Waziri Mkenda, kiokoe Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kwa kusimamia kauli yako

Waziri Mkenda, kiokoe Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kwa kusimamia kauli yako

Nakuandikia Waziri wangu wa Elimu, Prof. Adolf Mkenda,

Mnamo mwezi Disemba, 2022 wewe Mhe Waziri ulitoa kauli: Waziri Mkenda: Ajira ya Chuo Kikuu isiwe kuangalia GPA pekee lazima wapimwe, wafanye na usaili.

Mimi ni mstaafu chamani na Serikalini. Pamoja na kwamba nami pia nimehitimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa shahada zangu mbili za sheria, watoto wangu wawili nao wamehitimu Chuoni humo: mmoja amehitimu sheria kama mimi na mmoja amehitimu uchumi. Wa mwisho wangu naye amejiunga pale kwa shahada ya masuala ya biashara.

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni chuo kikuu kikongwe na bora kuliko vingine kwa Tanzania na kwingineko. Kinastahili heshima kubwa na tunakipenda. Lakini, kwasasa kinaelekea kukwama. Kinaelekea kubaya. Kinaongeza programu mbalimbali za kimasomo lakini hakiajiri Wahadhiri wa kutosha. Kinapata vibali vya kuajiri lakini hakiajiri.

Sababu kubwa zaidi ya zote ni GPA ya 3.8 au zaidi kwa Shahada ya Kwanza. Kupata au kukosa GPA hiyo katika Shahada ya Kwanza humtoa au humwingiza mhusika kwenye kuweza kupata ajira ya Uhadhiri. Hata watanzania na wasio watanzania wenye Shahada za Umahiri na Uzamivu lakini wasio na 3.8 Shahada ya Kwanza hawaajiriki.

Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) ilishatoa Muongozo juu ya sifa za Wahadhiri Vyuo Vikuu. Sifa inayoainishwa kwenye Muongozo wa TCU ni GPA ya kuanzia 3.5 kwa Shahada ya Awali/Kwanza. UDSM imekuwa ikiiacha mbali sifa hii kutoka TCU na kutaka 3.8 na zaidi. Zote, lakini, ni GPA za Daraja la Pili la Juu (Second Upper Division).

Kung'ang'ania 3.8 sasa kunaipa tabu UDSM. Inakosa Wahadhiri. Inaathirika kitaaluma kwakuwa Wahadhiri wachache waliopo wanaelemewa na majukumu mengi na makubwa na hivyo huduma za kitaaluma zinayumba. UDSM inashindwa kupata Wahadhiri kwa kwakuwa tu waombaji 'walitenda dhambi' ya kukosa 3.8 kwenye Shahada zao za awali.

Ifike wakati 3.8 isiwe kikwazo cha kuajiri na kusongesha mbele gurudumu la kitaaluma. UDSM ishauriwe na kuelekezwa kufuata Muongozo wa TCU huku ikichuja waombaji wake kwa umahiri wao katika kufundisha au kwenye usaili wa namna nyingine. Nayaongea haya kwakuwa kwasasa UDSM inakosa waombaji na matangazo ya ajira yanarudiwa: University of Dar es Salaam-. UDSM isaidiwe!

GPA kubwa si kigezo pekee cha uelewa na uwezo wa Mhadhiri kufundisha!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
GPA ya 3.8 haijawahi kuwa tatizo UDSM. Nimesoma pale.
 
Uko sahihi.Zamani wakati ajira hazikuwa za kupiga ramli ilikuwa wanapomaliza wale wanaohitajika kubaki kama tutorial assistant waliajiriwa.Shahada ya pili waliipata wakiwa kazini.Sasa hivi ni ngumu kuwapata kwa kuwa wahitimu wenye sifa hizo wanakuwa wamemezwa na soko huria.
Sahihi mkuu, Watu wanaangalia maslahi tu. Kama hilo ombwe limeshaonekana ni vizuri kuboresha maslahi yao ili kuwavutia wengi
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Acha hizo aisee, kama watoto wako walishindwa kupata GPA ya 3.8 basi kazi ya uhadhiri UDSM sio kwa ajili yao.

Tumeharibu sana shule za msingi na sekondari kwa kuleta siasa za ajabu ajabu, tuesiendelee mpaka kwenye chuo bora cha taifa.

