KERO Waziri wa Elimu Prof. Mkenda, tueleze mitihani ya kila wiki kwa kuwalipisha wazazi mchango wa Tsh. 1,500 kila Ijumaa , ndiyo sera uliyoiruhusu?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Katika vitu vinaudhi wazazi ni watoto wao kupigwa.Inaumiza sana.Buku jero kitu gani?Tutatoa tu ila wasipige watoto wetu.Unakuta asubuhi mtoto anakua mnyonge anasikilizia umpe 1500 ya mtihani,nauli 1000 na chakula 1000.
Kufauru ni galama wacheni malalamiko kupanua miguu na kuzaana mnaona rahisi ila kusomesha mnalalamika
 
Naamini kama umeoa basi mahari mwanamke alijilipia sio kwa upuuzii huu sasa ulipiwe na mchepuko wa mkeo ? Wajibika tafuta hela....kama elimu gharama mtoe ....jaribu ujingaa usituchoshee
 
Umenena vyema
 
Mtoto wako wajibika
Wewe unataka mtoto wako alipiwe na nani?
Ile mitihani inahitajika gharama za stationery a
Kulipa 1500 Kwa week hadi ufungue Uzi wa kulalamika
Kwahiyo unataka kuwaibia wazazi kwa njia hii!
 
Wewe ni mzazi?

Jambo hili ni la waziri?

Ni kwamba jambo hili linaishia kwa vikao vya wazazi wa shule husika.

Kama wewe huna uwezo; pitia vikao vya wazazi.
Sa km huna uwezo kwann umezaa tuache kudekeza wajinga sa km huna uwezo kwann umezaa afu unakuta ayo yanayosema hayana uwezo ndo unakuta yanazaa km paka watoto kibao

Kwaiyo km huna uwezo unataka nani akusomeshee mchukue uyo mwanao mkachome nae kikaa mponde mawe muishi
 
Km unaweza au unawaza kuzaa jua pia kuna majukumu na maitaji ya mtoto na itaji moja wapo la mtoto ni kusoma
so km ujui majukumu ww km mzazi bas ukutakiwa kuzaa
Lakin pia mtoto akipata elimu ni faida kwa familia na ukoo kwa ujumla somesha kwa maendelea ya mwanao familia yako na yake
 
Pole sana mzazi ila wenzio wanalipwa ada sh million Kumi ( 10,000,000) Kwa mwaka pale feza schools wewe unalia 78000!!! Kwa mwaka!? Kwa mwaka Kuna ijumaa 52 x 1500= 78000/ mwanao anafanya mtihani hata Hilo hutaki!? Pole Sana ndugu !! Kama elimu ni ghali jaribu ujinga wamesema wahenga
 
Wewe ni mmoja kati ya watu mnaofanya JF ionekane kituko!
1500 sio pesa ndogo, kuna Watanzania hawawezi kuwapa watoto wao hiyo pesa kila wiki. Kama familia yako inamudu kufanya hivyo shukuru sana.
Inafahamika sana ila hapa nashuka na mtoa mada sio hao walala juu ya vitanda njaa.
Mtoa mada hapa kapuyanga.
Namshauri awe amahudhuria vikao vya shule la sivyo tutakuwa tunaonekana wote ni viazi vitam kisa mtu mmoja asiyetaka kucheza nafasi yake.
Haya mambo hujadiliwa kwenye vikao/mikutano ikiwa walimu wanashare na wazazi na kutaka maon yao namna bora ya kutaka wanafunz wafanye vizur
 
Mshahara ni wa vipindi vya darasani na mazoezi na mitihani iliyopo kwenye ratiba.
Mitihani ya sasa ni very competence mjomba,
Mama yangu ni mwalimu Enzi hizo na alitulipia tusome shule jirani.

Aisee inasaidia sana mana mwalimu anajitoa kwa moyo wote.
Pia hayo ni makubaliano yenu kwenye vikao vyenu.Ungekataa kule kwenye vikao na sio kuwachoma walimu hapa.
 
Tunataka tamkola serikali. kama ni rasmi, wazazi tujue, kama ni miradi ya walimu tujue! Issue siyo kulipa, issue je unamlipa nani? Mradi wa mwalimu?
Halafu jamaa wewe! Ukute kila wiki inakunywa pombe ya 10,000/=. Shame!! Ukute unahonga 50,000/= kwa mwezi! Shame. Na mtu kama wewe unaona uchungu kuspend 1,500/= kwa mwanao. Hebu jitafakari. Huyo waziri unayemlilia ukute wa kwake wako Marekani
 
Mkuu umemaliza mjadala kwa hii comment
 
Walimu wa tz ni vilaza sana ndiyo maana wanafunzi wanahitimu wakiwa hawana uwezo wakushindana na wenzao afrika mashariki.Mleta mada kauliza kama ni sera ya wizara au ni mradi wa walimu kula pesa za wazazi?walimu wa tz mbulula sana ndiyo maana yanatumika kama toilet papers kwenye uchaguzi
 
Inaruhusuwa useme mwanangu asifanye mitihani hiyo aondolewe.....1500 tu inakutoa roho Tena Kwa week!! utakuwa na roho mbaya sana kwani hata kama walimu wakila kinakuuma nn? Wakati unazaa ulitegemea nani akulele watoto? Nyie ndo wale mwlm anakaa na mtt mwaka mzima lkn hata soda ya 500 humpi ...halafu unalia mtoto Hana matokeo mazuri.....Bomba linalopitisha Maji haliweki kutu....lisilopitisha kutu huota... Roho mbaya na uchoyo vimekujaa
 
Mtoto wa darasa la pili anachangia 2000 kwa mitihani miwili(copies) yenye gharama halisi ya urudufishaji ni Tsh 200 unaona ni sawa?
Kwani Mwlm naye akinywa soda ya 1000 kwenye 2000 inakuuma? Mbona beer mnalipia machawa na michepuko?
 
Watanzania elimu imeshakuwa mzigo, Hivi kuna mtu aliesoma shule za msingi za serikali asifanye mitihani ya kujipima akiwa ni darasa la 6 na 7?

Nilivoingia darasa la saba tulianza mitihani ya jumamosi hadi namaliza shule sept 14 na 15

500 x wiki 32 = Tshs 16,000 hii ni mwaka 2004
 
Usiwe serious sana na maisha yaani unaona shida hata mwalimu Alibaba hiyo 700.
Lakini bar, michepuko, Kwa manabii, pesa mnatoa
Kumpa mwalimu tip unafungua Uzi ili abanwe umharibie kazi.
Sasa kama mtoto mitihani kafanya tatizo nini
Inashangaza Mkuu lkn huyuhuyu ataenda lodge nusu saa 25,000 imekata Kwa mchepuko hawara ila ajabu Buku tu Kwa mwlm inamuuma
 
Tuliza wenge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…