Waziri Ummy Mwalimu: Maambukizi COVID-19 ya ndani kwa ndani yameanza, Watanzania wajiandae kwa maambukizi ya Jumuiya

Hawa kuna kitu wanatuficha hasa kwenye takwimu za walioambukizwa huu ugonjwa nchini. Ngoja ngoma isambae watafichua wenyewe.
Lete takwimu zako ulizonazo, usidhani kwamba ukisambaa wewe utabakia salama, hakuna alopangiwa kupata maambukizi bali yeyote yule anaweza kuambukizwa na wewe ukiwa miongoni mwao
 
Tumshukuru Mungu tumevuka kiunzi cha WHO na wale watz mavuvuzela wanaoiombea mabaya nchi yetu! Tutavuka salama tu kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu!
 
Tumuombee na Mangula apone aludi kweny majukumu yake kama kawaida pia tuwaombee na wazee wetu wenye visukari na presha na ukimwi wa ccm Mungu awaepushe na corona.
Mmmmh...! Peleka mapovu yako huko!
 
Mungu alitupenda sana, alitupa muda na nafasi ya kujipanga dhidi ya huu ugonjwa ila ndio hivyo tena tumekuwa wabishi! Yakitokea maafa serikali ya jiwe inalo la kujibu! Mungu Ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili nao tatizo kwakwel!!
Allah tuwe pamoja nasi kwa hili! Ili tuvuke salama
 
Nikilockiwa na wewe korona nitaisikilizia nje hukooo[emoji23][emoji23]

Usiombee lockdown tutaumbuka wengi haswa wale toka ndo ule sipati picha tutakavyopika hata magodoro[emoji23]
Ahahahaah dah, umenichekesha. Ingawa ni jambo la kuchukulia umakini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Namfikiria huyu myu sipati jibu, ilikuwaje akafika mwanza? Ina maana karantini ya 14 days inatamkwa tu utekelezaji hakuna, Mungu atusaidie sana
Itakuwa alitoa kiasi na kuachiwa
 
Kama serikali hamna strategy,xia watu wasitoke mkoa kwenda mkoa kwa kibalimaalumu
 
Watu wanahitaji sadaka
 
“Tunamshukuru Mungu, hadi sasa anatutendea maajabu, tumevuka kihunzi WHO, walisema mwezi Aprili tutapata wagonjwa 1,000 na kati kati ya mwezi Mei tutapata wagonjwa 10,000 lakini kila mtu akichukua nafasi yake, tunaweza kuvuka hicho walichotutabiria,” amesema Waziri Ummy.

Hakuna maajabu hapo wala miujiza ndio kwanza leo ni tarehe 9 Aprili. Tunaenda kuumia pakubwa. WHO wapo sahii.
Viongozi vilaza hawa sijuhi tumewatoa wapi..!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…