Waziri wa Nishati Mh Makamba amevunja kitengo cha habari na mawasiliano Tanesco akikituhumu kimeshindwa kulisemea shirika na kulitetea shirika kwenye nyakati ambazo kitengo na watu wake kimetakiwa kufanya hivyo!
Ikumbukwe kitengo cha habari na mawasiliano kinaongozwa na mwana dada Badra Masoud kwa misingi hiyo amekali kuti kavu ...
Maswali ya kujiuliza...
Ni kweli kitengo hichi ndicho tatizo kwenye shirika?
Ni kweli wameshindwa kuitetea tanesco?
View attachment 2095460
Kwanza ni kweli Kitengo cha Habari hakifanyi kazi ipasavyo.
Na naona Waziri Januari Makamba amevunja ahadi yake ya kutoingilia Utendaji wa Tanesco siku aliyomtambulisha Mkurugenzi Mkuu mpya.
Katika hili, nafurahi kwamba Mhe. Makamba ameona mwanga kuwa Serikali Kuu lazima iishikie kiboko Tanesco, maana Umeme ndiyo Injini ya Maendeleo na Ustaarabu wa Nchi.
Lakini ukitafakari, jinsi umeme unavyokatika ovyo ovyo, sehemu kadhaa katika Mji mmoja, au Mkoa mmoja, au Wilaya moja, sijui hicho Kitengo kitafanyaje kazi kukidhi mahitaji?
Unakuta sehemu ya Mji wa Morogoro haina umeme, sehemu nyingine upo.
Kijiji fulani hakina umeme, kingine upo!
Utoaji taarifa kutoka Dar es Salaam utakuwa mtihani mgumu.
Kwa hali ilivyo, Tanesco wanatakiwa kuwa na Namba za Simu zinazojulikana na kutangazwa muda wote ili kutoa taarifa za Umeme kukatika au Nguzo kuanguka au Waya kukatika na majibu yapatikane. Ikibidi Tanesco iweke utaratibu wa Namba kama za Jeshi la Zimamoto, yaani 'toll free number' maana tatizo ni kubwa kupita kiasi.
Ningetamani hizo Bilioni 70 zilizolipwa Kampuni ya India kwa ajili ya maboresho zisaidie pia katika hili la kuimarisha Miundombinu ya Tehama ya Kitengo cha Habari.