KERO Waziri wa Elimu Prof. Mkenda, tueleze mitihani ya kila wiki kwa kuwalipisha wazazi mchango wa Tsh. 1,500 kila Ijumaa , ndiyo sera uliyoiruhusu?

KERO Waziri wa Elimu Prof. Mkenda, tueleze mitihani ya kila wiki kwa kuwalipisha wazazi mchango wa Tsh. 1,500 kila Ijumaa , ndiyo sera uliyoiruhusu?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Mkuu tafadhari wewe unafanya kazi gani? Kwasbb naona uko ignorant sana kuhusu masuala ya elimu kama wewe sio boda boda utakua mlinzi au mkulima.
Ila wewe ni so naive!Kazi yangu inahusiana nini na kuhoji michango holela na ya kihuni mashuleni tena kwa watoto wa darasa la kwanza hadi la pili?Kijijini kwenu mtu akiwa mdadisi/wa kuhoji ndiyo mnamuita ignorant?Bure kama nini sijui wewe!
 
Kwahiyo hao walimu huo muda unatadhani anawalipa nani? Tusiwashushe morali wenye taaluma zao,kuliko mwanao arudishwe home mapema akibaki shule na kupata cha ziada unaona ni vibaya? Hiyo ya Harusi nimetolea mfano tu ila Elf 72 kwa mwaka kwa manufaa ya mwanao unaona ni nyingi? Angekuwa anasoma private? Hao Waalimu wanataka mwanao awe busy muda wote, wanaweza kuamua kuacha na kufuata utaratibu wa kawaida wa mitihani ya mihura,na wakaendelea na mishe zao za kutafuta kipato cha ziada,mwanao ndiyo ataathirika.
Siku ya kazi unaniuliza huo muda wanalipwa na nani?Wewe ni kichaa.Kazi yake anayolipwa mshahara anataka alipwe tena?Double wages/salaries?Tuliza kichwa,bangi haikufai.
 
Ww , kuna watu wanapitia mambo magum na bado wazazi wanapambana mtoto akapate hicho kidogo shule.
Kama ww umebarikiwa mshukuru Mungu sana
Na usitegemee kila mzazi atakua na hiyo 1500 kila jumatatu au ijumaa kwa ajil ya mtihani
Ila pesa ya vocha beer za ulinzi shirikishi, za kuzoa takataka bill za maji luku, usafiri anazo, lakini likija suala la elimu 1500 kwa wiki manaake sh 200 kila siku ni issue, hiyo ni neglegence ya hali ya juu.
 
Ila pesa ya vocha beer za ulinzi shirikishi, za kuzoa takataka bill za maji luku, usafiri anazo, lakini likija suala la elimu 1500 kwa wiki manaake sh 200 kila siku ni issue, hiyo ni neglegence ya hali ya juu.
Usiendeshwe kwa hisia hasi/potofu.Uliwaona wangapi wanafuja hela kwa bia na anasa nyingine?Unazijua hali za uchumi wa kila familia hapa nchini?Au mkishaiba 2000 za watoto mnajiona mambo bien?Bure beleshi.
 
Kila Ijumaa wazazi tunadaiwa shs 1,500 kama ada ya mtihani. Je walimu wanafanya haya kwa ruhusa ya Wizara kama examination policy?

Mtoto asipoleta hela anapigwa. Tupelekane mahakamani na walimu wako kwa kuwapiga watoto bila sababu? Kama mtoto hakupewa hela, unampiga ili hela aitoe wapi?

Au Ni miradi ya waalimu kujiongezea kipato?
Wazazi watashindwa

Nitakupa ushahidi kama ukihitaji uthibitisho
Muongozo ni kwamba, mchango wowote unaotolewa shuleni unapaswa kuridhiwa na wazazi katika vikao vya wazazi shuleni.

Kwahiyo kama huwa hauhudhurii vikao, basi uliza wazazi wenzio. Usiporidhika, nenda shuleni.
 
Siku ya kazi unaniuliza huo muda wanalipwa na nani?Wewe ni kichaa.Kazi yake anayolipwa mshahara anataka alipwe tena?Double wages/salaries?Tuliza kichwa,bangi haikufai.
Huo utaratibu wa kuwafanyisha mitihani kila ijumaa ni wa wizara? Au ni nyie wazazi kwenye vikao vyenu mmekubaliana kuwa keep watoto wenu busy? Hata kama ni muda wa kazi,wewe unaangalia kopi tu sijui mia 2 ,lakini huyo mwalimu anapoteza muda kusahisha mitihani hiyo unataka asinywe hata soda afanye bure? Bila shaka na-argue na mtu mbumbumbu sana na hii itakuwa last comment maana naona napoteza muda kumuelimisha mpumbavu,bora ungekuwa mjinga,maana mjinga huwa anaelewa ila mpumbavu ni ngumu sana kuelewa.Kama huwezi kulipa elf 72 kwa mwaka kwaajili ya mwanao,hizo bao vaa condoms.

Poleni sana Waalimu mnakutana na uncivilized wengi sana huko kwenye kazi yenu,
 
Enzi zetu Mitihani ya Kila weekend mchikichini ndio ilisababisha tukatoboa aisee na Kila mtihani unachangia hapo tena ni Mwalimu wa mtaani, walimu shule walikuwa hawana hata muda wakutupa Mitihani. Changia tuu dogo atoboe sie wengine na akili zetu mgando Bila kuchangamshwa na Ile Mitihani tusingekuwa watu Leo.
 
