Waziri Ummy, Usipotoshwe maamuzi yako kuhusu ADDO na wafamasia mtawaumiza Watanzania

Naona baada ya hili bandiko Famasia na mafundi dawa wanaishia kutukana na kusonya bila kujibu hoja za msingi

Naendelea kukazia, Ikiwa kazi zao ni kutengeneza dawa na kemikali zingine kuzihifadhi na kuzisambaza je hii mandatory ya kutoa dawa kwa nini watu wanaohusika na wagonjwa wasizifanye?

Nawaheshimu wafamasia kweli akianza kukuchambulia paracetamol ilivyo kuanzia umbo,rangi hadi radha wako vizuri, nafikiri wanafaa kuingeneza zaidi kuliko kazi ndogondogo za kuigawa kwa wagonjwa.
 
Mteremko wa Addo umefutwaa mnaanza kulia liaa...!! No shortcut vinajaa rudini darasanii kama ambavyo mnasema hatuyajui magonjwa bhasi na nyie Dawa hamzijui vile vileee...
Ungechambua kitalaamu bwana kimasihara ,unataka kushindana na huyo Prof ,mbona andiko lake limekaa poa Sana Tena kiprofeshino.

Wewe umeandika huku una emotions itakuwa ni ego so umeona inashambuliwa ego.

Ila Nina Imani ume specialize kwa matunda kimasihara. Jinsi ulivyoandika umejiabisha Sana kwa huyu prof.kwanza umeandika Kama mtu anaimba taarabu kimapasho.

Am sorry Kama nitakuwa nimeku attach Ila just my perception Sina shida na wewe personal Bali ulichoandika
 
Ila kiukweli waafamasia wana hela kuliko madaktari. Hata mie ningesoma afya nilipenda Sana famasi ili nije nifungue duka la dawa aka famasi. Hata hapa napambana ili niifungue iyo famasi.

Na nilikataa kusomea udaktari Mana Nina utu Sana halafu napenda pesa kuliko unavyoweza kuwaza. Mie kutomtibu mtu eti Hana hela ni ngumu Sana so nitachukiwa na wenzangu
 
Mkuu Prof Koboko, hongera Sana kwa kuleta mada hii. Kusema kweli, Tanzania siasa hizi zinatuharibu Sana. Sasa, siasa za wafamasia na Maduka ya dawa kwa maana ya Maduka ya dawa muhimu na famasia zinastaajabisha Sana. Walifanya lobbying wakaja na Sheria ya ajabu ya ADDO ambayo kimsingi haina mantiki Wala uhalisia. Imagine Daktari aliyesoma kozi ya pharmacology kwa mwaka mzima, anazuiwa kuuza duka la dawa muhimu ati ili auze, Basi sharti asomee ADDO kwa muda wa wiki sita. Kwamba Wiki sita zinatosha kwa mtu kupata ujuzi wa dawa kuliko ujuzi alioupata kwa kozi ya mwaka mzima( 2 semesters)?
Na ajabu zaidi ni kuwa dawa hizo hizo anazozuiwa Daktari kuuza, Sheria inasema zisitolewe bila kibali( prescription form) Cha Daktari.
Kwa faida ya wasio jua, dawa hizi za binadamu ziko za Aina mbili.

1. Over the counter drugs; hizi ni dawa ambazo mgonjwa anaweza kutumia bila kibali Cha Daktari. mf Panadol, Magnesium n.k. Na dawa hizi huweza kutolewa kwa ridhaa ya mtu yeyote mwenye uelewa sahihi au kulingana na matakwa ya mgonjwa.

2. Prescribed drugs; Hizi ni dawa ambazo haziruhusiwi kutolewa bila kibali (prescription form) Cha Daktari. Na hizi ndizo dawa zilizo nyingi.

Chakushangaza, huku kwetu, Daktari huyu anayeidhinisha dawa flani itolewe, haruhusiwi kumiliki/ kuuza duka la dawa ati mpaka awe na cheti Cha ADDO😅.
Nchi ya ajabu Sana hii.
 

