Waziri Mkuu aokoa mamilioni, atembea kwa miguu kwenda ofisini

Waziri Mkuu aokoa mamilioni, atembea kwa miguu kwenda ofisini

Umbali wa kutoka Goli moja la mpira wa miguu hadi goli lingine kisha ukarudi hata kama ni kwa gari utatumia mafuta ya Tshs ngapi??

Labda tuanze hesabu zetu kwa style hii. Tufanye makisio/assumptions zile gari za msafara wa Waziri Mkuu zinaenda kilometa 7 kwa lita 1 ya mafuta. Na tufanye labda kila lita 1 inauzwa Tshs 2,000. Kwa hiyo kwa afuta ya Tshs 2,000 ambayo ni lita 1 zitaenda umbali wa kilometa 7.

Sasa basi kilometa 7 hizo ni sawa na mita 7,000. Kwa hiyo mafuta ya Tshs 2,000 ambayo ni lita 1 yanaweza kwenda umbali wa mita 7,000. Ndio kusema kwamba kila Tshs 1 inayotumika kwenye mafuta ina uwezo wa kuifanya gari iende mita (7,000 / 2000) = mita 3.5.

Au pia unaweza kusema kila mita 1 ina uwezo wa kuchukua mafuta ya Tshs 2000/7000 = Tshs 0.28. Yaani gari hizi kila zikisogea umbali wa mita 1 zinakua zimekula mafuta ya Cent 28. Na kama zitasogea umbali wa mita 200 basi zitakula mafuta ya Cent 28 x 200 ambayo ni kiasi cha Tshs 57.

Hizi gari kama ziko 7 basi tufanye zinakula mafuta ya Tshs 57 x 7 = Tshs 400 kwa zote saba kutembea umbali wa mita 200. Na kama zitarudi jioni basi itakua ni ara mbili ambayo inafikia Tshs 800. Labda tuseme na sababu zingine zingine basi zinakula mafuta ya Tshs 1,000 jumla kwa safari ya kwenda kumpeleka PM na kurudi nae jioni kwa siku moja.

Ili Msafara huu uweze kuokoa tuseme kiasi cha Tshs 1illion tu kwa hesabu hizi za Tshs 1,000 kwa siku basi inatakiwa uwe umetembea siku zipatazo (Tshs 1,000,000/ Tshs 1,000 kwa siku) = siku 1,000. Yaani PM akifanya misafara au siku 1,000 inayookoa Tshs 1,000 kwa siku ndio atakua ameokoa kiasi cha Tshs 1,000,000. Sasa hizo "mamilioni" zilizookolewa sijui itakua ni siku ngapi.

Mi naishia hapa, ila hizi hesabu zina assumptions zake mbalimbali, na pengine zinaweza kukuchanganya kama kwako hesabu ni tatizo.
You mean, PM ame save buku tu. Oooh ame save Elfu moja tu!!!!!!
Very interesting...
 
Isichukuliwe kama dhihaka! Isichukuliwe kama maskhara na furahisha genge! Bali ikupe fikra fikirishi ya huko tunakoelekea na dhana nzima ya kubana matumizi.

Akiripoti kutoka Dodoma mwandishi wa kituo cha WAPO RADIO, amesema wananchi wa Dodoma Leo wamesifu kitendo cha Waziri Mkuu cha kutembea kwa miguu UMBALI WA MITA 200 kutoka makazi yake-Ikulu ndogo ya Dodoma hadi ofisini kwake (zingatia mita 200)akiwa na walinzi wachache.

Kitendo hicho kimetajwa kama kitendo cha aina yake chenye UADILIFU kilichookoa MAMILIONI YA PESA ambayo yangetumika kwenye msafara wa magari yasiyopungua sita.
Tuupinge kwa nguvu zote huu upuuzi, mwendo wa mita 200 katika uhalisia wake mtu anaweza kupanda gari na msafara?

Je kama Leo imeonekana ni ajabu ina maana siku zote ndivyo ilivyo?
Je kutembea mita 200 ni kubana matumizi?
Ni habari za namna gani hizi jamii inapewa?
Ina maana Dodoma leo kuanzia asubuhi hakukuwa na habari nyingine zaidi ya hii?

Hii breaking news imeniacha na maswali mengi.
Punguza povu kidogo mkuu.Hizi chuki zisizokua na mantiki zinaleta matatizo ya moyo
Umekasirika majaliwa kutembea kwa miguu?
Umekasirika hakuna kilichookolewa?
Au tu hukuipenda habari kutangazwa
 
Wameokoa mil ngapi kwa huo umbali?..mambo ya kijinga nchi hii yanapewa nafasi sana!!..wao waseme ukweli tu kwamba farasi wamempanda kinyume..hali ni mbaya...
kwa maskini shilingi anayokoa kwenye matumizi kwake haina maana lakini kwa tajiri kila shilingi INA maana sana akiokoa hata shilingi moja hujisikia vizuri.sio ajabu ndio maana kuna maskini wengi wewe ukiwemo sababu hujali thamani hata ya shilingi moja iliyookolewa kwa waziri mkuu kutembea kwa miguu.ulofa wako hauji kukutoka hadi uje ujue thamani ya shilingi hata moja
 
Isichukuliwe kama dhihaka! Isichukuliwe kama maskhara na furahisha genge! Bali ikupe fikra fikirishi ya huko tunakoelekea na dhana nzima ya kubana matumizi.

