Waziri Ummy: Bima ya Afya (NHIF) inakaribia kufa

Waziri Ummy: Bima ya Afya (NHIF) inakaribia kufa

Ila mashirika ya umma kwanini kila shirika ni hasara tu ninachojua ni usimamizi mbovu ona TTCL nayo suala la mda
 
Tatizo kubwa litakuwa kwenye manejimenti ya NHIF.
Watumishi wa umma wawe huru kuchagua mifuko ya kujiunga nayo.
Hii itafanya mfuko wa NHIF kushindana na mifuko mingine. Na watakuwa makini.
 
NHIF inaelemewa na wafanyakazi wa Serikali.

Ili mfuko usielemewe wategemezi waondolewe au mtu atibiwe kutokana na anavyochangia
Msitudanganye sababu ni CCM kuchota fedha za uchaguzi 2020.
 
Waziri hana aibu na uwezo wake wa kufikiri una walikini, hayo mashirika yanakusanya pesa nyingi sana na hadi kufikia uwezo wa kutumia hii michango kufanya biashara na majengo makubwa yanayopangishwa, huko kufa kunakujaje?
 
Hii ni moja ya mashirika yaliyoanzishwa bila upembuzi yakinifu.
Serikali ijifunze toka serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Benjamin William Mkapa.
Mkapa alianzisha kwa weledi mkubwa TANROADS na TRA ya sasa.
Tunashindwa nini kujifunza na tuna ma PhD yanaozea vichwani mwa kina Mwigulu.
NHIF ilianzishwa na Mkapa pia, 1999
 
Uwekezaji mbovu, ufisadi kutoka baadhi ya watumishi, utawala mbovu ni baadhi ya vyanzo vitavyomaliza mashirika mengi ya Serikali
 
Dhana ya Mfuko ni kuchangia kabla ya kuugua ili uwe na uhakika wa kutibiwa hata kama huna fedha kwa kutumia kadi ya bima ya Afya.

Pamoja na kuwepo kwa utofauti wa michango viwango vya huduma za matibabu vipo sawa kwa kila mwanachama na hakuna ukomo wa huduma kulinga na kiwango ulichochangia.
Viwango viko sawa kwa waajiriwa tu. Wanaojilipia wametungiwa vifurushi ambavyo hata ukichaguwa cha juu kabisa huduma utapata chini ya muajiriwa.
 
Inaonekana una chuki sana na wafanyakazi wa serikali.Kama wewe ukubahatika kuajiriwa usipambane walioajiriwa wakose privilage wanazozipata,badala yake leta michango ya maboresho sio mikwamo.Lengo la serikali ni kuwafikia watu wengi zaidi wawe ndani ya bima alafu wewe unakuja na zana yakuondoa wategemezi kama hizi sio chuki ni nini?
Swali ni kwa nini kuna ubaguzi wa kuwafanya wasiojiriwa wapate huduma ndogo kwa malipo makubwa zaidi.
 
Ila mashirika ya umma kwanini kila shirika ni hasara tu ninachojua ni usimamizi mbovu ona TTCL nayo suala la mda
Hivi kama sikosei, mwenyekiti wa bodi ya Shirika la Bima ya Afya ni Mama Anna Makinda ..... kaazi kwelikweli.
 
NHIF ina tatizo.... Moja la tatizo ni kutoa huduma sawa kwa kila mtu..

Waweke viwango vya huduma kutokana na mtu achangiavyo
Nani kakwambia hakuna viwango
 
Matatizo yanachangiwa na ujinga na ulimbukeni wa jamii kwa ujumla.
Kuna watu wanapewa huduma za afya na dawa zisizohitajika kwa sababu tu ya ujinga na ulimbukeni wa bima, pia hospitali kujaribu kuongeza mapato kwa sababu hizo hizo.
Haiwezekani wagonjwa na gharama ziwe kubwa hivyo.
Kuna shida ya utawala, utaalamu na wadau kwa ujumla.
 
Waziri anakosea anapokiri bima ya afya NHIF inakaribia kufa, kwanini wasitafute njia mbadala itakayowawezesha kumudu hayo mazingira ya kuongezeka gharama za matibabu?
Sasa ajira tu, si wapoteze mfuko unakata hela zetu wengine miaka miwili hatujatibiwa, je tukisema hela zetu zirudishwe ?
 
Mfuko unakusanya kiasi gani jumla kwa mwezi, mwaka toka kwa watumishi?