Well...katika Msingi wa Taaluma..Mfamasia ndiyo anatambua kuanzia dawa inavotengenezwa hadi inavyokuja kutumika kwa mtumiaji wa mwisho(mgonjwa)...kwa mantiki hiyo mchakato mzima hadi kwanini dawa fulani itumike kwenye Tatizo fulani la kiafya basi ni mfamasia anaweza toa maelezo sahihi zaidi ya kitaalam kuliko wataalam wengine wa afya.Hivyo fursa kwa wafamasia zinaanzia kwenye Viwanda vya dawa hadi Kwa watumiaji (hospitali na kwenye jamii)...Sasa hapa tunakuja kuwapata wafamasia ambao wanafanya kazi Viwandani....( Industrial Pharmacists).....wanaofanya kazi Hospitali ( Clinical and hospital Pharmacist)...waofanya kazi kwenye jamii ( Community Pharmacist)......... lakini pia wapo wafamasia wanaofanya kazi kwenye kampuni za Uingizaji na usambazaji wa dawa....bila kusahau wanao fanya kazi kwenye Mamlaka za udhibiti wa Ubora na ufanisi wa Dawa ... ...kulingana na mchanganuo huo majukumu huwa tofauti tofauti na ni sehemu ya taaluma pia !....Turudi Hospital & Community Pharmacy sasa ambako ndio kuna migongano ya ufanyaji kazi....Majukumu ya mfamasia ni haya
1)kuweka Kumbukumbu za dawa
2) Kuanisha mahitaji ya dawa kwa kipindi fulani mwaka au robo mwaka
3)kushirikiana na watu wa manunuzi katika kuagiza na kununua dawa sahihi kulingana na mahitaji ya hospitali/ Community Pharmacy
4) Kutoa dawa na vifaa tiba kwaajili ya kuhudumia wagonjwa hizi kazi utakutana nazo "Store za dawa"
5)"KUSIMAMIA MATUMIZI SAHIHI YA DAWA"" ...Daktari anapo prescribe dawa ...jukumu la kuangalia usahihi wa dawa kulingana na tatizo na dozi sahihi linabaki kwa "mfamasia"....Kifupi kazi ya kudispense ni ya watu wa famasi sio ya Daktari...na hapa ndio tatizo linapokuja Daktari anataka ""aprescribe yeye na kudispense yeye""" sio kazi ngumu lakini sio sehemu ya majukumu yake.
6) kutengeneza dawa hospitali /Community Pharmacy. ( compounding)
7)Kuelimisha watumishi wengine wote wa hospital juu ya matumizi ya dawa.
8)kutoa taarifa kuhusu madhara ya muda mfupi na muda mrefu yatokanayo na matumizi ya dawa....!
9) Kutambua muingiliano wowote wenye athari hasi kati ya dawa na dawa au dawa na chakula.

Kifupi ndio majukumu hayo hasaaa kwenye mazingira ya Hospital na Pharmacy za mitaani.
 
Wewe naye ni fake tu, daktari asijue namna dawa inayotolewa wakati ndiye anayejua ugonjwa na wadudu wake na kutoa Orders kwa Mfamasia atoe dawa leo unasemaje hajui?
profesa mbona unatoa maboko
😂😂😂
 
Acha Ulongo, hakuna sehemu Pharmacist anakosomea kutibu. Uko sahihi kuwa as Drs, wanafundishwa Basic pharmacology hata hivyo, kuuza dawa mtu hahitaji knowledge ya kiwango Cha Pharmacist ndio maana mkaona wiki sita za ADDO zinatosha kum equip mtu na basic knowledge ya kuuza dawa.
Pili, sio kweli kuwa pharmacist wanasomea kutibu. Tunaposema kutibu(Management of disease) tuna maana ya investigations( Vipimo) na treatment ( ambayo inaweza kuwa Dawa, Upasuaji au ushauri mahsusi), hapo mfamasia anaingia kwenye kipengele kimoja tuu Cha Dawa.

Tatu, ufahamu wa wafamasia kwenye magonjwa ni mdogo Sana hauwezi kulingana na robo ya ufahamu wa Daktari. Mna basic knowledge ya Anatomy, physiology, pathophysiology of different disease conditions, Pathology even Microbiology ukilinganisha na huyu Dr.
Ndio sababu Dr anabaki kuwa Kiongozi kwenye timu ya kutoa huduma.
 

Ungefuatilia lengo la kuanzishwa ADDO lilikuwa nini hasa!! ...Kwanini Daktari hatakiwi maabara wakati amesoma Parasitology??....Daktari au tabibu shughuli yake ni kuorder vipimo vya kufanyikaa ila mambo ya maabara wanabaki nayo lab scientists ...yeye anasubiri majibu.....ukipata jibu namnaa mgawanyo wa majukumu unavokuwa ndio utaelewa ...kuwa daktari akiprescribe .....mambo ya utoaji na usahihi wa dawa kwa mgonjwa wanabaki nayo wafamasia...Daktari akikosea nani wa kutambua kosa kama yeye anataka kuprescribe na kudispense yeye mwenyewe?..
 