Akiripoti kutoka Dodoma mwandishi wa kituo cha WAPO RADIO, amesema wananchi wa Dodoma Leo wamesifu kitendo cha Waziri Mkuu cha kutembea kwa miguu UMBALI WA MITA 200 kutoka makazi yake-Ikulu ndogo ya Dodoma hadi ofisini kwake (zingatia mita 200)akiwa na walinzi wachache.

Kitendo hicho kimetajwa kama kitendo cha aina yake chenye UADILIFU kilichookoa MAMILIONI YA PESA ambayo yangetumika kwenye msafara wa magari yasiyopungua sita.
Tuupinge kwa nguvu zote huu upuuzi, mwendo wa mita 200 katika uhalisia wake mtu anaweza kupanda gari na msafara?

Je kama Leo imeonekana ni ajabu ina maana siku zote ndivyo ilivyo?
Je kutembea mita 200 ni kubana matumizi?
Ni habari za namna gani hizi jamii inapewa?
Ina maana Dodoma leo kuanzia asubuhi hakukuwa na habari nyingine zaidi ya hii?

Hii breaking news imeniacha na maswali mengi.
Mwalimu Nyerere alikuwa binadamu huenda wa tofauti sana.Alilima mpaka mashamba akiwa Rais alipokuwa akienda butiama.Leo mtu kutembea umbali wa viwanja viwili vya mpira ni jambo kuu.
 
Punguza povu kidogo mkuu.Hizi chuki zisizokua na mantiki zinaleta matatizo ya moyo
Umekasirika majaliwa kutembea kwa miguu?
Umekasirika hakuna kilichookolewa?
Au tu hukuipenda habari kutangazwa
Nikipunguza povu nguo hazitatakata BTW jaribu kusoma tena kwa makini nilichoandika
 
Huu upuuzi wa kiki za kipuuzi sijui utatufikisha wapi.sasa matumizi yaliyobanwa hapo ni kiasi gani !!??

Pinda alikuwa anatembea kwa miguu mji wote wa mpanda huku akitafuna mahindi ya kuchoma akidhani ndio kitu watanzania wanahitaji kukiona lakini aliishia kupoteza mvuto kwa kuwa watu wanataka maendeleo na si maigizo.period
 
Punguza povu kidogo mkuu.Hizi chuki zisizokua na mantiki zinaleta matatizo ya moyo
Umekasirika majaliwa kutembea kwa miguu?
Umekasirika hakuna kilichookolewa?
Au tu hukuipenda habari kutangazwa
1d1092667e34de2179e72cdcb5b99681.jpg
 
Kuna wakati Mh. Sumaye akiwa Waziri Mkuu pia aliwahi kutembea kutoka hapo Ofisini kwake hadi nyumbani kwake, ni karibu mno...so mi nafikiri ni sahihi kufanya zoezi kunyoosha miguu na labda kijua cha asubuhi kilimvutia, lakini ni uwendawazimu wa kimagufuligufuli na kimakondakonda kusema ameokoa mamilioni ya shilingi!
 
Ameokoa kiasi gani? acha mbwembwe
...Mita 200 "yameokolewa" MAMILIONI...Ni Kiasi GANI "kinapotea" Pale Magari 6, yanapomupeleka JNIA akiwa anaelekea Dodoma, kisha "kukata mbuga" chini kwa chini "kumufwata" huko, "kumuhudumia" na kisha, baada ya kumpeleka tena Uwanjani, "yanachanja" mbuga kurudi Sadalamu....?
 
Isichukuliwe kama dhihaka! Isichukuliwe kama maskhara na furahisha genge! Bali ikupe fikra fikirishi ya huko tunakoelekea na dhana nzima ya kubana matumizi.

Akiripoti kutoka Dodoma mwandishi wa kituo cha WAPO RADIO, amesema wananchi wa Dodoma Leo wamesifu kitendo cha Waziri Mkuu cha kutembea kwa miguu UMBALI WA MITA 200 kutoka makazi yake-Ikulu ndogo ya Dodoma hadi ofisini kwake (zingatia mita 200)akiwa na walinzi wachache.

Kitendo hicho kimetajwa kama kitendo cha aina yake chenye UADILIFU kilichookoa MAMILIONI YA PESA ambayo yangetumika kwenye msafara wa magari yasiyopungua sita.
Tuupinge kwa nguvu zote huu upuuzi, mwendo wa mita 200 katika uhalisia wake mtu anaweza kupanda gari na msafara?

Je kama Leo imeonekana ni ajabu ina maana siku zote ndivyo ilivyo?
Je kutembea mita 200 ni kubana matumizi?
Ni habari za namna gani hizi jamii inapewa?
Ina maana Dodoma leo kuanzia asubuhi hakukuwa na habari nyingine zaidi ya hii?

Hii breaking news imeniacha na maswali mengi.
Sifa za kijinga
 
leo katembea kwa mguu mita 200 kesho inakodishwa ndege kumpeleka dar na baada ya siku mbili inamrudisha dom kweli tunabana matumizi
 
Eti mita 200? Kwa hiyo wao huwa wanatembea mita ngapi kwa siku?sifa za kijinga hizi
 
Mita 200 ni kama uwanja wa mpira mara mbili... [emoji2] [emoji2] [emoji2]
 
Back
Top Bottom