Waziri Makamba: Bwawa la Mwalimu Nyerere sasa kazi ni usiku na mchana

Waziri Makamba: Bwawa la Mwalimu Nyerere sasa kazi ni usiku na mchana

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
unnamed (4).jpg

Waziri wa Nishati, January Makamba ametembelea mradi wa Bwawa la kufua Umeme la Mwalimu Nyerere Agosti 08 2022 ili kukagua na kuangalia hatua mbalimbali zilizofikiwa na mradi huo.

"kwa sasa tumefika asilimia 67, Katika Miaka Miwili na nusu ya Mwanzo (Kuanzia Disemba 2018 - June 2021) tulifikia asilimia 37. Leo tuko asilimia 67 ni kasi kubwa katika kipindi hiki kifupi, Sasa hivi hapa kazi inafanyika saa 24 hakuna mapumziko kwa hiyo kasi imeongezeka" Makamba"

Katika kipindi hiki cha serikali awamu ya sita, tumeshuhudia kasi zaidi katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati. Na hili limekuwa ni kielelezo cha mhe rais Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha miradi yote mikubwa ya kimkakati inakamilika kwa uharaka.

Hakika Mama anaupiga Mwingi Sana.
 
Honourable Makamba blind your ears to noise makers chanting slogans of hate against you.

Theiy are spreading lies that you are incompetent. This is unscrupulous lie. They know your strength and are unspeakably afraid of your charisma and mental ability.

For this reason, they are cheating the innermost parts of their hearts by spreading smear campaign over you (Makamba).

Go on and carry on! You are the next president.
 
Hana credibility ya kuwa JMT AT TOP OFFICE
 
Je hakidhi vigezo? Mtanzania yeyote mwenye akili timamu anaweza kugombania nafasi ya Uraisi wa Jamhuri ya Muungano.

Acheni majungu dhidi ya Makamba jr.
Haenei
 
Hivi kwani sometimes ni lazima mtu au wanasiasa awe rais??
 
Je hakidhi vigezo? Mtanzania yeyote mwenye akili timamu anaweza kugombania nafasi ya Uraisi wa Jamhuri ya Muungano.

Acheni majungu dhidi ya Makamba jr.
Akituambia crane la tani 26 liko wapi, pengine mashaka niliyonayo juu ya utimamu wake wa akili yanaweza yakaniondoka
 
Akituambia crane la tani 26 liko wapi, pengine mashaka niliyonayo juu ya utimamu wake wa akili yanaweza yakaniondoka
Kuna Video ya ufafanuzi kuhusu Crane hilo lakini kama walivyo wanasiasa wengi walioko CCM porojo ni nyingi.
 
Tuombe Mungu Bwawa hili liishe labda umeme utashuka bei.
 
Back
Top Bottom