Waziri Mkuu Majaliwa ashangaa kukuta wanafunzi wanakaa chini Mkuranga, atoa wiki mbili madawati yapatikane!

Waziri Mkuu Majaliwa ashangaa kukuta wanafunzi wanakaa chini Mkuranga, atoa wiki mbili madawati yapatikane!

SASA kama hapo mkuranga tuu hali ipo hivyo akija huku Jitombashisho shinyanga vijijini si atajinyanga huyu majaliwa???
Hapo sasa, nashangaa kipindi hiki kuelekea uchaguzi ndio wanajifanya kushangaa na kutoa maagizo ya harakašŸ˜‚šŸ˜‚
 
Waziri mkuu mh Majaliwa amefanya ziara ya kushtukiza katika moja ya shule za wilaya ya mkuranga na kukuta wanafunzi wa msingi na sekondari wamekaa chini.

Mh Majaliwa ameshangazwa na hali hiyo na kutu muda wa wiki mbili madawati yapatikane na watoto wote wakae.

Majaliwa amesema wilaya hiyo ina viwanda zaidi ya 70 sasa inakuwaje DC na DED wanashindwa kutumia fedha za CSR kununulia madawati.

Chanzo: ITV habari!
Uchumi wa kati wa chini wanafunzi wanakaa chini!
 
Kwani Serikali ya CCM haijafika au haipo pia huko Mkuranga Mkuu? Sasa kama hapa tu Mkuranga hali ni hiyo je, huko Kyaka Nkunde kutakuwaje?
Haya ndio matunda ya five years of HAPA KAZI TU! Tukiwaambia tuna mabingwa wa utapeli wa kisiasa, mnabisha! Kama angekwenda mwenyewe kitu cha kwanza angeuliza mbunge wa eneo hilo ni nani. Akiambiwa ni wa Upinzani, basi anawatukana wananchi kuwa hawapati maendeleo kwa sababu walichagua vibaya - walichagua mpinzani. Akiambiwa ni m-CCM, basi anafanya political gimmicks zake kwa kumtumbua mkurugenzi ili kuonesha kuwa ni mchapa kazi na amekasirika!! Uchapa kazi ni kufuatilia kila mwaka kwa kutaka uletewe ripoti kupitia channels za kiutawala na kuchukua hatua kiutawala. Kwa sababu mkuu wa nchi hawezi kwenda kila jimbo au halmashauri kuona nani anafanya nini. Kuna channels za kiutawala. Hiki alichofanya huyu WM ni mtindo ule ule wa bosi wake, political gimmick, tofauti ni kwamba hana mamlaka ya kutumbua!!! Tunasubiri miaka mingine mitano ya maendeleo hayana chama!! HAPA KAZI TU
 
Waziri mkuu mh Majaliwa amefanya ziara ya kushtukiza katika moja ya shule za wilaya ya mkuranga na kukuta wanafunzi wa msingi na sekondari wamekaa chini.

Mh Majaliwa ameshangazwa na hali hiyo na kutu muda wa wiki mbili madawati yapatikane na watoto wote wakae.

Majaliwa amesema wilaya hiyo ina viwanda zaidi ya 70 sasa inakuwaje DC na DED wanashindwa kutumia fedha za CSR kununulia madawati.

