Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 15,819
- 33,255
Kama ulikuwa umekufa tangu mwanzo Mbona mwanzoni hakukuwa na shida na mradi ulikuwa unaenda vizuri?Maskini hujui usemalo. Mwendokasi tangu mwanzo ulikuwa mradi uliokufa kabla ya kuanza kazi hasa ikizingatiwa kuwa akina SImon Kisena waliopoka UDA waliishauua. Magufuli amesaidia hata kufikia hapo ulipo baada ya kuwakamata na kuwasweka ndani akina Kisena. Kama hujui uliza ujuzwe badala ya kuja na mambo ya ajabu ajabu yaliyojaa ujinga na uongo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo amefanya ziara ya kushtukiza kituo cha mwendokasi eneo la gerezani na kukuta mfumo wa kusoma tiketi haufanyi kazi, mtendaji mkuu alisema mfumo haufanyi kazi baada ya kutokea mgogoro kati ya supplier na alieununua. Meneja huyo amesema mfumo mpya unajengwa na waziri mkuu kumuhoji inatumia miaka mingapi kukamilika?
Majaliwa amesema wanaibiwa mapato kwani wao wanatumia mtambo na wengine wanatumia mtambo mwingine na hawana namna ya ku-check.
Pia Meneja amehojiwa tangu aingie amenunua mabasi mangapi baada ya serikali kununua mabasi 140 huku mabasi yanayokadiriwa kuwa barabarani ni wastani wa 100.
Mtoa huduma ya mwendokasi aliagiza mabasi 70 ambayo yamekwama kuingia barabarani kutokana na mgogoro na waziri mkuu akasema anaenda kuyaona. Majaliwa amesema wananchi wanalalamika mabasi hayatoshi akitolea mfano Kimara watu wanaingilia dirishani na kuhoji mapato wanayokusanya wanapeleka wapi kama wanashindwa kununua mabasi.
Pia waziri mkuu amepita karakana ya Jangwani na sasa anaelekea Ubungo kuangalia mabasi yenye mgogoro
Hakuna kukatavtiketi kama daladala, hakuna konda UDART. Mwongo mkubwa.Hujui kuwa wanatumia ticket na zinakatwa?? Hujui mwanzoni kulikuwa na kadi na watu walikuwa wanaswap na mapato yanasoma???
Uko chato au Burundi?
Ila kiongozi huyu kisena ni nani kwakoKwani kwenye korosho walifanikiwa?😂😂😂
Kufukuzwa kazi.Na aliyemuondoa bila kujipanga na hiyo kuleta hasara zaidi sehemu yake ni wapi?
Namsikia Mkurugenzi akisema tuko kwenye mkakati...Mwendokasi una changamoto nyingi sana.Wakazi wa Kimara wanateseka sana
Umejuaje mimi ni maskini? Umejuaje nachukia matajiri? Kusema huu mradi ulikuwa wa kifisadi ndiyo nimechukia matajiri? Nachukia mafisadi siyo matajiri.Ufisadi upi ulikuwepo?? Acheni kuchukia matajiri ndo mana mnakuwa masikini na makapuku milele!
Kuna watu mnaidhalilisha jamii forum kwa kudandia vitu msivyovifahamu au kwa kutumwa kuwasifia watu. Mjitahidi kabla ya kuandika masuala makubwa kama haya ili kuepuka upotoshaji mnatakiwa kufanya utafiti siyo kuandika mkiongozwa na chuki. Zamani niliamini JF ni sehemu ya kuoata habari za kiuchunguzi lakini imegeuka kuwa jukwaa la wambea na wafitishi kwa habari za kutunga kama hizi.Nilikuwa siamini kwamba kwenye kila analogusa Magufuli huwa ana haribu Ila kwenye Mwendokasi ndo sehemu niliyokuja kuamini kwa Mara ya kwanza!
Kwanza inabidi wote tujiulize mwendokasi ilianzia wapi?
Mradi wa mabasi ya mwendokasi ukianzishwa na kuasisiwa na Rais wa Awamu ya nne. Kwa Jinsi mradi ulivyokuwa umeandaliwa ulitakiwa kusimamiwa na kampuni binafsi na tangu mwanzo ulisimamiwa kwenye mfumo huo. Mradi huu ulikuwa chini ya Kampuni na Kisena na wakati unaanza kila kitu kilikuwa kinaendeshwa katika dunia ya kisasa. Ticket zilikatwa kielectronic na watu waliweka hadi kuwa na kadi ya kutumia mwezi mzima.
