Waziri Ndumbaro azindua Jengo la Utalii wa mashamba ya misitu Biharamulo-Chato, atoa maelekezo kwa Sekta ya Utalii nchini

Waziri Ndumbaro azindua Jengo la Utalii wa mashamba ya misitu Biharamulo-Chato, atoa maelekezo kwa Sekta ya Utalii nchini

Daaah,Chato tena kwenye headlines!Huo mjengo sio wakitoto aisee,na hiyo ni ofisi tu ya miti!?[emoji16][emoji16][emoji16]

Utalii wa mashamba ya misitu maana yake nini?
Shiiiiiiiii, acha kuhoji hoji we jua tu ni utalii, hata kama hao watalii hawaendi huko...ebo[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Waziri wa maliasili na utalii Dkt. Damas Ndumbaro leo January 12 akizindua jengo la utalii wa mashamba ya misitu Biharamulo-Chato ameiagiza bodi ya utalii nchini kuhaakikisha kuwa inapeleka watalii wa kutosha kwenda kujionea maajabu ya msitu mnene wa Biharamulo-Chato hivyo kuongeza mapato ya serikali

Picha: Waziri Ndumbaro akiwa na bodi ya utalii nje ya jengo alilozindua leo Biharamulo-Chato


"bodi ya utalii nchini kuhaakikisha kuwa inapeleka watalii" TANZANIA YANGU UMEPATWA NA NINI? KWA HIYO bodi ndo inaamua impeleka wapi mtalii? Jamani, Jamani, tuendeshe hii nchi kiutaalam na sio kwa hisia!
 
Afu nashangaa hata kwanini wanatangaza kuzindua ni kuji aibisha tu kama Taifa, jengeni yatumike kimya kimya kwa wenye ufahamu wao mna wakera sana baadhi ya watu kwa kujua mchezo wa kitoto wanao chezewa wananchi na kufanywa Mazwazwa kwa ka kikundi ka dogo ka wachache.
 
Watalii waje waende wakajionee kiwanja cha ndege kilichojengwa kijijini ambako watu kupanda hata basi tu ni shida.
 
Ningekua mimi ninge-step down nafasi yangu ya uwaziri, huwezi kusimama pale mbele na kujidai tumeleta maendeleo wakati clearly hata kwenu maendeleo hayajaletwa! Unaona kabisa intrest ni za mtu mmoja mwenye ego na sio interest za Tanzanian public. Magufuli hana mshipa wa aibu anawadhalilisha sana kwa kuwafanya muonekane vituko mbele ya jamii
"---tumeleta maendeleo", tafsiri yake bado huijui mkuu wangu 'Rebecca83'?

Hayo ni maendeleo yake na familia yake mkuu.

Woooote waliomo kwenye serikali hiyo, kama akina "waliookotwa "JALALANI'" wapo katika nafasi hizo sio kwa 'interests' za waTanzania, wapo kutimiza 'interests' zao binafsi wakati wakihakikisha hizo za aliyewateua zipo juu ya kila kitu. Vinginevyo, hata hizo za kwao zitayeyuka wasipolinda za huyo mkubwa.
 
Hivi na nyie mnaamininbodi ya utalii ndio inapeleka watalii? Umeshaona wazungu wanalazimishwa kufanya kitu? Hakuna mzungu atakayeenda chato. Mtu aache serengeti, ngorongoro, eti aende mbali huko chato? Majibu mtayapata baada ya muda tu. Sad jinsi pesa ya umma inavyowekezwa vibaya wakati ajira kwa vijana hakuna.
itaanza watumishi wote lazima wafanye utalii buricha ili wabaki na ajira,next mikutano yote ya mambo ya utalii italazimishwa kufanyika huo,then wafanyabiashara wataambiwa wakafanye utalii kama hujaenda urgency note,Makampuni ya utalii yatapewa target ya kupeleka watalii hata kama hawataki then tutapewa data za watalii waliotembelea Over.
 
Biharamulo ni wilaya kama ilivyo Chato-Mkoa ni Geita. Ni baada ya Geita kumegwa kutoka wilaya(mkoa-Mwanza) na kuwa mkoa.

Wilaya ya Biharamulo bado hipo Mkoa wa Kagera - lakini mambo yanavyo elekea tusishangae siku moja tuka ambiwa B'mulo amehamishiwa kwenye Mkoa mwingine muda si mrefu kuanzia sasa.
 
Ningekiwa mbunge ningeleta hoja serengeti ihamishiwe huko huko
 
Wilaya ya Biharamulo bado hipo Mkoa wa Kagera - lakini mambo yanavyo elekea tusishangae siku moja tuka ambiwa B'mulo amehamishiwa kwenye Mkoa mwingine muda si mrefu kuanzia sasa.
Kuna wilaya kama ngara tupa kule haimo kwenye ramani anymore.mizigo ya kwenda Rwanda inapatabshida sana
 
Back
Top Bottom