Chanzo: ITV habari!
Aende Kisarawe akaone pia wanakaa chini baadhi ya shule
 
Haya ndio matunda ya five years of HAPA KAZI TU! Tukiwaambia tuna mabingwa wa utapeli wa kisiasa, mnabisha! Kama angekwenda mwenyewe kitu cha kwanza angeuliza mbunge wa eneo hilo ni nani. Akiambiwa ni wa Upinzani, basi anawatukana wananchi kuwa hawapati maendeleo kwa sababu walichagua vibaya - walichagua mpinzani. Akiambiwa ni m-CCM, basi anafanya political gimmicks zake kwa kumtumbua mkurugenzi ili kuonesha kuwa ni mchapa kazi na amekasirika!! Uchapa kazi ni kufuatilia kila mwaka kwa kutaka uletewe ripoti kupitia channels za kiutawala na kuchukua hatua kiutawala. Kwa sababu mkuu wa nchi hawezi kwenda kila jimbo au halmashauri kuona nani anafanya nini. Kuna channels za kiutawala. Hiki alichofanya huyu WM ni mtindo ule ule wa bosi wake, political gimmick, tofauti ni kwamba hana mamlaka ya kutumbua!!! Tunasubiri miaka mingine mitano ya maendeleo hayana chama!! HAPA KAZI TU

You're very Intelligent Chap. I dovetail with you 100%.
 
Harafu hizi ziara za kushtukiza mashuleni hazina tija na haiwezekani kutatua shida hii kwa staili hii ya kuzima moto na kutishia kutumbua

Na hapo kaenda shule moja tu. Sijui hata kama alipata akili ya kuomba apewe status ya majengo ya madarasa na madawati japo kwa mkoa mzima?
 
Eti ndio kashituka.
Manunuzi ya midege iliyoanikwa pale JKNIA kama nsansa na michembe, ingeweza kumaliza matatizo yote ya uhaba wa madawati, vyoo, vyumba vya madarasa, ofisi na samani za Walimu, chaki hapa nchini.
Pia ingelipa nyongeza za mishahara ya Walimu na mihela mingi ikabaki.
Manafiki haya mazee matatizo ya eli mu nchi yanajulikana sana na sio shule hiyo tu , hapo muheshimiwa Yuko kwenye sanaa za maonyesho ya awamu ya tano maana kwa maigizo hawajambo.
 
Waziri mkuu mh Majaliwa amefanya ziara ya kushtukiza katika moja ya shule za wilaya ya mkuranga na kukuta wanafunzi wa msingi na sekondari wamekaa chini.

Mh Majaliwa ameshangazwa na hali hiyo na kutu muda wa wiki mbili madawati yapatikane na watoto wote wakae.

Majaliwa amesema wilaya hiyo ina viwanda zaidi ya 70 sasa inakuwaje DC na DED wanashindwa kutumia fedha za CSR kununulia madawati.

Chanzo: ITV habari!
C walisema wamevuka lengo ishu ya madawati wameimaliza????
 
Miaka 51 bado tu watoto wanakaa chini, maji hakuna, umeme wa uhakika nchi nzima bado. MIAKA 51 imepita mtatuambia nini tuwaelewe? Nashindwa kuelewa hawa jamaa kipaumbele chao ni nini hasa?

Lissu aje atubadilishie katiba sasa tuone huu upuuzi kama utaendelea tena.
 
CCM Mpya wanahaha na kuhangaika dakika za majeruhi kila kona ya nchi lakini wananchi hawashawishiki na hatua hizi kuelekea 2020 tayari wanasema , Sasa Basi !

12 August 2020
Mbeya, Tanzania

TAZAMA YAKABIDHI MADAWATI 200 KWA TULIA TRUST , DKT TULIA AMKABIDHI RC MBEYA"

Leo Dr. Tulia Ackson amepokea madawati kwa niaba ya Tulia Trust Home - Tulia Trust toka Kampuni ya Tanzania Zambia Mafuta TAZAMA Pipelines Ltd pipeline maararufu kama TAZAMA inayosafirisha mafuta kupitia bomba la mafuta toka Dar es Salaam hadi Ndola Zambia watoa msaada wa madawati.

Madawati hayo baadaye Dr. Tulia Ackson aliyakabidhi kwa Albert Chalamila ambaye ni mkuu wa mkoa wa Mbeya.
Source : MbeyaYetuOnlineTV
Tulia Trust was founded in 2015 by Hon. Dr. Tulia Ackson, Deputy Speaker, Parliament of the United Republic of Tanzania About Us - Tulia Trust
 
Viongozi wa chini yake.. wanaonesha ni kuna wasiwo na ujuzi.. wa kazi zao

Kweli makada wa CCM Mpya na UVCCM waliopewa vyeo vya Mtendaji wa Kata, Afisa tarafa, DED, DC na RC wanaonesha kukosa weledi wapo kisiasa zaidi badala ya kuangalia mahitaji ya maendeleo ya watu katika maeneo yao.

