Waziri Mkuu, Majaliwa amuwakilisha Rais Samia kumjulia hali Lowassa

Waziri Mkuu, Majaliwa amuwakilisha Rais Samia kumjulia hali Lowassa

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
790
Reaction score
964
MAJALIWA AMUWAKILISHA RAIS SAMIA KUMJULIA HALI LOWASSA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwakilisha Dkt. Samia Suluhu Hassan kumjulia hali Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa anayeendelea na matibabu Afrika ya Kusini.

Akizungumza na wanafamilia kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Samia, Waziri Mkuu amewasilisha salaam za pole kutoka kwa Mheshimiwa Rais na kusema Mheshimiwa Rais anafuatilia hali ya Mheshimiwa Lowassa kwa ukaribu na anamuombea afya njema.

Waziri Mkuu ametoa salamu hizo leo (Jumatano, Desemba 28, 2022) jijini Johannesburg, Afrika Kusini ambako alienda kumjulia hali Mheshimiwa Lowassa.

Kwa upande wake, Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu, Mama Regina Lowassa amemshukuru Mheshimiwa Rais kwa jinsi ambavyo amekuwa karibu na wanafamilia na namna ambavyo anafuatilia matibabu ya mpendwa wao.

Naye mtoto mkubwa wa Mheshimiwa Lowassa na Mbunge wa Monduli, Bw. Fredrick Lowassa amewashukuru Watanzania kwa maombi yao ya kumtakia afya njema baba yao.

IMG-20221228-WA0484(2).jpg


Ilikotoka: Kwanini Rais Samia hajawahi kumjulia hali Mzee Lowassa?
 
MAJALIWA AMUWAKILISHA RAIS SAMIA KUMJULIA HALI LOWASSA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwakilisha Dkt. Samia Suluhu Hassan kumjulia hali Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa anayeendelea na matibabu Afrika ya Kusini.

Akizungumza na wanafamilia kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Samia, Waziri Mkuu amewasilisha salaam za pole kutoka kwa Mheshimiwa Rais na kusema Mheshimiwa Rais anafuatilia hali ya Mheshimiwa Lowassa kwa ukaribu na anamuombea afya njema.

Waziri Mkuu ametoa salamu hizo leo (Jumatano, Desemba 28, 2022) jijini Johannesburg, Afrika Kusini ambako alienda kumjulia hali Mheshimiwa Lowassa.

Kwa upande wake, Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu, Mama Regina Lowassa amemshukuru Mheshimiwa Rais kwa jinsi ambavyo amekuwa karibu na wanafamilia na namna ambavyo anafuatilia matibabu ya mpendwa wao.

Naye mtoto mkubwa wa Mheshimiwa Lowassa na Mbunge wa Monduli, Bw. Fredrick Lowassa amewashukuru Watanzania kwa maombi yao ya kumtakia afya njema baba yao.
Baba alikua waziri mkuu first born ni mbunge, hao ndo wamenjoy matunda ya nchi hi, sisi wengine tunaishi tu ili mradi.
 
Kwa nini unasema amemuwakilisha?! Kwamba ni lazima waziri mkuu mstaafu ajuliwe hali na Rais?
MAJALIWA AMUWAKILISHA RAIS SAMIA KUMJULIA HALI LOWASSA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwakilisha Dkt. Samia Suluhu Hassan kumjulia hali Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa anayeendelea na matibabu Afrika ya Kusini.

Akizungumza na wanafamilia kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Samia, Waziri Mkuu amewasilisha salaam za pole kutoka kwa Mheshimiwa Rais na kusema Mheshimiwa Rais anafuatilia hali ya Mheshimiwa Lowassa kwa ukaribu na anamuombea afya njema.

Waziri Mkuu ametoa salamu hizo leo (Jumatano, Desemba 28, 2022) jijini Johannesburg, Afrika Kusini ambako alienda kumjulia hali Mheshimiwa Lowassa.

Kwa upande wake, Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu, Mama Regina Lowassa amemshukuru Mheshimiwa Rais kwa jinsi ambavyo amekuwa karibu na wanafamilia na namna ambavyo anafuatilia matibabu ya mpendwa wao.

Naye mtoto mkubwa wa Mheshimiwa Lowassa na Mbunge wa Monduli, Bw. Fredrick Lowassa amewashukuru Watanzania kwa maombi yao ya kumtakia afya njema baba yao.
 
Muhimbili iboreshwe hii ya viongozi kutibiwa nje haijakaa sawa

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Iboreshwe kwa namna gani?hata sasa Muhimbili, KCMC,Bugando..hizo ni hospita nzuri tu na anaweza kutibiwa kiongozi yoyote,kiongozi ni mtu kama watu wengine,ila ni swala la kujiaminisha tu na kiburi cha pesa pia
 
Kumbe waziri mkuu wetu mstaafu anaumwa na yuko kwenye matibabu?Nilikuwa sijui.I wish you a getwell soon.Bado nakumbuka kwamba wakati wa uongozi wako kuna alama umeacha. Wewe ndiyo muasisi wa zahanati kila kata.sekondari kila kata pia na zile barabara tatu za baadhi ya maeneo ya Dar.pia uliasisi wazo la mradi wa kutoa maji toka ziwa victoria mpaka Shinyanga.
 
Back
Top Bottom