Alipokuja Magufuli kwanza alianza ku deal na kisena kwa sababu kisena hakuwa kwenye kundi la watu waliomuunga mkono kwenye uchaguzi wa mwaka 2015. Alimtesa kisena kumpa kesi za uhujumu uchumi na mkewe na baadae kumnyang’anya mradi na hatimaye akaondoa utaratibu wote mzuri uliokuwa umewekwa kwa ajiri ya kuendesha mradi.
Matokeo yake akawapa wanajeshi, na hapo ndo Tatizo lilipoanza. Mradi ulianza kuendeshwa kwa tabia za kiswahili na watu wakaanza kukata ticket kama daladala.
Mradi huu hadi kufikia sasa ulitakiwa uwe umeshaanza kujiendesha kwa faida Ila kwa roho mbaya ya magufuli na tabia zake za kuchukia matajiri ndo amefanya mradi ule uwe kituko na usifike popote.
Polee kisena. Buriani Mwendokasi.
Kumuondoa ilikuwa sawa kabisa. Na zaidi alitakiwa kuwa jela. Mradi kufa haihalalishi ufisadi aliofanya usiwe kosa!Sasa mmemuondoa na mradi umewafia. Hiyo ni akili au matope?
Chuki na roho mbaya. Kama hujapata upenyo wa kupiga utafute na sio kua roho mbaya haikusaidii.Kazi kazi.
mapigaji yanataka kurudi.
safi sana waziri mkuu
Wewe unaweza kuwa unaongozwa na ujinga. Unataka ku-suggest kuwa watu hata wakiiba ilimradi wanakwenda kufanya vizuri basi tusiwahesabu kuwa wana makosa? Unatumia nini kufiri wewe? Au wewe ndiye huyu mwizi? Au mke wake?Sasa mmemuondoa na mradi umewafia. Hiyo ni akili au matope?
Tunajua kinachoendelea nyuma ya pazia. Hata hizi kelele na huu ujinga unaondika hapa tunajua sababu yake.Juhudi gani wakati mwendokasi inajifia?? Ushawai kupanda mwendokasi wewe au ndo unaongea tu kutoka chato?
EhehhNyuma ya kisena kuna rizi-1, juhudi kubwa sana zinafanyika kuirudisha miradi ya kifisadi ya Kikwete iliyo chinjiwa baharini na Makufuli, kosa kubwa alilofanya Makufuli ni kutowanyonga haraka haraka Kisena, Rugemalila na Sethi
mbonaa anahangaika na hawa,,maadudu ya CAG wanawacha?Hujui kuwa wanatumia ticket na zinakatwa?? Hujui mwanzoni kulikuwa na kadi na watu walikuwa wanaswap na mapato yanasoma???
Uko chato au Burundi?
Eti anamlaumu jpm,wakati jpm alijaribu kuirudisha mwendokasi kwenye mstariMaskini hujui usemalo. Mwendokasi tangu mwanzo ulikuwa mradi uliokufa kabla ya kuanza kazi hasa ikizingatiwa kuwa akina SImon Kisena waliopoka UDA waliishauua. Magufuli amesaidia hata kufikia hapo ulipo baada ya kuwakamata na kuwasweka ndani akina Kisena. Kama hujui uliza ujuzwe badala ya kuja na mambo ya ajabu ajabu yaliyojaa ujinga na uongo.
Yeah true hasa mchicha tembele na kisanvu muhimu kwa afya...Chuki na roho mbaya. Kama hujapata upenyo wa kupiga utafute na sio kua roho mbaya haikusaidii.
Wenzako wanakula maisha kwa upigaji we endelea kula majani kama mbuzi!
Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
Kaza boot MajaliwaWaziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo amefanya ziara ya kushtukiza kituo cha mwendokasi eneo la gerezani na kukuta mfumo wa kusoma tiketi haufanyi kazi, mtendaji mkuu alisema mfumo haufanyi kazi baada ya kutokea mgogoro kati ya supplier na alieununua. Meneja huyo amesema mfumo mpya unajengwa na waziri mkuu kumuhoji inatumia miaka mingapi kukamilika?
Sijui kama unaelewa.Kazi kazi.
mapigaji yanataka kurudi.
safi sana waziri mkuu