Waziri Mkuu auponda mpango wa kutumia viberenge kupanda Mlima Kilimanjaro

Waziri Mkuu auponda mpango wa kutumia viberenge kupanda Mlima Kilimanjaro

Wachaga wana mambo ya kizamani sana!
Majaliwa hajui . Inaelekea hana exposure. Watalii wengi bado watalenda kupanda kwa Maui. Kwao suala muhimu ni endurance ikiwamo kufika kileleni. Watu Kama hao hawawezi kupata hitaji lao kwa kuapanda na kiberenge. Mwaka juzi nilikwenda Cape Town na baada ya shuguli zangu niliamua kwenda kwenye Table Mount. Pale kuna option ya kupanda na cable cars na kupanda kwa mguu. Tulipokuwa tunanunua ticket niliona watu wengi wananunua ya kupanda kwa mguu. Mimi nikapanda na cable car. Hivyo PM asiwe na wasiwasi. Soko la wapanda mlima kwa mguu litendelea kuwapo kwa muda mrefu na halitakufa.
 
Serikali hii haiwezi kuendesha hivyo viberenge. Vitakuwa vinakwama kila siku na umeme wa mgao. Waache wawekezaji wafanye hizo kazi.
 
Waziri mkuu nae ni mshamba tuu! Kiberenge kitaongeza idadi ya watalii sana maana hata wale ambao hawana uwezo wa kupanda watapanda!

Sasa kiberenge kitaaribu vipi miti? Hivi waziri mkuu hata anaelewa anacho ongea?
Kwaninj huduma zote zisiwepo na ziwe na gharama tofauti mfano kwa njia ya kiberenge iwe bei juu zaidi ya kupanda kwa kawaida!

Hivi kweli tungegoma kutumia mashine viwandani kisa kuogopa watu watapoteza kazi?
Waziri mkuu hana hoja za msingi maana ni wazi hajui anaongelea kitu gani!

Hivi hivyo viberenge vitaaribu vipi mlima? Ni wazi viberenge vitaongeza idadi ya watalii maana hata wasio na uwezo watapanda!
 
Waziri mkuu toka ile siku akiwa msikitini atuambie JPM ni mzima wa afya na anachapa kazi sijawahi kumuelewaga tena.

Viberenge ni njia mpya ya kuingiza new customers kuna aina ya watalii ambao hawapendi kupanda mlima kwa miguu kama mimi yaani. Hicho kiberenge kitanipa nafasi ya kutalii bila kupoteza muda.

Wm ni sawa anamaanisha kuwa tusitumiane sms kwa sababu itaus barua za posta
 
Hao wapagazi ni kama wapiga debe wa stendi..
Najiuliza hivi hawana shughuli zingine..mpaka wanze kungangania kubeba mizigo?

Kwa akili za waziri mkuu tusitumie machine viwandan kwa sababu zitapunguza ajira?


Na Tesla wakileta truck zao zenye auto pilot zisiruhusiwe kwa sababu zitaua ajira ya madereva wa malori?
 
Kabisaa.
Yani safari ya siku 8 ifanyike kwa 1 hour mlima utachukuliwa poa kama kichuguu tu na hautakua na value tena coz safari ya usd 2500 itafanyika kwa usd 100.
Safari ambayo ingewahusisha wafanyakazi 12 itakua inachukua mfanyakazi 1 tu.
Mnashindwa kuelewa maana pana ya utalii. Kuna adventure tourism - watu wa kupanda kwa siku 8 wataendelea kuwapo na hao wa siku moja watakuwepo...kumbukeni kuna watu wenye matatizo ya afya lakini wanataka kupanda mlima...pia wako watalii wana budget ndogo au kubwa na muda mchache wa safari...hii ni fursa.

Tujiulize mamia ya watu waliokufa na watakaoendelea kufa ktk harakati za kupanda mlima Everest ni kwamba mamlaka hazioni? NO! Watu wanajua ni risk na wangeweza buni njia badala, ILA bado kuna watu wanataka kupanda wenyewe kwa nguvu ya miili yao.

Tuangalie kwanza motivations na interests behind travel to the destination - ni nini motisha na nia ya kupanda mlima? Je, ni kuona tu au ni kushiriki na kushinda changamoto za kupanda mlima.

Tujifunze toka sehemu nyingine wanakotumia viberenge/cables
 
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewataka wadau wanaopendekeza matumizi ya viberenge katika kupanda Mlima Kilimanjaro kutathimini kwa kina mpango huo ambapo ameonyesha kutoridhia mikakati hiyo.

"Nasikia mnataka kuweka kiberenge cha kupanda Mlima Kilimanjaro, mnataka kuua mlima? Mkiweka machuma ya kupanda mlima mtaharibu, nataka mje mseme wapagazi mtawapeleka wapi na hizo ndiyo ajira zao, endeleeni kulijadili hilo mje na sababu zilizo tosha,” amesema Waziri Mkuu.

