Mambo ni magumu kwake:Dkt. Gwajima D njoo huku kuna issue
View: https://www.youtube.com/watch?v=xtinj83xrDo
Tumsamehe maana
View: https://www.youtube.com/watch?v=4P27_JwV6F8
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mambo ni magumu kwake:Dkt. Gwajima D njoo huku kuna issue
Dkt. Gwajima D njoo huku kuna issue
Tunahitaji waziri na wizara yake ya Afya watuambie kwann kadi iandikwe haiuzwi na Bado inauzwa!?Sio huko tu mkuu.
Hospitali nyingi wanauza kadi za clinic.
Nilishuhudia hii Chanika hospitali ya nguvu kazi. Wanaambiwa kadi zimeisha na kuelekezwa sehemu ya kwenda kununua, nje ya jengo la hospitali.
Hiyo inayonunuliwa imeandikwa "Haiuzwi'
Hii nchi kwa sasa ina ujinga mwingi wakutojali.
Watu kama hao utazani wanaishi Nchi jirani au hawana ndg wanao kumbana na kadhia hii au hawazai kabisa.Wale Wa Lumumba FC Wanapita Kimya Kimya Tu
Mkuu soma vizuri aliesababisha nikajua ni muhanga mwingine sio Mimi na nikauliza watu kadhaa ndo wakaniambia na hiyo tofauti ya bei ya kuzaa mtoto wa kiume na wakike.Wewe Kwa nini ulitoa buku 10 badala ya kumripoti huyo mtumishi asiyekuwa mwaminifu?
Pia Nape atueleze inakuaje vocha imeandikwa 500 then inauzwa 600 Kwa maelezo ya kinyemela?
Mwisho kama gharama zinapanda taarifa itolewe,binafsi huwa sitoa kama ninajua hiyo gharama sio ya kulipia unless nihakikishiwe kwamba zimeisha na huwezi subiria Serikali Hadi ilete ndio wanapitia humo humo maana hapo utakuata karibu wateja wote wameuziwa huwezi kubisha.
Hatukatai kununua wao waandike tu kadi hii inauzwa Tsh10,000/=No ujinga Kwa Watanzania kuendelea kulalamika kana kwamba hamjui Ofisi za Viongozi au TAKUKURU.
Watumishi wasio waaminifu wako Kila sehemu ingawa kweli zinaweza kuwa zimeisha na Huduma lazima ziendelee hapo no way out maana mnazaana hovyo na Kwa Kasi sana kiasi kwamba mahitaji yanaongezeka Kwa Kasi kubwa
Labda huko huku Bado Kuna kadi. Hilo likitabu ndo linauzwa mkuu?Siku hizi hakuna kadi
Kuna vitabu
Inasikitisha sanawatanzania wengi wanshindwa kuzijua haki zao
watanzania hatuna umoja kwenye kuitaka haki utalia mwenyewe likikukuta tumejawa tamaa na uwoga
mimi apo kwenye bei tofauti ndokumenimaliza nikama viingilio regular na vip😃
Ndo inafanya hata kuzaa kuwe na gharama tofauti?Men are always the expensive brand.
Aje tu maji yamezidi unga mkuuGwajima anaingiaje hapo
Nimeongea nje ya perspective ya mada.Ndo inafanya hata kuzaa kuwe na gharama tofauti?
Sasa kwanini serikali ijifiche kwenye kuwatangazia watu kuwa huduma ni bure mtu akiwa anajua ni bure aende na pesa kidogo. Isifiche na wakati mwingine waziri kutoka huko aendelee kusisitiza kuwa kitu fulani ni bure, waseme wazi kuwa huduma zinalipiwa basi watu wajue. Mbona huduma ambazo wananchi wanajua zinalipiwa mfano maji au luku hakuna anaye zidemand bure. Serikali kusema uongo ndipo shida ilipo waseme wazi wazi kuwa huduma kwa wajawazito zinalipiwa, waseme kuwa elimu si bure. Waache kudanganya kwa ajli ya manufaa ya kisiasa.Mimba sio dharula, ni maandalizi na unakaa na ujauzito miezi 9, changia huduma kwa maendeleo yako na afya ya mtoto wako, Watanzania tubadilike maana hakuna kitu cha Bure.