BTW, GPA sio kigezo pekee, ndio maana kuna usaili. Kwenye usaili mwenye GPA ya 4.0 anaweza kumshinda mwenye 4.4.
Wakati utawaacha sana vyuo vikuu na GPA zao kubwa. Sisi wengine tuna hizo GPA kubwa lakini lazima ukweli usemwe. Wanaachwa na wakati. Kufundisha vyuo vikuu is no longer an attractive employment. Sekta zingine zimekuja juu. Zina maslahi mazuri zaidi na hazihitaji GPA kubwa zaidi. Halafu ni rahisi kufanya na hazina mzigo mkubwa kama kufundisha vyuo vikuu.
Reforms zinahitajika.
 
Wenye GPA ya 3.8 wapo wengi sana tena sana ulizia competition ya waliooata hiyo GPA sema cha muhimu waongeze maslahi haiwezekani mwenye 3.8 alipwe take home chini ya milioni mbili na ukasema utapata watu
 
Mzee sasa hivi kila chuo kinaajili wahadhiri wenye GPA 3.8 undergraduate hakuna njia ya mkato utaratibu ni huo.Hao wa 3.5 wakafundishe vyuo vya Kati huko tengeru,hombolo,Utumishi na vingine vinavyofanana na hivyo.ACHA LAWAMA
 
Nadhani vyuo vilivyo chini ya TCU ndio degree ya kwanza angalau uwe na 3.8 GPA; na vile ambavyo viko chini ya NACTE (NACTVET) ndio wanaanzia GPA ya 3.5.

Kuilinda elimu ya chuo kikuu, lazima sifa moja wapo iwe ni GPA kubwa; kama mtagongana na nafasi ni chache, ndio wataangalia hayo mambo mengine.

Kufundisha chuo kikuu kuna faida nyingi, kama ni mpambanaji utaweza kufikia ata u-profesa kwa gharama za chuo; sasa kwa nini upate hizo faida wakati GPA ilikuwa ya kawaida?
Kama unataka vitu vizuri, pambana uwe na GPA kubwa.​
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Acha hizo aisee, kama watoto wako walishindwa kupata GPA ya 3.8 basi kazi ya uhadhiri UDSM sio kwa ajili yao.

Tumeharibu sana shule za msingi na sekondari kwa kuleta siasa za ajabu ajabu, tuesiendelee mpaka kwenye chuo bora cha taifa.

BTW, GPA sio kigezo pekee, ndio maana kuna usaili. Kwenye usaili mwenye GPA ya 4.0 anaweza kumshinda mwenye 4.4.

Kama unakubali GPA sio kigezo huku ukibeza kwenye ubeti wa kwanza nashindwa kukuelewa.

Shida ni kukwepa gharama za usaili katika kutafuta watu bora.
Wangeweza kuweka dirisha wazi kisha waanzishe mchakato wa kutafuta watu wenye uwezo.

Hii itasaidia kupata watu wenye uweza wa kutoa nondo na kuwaelekeza wanafunzi. Mbona huko shule za msingi na sekondari tumefundishwa na walimu walionekana kama wamefeli lkn bado wametengeneza watu wa maana.

Mie naamini wakubali gharama, waandae taratibu za usaili, iwe wa darasani na mahojiano watajuta kuwa hizi GPA zao sio vigezo tu.

Kuna watu wanauelewa mpana wa mambo na kujua kuyawasilisha.
GPA hoyeee…. Aione Kabudi.
 
Ni kweli Mkuu, tusije kuzalisha Vilaza kwa kuendekeza Siasa kwenye Taaluma.

Standard lazima ifuatwe, kama mtoto ana wiwa kuwa Mkufunzi wa Chuo kikuu ni lazima asome kwa bidii na kufauru

Sahihi kabisa mkuu, ni lazima asome kwa bidii na kufaulu.

Lakini ni lazima tuwapime uelewa wao kwa mapana zaidi kuliko kuzingatia marks tu za darasani.

Walau amefaulu tu, apewe nafasi katika usaili, tuna mifano mingi jamaa wanaelewa mambo nakujua kuywasilisha vizuri. Njoo kwenye GPA sasa, mliokuwa mnalishwa nondo mnapunga upepo [emoji28]. Nipe darasa sasa uone, naaona kila mtu anaweza tu.

