Waziri wa Elimu na TAMISEMI, ni sawa Wanafunzi Shule za Serikali kuambiwa waende na dissecting kit na vitabu vya tahasusi?

I totally understand...

Lakini hivi ndivyo mambo haya yanavyopaswa kwenda..?

Tatizo liko wapi?

Je unadhani tatizo ni vipaumbele (priorities) huko serikalini? Au siyo...?

Nimeibua mjadala huu kwa staili hii si kwa sababu yoyote isipokuwa kwa kuwafikiria na kuwasaidia ndugu zetu wengine kutoka familia fukara wasio na uwezo wa kujikakamua kupeleka watoto wao shule binafsi kama tunavyojikakamua sisi wengine...

Huyu kwangu amesoma private school. Kuchaguliwa kwenda shule za serikali kumekuja kwa sbb tunajua hata waliosoma private schools, huchaguliwa shule za serikali kwa masomo ya A'Level Secondary Education...

Ni decision ya mzazi aende huko au aendelee na mkondo wa private. Mimi niliona acha nipumzike kidogo, asome tu ya serikali kwa level hivi kwa sbb ni boarding...

Ile kuona maelekezo haya, ikanitia shaka sana. Kwamba mtoto aende na boksi la vitabu. Ndipo nikaibua mjadala huu kwa staili hii ili wadau wa elimu tujadiliane. Tujue tatizo ni nini? Kama nchi tumejwama wapi? Tufanyeje ili twende kuzuri...?

Kwa hiyo ishu ya gharama kwangu wala siyo tatizo. But why these things in public schools...?.

Asante
 
Apa nimekuelewa mzazi
 
Hadi nakuhurumia unavyojitahidi kuwaelewesha hawa viumbe[emoji23] tulia tu kunywa maji ulale it's too complicated! Bongo wajinga wengi mno.

Hapana, tuendelee kujadiliana...

Tunatofautiana upeo, ufahamu na uelewa...

Kila wazo na mchango wa mtu tuuheshimu maana that's how they see things...

Huu ndiyo uhuru wa majadiliano alioukataa Mwendazake John Pombe Magufuli...

Angekuwepo, JF management ingeshaamuriwa kusitisha mjadala kwa sababu unajadili mapungufu ya serikali...!!!
 
Hivi ni nani aliwambia huko. A-Level elimu inatolewa bure?!

Kwanza Elimu Bure siyo sela ya taifa.
Ndiye maana tunauliza kwa sababu hatujawahi kusikia neno kulipa ada zaidi ya elimu bure. Na Kama kuna kulipia ada ni kwa shule zote kwa kutumia mwongozo au ni kila shule ina gharama zake na mwongozo wake.

Embu tufafanulie vizuri.
 
Serikali yetu haiko serious na elimu, shule hazina vitabu/vifaa hata zile shule kongwe zilizokua na vitabu/vifaa leo hazina. Nakushauri umnunulie mwanao vitabu na vitu vingine vitakavyoweza kumsaidia.
Hii serikali haiaminiki sababu haijali ubora wa utoaji wa elimu kwa wanafunzi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nijuavyo mimi kwa advance inahitaji mtoto walau kuwa na vitabu vya kutosha tena kwa sayansi yahitaji kujiandaa.Lakini kama utaona private ni bora nayo sawa!

Sent from my Nokia 2.4 using JamiiForums mobile app
 
Siasa zimetawala sana kwenye Elimu...
Serikali inatakia kununua vitabu ila hivyo vitabu kuna shule hakuna, kuna muda inabidi mwalimu aingie mfukoni kununua vitabu, ni changamoto sana.
 
Pitia comment zote ujione ulivo mbwiga umekuja kutafta kuungwa mkono kwa upuuzi wako?
 
1.Understanding biology yenye visual DVD inauzwa 350,000 ambayo haina DVD inauzwa 80,000
2. Biological science inauzwa 40,000
3. Martin Rowland inauzwa 150,000
CHEMISTRY
1. Ramsden for advanced level inauzwa 50,000
2. Rambert inauzwa 70,000
3. Organic chemistry TIE 15,000
4. In organic chemistry TIE 15,000
5. Chand XI inauzwa 35,000
6. Chand XII inauzwa 35,000
7. Kuna pamplets za akina ngaiza na issue boy

GEOGRAPHY - SIKUSOMA SO SIJUI


Lakini niwaambieni vitabu vya advance ili mwanao akamilike ktk field ya sayansi vinahitaji uwe na takribani 500k ama uwe navyo vichache uwe unagongea shule km wenzako so wabinafsi!
Kwa ufupi kuna haja ya serikali kupitia upya mitaala na kuchagua TEXT &REFERENCE BOOKS zinazohitajika na kuzipeleka kwenye shule zake zote. Maana mjue kuna familia huko vijijini hawana chochote cha kuweza kuwaingizia hata 100,000 kwa mkupuo na wana mtoto, mtoto mpaka adhaminiwe na diwani au kanisa!
WAO WALISOMA BURE NA KULIPIWA NAULI WKT WA NYERERE KWAHIYO WAFANYE HIVYO HIVYO KWA WENGINE
 
wale tuliokuwa tuna lala chini mikono juu, incase elimu ya advance ni gharama sana mimi nilikuiwa siend shule miezi miwili, watatu natokea mwezi mmoja nautumia kibaha, mwingine minaki , na mwenge pre medic na mzumbe motto, gharama niliyotumia kwenye tution ni kama nimesoma private tu, kuhusu vifaa hata kwetu vilikuwepo
ingawa ni miaka zaid ya nane nyuma
, ila dawa ya chooni na mifagio hilo jipya
 
@The Palm Tree ,mkuu umeongelea mengi mazuri sana !!!! Na lawama zote lazma SERIKALI iwajibike tu na lazma serikali iajiri walimu ili watoto wasome kwa usawa zaidi!!!


Na wakati mwingine serikali inakaa kimya ili watoto wengi wafeli zaidi halafu ifurahi yenyewe
 
Usimnunulie vitabu mtoto wako sawa Rafiki yangu mpendwa
Serekali itamnunulia mtoto wako mzuri sana

Kanywe bia tuu
 
Kodi anazolipa mzazi ikiwemo tozo za miamala zinaenda wapi ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…