Waziri Makamba avunja Kitengo cha Habari na Mawasiliano TANESCO kwa tuhuma za kushindwa kulisemea Shirika

Mpaka huyo Waziri anakuja kuvunja Idara ya shirika huyo MD yuko wapi? Inaelekea Waziri Makamba is micromanaging TANESCO kwa maslahi yake mwenyewe sio ya nchi!!! Sasa alitaka hicho kitengo kiseme uongo kuhusu utendaji mbovu wa shirika?

Alitaka waseme umeme unawaka kila kona
 

This loony’s action is ultra vires!

Kitu gani kinampa uhalali wa kufanya kazi za Management ya TANESCO?
 
Tanesco wsmrejeshe Mramba huyu Maharage wampe ubunge wa kuteuliwa akachape usingizi bungeni na covid 19.
Tanesco Ni kampuni kubwa sana sio sehemu ya kufanyia majaribio
Mramba saizi ni boss mkubwa,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara
 
Kwani akija Waziri mwingine ndio inaenda kufunga nati kwenye karakana za Tanesco?

Waziri yuko sahihi kuwafuta Kazi hao wapuuzi.
Kitengo cha habari hawana lawama yoyote.
Mimi nikifikiri January ana akili, kumbe ni wash out.
Haya kafukuza kitengo umeme utaacha kukatika?
Kwa kweli hakutumia busara, umeme si maneno maneno ya utetezi, akafanye kazi, si bla bla!
 
Reactions: Qwy
Waziri hana mamlaka ya kumfukuza kazi mfanyakazi wa shirika.
 
Kitengi cha habari hawana lawama yoyote.
Mimi nikifikiri January ana akili, kumbe ni wash out.
Haya kafukuza kitengo umeme utaacha kukatika?
Kwa kweli hakutumia busara, umeme si maneno maneno ya utetezi, akafanye kazi, si bla bla!
Swala si kuacha kukatika,swala ni kutotoa sababu za kukatika kiasi kwamba malalamiko yanakuwa mengi.

Shida kubwa ya Tanesco ni miundombinu ya usambazaji iliyochoka na hata ukihitaji huduma kuna foleni,huu upuuzi wa Tanesco haujawahi kuisha.
 
Tanesco wsmrejeshe Mramba huyu Maharage wampe ubunge wa kuteuliwa akachape usingizi bungeni na covid 19.
Tanesco Ni kampuni kubwa sana sio sehemu ya kufanyia majaribio
Nakubaliana kabisa!
 
Kwani ni kitengo cha Propaganda ?

Angefanya la maana kama angejitengua mwenyewe..., unadhani kama kuna mazuri ya kusema watu hata hawatahitaji kuambiwa
 
Makamba angeweza kuleta kampuni la kigeni litushauri kuhusu ATCL , ujenzi wa bwawa na SGR maana tayari amefanya hivyo Tanesco amewapa wahindi na TPDC amewapa waingereza

Teh Teh na umeme bado ni shida[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Dictatorship all over, anamfuatisha mama yake
 
Kwani ni kitengo cha Propaganda ?

Angefanya la maana kama angejitengua mwenyewe..., unadhani kama kuna mazuri ya kusema watu hata hawatahitaji kuambiwa

Badra Masoud alitakiwa kusema umeme upo nchi nzima
 
Watafukuzwa wangapi? Acheni kuingilia utendaji wa Tanesco muacheni MD afanye kazi...MD ndiye alitakiwa kuvunja hicho kitengo kama anaona kuna shida Makamba anaingilia utenda kazi wa MD
Kazi ndio haionekani sasa,waje na Mpango mkakati wa kuhakikisha umeme haukatiki hovyo hovyo tuu.

Pili huduma zao ziwe kwa wakati,haiingii akilini unaomba kuunganishwa umeme danadana na urasimu vinaanza.
 
Hapa tatizo ni tanesco kukosa mshindani wake kibiashara wizara iruhusu usajili wamakampuni mengine yakuzalisha nakusambaza umeme uzalendo umekua mgumu sana
 
Tatizo ndio kwaanza Linaongezwa
Kupatwa kwa Tanzani
 
Badra left tanesco many years ago
 
Makamba angeweza kuleta kampuni la kigeni litushauri kuhusu ATCL , ujenzi wa bwawa na SGR maana tayari amefanya hivyo Tanesco amewapa wahindi na TPDC amewapa waingereza
Hii ndio nchi yetu pendwa kwamba tunatumia mabilioni ya kodi za walala hoi kulipa makampuni ya nje yaje yafanye kazi yetu ya kufikiri.

Yaani waziri hapo alipo technically ameoutsource majukumu yake at the expense ya kodi zetu jambo ambalo halina tija.

Kama kashindwa kazi kwani ni lazima awe Waziri wa Nishati??

Rais is ateue mtu mwingine ambaye anaweza fanya kazi bila kutegemea washauri kwa mabilioni ya pesa??

Huyu makamba anatugharimu na ubrazameni wake.

Rais tuondolee huyu mtu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…