Waziri Mkenda hawa walimu walikosea nini hadi wapewe hii adhabu ya kuporwa madawati ya kukalia?

Waziri Mkenda hawa walimu walikosea nini hadi wapewe hii adhabu ya kuporwa madawati ya kukalia?

Hii hali ndio inafanya watu wachukie kazi ya ualimu na wengine waione ni kazi ya utumwa na inayo dharauliwa kabisa!

Hivi inakuwaje Mwalimu anaporwa kiti au dawati la kukali kisha anakwenda kupewa mwanafunzi?

Haki za walimu ziko wapi kwanini mnawadhalilisha na kutweza utu wao namna hii?

Kwanini hiyo Kamati na watendaji walishindwa kutafita meza au madawati halafu walimu wana adhibiwa kwa kukosa pa kukaa?

Hivi hawa walimu ilikuwa jukumu lao kutafuta madawati? Kwanini hawa walimu wasichukie hii kazi? Wamekosa nini hadi wapewe hii adhamu?

View attachment 2882400
Kama waliweza kumnunulia fomu ya uchaguzi mama inakuwaje washindwe kujinunulia viti vyao, usiwatetee hao, pia wapigwe marufuku kukalia vitabu kwani kutabu hakisomwi kwa makalio kinasomwa kwa macho.
 
Hivi kwanini hawa madiwani sijui watendaji wanapenda sana kuwaoshea walimu? Wamewafanya kama vile ndo wanyonge wao yaani
Mbona huwa hawajaribu kwenda kwenye kada zingine kuleta utemi wao? Huu udhalilishaji wanaofanyiwa walimu inatakiwa utaratibu uangaliwe upya maana wamekua na maboss wengi sana kuliko watetezi kiasi kwamba wanafanywa kama watu wasio na maana yoyote
 
Hii hali ndio inafanya watu wachukie kazi ya ualimu na wengine waione ni kazi ya utumwa na inayo dharauliwa kabisa!

Hivi inakuwaje Mwalimu anaporwa kiti au dawati la kukali kisha anakwenda kupewa mwanafunzi?

Haki za walimu ziko wapi kwanini mnawadhalilisha na kutweza utu wao namna hii?

Kwanini hiyo Kamati na watendaji walishindwa kutafita meza au madawati halafu walimu wana adhibiwa kwa kukosa pa kukaa?

Hivi hawa walimu ilikuwa jukumu lao kutafuta madawati? Kwanini hawa walimu wasichukie hii kazi? Wamekosa nini hadi wapewe hii adhamu?

View attachment 2882400
Hivi kumbe mtendaji wa Mtaa ni Boss wa Mwalimu, yaani kweli unamaliza ujana wako kusomea BAed kuja kuendeshwa na takataka za certificate zinazosubiri rushwa na hela za wauza viwanja ili ziishi.... ningemchapa kofi huyo mtendaji na kazi yake naacha apo
 
Habari ya upande mmoja hii itawachanganya sana katika kutoa maoni!

Mleta mada hajaeleza nini kilisababisha kunyang'anywa viti na meza walizokuwa wakitumia na wakaridhika.

Waweza kuta walikula hela ya kununulia samani za shule na hapo wamewajibishwa.

Kusikiliza maneno ya upande mmoja huleta taharuki sana.

Niliwahi shuhudia ofisini mtu mzima akilambwa mboko za nguvu na akanyanyuka hapo na kushukuru huku akisema "ahsante mkuu"!

Ilikuwa hivi: kazini kwetu kosa la "utoro" linachukuliwa kwa uzito mkubwa sana.

Utoro wa siku3 usijulikane ulipo, adhabu ya chini ni kunyang'anywa cheo na adhabu ya juu ni kifungo ama kufukuzwa kazi kwa aibu.

Jamaa alihuni kazi zaidi ya miezi6 asijulikane alipo, yalipomshinda maisha alikokwenda, akaamua kurudi ili liwalo na liwe.

Alivorejea, akakutana na kiongozi mbabe.

Katika kuhojiwa akawa anakiri na kuomba msamaha.

Huyo kiongozi akasema hapana, jambo kubwa kama hilo haliwezi likaisha kwa "samahani", akampatia option achague, amshitaki ili akumbane na lango la jela au amrarue mboko, tena zile hamsa ishirini ili wayamalize😀😀!

Jamaa akachagua mboko ili yaishe.

