Waziri Lukuvi awataka wamiliki wa ardhi kujenga kwa kufuata sheria

Kwa nini anawataka? Chukua hatua kila siku blah blah tu, watu wanaendelea kuvunja sheria, chukua hatua na siyo matamko, ...
 
 
Pia inakuwaje mpaka leo kuna vijiji vimo ndani ya halmashauri za manispaa? Hii inachochea ujenzi holela unaofanywa na watu kutoka mjini kati.
 
Halafu siku hizi mtu anatakiwa kulipia land rent kwenye kiwanja kisicho na hati?

Haya yameanza lini jamani?

Kwanini msipimie watu kwanza wakishapata hati ndiyo walipie?
 
Eti ukienda Manispaa wanakwambia eneo lako liko wapi? Unawajibu sehemu fulani, wanakwambia leo hatushulikii maeneo ya huko, njoo wiki ijayo siku fulani !

Siku utakayoenda utaambiwa kanunue ramani wizara ya ardhi kwanza halafu uje nayo Hapa Manispaa.

Ukishaenda kununua ukija afisa ardhi anakwambia kuja kuona site shilingi 100,000 na kuendelea.

Bado gharama ya kibali chenyewe na nauli ya kufuatilia nenda rudi.

Hapo bado uambiwe eneo lako limeingiliana na eneo la jirani yako kwenye ramani,

Sasa kama limeingiliana na eneo la jirani mimi mwananchi nifanyeje?

Je wizara haijaweka utaratibu wa nini kifanyike iwapo ikitokea hivyo?

Au uambiwe ramani inaonesha eneo ni bonde, unamuuliza ulivyoenda kuona uliona bonde pale? Anakwambia hapana sikuona bonde.

Basi baada ya hapo ni nenda rudi utapigwa danadana hadi ujikatie tamaa mwenyewe na kugairi kujenga!

Watu wengi sana wamegairi kujenga kwa huo usumbufu ulojitokeza!
 
Sheria ilikuwepo kitambo sema swala ilikua kumpata mtu wa kuitekeleza tu.

Tanzania tuna mambo mengi sana mazuri ila yapo kwenye makaratasi hakuna wa kuyafanya yakaonekana.
 
Sheria ilikuwepo kitambo sema swala ilikua kumpata mtu wa kuitekeleza tu.

Tanzania tuna mambo mengi sana mazuri ila yapo kwenye makaratasi hakuna wa kuyafanya yakaonekana.
Kuna mda akili zikiwarudia hadi mnafurahisha
 


Nadhani lengo la lukuvi ilitakiwa kwa skwata tu ili wakusanye kodi na kupanga vizuri ,sasa maeneo yaliyopimwa si kila mtu anajua mipaka yake na pia matumizi ya eneo lake kama residential,comercial au social services etc hapa kibali ni kwa ajili ya kukusanya kodi tu.
 
Hivi mbona watu wengi wanajijengea tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…