Ameyasema hayo katika hotuba yake aliyoitoa akiwa Chuo Cha Ushirika Moshi katika kilele cha mbio za Kilimanjaro Marathon mkoani Kilimanjaro, leo Jumapili Februari 27, 2022 alipokuwa mgeni rasmi.
Wanaccm hawaachiani maji ya kunywa mezani - Kikwete
 
Yuko sahihi kwani uharibifu mkubwa sana wa kukata miti utafanyika, ni wazi kutakuwa na barabara mbili ya kupanda na kushuka, pia muda wa watalii kukaa hotelini utakwisha na ajira za wapagazi zitakoma pamoja na wauza kahawa na vitu vya asili watakosa wanunuzi na mwisho watalii wa mazingira watasusa kuja kutokana na uharibifu utakaofanyika.

Kweli uharibifu wa mazingira unaweza kutokea, kama ujenzi wa njia za trolleys utafanyika. Economically, however, upo uwezekano wa negative impact kuwa minimal, kwasababu ya volume ya wapanda mlima kuongezeka. Wale watu ambao, for age or health reasons, sasa hivi hawawezi kuupanda huo mlima, nao watageuka kuwa wateja. Volume ikiongezeka sana, hopefully, wapagazi watakuwa absorbed na ukuaji wa shughuli za kiuchumi utakasababishwa na hilo ongezeko.

All in all, without data-driven analysis, it’s hard to gauge the economic viability of this contemplated move!
 
upo sahihi,lakini simuelewi PM hoja yake ya kwamba machuma yataharibu mlima
Kasema yataua Mlima.....! Hajasema yataharibu Mlima....
Wewe huoni kuna tofauti kati ya kuharibu Mlima na Kuua Mlima...!?
 
kwa ss wapagazi wa marangu mtatuua na njaa jamani,familia zetu na watoto tunategemea mlima nyumba zetu ni za block umnataka turudi zama za ujima tujenge za udongo? istoshe makampuni meng yatakufa,
 
Kitaaluma viberenge haviwezekani kwa mlima Kilimanjaro kwkuwa itakuwa unamtoa mtu kutoka kwenye altitude 1000m usawa wa bahari nakumpeleka mita 5895m kilele cha mlima kwa saa moja bila ku-regulate pressure na kuwapo kwa acclamatization, watu wengi watakufa kwa mshtuko wa moyo!
 
Kweli uharibifu wa mazingira unaweza kutokea, kama ujenzi wa njia za trolleys utafanyika. Economically, however, upo uwezekano wa negative impact kuwa minimal, kwasababu ya volume ya wapanda mlima kuongezeka. Wale watu ambao, for age or health reasons, sasa hivi hawawezi kuupanda huo mlima, nao watageuka kuwa wateja. Volume ikiongezeka sana, hopefully, wapagazi watakuwa absorbed na ukuaji wa shughuli za kiuchumi utakasababishwa na hilo ongezeko.

All in all, without data-driven analysis, it’s hard to gauge the economic viability of this contemplated move!
Unapozungumzia hizo cable ondoa swala la wapagazi, kambi za kulala mlimani na siku za kulala hotelini.
 
PM mbona ameonekana mshamba sana kwa hili...

Au anafikiri ni reli inatandazwa mlimani.?
 
Ziwepo means zote za kufika huko....akigoma tunasubiri atoke tunaluanzisha angesema waje full business plan na projections sighing na references cables zingine duniani .....ile ya table mountain
 
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewataka wadau wanaopendekeza matumizi ya viberenge katika kupanda Mlima Kilimanjaro kutathimini kwa kina mpango huo ambapo ameonyesha kutoridhia mikakati hiyo.

"Nasikia mnataka kuweka kiberenge cha kupanda Mlima Kilimanjaro, mnataka kuua mlima? Mkiweka machuma ya kupanda mlima mtaharibu, nataka mje mseme wapagazi mtawapeleka wapi na hizo ndiyo ajira zao, endeleeni kulijadili hilo mje na sababu zilizo tosha,” amesema Waziri Mkuu.

Ameyasema hayo katika hotuba yake aliyoitoa akiwa Chuo Cha Ushirika Moshi katika kilele cha mbio za Kilimanjaro Marathon mkoani Kilimanjaro, leo Jumapili Februari 27, 2022 alipokuwa mgeni rasmi.

Huyu MP ni empty headed
 
Unapozungumzia hizo cable ondoa swala la wapagazi, kambi za kulala mlimani na siku za kulala hotelini.

Kama nilivyosema, mitigating factor ni increased volume ya wapanda mlima. Wapagazi sio lazima waendelee kuwa wapagazi. Ongezeko la shughuli za kiuchumi linaloweza kuchochewa na increased volume ya wapanda mlima, hopefully, linaweza kuwapa (watu ambao kwa sasa ni wapagazi) fursa mpya za kujipatia riziki zao!
 
Back
Top Bottom