Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatakiwa kuwajibika kwa kudanganya Taifa lililokuwa na taharuki kubwa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatakiwa kuwajibika kwa kudanganya Taifa lililokuwa na taharuki kubwa

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2020
Posts
4,170
Reaction score
6,757
Wanabodi najua kabisa tupo kwenye msiba mkubwa. Msiba ambao umemgusa kila mtu na mpaka sasa kila Mwananchi haamini kilichotokea.

Lakini yapata kama wiki moja iliyopita taifa zima lilikumbwa na taharuki kubwa. Kila raia mwenye mapenzi na mkuu wa nchi yetu alitaka kujua kama anaumwa au haumwi. Wapo waliojitolea kuwa wapiga mbiu. Wao walisema kuwa Rais anaumwa na yupo hoi

Ghafla akaibuka Waziri mkuu akiwa ziarani huko nyanda za juu kusini. Alitoa tamko ambalo sababu yeye ndio msimazi wa shughuli za serikali kila mwananchi alimuamini. Aliwahakikishia watanzania kuwa Rais haumwi na anachapa kazi kama kawaida.

Tamko la Waziri mkuu kuwa Rais alikuwa mzima linakinzana na taarifa tuliyopewa na Makamu wa Rais kuwa tangu tar 6 Macih Rais amekuwa mgonjwa tena aliyekuwa amelazwa.

Je, kwa hali ya kawaida kuna raia ambae bado anaweza kumuamini Waziri Mkuu tena?
 
Mmeanza mapema hivi? But Mungu ataipigania Tanzania.
Mashujaa wote hawawezi kuanguka siku moja
 
Sioni utendaji wake, akiwa kiongozi sikuona chochote cha maana alichofanya na alistahili kutumbuliwa, kama mnampenda kwa sura yake hapo sawa, au akawe PM wako wa twitter.
Jikite kwenye mada
 
Naunga mkono hoja, Mh Kassim Majaliwa kapoteza sifa za kuwa kiongozi - hivyo atolewe kwenye Uwaziri Mkuu. Ni vile ubunge hawezi fukuzwa lakini angekuwa mstaarab na mwajibikaji angejiuzulu Ubunge kisha u PM.

Majiliwa amekufa kisiasa.
Kama watu hawana imani naae tena asisubiri kupigiwa kura ya kutokuwa na imani nae
 
Watawala wanachotakiwa kujifunza ni kutokutoa majibu mepesi kwenye maswali magumu. PM amejishusha sana na tena sana na kukidhalilisha kiti cha uwaziri Mkuu. Tujifunze kusema ukweli ili kuondoa maswali yasiyokuwa na ulazima.

Akina Mwigulu Nchemba, Chalamila na musiba (sijui ni uanaharakati wa aina ipi?) walikuwa wanabwatuka tu bila kufahamu hatima ya ndimi zao. Mmetuumiza sana tena sana kwa kutudanganya kuwa Rais wetu ni mzima wakati anaumwa, mkatunyima nafasi na HAKI ya kumuombea Rais wetu na tumetangaziwa tayari akiwa marehemu.

Muhimu na cha kuzingatia kwa Kaimu Rais ni kutokuruhusu kila mwanaCCM kujinasibisha kuwa yeye ni msemaji wa serikali. Kwa maoni yangu, waliotakiwa kukamatwa wa kwanza ni Mwigulu Nchemba na Albert Chalamila kwa kudhihaki taifa letu. Pili, kaimu Rais hakikisha kuwa nchi inamuenzi Dr. John Magufuli kwa kukamilisha miradi aliyoianzisha. Mungu akusaidie katika kutekeleza majukumu mazito uliyoachiwa kwa ustawi mpana wa nchi yetu.

Pumzika kwa amani daktari John Pombe Joseph Magufuli.
 
Kwenye taarifa ya VP alisema Rais aliruhusiwa kutoka hospital trh 7 na aliendelea na kazi zake kabla ya kuzidiwa tena, Kwa hiyo PM alikuwa correct aliposema kuwa Rais anachapa kazi zake hakudanganya wakuu unless kama tulichopewa kwenye taarifa siyo sahihi lakini kama ndivyo PM alisema kweli
 
Back
Top Bottom