anadai, amesikia mzigo ulishawekwa mezani ila yeye hajapokea mgao kwa sababu Biblia imekataza hayo mambo

Mlale Unono 😃😃
 
Inawezekana mnyororo wa thamani ulikuwa mrefu bwashee Mwekezaji katoa B 3 Waziri anapelekewa M 3 yaani 10%

Hata Wewe usingekubali Wahuni waondoke na 90%

Waziri Silaa anadai, amesikia mzigo ulishawekwa mezani ila yeye hajapokea mgao kwa sababu Biblia imekataza hayo mambo

Mlale Unono 😃😃
Huyo jerry kitambo mimi namuona hasomeki!
 
Back
Top Bottom