Hizi GPA ndo zinawafanya hawa jamaa wanakula bata tu akija class anapiga blah blah imeisha hiyo, kazi kwenu mkasomeshane wenyewe.
 
Wenye GPA ya 3.8 wapo wengi sana tena sana ulizia competition ya waliooata hiyo GPA sema cha muhimu waongeze maslahi haiwezekani mwenye 3.8 alipwe take home chini ya milioni mbili na ukasema utapata watu

Mkuu hizi GPA nyingi za vyuo gani? Unadhani pia zinauwezo kudeliver mavitu.
Kuna vyuo huko GPA zinagawiwa tu, je uwezo upo wa kuitetea hiyo GPA yako kabla ya kudai maslahi makubwa?
 
Hizi GPA ndo zinawafanya hawa jamaa wanakula bata tu akija class anapiga blah blah imeisha hiyo, kazi kwenu mkasomeshane wenyewe.
Nimekumbuka mbali sana kwa hii kauli 😆🙌

Me nadhani kufundisha ni kipaji

Kuna Profesa mmoja alikuwa anatufundisha Structural Analysis I, kitu hakiendi wala nini.

Tukaja kufundishwa Structure analysis II na Eng. Mmoja yeye alikuwa ana Masters tu yaani unaona Jinsi Engineering inavyokuwa rahisi. Jamaa anaeleweka hadi basi.

Unapewa zako hata jengo la ghorofa 30+ unalishusha kama kumsukuma mlevi tu
 
UDSM kukosa wahadhiri hakujasababishwa na wanagunzi kutofika GPA ya 3.8 kama ulivyoelezea hapa.ngoja Leo niwape elimu kidogo kwa nini hali hiyo imetokea.

Adaptation ya sera na matamko ya Serikali,mwanzoni UDSM na vyuo vingi vilikuwa binabakisha wanafunzi waliofauli vizuri kila mwaka-badaye process za ajira zinafanyika wanaajiriwa na kuingizwa katika mfumo rasmi wa ajira wa Serikali.

Badaye Sera hiyo ilibadilika,Vyuo vyote vilitakiwa kupeleka mahitaji yao Serikalini ili watu waajiriwe kwa pamoja,kupitia Secretariat ya ajira-yaani watu wrote wawe na chance ya Ku apply na kushindana katika kupata ajira.

Issue,kubwa ni kuwa ajira za jumuishi zinaangalia mambo mengi na zinachukua muda,hivyo by the time ajira zinatangwaza wale wanafunzi waliokiwa bora wengi wanakuwa tayari wameajiriwa sehemu zingine na wengine unakuta wamisha anza mishe zao.Wachache waliobaki nao unakuta kulingana na muda mrefu wa kuwa nje ya mfumo wa masomo unakuwa wamisha sahau vitu vingi hasa ukizangatia interview zetu kwa kutaguta wakufunzi zipo theoretical zaidi.

Kama tunataka vyuo vyetu viendelee kupata walimu bora,lazima Serikali iendelee na utaratibu ule ule wa mwanzo vyuo viendelee Ku hold best students kila mwaka.
 
Mkuu hizi GPA nyingi za vyuo gani? Unadhani pia zinauwezo kudeliver mavitu.
Kuna vyuo huko GPA zinagawiwa tu, je uwezo upo wa kuitetea hiyo GPA yako kabla ya kudai maslahi makubwa?

Nimesoma UDSM na nakuambia watu wanatusua sana hiyo GPA nakumbuka darasa langu wapo watatu walifikisha hiyo GPA ni Bachelor of science
 
Nishaelewa mzee mwenzangu,wanao hawana hiyo gpa ya 3.8.

Waambie warudie chuo tu wawe na sifa ya kuwa wahadhiri hapo,no short cut.

Udsm isimamiaehapo hap, hatutaki vilaza wafundishe chuo kikuu hiki cha Taifa nambari moja kabisa nchini kwa ubora wake.

Kwa kufanya hivyo kitazidi kushuka hadhi yake.

Wapeleke wanao VETA,huko wanafit bila tabu bloangu
 
Utaratibu wa G..P.A ya 3.8 ni mzuri, mimi nadhani kuondoa watu wanao fluke waanzie kuanzia secondary, yaani mtu asiwe chini ya division two, na hizo G.P.A
 
Back
Top Bottom