Memento
JF-Expert Member
- Jun 13, 2021
- 4,423
- 9,986
Waziri Makamba umeonyesha kiwango kidogo cha ukomavu, kwa kusema wabunge wanakubana kwa sababu ya uwaziri wako.
Hii ni kauli inayopaswa kutolewa na mtu ambae sio msomi, hakuna wabunge wenye shida na uwaziri wako bali wanachofanya ni wajibu wao kwa maana wanawakilisha wananchi.
Wabunge wanarudi majimboni wanaulizwa kuhusu umeme kwa kuwa unaathiri shughuli zao, wao ndio wanakuja bungeni kueleza kero hiyo. Wewe hutaki uulizwe.
Pia waziri unapaswa kufahamu sio wewe tu ambae unabanwa kwenye utendaji hasa Jambo fulani likienda vibaya. Ni mawaziri wote hubanwa hivyo, waziri wa afya amekuwa akibanwa kuhusu vituo vya afya.
Waziri wa maji juma aweso amekuwa akibanwa sana bungeni kuhusu upatikanaji wa maji, waziri wa ujenzi amekua akibanwa kuhusu ubovu wa miundombinu Ila wote hao hawakuwahi kusema tatizo ni uwaziri wao.
Majibu yako mh.makamba ni ya kushangaza, sasa unasema waya kwenye substation ya ubungo zipo uchi hivyo upepo ukipuliza tu umeme unakatika.
Kwa majibu ya namna hiyo unategemea watu wataacha kukuuliza maswali?
Kamati ya nishati ya bunge ni haki yao kuhoji na wamesema hakuna sababu za msingi za umeme kukatwa.
Makamba maswali ya kuhusu wizara ya nishati unataka aulizwe nani? Mbona mawaziri wengine wanaulizwa maswali kuhusu wizara zao na wanajibu bila shida, kwa nini wewe uone unaonewa wivu? Hutaki watu/wabunge waulize kuhusu wizara ya nishati?
Wajibu maswali yao kiuweledi na sio kusingizia uwaziri wako.
Hii ni kauli inayopaswa kutolewa na mtu ambae sio msomi, hakuna wabunge wenye shida na uwaziri wako bali wanachofanya ni wajibu wao kwa maana wanawakilisha wananchi.
Wabunge wanarudi majimboni wanaulizwa kuhusu umeme kwa kuwa unaathiri shughuli zao, wao ndio wanakuja bungeni kueleza kero hiyo. Wewe hutaki uulizwe.
Pia waziri unapaswa kufahamu sio wewe tu ambae unabanwa kwenye utendaji hasa Jambo fulani likienda vibaya. Ni mawaziri wote hubanwa hivyo, waziri wa afya amekuwa akibanwa kuhusu vituo vya afya.
Waziri wa maji juma aweso amekuwa akibanwa sana bungeni kuhusu upatikanaji wa maji, waziri wa ujenzi amekua akibanwa kuhusu ubovu wa miundombinu Ila wote hao hawakuwahi kusema tatizo ni uwaziri wao.
Majibu yako mh.makamba ni ya kushangaza, sasa unasema waya kwenye substation ya ubungo zipo uchi hivyo upepo ukipuliza tu umeme unakatika.
Kwa majibu ya namna hiyo unategemea watu wataacha kukuuliza maswali?
Kamati ya nishati ya bunge ni haki yao kuhoji na wamesema hakuna sababu za msingi za umeme kukatwa.
Makamba maswali ya kuhusu wizara ya nishati unataka aulizwe nani? Mbona mawaziri wengine wanaulizwa maswali kuhusu wizara zao na wanajibu bila shida, kwa nini wewe uone unaonewa wivu? Hutaki watu/wabunge waulize kuhusu wizara ya nishati?
Wajibu maswali yao kiuweledi na sio kusingizia uwaziri wako.