Kwa hiyo idadi iliyotajwa × 15,000 × Miezi 12 = Takribani Trilioni moja kwa mwaka. Hapo ni kama watumishi wote wanachangia sh 15,000

Sasa kulipa hiyo 100bn kwa mwaka ndo shirika life?
 
Hii ni moja ya mashirika yaliyoanzishwa bila upembuzi yakinifu.
Serikali ijifunze toka serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Benjamin William Mkapa.
Mkapa alianzisha kwa weledi mkubwa TANROADS na TRA ya sasa.
Tunashindwa nini kujifunza na tuna ma PhD yanaozea vichwani mwa kina Mwigulu.
Phd za mchongo haziwez leta mafanikio kwenye jamii
Mkapa hakuwa na phd lkn check tra na tanroad

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Wakati mikakati ya kuboresha huduma za afya ikiendelea kuwekwa, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amebainisha dalili za kufa kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kutokana na kulemewa na madeni ya matibabu ya wanachama wake.

Akifungua mkutano wa siku tano wa kikanda wa kuwajengea uwezo kuhusu ugonjwa wa kipindupindu jijini hapa jana, Waziri Ummy alitaja magonjwa yasiyoambukiza ndiyo sababu kuu ya gharama kubwa.

“Kuongeza uelewa ni jambo la msingi, kwa mfano bima yetu ya afya (NHIF) inakaribia kufa kwa kuwa umeelemewa na ongezeko la madai yanayohusu NCD (magonjwa yasiyoambukiza),” alionya Ummy.

Magonjwa yasiyoambukiza yanajumuisha moyo, saratani, mfumo wa upumuaji na kisukari yanayochangia asilimia 71 ya vifo vinavyotokea duniani ambapo ni sawa na watu milioni 41 kila mwaka.

Akisisitiza kuhusu uelewa wa dalili za magonjwa na jinsi ya kujikinga nayo, Waziri Ummy alisema “fanyeni kuwa jukumu la msingi ili kuzuia kuenea kwa maambukizi, najua tutafanikiwa kupambana na kipindupindu katika nchi zetu.”

Kutokana na hali hiyo, waziri huyo ameiagiza NHIF kuachana na utaratibu iliouanzisha hivi karibuni wa kudhibiti idadi ya wagonjwa wanaohudhuria vituo vya afya.

Taarifa ya NHIF

Akizungumza na waandishi wa habari Agosti 11 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernard Konga alisema wametumia Sh99.09 bilioni mwaka 2021/22 kulipia magonjwa yasiyoambukiza.

Alisema kiasi hicho ni sawa na asilimia 18 ya fedha zote zilizolipwa huku dawa za saratani na huduma ya kusafishwa figo (dialysis) zikitumia fedha nyingi zaidi. Alisema magonjwa yasiyoambukiza ni mzigo mkubwa kwa mfuko huo.

“Dawa za saratani zinaila zaidi NHIF. Haya ni magonjwa yanayotokana na mtindo wa maisha, kuna huduma ya kusafishwa damu kwa wagonjwa wa figo, tunatumia Sh35.4 bilioni kwa mwaka,” alisema.

Konga, alisema mpaka sasa mfuko huo una wanachama 4,831,233 sawa na asilimia nane ya Watanzania wote huku asilimia sita wakihudumiwa na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) huduma nyingine za bima zikihudumia asilimia moja. Hata hivyo, alisema kuna udanganyifu mwingi unaofanywa na watoa huduma hali inayouumiza mfuko huo lakini wanapambana na hali hiyo.

“Udanganyifu upo na tumekuwa tukichukua hatua, tutasitisha mikataba itakayoonekana inahatarisha uendelevu wa mfuko. Tumekuwa tukichukua hatua ikiwamo kupiga faini, kuwaripoti wahusika katika mabaraza yao kuhakikisha tumelipia huduma halali kulingana na miongozo,” alisema Konga.

Taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mashirika ya umma ya Machi 2022, inaonyesha NHIF ilipata hasara ya Sh109.71 bilioni.

Chanzo: Mwananchi
Ummy kazidi lopolopo, siasa nyingiii,
 
Mwananchi apewe ruhusa kuchagua bima ya afya. Ataingia makubaliano yeye binafsi ie makato, coverage. NHIF inaendeshwa kisiasa zaidi. Bunge plus wizara are to blame. This was pointed out by the CAG. What action was taken???
Tulia kimya tulambe asali wewe

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom