Waziri Ummy: Bima ya Afya (NHIF) inakaribia kufa

Waziri Ummy: Bima ya Afya (NHIF) inakaribia kufa

Wakati mikakati ya kuboresha huduma za afya ikiendelea kuwekwa, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amebainisha dalili za kufa kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kutokana na kulemewa na madeni ya matibabu ya wanachama wake...
Magonjwa yasiyoambukiza yameongezeka miongoni mwa wananchi ambayo yana gharama kubwa katika kuyatibu.

Kutokana na ongezeko la magonjwa hayo Mfuko umelazimika kulipia gharama kubwa ya matibabu hayo kwa wanachama wanaougua maradhi hayo.
 
Mfuko bado uko imara kuendelea kutekeleza majukumu yake ikiwemo kufanya malipo kwa wanufaika wake.

Hatua zinazotakiwa kuchukuliwa kwa sasa ni wananchi wengi zaidi kujiunga ili kuimarisha zaidi uhai wake.
Habari imeletwa na waziri kuwa mfuko unakaribia kufa, wewe unasema upo imara. Unamkana waziri mwenye dhamana?
 
Tukirudisha mfumo wa zamani kuna ubaya gani? Tukawa tunatibiwa kwa kulipa kidogo na serekali inabeba kiasi.
 
Ukweli mchungu NHIF haina watu wenye weledi na uwezo stahiki mambo ya kuteua ndugu na jamaa na watu wenye itikadi fulani bila kuzingatia sifa stahiki haya ndo mazao yake.

Shirika kujiendesha kwa kauli za kisiasa kwa sababu ya ujinga wa viongozi wetu mwisho huleta madhara kwa umma.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
NHIF ni taasisi ya Serikali ambayo inazingatia taratibu zote za Utumishi katika kuajiri watumishi wake.
 
Hii ni moja ya mashirika yaliyoanzishwa bila upembuzi yakinifu.
Serikali ijifunze toka serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Benjamin William Mkapa.
Mkapa alianzisha kwa weledi mkubwa TANROADS na TRA ya sasa.
Tunashindwa nini kujifunza na tuna ma PhD yanaozea vichwani mwa kina Mwigulu.
NHIF imeanza kutoa huduma mwaka 2001 wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu baada ya kufanyika kwa upembuzi yakinifu na wa kitaalam.
 
Watanzania tuwe waelewa hakuna tatizo lisilo na jibu..nature ya matatizo ya kufilisika be it kampuni, mtu binafsi, kikundi nk ni poor planning na uwezo mdogo kwenye usimamizi...
Uongozi wa Mfuko uko imara na unayo mikakati thabiti na endelevu ya kuhakikisha Mfuko unazidi kuimarika na kutoa huduma kwa wanachama wake.
 
Bima Haina maana kwamba unapata sawa na kile unachochangia. Kama hujaugua kabisa hupati au huhudumiwi chochote. Lakini ukiugua utahudumiwa Kwa gharama hata mara kumi ya mchango wako. Hiyo ndiyo maana na faida ya bima. Hata kwenye mali unazowekea bima, eg. gari, unaweza lipia bima sh. 500,000=/, gari ikipata ajali unalipwa gharama ya matengenezo, labda milioni Tano au zaidi au gari nyingine, na pia kama Kuna majeruhi ktk ajali hiyo analipwa.
Dhana ya bima ya afya ni kuchangia kabla ya kuugua na ili huduma ziimarike zaidi inahitaji wananchi wengi zaidi kujiunga ili mmoja wetu anapougua atibiwe bila ukomo.
 
Wanajifilisi wenye kwa gharama kubwa kwenye hospitali za mikoa na rufaa.double standard inawakamua wenyewe.

Imagine kwenye hospitali ya wilaya upasuaji mkubwa ni 110,000, upasuaji huo huo kwenye hospitali ya mkoa ni 320,000 na kwenye hospitali ya rufaa ni 600,000 au 700,000

Lakini kwa sasa si tunalipa matozo mengi, nafikiri serikali ipeleke ruzuku huko NHIF kuokoa jahazi
 
Hata mimi nimeliongelea hili swala

Kuwa wanaokwamisha huu mfuko ni wafanyakazi wa Serikali na wategemezi wao.

Serikali kunusuru huu mfumo wabadilishe mfumo wa matibabu, mtu atibiwe kulingana na michango yake, tegemezi waondolewe.
Inaonekana una chuki sana na wafanyakazi wa serikali.Kama wewe ukubahatika kuajiriwa usipambane walioajiriwa wakose privilage wanazozipata,badala yake leta michango ya maboresho sio mikwamo.Lengo la serikali ni kuwafikia watu wengi zaidi wawe ndani ya bima alafu wewe unakuja na zana yakuondoa wategemezi kama hizi sio chuki ni nini?
 
NHIF imeanza kutoa huduma mwaka 2001 wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu baada ya kufanyika kwa upembuzi yakinifu na wa kitaalam.
Its a failure.
Ndio maana kuna matatizo ambayo ni structural.
Waliofanya huo upembuzi must be mediocre.
 
Ina maana wanakiri kuwa wameshindwa kuusimamia huo mfuko hadi kutoa hiyo kauli.....
 
NHIF inaelemewa na wafanyakazi wa Serikali.

Ili mfuko usielemewe wategemezi waondolewe au mtu atibiwe kutokana na anavyochangia
Kuliko wategemezi waondolewe bora mfuko ufe tu.
 
Kwani magonjwa yasio ya kuambukiza ndo hayatakiwi kutibiwa kwa bima? Au mim ndo meelewa vibaya
 
Wafanye utafiti wa kina juu ya hosp. Zenye huduma ya bima waangalie Kama Kuna udanganyifu au hapana na ikigundulika tu adhabu Kali itolewe kwa kituo huska na ikibidi wafungiwe kabisa, wakiwa strict wataliokoa sana shirika.
 
Unahisi unaweza changia strategies, jubilee? Hawa gharama zao kwa mwaka ni kubwa sana ila wanakulimit kutibiwa mwisho 500,000 kwa mwaka.
Unahakika unachoandika? Why don't they have same problems like NHIF? NHIIF isn't telling us the real story. Let them come with actual figures kimkoa na hospitals.
 
Back
Top Bottom