Waziri Masauni ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi

Waziri Masauni ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamadi Masauni, ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi na zenye mrengo wa kutaka kuligawa taifa, ambapo amesema serikali haitavumilia vitendo hivyo.
View attachment 2682444

..Wazanzibari kama Othman Masoud, Juma Duni, Ismail Jussa,.wakiukosoa muungano hatusikii wakitishiwa na Bwana Masauni.

..Watanganyika wakikosoa muungano ndipo Bwana Masauni anajitokeza kuelekeza vyombo vya dola dhidi yao.
Haswaa ! Kila siku Othman Masoud (OMO), Juma Duni Haji, Ismaili Jussa wapo majukwaani wakihoji, kejeli na kutukana Muungano. Wamefikia mahali hawana hata heshima wakiita Tanganyika mkoloni mweusi.
Jussa majuzi kasema tugawane mbao, OMO akitoa tuhuma za uongo na Duni akitaka muungano uvunjwe

Hatukumsikia Waziri Masauni akikemea au kudai kuna tishio la usalama au kugawa Taifa kwasababu tu Wazanzibar wana haki ya kuzungumzia Muungano kadri wanavyotaka. Wazanzibar wana haki ya kudai uwepo wa KERO na zikatatuliwa tena wakiwa wenyewe. Sasa imefikia mahali wanadai hawalipi Umeme na wanakubaliwa tu kwasababu ni Wazanzibar

Akizungumza Mtanganyika tunamsikia Masauni na kauli za kutisha.
Waziri Masauni nenda kawaambie Wazanzibar hayo maneno kwanza.
 
Haswaa ! Kila siku Othman Masoud (OMO), Juma Duni Haji, Ismaili Jussa wapo majukwaani wakihoji, kejeli na kutukana Muungano. Wamefikia mahali hawana hata heshima wakiita Tanganyika mkoloni mweusi.
Jussa majuzi kasema tugawane mbao, OMO akitoa tuhuma za uongo na Duni akitaka muungano uvunjwe

Hatukumsikia Waziri Masauni akikemea au kudai kuna tishio la usalama au kugawa Taifa kwasababu tu Wazanzibar wana haki ya kuzungumzia Muungano kadri wanavyotaka. Wazanzibar wana haki ya kudai uwepo wa KERO na zikatatuliwa tena wakiwa wenyewe. Sasa imefikia mahali wanadai hawalipi Umeme na wanakubaliwa tu kwasababu ni Wazanzibar

Akizungumza Mtanganyika tunamsikia Masauni na kauli za kutisha.
Waziri Masauni nenda kawaambie akina Wazanzibar hayo maneno kwanza.
Alikuwa anasubiri kidogo mambo hayo yazidi kidogo hasa kutoka bara ili mizani ipimike.Wao kwa wao wanaogopana.Anajua akiwatishia "wasukuma"/wabara kwamba atawapeleka korokoroni/polisi wataogopa.
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamadi Masauni, ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi na zenye mrengo wa kutaka kuligawa taifa, ambapo amesema serikali haitavumilia vitendo hivyo.
View attachment 2682444
Ni Masauni yupi Kwanza? Si huyu aliyedanganya Bunge la bajeti kwamba Polisi wamepewa hela ya mafunzo huko wakiteseka mikoani Kwa kujilipia Kila kitu?
 
..Wazanzibari kama Othman Masoud, Juma Duni, Ismail Jussa,.wakiukosoa muungano hatusikii wakitishiwa na Bwana Masauni.

..Watanganyika wakikosoa muungano ndipo Bwana Masauni anajitokeza kuelekeza vyombo vya dola dhidi yao.
Ccm wa wamefanya jinai mtanganyika kukosoa muungano ,ila kwa wazanzibar wanaita kelo za muungano
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamadi Masauni, ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi na zenye mrengo wa kutaka kuligawa taifa, ambapo amesema serikali haitavumilia vitendo hivyo.
View attachment 2682444
Moto hauzimwi kwa moto.

Serikali iandae mjadala wa kitaifa, wa wataalamu nguri na wazoefu wa masuala ya bandari na sheria za uwekezaji kujadili IGA (mkataba wa uwekezaji bandarini) ili kuondoa sintofahamu zilizojitokeza, badala ya vitisho.
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamadi Masauni, ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi na zenye mrengo wa kutaka kuligawa taifa, ambapo amesema serikali haitavumilia vitendo hivyo.
View attachment 2682444
Uamuzi mzuri sana, kwani baadhi ya watu wamezidi hadi comments zao zinatia kichefuchefu. Washughulikiwe.
 
Hawa wazanzibari wasijaribu kutugeuza watanganyika kama watumwa wao, tunazitaka bandari zetu mlizowapa wajomba zenu milele, acheni ujinga.
 
Wazanzibar warudi kwao watuachie tanganyika yetu wakome kutufokeafokea
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamadi Masauni, ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi na zenye mrengo wa kutaka kuligawa taifa, ambapo amesema serikali haitavumilia vitendo hivyo.
View attachment 2682444
Huyu waziri mbona underground sana...anyway DJ tuletee DP World vijana tupate kazi.
 
Kiongozi ataenionya kwa sasa nimsikilize ni yule ambae kazaliwa Tanganyika tu.
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamadi Masauni, ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi na zenye mrengo wa kutaka kuligawa taifa, ambapo amesema serikali haitavumilia vitendo hivyo.
View attachment 2682444
Masauni ni Mtanganyika au mtu wa nchi nyingine!.
 
Back
Top Bottom