Waziri Ummy: Bima ya Afya (NHIF) inakaribia kufa

Waziri Ummy: Bima ya Afya (NHIF) inakaribia kufa

Hii ni moja ya mashirika yaliyoanzishwa bila upembuzi yakinifu.
Serikali ijifunze toka serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Benjamin William Mkapa.
Mkapa alianzisha kwa weledi mkubwa TANROADS na TRA ya sasa.
Tunashindwa nini kujifunza na tuna ma PhD yanaozea vichwani mwa kina Mwigulu.
Alianzisha au alicopy na kupaste kutoka nchi nyingine
 
Mwananchi apewe ruhusa kuchagua bima ya afya. Ataingia makubaliano yeye binafsi ie makato, coverage. NHIF inaendeshwa kisiasa zaidi. Bunge plus wizara are to blame. This was pointed out by the CAG. What action was taken???
 
Watumiaji wakubwa wa NHIF ni watumishi wa serikali na mashirika ya umma. Niliwahi kuuliza humu nikajibiwa kwamba wanakatwa 3% ya mshahara kama ada ya uanachama. Maana yake anayepokea milioni moja kwa mwezi atakatwa 30,000 na kwa mwaka 360,000.

Kijana wa miaka 25 anachangia zaidi ya 500,000 kwa mwaka kama si muajiriwa. Mfanyakazi anapata huduma kwa hadi watu sita. Mtu binafsi ni yeye peke yake.

Hawa wanaochangia binafsi wamepunguziwa huduma ambazo wafanyakazi na wategemezi wao wanapata pamoja na kwamba wao wanalipa zaidi ya wafanyakazi.

Hili linahitaji kuangaliwa.
 
Waziri anakosea anapokiri bima ya afya NHIF inakaribia kufa, kwanini wasitafute njia mbadala itakayowawezesha kumudu hayo mazingira ya kuongezeka gharama za matibabu?

Kuna watu wanaweza kupoteza ajira zao hapo kutokana na kufa kwa hicho kitengo, wasiwe wepesi kukiri kushindwa bila kwanza kutafuta majibu ya changamoto zinazoukabili huo mfuko.

Mfano, kama inapoonekana gharama za matibabu anazopata mwanachama ni kubwa zaidi ya kile anachochangia mwanachama, kwanini NHIF wasigawane gharama za matibabu na mwanachama 50/50 ili kuepuka tatizo la mfuko kuzidiwa na gharama mwishowe kutengeneza madeni?

Hili nimeona linatokea kwa bima nyingine za afya, licha ya wanachama kulipiwa na mifuko hiyo, bado hutakiwa kutoa sehemu nyingine za gharama ya matibabu yao toka mifukoni mwao ili kufidia nyongeza ya kile wasichochangia kwenye bima zao za afya.

Kama hilo lisipowezekana, basi nashauri kiasi cha pesa anazochangia mwananchama ambaye ni mgonjwa wa hayo magonjwa makubwa yasiyoambukiza kiongezwe ili kuendana na gharama halisi za matibabu yao.
Changamoto huo mfuko wanaua wenyewe wanaenda kukopa matokeo yake hawalipi madeni, staff wa NHIF wanalipana posho na kucheza dili.
 
Mwananchi apewe ruhusa kuchagua bima ya afya. Ataingia makubaliano yeye binafsi ie makato,coverage. NHIF inaendeshwa kisiasa zaidi. Bunge plus wizara are to blame. This was pointed out by the CAG. What action was taken???
Unahisi unaweza changia strategies, jubilee? Hawa gharama zao kwa mwaka ni kubwa sana ila wanakulimit kutibiwa mwisho 500,000 kwa mwaka.
 
Watumiaji wakubwa wa NHIF ni watumishi wa serikali na mashirika ya umma. Niliwahi kuuliza humu nikajibiwa kwamba wanakatwa 3% ya mshahara kama ada ya uanachama. Maana yake anayepokea milioni moja kwa mwezi atakatwa 30,000 na kwa mwaka 360,000.
Kijana wa miaka 25 anachangia zaidi ya 500,000 kwa mwaka kama si muajiriwa.
Mfanyakazi anapata huduma kwa hadi watu sita. Mtu binafsi ni yeye peke yake.
Hawa wanaochangia binafsi wamepunguziwa huduma ambazo wafanyakazi na wategemezi wao wanapata pamoja na kwamba wao wanalipa zaidi ya wafanyakazi.
Hili linahitaji kuangaliwa.
Hata mimi nimeliongelea hili swala

Kuwa wanaokwamisha huu mfuko ni wafanyakazi wa Serikali na wategemezi wao.

Serikali kunusuru huu mfumo wabadilishe mfumo wa matibabu, mtu atibiwe kulingana na michango yake, tegemezi waondolewe.
 
Kitakachoiua NHIF siyo gharama za matibabu bali udanganyifu. Natamani ningekuwa na mamlaka nchi hii ili nioneshe mfano ila ndo hivyo wenye mamlaka wengi uwezo ndo hivyo na wenye uwezo wengi hawana mamlaka.
Huu ndio ukweli, Kuna mmoja alinisimulia kinachofanyika Muhimbili nikabaki nashangaa tu. Kuna udanganyifu mkubwa usio wa kawaida.
 
Wakati mikakati ya kuboresha huduma za afya ikiendelea kuwekwa, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amebainisha dalili za kufa kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kutokana na kulemewa na madeni ya matibabu ya wanachama wake...
Mfuko bado uko imara kuendelea kutekeleza majukumu yake ikiwemo kufanya malipo kwa wanufaika wake.

Hatua zinazotakiwa kuchukuliwa kwa sasa ni wananchi wengi zaidi kujiunga ili kuimarisha zaidi uhai wake.
 
Wakati mikakati ya kuboresha huduma za afya ikiendelea kuwekwa, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amebainisha dalili za kufa kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kutokana na kulemewa na madeni ya matibabu ya wanachama wake...
Dhana ya Mfuko ni kuchangia kabla ya kuugua ili uwe na uhakika wa kutibiwa hata kama huna fedha kwa kutumia kadi ya bima ya Afya.

Pamoja na kuwepo kwa utofauti wa michango viwango vya huduma za matibabu vipo sawa kwa kila mwanachama na hakuna ukomo wa huduma kulinga na kiwango ulichochangia.
 
Back
Top Bottom