Robert S Gulenga
JF-Expert Member
- Jan 3, 2013
- 2,255
- 1,565
Ukitaka ujue kuna tatizo la msingi ruhusu kila Mtumishi au Taasisi kuchagua bima wanayoitaka.NHIF inaelemewa na wafanyakazi wa Serikali.
Ili mfuko usielemewe wategemezi waondolewe au mtu atibiwe kutokana na anavyochangia
Alianzisha au alicopy na kupaste kutoka nchi nyingineHii ni moja ya mashirika yaliyoanzishwa bila upembuzi yakinifu.
Serikali ijifunze toka serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Benjamin William Mkapa.
Mkapa alianzisha kwa weledi mkubwa TANROADS na TRA ya sasa.
Tunashindwa nini kujifunza na tuna ma PhD yanaozea vichwani mwa kina Mwigulu.
Changamoto huo mfuko wanaua wenyewe wanaenda kukopa matokeo yake hawalipi madeni, staff wa NHIF wanalipana posho na kucheza dili.Waziri anakosea anapokiri bima ya afya NHIF inakaribia kufa, kwanini wasitafute njia mbadala itakayowawezesha kumudu hayo mazingira ya kuongezeka gharama za matibabu?
Kuna watu wanaweza kupoteza ajira zao hapo kutokana na kufa kwa hicho kitengo, wasiwe wepesi kukiri kushindwa bila kwanza kutafuta majibu ya changamoto zinazoukabili huo mfuko.
Mfano, kama inapoonekana gharama za matibabu anazopata mwanachama ni kubwa zaidi ya kile anachochangia mwanachama, kwanini NHIF wasigawane gharama za matibabu na mwanachama 50/50 ili kuepuka tatizo la mfuko kuzidiwa na gharama mwishowe kutengeneza madeni?
Hili nimeona linatokea kwa bima nyingine za afya, licha ya wanachama kulipiwa na mifuko hiyo, bado hutakiwa kutoa sehemu nyingine za gharama ya matibabu yao toka mifukoni mwao ili kufidia nyongeza ya kile wasichochangia kwenye bima zao za afya.
Kama hilo lisipowezekana, basi nashauri kiasi cha pesa anazochangia mwananchama ambaye ni mgonjwa wa hayo magonjwa makubwa yasiyoambukiza kiongezwe ili kuendana na gharama halisi za matibabu yao.
Wanakimbilia kununua ndege badala ya kuhudumia wananchiHapo MSD Hajabwatuka na vilio haki ya nani ccm ni jipu chungu katika kutuvusha
NHIF ina tatizo.... Moja la tatizo ni kutoa huduma sawa kwa kila mtu..ukitaka ujue kuna tatizo la msingi ruhusu kila Mtumishi au Taasisi kuchagua bima wanayoitaka.
Unahisi unaweza changia strategies, jubilee? Hawa gharama zao kwa mwaka ni kubwa sana ila wanakulimit kutibiwa mwisho 500,000 kwa mwaka.Mwananchi apewe ruhusa kuchagua bima ya afya. Ataingia makubaliano yeye binafsi ie makato,coverage. NHIF inaendeshwa kisiasa zaidi. Bunge plus wizara are to blame. This was pointed out by the CAG. What action was taken???
Kuna sehemu nimesikia kimelipuka, nimeshangaa sana.Mpaka leo tunatamka neno kipindupindu!! Ningekuwa kiongozi nisinge tamka neno hilo kamwe. Aibu iliyoje!
Hata mimi nimeliongelea hili swalaWatumiaji wakubwa wa NHIF ni watumishi wa serikali na mashirika ya umma. Niliwahi kuuliza humu nikajibiwa kwamba wanakatwa 3% ya mshahara kama ada ya uanachama. Maana yake anayepokea milioni moja kwa mwezi atakatwa 30,000 na kwa mwaka 360,000.
Kijana wa miaka 25 anachangia zaidi ya 500,000 kwa mwaka kama si muajiriwa.
Mfanyakazi anapata huduma kwa hadi watu sita. Mtu binafsi ni yeye peke yake.
Hawa wanaochangia binafsi wamepunguziwa huduma ambazo wafanyakazi na wategemezi wao wanapata pamoja na kwamba wao wanalipa zaidi ya wafanyakazi.
Hili linahitaji kuangaliwa.
Huu ndio ukweli, Kuna mmoja alinisimulia kinachofanyika Muhimbili nikabaki nashangaa tu. Kuna udanganyifu mkubwa usio wa kawaida.Kitakachoiua NHIF siyo gharama za matibabu bali udanganyifu. Natamani ningekuwa na mamlaka nchi hii ili nioneshe mfano ila ndo hivyo wenye mamlaka wengi uwezo ndo hivyo na wenye uwezo wengi hawana mamlaka.
Pitia hotuba ya wizara ya afyaNHIF wanakusanya shilingi ngapi kwa mwaka?
Mfuko bado uko imara kuendelea kutekeleza majukumu yake ikiwemo kufanya malipo kwa wanufaika wake.Wakati mikakati ya kuboresha huduma za afya ikiendelea kuwekwa, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amebainisha dalili za kufa kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kutokana na kulemewa na madeni ya matibabu ya wanachama wake...
Dhana ya Mfuko ni kuchangia kabla ya kuugua ili uwe na uhakika wa kutibiwa hata kama huna fedha kwa kutumia kadi ya bima ya Afya.Wakati mikakati ya kuboresha huduma za afya ikiendelea kuwekwa, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amebainisha dalili za kufa kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kutokana na kulemewa na madeni ya matibabu ya wanachama wake...