Lambwa mboko sana humo ofisini jamaa kugaragara vibaya na hadi chozi la mtu mzima juu, yakaisha kwa njia hiyo.

Sasa kama mtu siku hiyo alichungulia dirishani na kuangalia huo udhalilishaji bila kusikiliza maelezo ya pande zote, lazima angelimtetea huyo mtoro, wakati huo kumbe mboko hizo zilikuwa ni za ridhaa ili kulinda utu na heshima ya mpigwaji.

Sasa na hao walimu usikute picha imechukuliwa wakati wa muwambo, wakisubiri mishahara itoke ili kwenda kununua madawati yaliyostahili kununuliwa zamani, wao wakazilamba fedha hizo.

Haiwezekani mwalimu akakalishwa chini mavumbini bila sababu na akaridhika, wakati jukumu la kununua samani za shule na vitendea kazi si la walimu ni jukumu la ofisi.
Aliona kuliko apoteze kazi bora achezee bakora kwa hiyari akirudi nyumbani akakandwe michirizi ya bakora za mapaja na mke wake

Sasa siku zote hizo kawa mtoro karudi kasamehewa kirahisi hivyo inamaana taarifa za utoro zilikua hazitolewi kwenye mamlaka za juu?
 
Waweza kuta walikula hela ya kununulia samani za shule na hapo wamewajibishwa.

Mwalimu huyo wa kawaida ndo amepewa hela? Kwa lipi labda! Kua basi
Hiyo ni dhana tu. Lazima ipo sababu "ya maana" iliyowapelekea 'kuishi mavumbini' na wakaridhia.

Nilitangulia kusema, habari inayotolewa kwa upande mmoja hufikirisha na kupelekea kutoa maoni yasiyo sahihi sana.

Ujue nini, hapa kila mmoja anaunga unga dot ili kutafuta sababu iliyopelekea kutokea jambo hilo, maana mleta mada katuacha kwenye ombwe.
 
Hiyo ni dhana tu. Lazima ipo sababu "ya maana" iliyowapelekea 'kuishi mavumbini' na wakaridhia.

Nilitangulia kusema, habari inayotolewa kwa upande mmoja hufikirisha na kupelekea kutoa maoni yasiyo sahihi sana.

Ujue nini, hapa kila mmoja anaunga unga dot ili kutafuta sababu iliyopelekea kutokea jambo hilo, maana mleta mada katuacha kwenye ombwe.
Leak , njoo na taarifa kamili.

Mkuu, GGM imejitahidi kusaidia kila kona, kweli hata wangewaomba wangewanyima! Wazazi,walikataa! Walimu wakuu na kamati walizifanyia mambo yao.
 
Aliona kuliko apoteze kazi bora achezee bakora kwa hiyari akirudi nyumbani akakandwe michirizi ya bakora za mapaja na mke wake

Sasa siku zote hizo kawa mtoro karudi kasamehewa kirahisi hivyo inamaana taarifa za utoro zilikua hazitolewi kwenye mamlaka za juu?
Hiyo ndiyo sababu iliyofanya huyo kiongozi amalizie hasira zake kupiga.

Kiukweli nilivokuja kufuatilia mambo kwisha kishikaji namna hiyo, nilikuja kugundua kumbe ofisi walizembea kutuma ripoti yake ya utoro ngazi za juu kwa wakati ndiyo maana wakaamua 'kila mtu apate'
 
Hivi kumbe mtendaji wa Mtaa ni Boss wa Mwalimu, yaani kweli unamaliza ujana wako kusomea BAed kuja kuendeshwa na takataka za certificate zinazosubiri rushwa na hela za wauza viwanja ili ziishi.... ningemchapa kofi huyo mtendaji na kazi yake naacha apo
Hasa wanawaonea primary wenye certificate, sekondari hawaendagi kufanya ujinga wao....
Na huku primary ukiwa na bachelor wanakuchukia kuanzia walimu wenzio hadi halmashauri.....wanapendaga mizezeta ya kutafutia kiki
 
Hasa wanawaonea primary wenye certificate, sekondari hawaendagi kufanya ujinga wao....
Na huku primary ukiwa na bachelor wanakuchukia kuanzia walimu wenzio hadi halmashauri.....wanapendaga mizezeta ya kutafutia kiki
Wana wanyanyasa wote tuu matukio ni menginwalimu hawana pakusema na haluna wa kuwatetea
 
Back
Top Bottom