Kazi yao kubwa ni kusifia Flyovers, Dreamliner/ bombardier n.k zilizopo Dar es Salaam ambazo hazitatui mahitaji ya wananchi ktk maeneo yao.
Taarifa na Maarifa ya Uendeshaji wa Halmashauri za Mitaa - Mwanza
Ngazi ya Tarafa. Kazi za Afisa Tarafa. Katika kurahisisha mawasiliano Afisa Tarafa ni kiungo kati ya ngazi ya Kata na Halmashauri kwa upande mmoja na Serikali

FAHAMU MAJUKUMU YA WATEULE WA RAIS:
Rais Magufuli Afanya Kikao Cha Kazi Na RC, RAS, DC, DAS Na DED Wote


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Magufuli amewataka Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji kujenga ushirikiano na uhusiano mzuri baina yao ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu yao.

Mhe. Rais Magufuli ametoa maelekezo hayo leo tarehe 16 Mei, 2019 katika kikao cha kazi kati yake na viongozi hao kilichofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, baadhi ya Mawaziri na Makatibu Wakuu.

Mhe. Rais Magufuli amewaonya baadhi ya viongozi hao ambao wamekuwa na migogoro baina yao na hivyo kuathiri utendaji kazi na amesema endapo vitendo hivyo vitaendelea hatasita kuchukua hatua ikiwa ni pamoja kuwaondoa katika nyadhifa zao.

Pamoja na kuwataka kuwa waadilifu na wenye nidhamu kazini, Mhe. Rais Magufuli amewataka kusimamia kwa ukaribu miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao, kusimamia ukusanyaji wa mapato yote ya Serikali, kusimamia ulinzi na usalama na kusimamia rasimali za umma.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewapongeza viongozi hao kwa kazi nzuri wanazozifanya zinazowezesha mipango na mikakati mbalimbali ya Serikali kwenda vizuri na amewahakikishia kuwa anawaamini na anatarajia wataendelea kufanya vizuri katika utekelezaji wa majukumu yao.

ā€œNi matumaini yangu baada ya kikao hiki cha leo sote tutakwenda kwa mwelekeo mzuri zaidi, nendeni mkachape kazi, mimi ndiye niliyewaweka kwenye nafasi hizo na ninafuatilia utendaji kazi wa kila mmoja wenu, sitarajii kusikia tena hamuelewani miongoni mwenuā€ amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Katika kikao hicho Mhe. Rais Magufuli amesikiliza kero na changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili viongozi hao katika maeneo yao ya kazi na ameahidi kwenda kuzishughulikia.


Kabla ya kuanza kwa kikao hicho, Mhe. Rais Magufuli amemuapisha Mhe. Juma Zuberi Homera kuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi.

Mhe. Homera pia amekula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Mstaafu Harold Nsekela.

Baada ya kikao hicho, viongozi hao wamekula futari na Mhe. Rais Magufuli aliyoiandaa kwa ajili yao.


Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

16 Mei, 2019
Source: Rais Magufuli Afanya Kikao Cha Kazi Na RC, RAS, DC, DAS Na DED Wote
 
Sio huko tu hata hapa hapa Dar shule ya msingi Mzambarauni iliyopo Jimbo la Ukonga wanafunzi wanakaa chini.
Huko Mwanza hali hiyo niliiona Pamba sekondari, meli mmoja akaniambia kuwa kama mzazi anataka kuchonha dawati kwa mwanae lazima apitie kwa mkuu wa wilaya ampe ruhusa na alikabidhi huko kwa mkuu wa wilaya!.
 
Back
Top Bottom