Waziri Mkuu: Mabasi mabovu ya mwendokasi ni bora Serikali iyauze kuliko kuyaacha yakiozea pale yard

Kuna mambo zaidi ya moja. Eitha watumishi wengi wa UDART wana biashara inayo fanana na hiyo au, kuna wizi mkubwa sana hapo Udart ndio maana shirika lina yumba. Au walio kwenye nafasi za utawala hawana uelewa wa hiyo biashara. Huwezi niambia kwa utitiri wa abiria Dar ati kampuni ina fanya hasara.
 
That's Whats'UP
 

kiukweli huu mradi unaendeshwa hovyo sana, japokua kupewa mwekezaji sidhan kama itakua sahihi kwa sababu ya ile exclusivty yake na kutokua na competition
 
Serikali ya CCM kama biashara ya mabasi ya Mwendokasi mmeishindwa hivi biashara ya ndege mtaiweza kweli?
Ww huna adabu kabisa. πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚Mbona huwa unaongea ukweli tu? Hawa jamaa hawapendi ukweli. Mara moja moja uwe unadanganya wasije wakajinyonga wazee wa buku 7. Nice post mkuu. Nimecheka kweli kweli πŸ™πŸ™πŸ™
 
SGR imekufa hata kabla haijaanza.

ATCL ndege zilizopo haziruki huku tunaendelea kununua nyingine, sio moja.

Tatu ndege moja tungenunua mabasi zaidi ya Mia mbili
Ile MV Bagamoyo iliyonunuliwa kwa Bei pouwer iko wapi?
We don't have priorities.
Wanachezea tu mali ya umma. Inaudhi sana😑😑😑
 
Siasa! Siasa! Siasa! Tatizo lilianza pale walipoanza kumpangia mwekezaji nauli za kutoza.

Nauli ilipaswa kuwa 1000 ili mwekezaji apate hela ya kulipa mkopo na kufanya maintenance

Sasa serikali ikakomaa nauli iwe 600 matokeo mradi hauingizi faida ni hasara tupu hta marekebisho hawawezi kufanya.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Nani anunue hio shida? Yani shida yao badala waitatue wao wanataka wamuuzie mwingine? Na biashara ya basi wameshaivuruga sana.
 
hivi mkuu huyu amandla huwa ni nani yako..
 
Bakhresa aliutaka huu mradi wakamtosa
Ila nae anavyotunyoosha kwenye king'amuzi na kwenye usafiri angepata tu namna ya kutunyoosha,kikubwa naonelea watangaze tender na kampuni ambazo ziruhusiwe kuomba hiyo tender ziwe zile ambazo tayari zinaendesha mradi kama ule nje ya nchi,lakini hawa wengine wa kuzuka matokeo yake yatakua haya haya
 
Mkuu, huu mradi ni hatari ila kwa kifupi ntakwambia niliyoyaona pale coz niliwahi fanya kazi pale kama machanical and automobile technician,

1) upande wa uongozi, kaka hakuna muunganiko kabisa kati ya idara zake ( watu wanaokaa maofisini na wanoashughulikia magari moja kwa moja), yaan hao matransport officer ni kazi bure tu.

2) upande wa maintanance kaka hapo ndo hatar sasa, kwanza asilimia 70 ya technician mule ni mafundi uchwara, hawana uzoefu na system za yale magar kabisa kazi yao ni kutumia nguvu bila akili.

Kama fundi hana uwezo usitegemee gar itakua poa mkuu thats why zinakufa kila kukicha.

Mkuu kama zile gari zingekua zinahudumiwa vizur basi zingekua kwenye ubora wake kwa zaidi ya miaka 15-20.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mienaona ni wazo zuri, ukienda temesa utakuta magari ya zamani yalishabaki bodi tu, tuweke utaratibu gari itumike miaka mitano au ikifika km lakimbili iuzwe hatakama ni nzima.

kuhusu haya magari ya udart tulishauri tangu enzi ya JK kuwa yakichakaa hayatengeneziki, engene ni comic, brake wabco, bodi youtong usukuni sijui wa isuzu, hata afisa manunuzi hajui spear atapata wapi! na sio mara ya kwanza kufanyika haya mambo ya hovyo, leo hii yale mabus ya icurus yako wapi?

Yapo makampuni ya maana yalijitokeza kuendesha huu mradi kama scania ya spain MAN ya ujerumani marcopolo ya brazil na TATA ya india, tukatanguliza uswahili tukaenda leta magari ya wachina ona yaliyotukuta.

Kusema hawajawahi nunua magari sidhani kama ni kweli, nachojua kuna bus 70 ziko tra mwaka wa tatu sasa waziri kaambiwa kasema wakae chini na tra wazungumze wazungumze nini wakati mkurugenzi wa fedha keshamfukuza kazi. isitoshe CEO wa udart Mr kisena yuko jela nani anaesimamia kampuni? yule DG wa zamani alitolewa ofisini kwa kunigwa tai na akapigwa na mtama na hakuna aliyemtetea halafu mnakwenda na makamera huku mumefura kama koboko wakati matatizo manayajua.

Waziri mkuu hawezi kumfuta kazi DG sasa anasema kawaachia mamlaka za uteuzi, mbona mambo ya hovyo, sasa kama waziri mkuu hawezi kumwajibisha huyu mungumtu nani anaweza msimamia? hilo kampuni si ni msitu wa manyani! weita leta bia ingine, hivi hii bar inaitwaje kwanza
 
Hesabu mbaya sana hizi umepiga lkn ndio ukweli
 
kiukweli huu mradi unaendeshwa hovyo sana, japokua kupewa mwekezaji sidhan kama itakua sahihi kwa sababu ya ile exclusivty yake na kutokua na competition
Kweli mkuu,
Mradi unaendeshwa kihuni huu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…