Waziri wa Utumishi aanzisha mfumo wa kielekroniki unaoitwa "Sema na Waziri" kupoke malalamiko ya watumishi na wananchi

Waziri wa Utumishi aanzisha mfumo wa kielekroniki unaoitwa "Sema na Waziri" kupoke malalamiko ya watumishi na wananchi

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
WAZIRI wa Nchi, Ofi si ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa, amesema serikali haitomvumilia mkuu wa idara katika taasisi ya umma atakayesababisha mtumishi akose stahili yake au mwananchi kukosa huduma bora.

Mchengerwa amesema hayo Dodoma wakati akifungua Kikao Kazi cha Mwaka cha Wakuu wa Idara za Utawala na Rasilimaliwatu Katika Utumishi wa Umma.

Aliwataka wakuu hao kutekeleza majukumu yao kikamilifu ili kutekeleza agizo la Rais Samia Suluhu ambaye ameelekeza viongozi katika taasisi za umma kutenda haki kwa watumishi walio chini yao na wote kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mchengerwa alisema atakapofanya ziara katika maeneo yao, hategemei kukuta foleni ya wananchi wakisubiri huduma.

“Mimi, Naibu Waziri wangu na watendaji wa ofisi yangu tukifanya ziara katika taasisi yako, hatutegemei kukuta foleni ya wanananchi wakisubiri huduma pasipo na matumaini,” alisema.

Mchengerwa alisema ameanzisha mfumo wa kielektroniki unaoitwa ‘Sema na Waziri wa Utumishi’ unaotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni ili kutoa fursa kwa watumishi na wananchi kuwasilisha malalamiko.

“Kupitia mfumo huu, nitakuwa na uwezo wa kuona malalamiko yanayowasilishwa popote nitakapokuwa na kufanya ufuatiliaji wa namna yalivyofanyiwa kazi na ofisi yangu,” alisema.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Festo Dugange, alisema Rais Samia amekuwa akisisitiza mara kwa mara matokeo chanya katika utekelezaji wa majukumu ya watumishi kwenye maeneo yao ya kazi.

Alisema ili matokeo hayo yaonekane, wakuu wa idara za utawala na rasilimaliwatu wanapaswa kusimamia utekelezaji wa majukumu ya watumishi wa umma kwa ufanisi.
 
Ni hatua nzuri ila tutampima kwa utekelezaji na sio uanzishaji wa huu mfumo.

Ili afanikiwe, mfumo uruhusu watu kutoa maoni au taarifa bila kulazimika kujisajili au kutumia majina yao halisi vinginevyo anaweza asifanikiwe kupata anachokusudia kutoka kwa walengwa( watumishi na wananchi).

Wengine nao sio vibaya wakaiga.
 
"Sema na Waziri" umeanzishwa, halafu anasema utazinduliwa hivi karibuni. Hapo sijaelewa.
 
Ni hatua nzuri ila tutampima kwa utekelezaji na sio uanzishaji wa huu mfumo.

Ili afanikiwe, mfumo uruhusu watu kutoa maoni au taarifa bila kulazimika kujisajili au kutumia majina yao halisi vinginevyo anaweza asifanikiwe kupata anachokusudia kutoka kwa walengwa( watumishi na wananchi).

Wengine nao sio vibaya wakaiga.
Ww mpaka Mbowe awe raisi ndio utakuwa huna kwere
 
Ni hatua nzuri ila tutampima kwa utekelezaji na sio uanzishaji wa huu mfumo.

Ili afanikiwe, mfumo uruhusu watu kutoa maoni au taarifa bila kulazimika kujisajili au kutumia majina yao halisi vinginevyo anaweza asifanikiwe kupata anachokusudia kutoka kwa walengwa( watumishi na wananchi).

Wengine nao sio vibaya wakaiga.
Kabisa aisee huyu jamaa yupo vizuri
 
Waziri mmoja na naibu wake wapokee malalamiko ya watumishi nchi nzima??

Au ndio yatapitia kwa watendaji waya-filte ndio wafoward kwa waziri, na hapo kuna genuine issues zitapotelea hapo
 
Mchengerwa alisema ameanzisha mfumo wa kielektroniki unaoitwa ‘Sema na Waziri wa Utumishi’ unaotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni ili kutoa fursa kwa watumishi na wananchi kuwasilisha malalamiko.

“Kupitia mfumo huu, nitakuwa na uwezo wa kuona malalamiko yanayowasilishwa popote nitakapokuwa na kufanya ufuatiliaji wa namna yalivyofanyiwa kazi na ofisi yangu,” alisema.
Hongera sana Waziri hili ni jambo zuri sana, utaibua uchafu mwingi ambao watumishi walikosa pakuusemea ukizingatia watumishi wako hapohapo wizarani wamejaa vitisho kwa watumishi toka mikoani na wilayani
 
WAZIRI wa Nchi, Ofi si ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa, amesema serikali haitomvumilia mkuu wa idara katika taasisi ya umma atakayesababisha mtumishi akose stahili yake au mwananchi kukosa huduma bora.

Mchengerwa amesema hayo Dodoma wakati akifungua Kikao Kazi cha Mwaka cha Wakuu wa Idara za Utawala na Rasilimaliwatu Katika Utumishi wa Umma.

Aliwataka wakuu hao kutekeleza majukumu yao kikamilifu ili kutekeleza agizo la Rais Samia Suluhu ambaye ameelekeza viongozi katika taasisi za umma kutenda haki kwa watumishi walio chini yao na wote kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mchengerwa alisema atakapofanya ziara katika maeneo yao, hategemei kukuta foleni ya wananchi wakisubiri huduma.

“Mimi, Naibu Waziri wangu na watendaji wa ofisi yangu tukifanya ziara katika taasisi yako, hatutegemei kukuta foleni ya wanananchi wakisubiri huduma pasipo na matumaini,” alisema.

Mchengerwa alisema ameanzisha mfumo wa kielektroniki unaoitwa ‘Sema na Waziri wa Utumishi’ unaotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni ili kutoa fursa kwa watumishi na wananchi kuwasilisha malalamiko.

“Kupitia mfumo huu, nitakuwa na uwezo wa kuona malalamiko yanayowasilishwa popote nitakapokuwa na kufanya ufuatiliaji wa namna yalivyofanyiwa kazi na ofisi yangu,” alisema.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Festo Dugange, alisema Rais Samia amekuwa akisisitiza mara kwa mara matokeo chanya katika utekelezaji wa majukumu ya watumishi kwenye maeneo yao ya kazi.

Alisema ili matokeo hayo yaonekane, wakuu wa idara za utawala na rasilimaliwatu wanapaswa kusimamia utekelezaji wa majukumu ya watumishi wa umma kwa ufanisi.

Ule wa wizara ya sheria na katiba uliishia wapi?
 
Back
Top Bottom