Waziri Mkuu auponda mpango wa kutumia viberenge kupanda Mlima Kilimanjaro

Waziri Mkuu auponda mpango wa kutumia viberenge kupanda Mlima Kilimanjaro

Huduma zote ziwepo hiari ni kuchagua upande lift siku moja na kushuka au utembee wiki kupanda na kushuka.
Cable zitaongeza watalii kuna watu nje na ndani kwa ajili ya Kazi hawana mda na wanatamani kupanda juu. Panapo cable wanapanda jumamosi asubui jioni wanashuka jtatu wanaingia kazini.
 
Hata mimi nimeshindwa kumuelewa, maybe he is misinformed... ona hii cable hapa [emoji116]View attachment 2132980

JK mwenyewe tena akiwa mheshimiwa sana tumepanda nae pale The Great Wall aka ukuta mkuu wa China kwa Cable car aka viberenge pale Uchina. Na wakati ni ka safari ka saa kadhaa tu kutegemea na njia uliyoingilia. Majaliwa anawaza uchumi wa wapagazi aisee
 
Mambo ya kupanda mlima wiki ni ya kizamani. Cable itaongeza watalii wala haiwezi athiri Kazi za upagazi
 
So
JK mwenyewe tena akiwa mheshimiwa sana tumepanda nae pale The Great Wall aka ukuta mkuu wa China kwa Cable car aka viberenge pale Uchina. Na wakati ni ka safari ka saa kadhaa tu kutegemea na njia uliyoingilia. Majaliwa anawaza uchumi wa wapagazi aisee

Mabadiliko hayakwepeki awatosa Kazi za kufanya,ujio wa crane,lift umeua ajira za wabeba zege
 
Hivi anaepelekwa kwa kiberenge hadi kileleni nae anajihesabu kwamba kapanda mlima?
 
PM aelimishwe

Sasa kama na yeye ameshalishwa matango pori na wasaidizi wake, ataelewa kweli?

Binafsi sijaona kabisa logic ya kulazimisha kupanda huo mlima kwa miguu, eti kisa kuna wapagazi sijui watakosa ajira!!! Kwani hao wapagazi hawawezi kufanya kazi nyingine, isipokuwa kubeba tu mizigo ya watalii?

Wangeweka options mbili. Ya kupanda kwa miguu, na hiyo ya kupanda kwa hivyo viberenge vya umeme. Masuala ya kulazimishana kupanda kwa miguu hayakubaliki hata kidogo kwenye dunia hii ya sasa ya sayansi na teknolojia.
 
PM yuko sahihi.
Ingependeza tupate a detailed report ya athari yake - evolution haizuiliki hasa Kwa era hii ya digitali

Watanzania tumekua too emotional sometimes

I am sure pm is right, lakini natamani tupate detailed reports
 
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewataka wadau wanaopendekeza matumizi ya viberenge katika kupanda Mlima Kilimanjaro kutathimini kwa kina mpango huo ambapo ameonyesha kutoridhia mikakati hiyo.

"Nasikia mnataka kuweka kiberenge cha kupanda Mlima Kilimanjaro, mnataka kuua mlima? Mkiweka machuma ya kupanda mlima mtaharibu, nataka mje mseme wapagazi mtawapeleka wapi na hizo ndiyo ajira zao, endeleeni kulijadili hilo mje na sababu zilizo tosha,” amesema Waziri Mkuu.

Ameyasema hayo katika hotuba yake aliyoitoa akiwa Chuo Cha Ushirika Moshi katika kilele cha mbio za Kilimanjaro Marathon mkoani Kilimanjaro, leo Jumapili Februari 27, 2022 alipokuwa mgeni rasmi.
Yan hili jamaa lilitakiwa liondoke na Mwendazake, bado lina akili za kujifukiza hovyo kweli yan
 
Sasa kama na yeye ameshalishwa matango pori na wasaidizi wake, ataelewa kweli?

Binafsi sijaona kabisa logic ya kulazimisha kupanda huo mlima kwa miguu, eti kisa kuna wapagazi sijui watakosa ajira!!! Kwani hao wapagazi hawawezi kufanya kazi nyingine, isipokuwa kubeba tu mizigo ya watalii?

Wangeweka options mbili. Ya kupanda kwa miguu, na hiyo ya kupanda kwa hivyo viberenge vya umeme. Masuala ya kulazimishana kupanda kwa miguu hayakubaliki hata kidogo kwenye dunia hii ya sasa ya sayansi na teknolojia.
Majaliwa na Dr Mpango wana akili za Magufuli za kujifukiza, huyu na akina Kabudi walitakiwa waondoke serikalini siku Magu alipokufa, hovyo kweli aisee
 
Pm yupo sahihi hasa upande wa ajira! Lkn usahihi zaidi ni kupanda mlima mtu mwenyewe huo hasa ndio utalii wenyewe! Sifa ya mlima kilimanjaro sio kwamba ni mrefu kivile! Sifa yake ni stand alone mountain! mita hzo Pekee hapa dunian! Hivyo mtalii anaona fahar kujiandikia historia yake kwa kupanda bila msaada wa mashine!
 
Back
Top Bottom