Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anasubiri nini ofisini au Afrika kujiuzulu ni dhambi?

Chikenpox

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2022
Posts
784
Reaction score
1,246
Licha ya madudu yote hayo yaliyooneshwa na CAG lakini bado anakalia ofisi tu? Hebu fikiria Waziri Mkuu wa Iingereza alijiuzulu kwa kosa tu la kucheza mziki kipindi Cha COVID 19 lakini sisi huku Waziri Mkuu ndo kwanza anachekelea. Hivi nchi za kiafrika tunelaaniwa?

Rais hawezi kumwambia Waziri Mkuu eti jiuzulu bali PM mwenyewe ndo nafsi inapaswa imsute. Jana Rais Samia kaongea very logical issues akimlenga pm kwamba hana lolote analojua kama mtendaji Mkuu wa Serikali.
 
Kuna udhaifu kuanzia juu kule, wacheni kuhangaika na PM, ndio maana mafisadi wameanza kuvimba tena sababu wanajua hayupo wa kuwafanya chochote mama yao yuko upande wao, wale kina Silent Ocean ni mfano wao.
 
Kuna udhaifu kuanzia juu kule, wacheni kuhangaika na PM, ndio maana mafisadi wameanza kuvimba tena wanajua hayupo wa kuwafanya chochote mama yao yuko upande wao.
Rais anasimamia viongozi wa chini wafanye kazi. Katiba haimruhusu kukimbizana na wafanyakazi kama.alivyotaka jpm kupindua katiba
 
Ajiudhuru kwanza Kikwete ili Majaliwa afanye kazi. Kuendelea kuwepo kwa kikwete na katibu wake mkuu Nape hakuna litakalofanyika.
Wazri mkuu ndo mtendaji mkuu wa serikali unless atwambie kama kadelegate kwakikwete au hajua anapaswa afanye nini kwa mana kwamba uwziri mkuu ni mzigo kwake
 
Mzee wa kuzindua magereza na mambo ya uwajibikaji wapi na wapi,kitendo cha kuadaa umma tena akiwa katika nyumba ya ibada mpaka sasa hakustahili kuwa katika nafasi hiyo.

"Mwafrika hawezi kujitawala" Botha
 
Point sn ilitakiwa kuanzia PM, Spika/ Waziri husika, KM/CEO wote washitakiwe wameshindwa kazi
 
Umetoa mfano wa PM wa Uingereza. Kwao wao ndiyo Kiongozi wa juu hawana Raisi. Sisi tuna Raisi so kwa mfano wako wewe, ni Raisi ajiuzulu kwa hayo madudu. Kwa nchi kama hii, PM anafata maelekezo toka juu. Hapo utakuwa umemuonea labda useme uongozi wote utoke.

Ila unapita kila comment kukanusha kitu ambacho umekiandika mwenyewe. TZ na nchi karibu zote za kiafrika, zinamtukuza Raisi kama Mfalme ama Malkia. Si sawa yeye ndiyo mtumishi wa wananchi, anatakiwa atumikie wananchi na kama hatoshelezi ni kuachia hayo majukumu kwa anayeweza.
 
TAMISEMI angepewa mtu kama Kalemani pamoja na madhaifu yake lakini ni mfuatiliji mzuri sn
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…