Itoshe kusema na ufahamu wa daktari kwenye dawa ni mdogo sana sababu ana basic knowledge ya Pharmacology tuu.

ADDO Ilianzishwa kukabiliana na uhaba wa wafamasia Nchini Tanzania na sio kwamba inatambulika Dunia nzima...Sasa wafamasia wamekuwa wengi ....hatuna uhitaji wa Addo tena ndio maana wizara imesitisha sasa...kila mtu afanye majukumu yanayo muhusu kwa usahihi zaidi...tutapunguza pia Vifo na madhara yatokanayo na matumizi yasiyo sahihi sana ya dawa
 
So leave the profession about medicines to pharmacists, they are kings of medicines, nobody else... kila mtu afanye majukumu huku wakishauriana (wafamasia, manesi, madaktari na maabara) thats team work..
My point is mfamasia anaweza kudiagonis, akampima mgonjwa na kumpa dawa lakini HIYO SIO KAZI YAKE, Hivyo ASIIFANYE. DAKTARI HIVYO HIVYO, ATAFANYA YA KWAKE IKIWEMO KUPRESCRIBE DAWA, LAKINI IKIFIKA KUDISPENSE HILO LIPO KWA MTAALAMU WA DAWA
 
Prop yupo sahihi kwa walofanya kazi hospitali kazi nyingi za utoaji dawa zinafanywa na manesi baada ya kukotoa mahitaji yalioagizwa na madaktari,na kwenda kuchukua famasi au stoo waliko wafamasia na manesi wanao tunza stoo.
Nadhani ni kwasababu ya uchache wa wafamasia.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shida ni njaa madaktari wengi wamepishana na pesa..hivyo wakiona kada flani inapiga pesa wanakimbilia kujibanza hapo.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1.Nesi anagawa dawa kulingana na prescriptions za daktari.
2.Mfamasia anaweza kugawa dawa kwenye hospitali kubwa,ambako advanced knowledge inahitajika.

NB: Tofautisha kugawa na kutoa dawa.
Tatizo unazungumza kutoka na unachokiona hapa tanzania angalia Nje
 
Kumbe ndo maana huku kwetu mtu akiwa na duka la dawa huitwa daktari
 
Tanzania degree ya pharmacy inasomwa miaka 4 na degree ya udaktari ni miaka 5. Tuache kuandika bila kufanya utafiti japo kidogo wa kile tunachoandika! Acha upotoshaji!
 
Wewe bwana mimi ni Mtanzania ninayeishi South Africa, nimesajiliwa huku ingawa nafundisha madaktari and soon nitaanza kufundisha huko na pia Tanzania namiliki hospitali. Wanaonijua wapo humu humu hawaongei.

Shut up!!
Fanya utafiti kuhusu course content ya pharmacy ya Tanzania kabla hujaandika kuhusu pharmacists na kushusha thamani ya taaluma ya pharmacy.
 

Unapotosha sana wewe! Pharmacist anasoma pharmacotherapy akiwa mwaka wa nne, ndani ya hiyo course kuna components za pathophysiology na kabla ya hapo amesoma physiology, pathology, microbiology na biochemistry sasa unaposema hawezi kubaini ugonjwa unapotosha umma ingawa diagnosis sio kazi yake lakini haina maana kwamba ana zero idea.

Besides kuna thousands of over the counter drugs ambazo Pharmacist anaweza kutumia ku manage minor ailments ambazo sio lazima mgonjwa afike kwa MD ili atibiwe.

Na ndio kazi ya community pharmacies kuwa ni primary health facility ili kupunguza mlundikano wa wagonjwa wenye cases ndogo tu ambao wata clog the hospitals.

Pharmacist ana kazi kubwa ya kumlinda mgonjwa from drug errors ambazo clinician anaweza kuwa amefanya, pia kuna issue ya drug interactions ambazo zinaweza kutokea ambapo ni kazi ya Pharmacist ku screen hizo potential interactions kama imetokea clinian ame prescribe dawa zenye interactions na hiyo inatokea in practice.

Tuache dharau kwa taaluma za watu wengine!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…