Dunia ni yao hii.. mfukuzwe shauri zenu
Mnaletewa mikondomu mnatumia
Midawa ya ukimwi ni yao pia na ukimwi wao sisi tumeukubali et!!
Mnaletewa dawa za kubadirisha ngozi mnatumia
Mnafanyiwa na kubadirishwa maumbo mnalipia pesa nyingi kisha mnakuja kulalamika inawadhuru
Dawa zote zilizojaa muhimbili na hospital zote Tanzania “ wao ndio chanzo kikuu
Dawa za korona, chanjo na hiyo corona yenyewe yao na wametuletea na tumekubali
Mashine za kupima magonjwa yote kifua kikuu, ukimwi, damu, zote ni zao
Madini/mafuta mashine za kuchakata zote zimetoka kwao
Magari na ndege zote tulizokopa ni zao na hayo madeni wanayotudai pia “ nchi ni yao
Nguo/viatu za nchini karibia zote wanatengeneza wao
Mabarabara yote yenye grade nzuri wao ndio wenye wakandarasi wazuri
Nchi inashindwa kutengeneza hata kiwembe hii
Simu,laptop, zote zinatoka kwao
Mabinti wadogo wa Africa wana olewa na mababu wa kizungu.. mabinti ni wao
Kama unaona kuna kampun ya soda sijui biscut na ubuge mwengine kwenye hiyo kampuni lazima kuwe na mzungu analipwa fungu kubwa kwa kusimamia kazi ni wao pia
Kweli nimeamini tenda wema 99% na uje kufanya kosa 1% tu mema yote yatafutika kwa sababu ya kosa dogo tu.. na hata hiyo vita inayoendelea huko ni yao ila sisi huku mafuta na bidhaa zingine zishaanza kutushinda..
Sisi sio wapumbavu sana..
Hahahahaaa huyu mleta mada amefanya nimuone wa ajabu sana aiseee. Wazungu kwa vitu wanavyofanya Unaweza ukahisi labda sio binadamu wenzetu.