Muongozo ni kwamba, mchango wowote unaotolewa shuleni unapaswa kuridhiwa na wazazi katika vikao vya wazazi shuleni.

Kwahiyo kama huwa hauhudhurii vikao, basi uliza wazazi wenzio. Usiporidhika, nenda shuleni.
Kwa uzoefu wangu wa kipelelezi,huwa hakuna vikao huru vya wazazi na walimu.Zaidi ni walimu kwa kushirikiana na kamati majambazi kupitisha agenda zao tamutamu(za kuwafaidisha wao)kwa kutumia mihutasari yenye mahudhurio ya wazazi/walezi.Wazazi huwa wanaburuzwa,kupewa lugha za vitisho na agenda kupita kihunihuni tu.
 
Enzi zetu Mitihani ya Kila weekend mchikichini ndio ilisababisha tukatoboa aisee na Kila mtihani unachangia hapo tena ni Mwalimu wa mtaani, walimu shule walikuwa hawana hata muda wakutupa Mitihani. Changia tuu dogo atoboe sie wengine na akili zetu mgando Bila kuchangamshwa na Ile Mitihani tusingekuwa watu Leo.
Viwango viwe rafiki.
 
Mkuu huo ni utaratibu wa zamani sasa hivi mitihani yote inafanyika kuanzia na wa hesabati asubuhi mpaka wa maarifa jioni hiyo ratiba na ofisa elimu kata anaijua vzri tu.
Shule unayofundisha ww lakini shule nyingi wanafanya mitihani miwili na wanaandikiwa maswali ubaoni.
Ila pesa ya vocha beer za ulinzi shirikishi, za kuzoa takataka bill za maji luku, usafiri anazo, lakini likija suala la elimu 1500 kwa wiki manaake sh 200 kila siku ni issue, hiyo ni neglegence ya hali ya juu.
Hivi we unayajua maisha ya kimasikini kabisa au unasema tu maji, umeme.
 
Shule unayofundisha ww lakini shule nyingi wanafanya mitihani miwili na wanaandikiwa maswali ubaoni.

Hivi we unayajua maisha ya kimasikini kabisa au unasema tu maji, umeme.
Kwani mkuu wanaisha gizani, Tanesco inawapa umeme wa bure au Dawsco hawapelekee bill za maji,? Takataka zao azikusanyi wanaziweka wapi? Medical bill zao nani anawalipia au hawauguwi? Kuna vitu basics vya gharama lazima na elimu wa iweke tu.
 
Kwani mkuu wanaisha gizani, Tanesco inawapa umeme wa bure au Dawsco hawapelekee bill za maji,? Takataka zao azikusanyi wanaziweka wapi? Medical bill zao nani anawalipia au hawauguwi? Kuna vitu basics vya gharama lazima na elimu wa iweke tu.
Hivi we unayajua maisha ya watanzania vizuri kabisa
 
Sio mradi wa walimu bali ni makubaliano ya wazazi katika vikao, kuomba watoto waongezewe ufaulu..... Hivyo walimu ni watekelezaji.

Kama unachukua hatua chukua tu, hakuna serikali itakuja kukupa tamko kwenye hilo.
hatujawahi kuwa na mkutano kama huo, actually wote wanalalamika. Ni watu masikini, hawawezi kumudu. Mimi namudu lakini sitaki miradi ya walimu ya kijinga! (and actually ni mtoto simjui as such, namsaidia tu. alikuja kufanya kazi za nyumbani akiwa mdogo nikaamua kumsaidia asome maana alikuwa at the age of 10 yrs na hakuwa amewahi kwenda shule, eti wanamleta kufaya kazi za ndani, nikasema siwezi kutenda kosa kama hilo, nikampeleka shule. sasa huu usumbufu wa kijinga siutaki)
 
Mzazi nenda shule kamuone mkuu wa shule mwambie "sitaki mwanangu afanye hiyo mitihani, sitaki kuombwa hiyo hela wala sitaki mwanangu aguswe"

Pia usisahau kwenye vikao vya wazazi chukua mic sema hautaki hiyo mitihani haukubaliani na hilo swala hivyo hautatoa pesa
Wakuu wenyewe ndio chapuo la haya yote. Yaani ni sawa kesi ya Ngedere umpelekee nyani. Ni hivi wazazi wamegawanywa wapo walio upande wa wakuu na wengine ni neutral hawajui wanataka nini si unajua akili za mtanzania ( ujinga).
Chini ni kapeti ni kuwa kuna maafisa Taaluma wanashinikiza wakuu waondoe zero la sivyo vibarua vya ukuu vinaota nyasi na kupewa wengine. Wakuu wanaweka mikakati ya kupandisha ufaulu na hii bila ya pesa hsiwezekani kilichopo ni vikao na wazazi kwa kuwatafuta wanaojiweza pembeni sasa wasiojiweza ndio kimbembe kinapoanzia kwa watoto hao kupokea kichapo cha haja na kuundiwa mizengwe ya kufukuzwa shule kwa makosa ya kubambikiwa. Hali si shwali kwa wasiojiweza kwa sasa.
 
Back
Top Bottom