masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 18,207
- 13,839
- Thread starter
- #161
Tena chuma haswa!JK katuletea chuma! Ova!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tena chuma haswa!JK katuletea chuma! Ova!
Kuna account zilipotea kabisa. Ujio wa mama umekuja na Mengi. ASPRIN ulikuwa wapi kaka?
AiseeeeTunashukuru Mungu mwendazake kendazake.... hallelujah
Kile kilikuwa chuma kina matatizo makubwa.Huyo Kikwete si yeye aliyejitapa kawaletea chuma, mzigo mzito mpe Mnyamwezi?
Leo unataka kumfanya kama si sehemu ya mfumo uliomuweka Magufuli?
Mataga huwa wakisikia hiyo kauli wanafurahi sanaSamia na kikwete ni ndugu mtoto wa mjomba mtoto wa shangazi...lao ni moja hao hiyo ya kusema "Samia na JPM ni kitu kimoja" ni kuwalaghai mazuzu.
Aaaah, ninakuelewa vizuri sana mkuu 'Masopa'; hakika CCM ya miaka mitano iliyopita, hiyo ilikuwa ni CCM ya aina yake kabisa, sitarajii kuwa itatokea tena katika miaka ya hivi karibuni. Hiyo ilikuwa ni CCM "iliyotekwa" na mtu mmoja mwenye mabavu mengi.CCM ni principles na imani ya misingi yake.
Majadiliano tuliyoyaona ndiyo CCM tunayoifahamu.
CCM FAKE ile ya kuchagua wapinzani kuiendesha, visasi, na kufanyiziana tumeona ukomo wake.
Niliweka kambi jukwaa la wakubwa kiongozi. Yule kiongozi wa malaika alikuwa ananichefua na uongozi wake wa kizwazwa...Kuna account zilipotea kabisa. Ujio wa mama umekuja na Mengi. ASPRIN ulikuwa wapi kaka?
🤣🤣majina makubwa kama wewe nilijiuliza umepotelea wapi. Ashukuriwe Mungu ametuondolea mikosi.Niliweka kambi jukwaa la wakubwa kiongozi. Yule kiongozi wa malaika alikuwa ananichefua na uongozi wake wa kizwazwa...
Namshukuru Mungu kwa kutufanyia wepesi...
Mtaishi kwa amani siku ccm ikifa rasmiMkuu unyenyekevu una thamani yake.
Sasawatu ndio tumeona "wasiojulikana " walitoka wapi, walioanzishiwa kesi hewa za kuhujumu uchumi nani alikuwa nyuma yake, kuibiwa wafanyabiashra kupitia TRA aliyeasisi mambo hayo.
Kwa kweli Tumpe mama Samia support yote hali ya utulivu na kawaida katika mustakabali wa nchi urudi tena, na watu waishi kwa amani.
Una mawazo sawa na fisi anayesubiri mkono uanguke akifikiri ni pande la nyama linalotaka kunyofoka.Mtaishi kwa amani siku ccm ikifa rasmi
Mungu yu mwema sana. Yale mamitutu ya bunduki na walinzi mia nane hawakufua dafu mbele ya ziraili mmoja asiye na silaha...🤣🤣majina makubwa kama wewe nilijiuliza umepotelea wapi. Ashukuriwe Mungu ametuondolea mikosi.
Aaaah, ninakuelewa vizuri sana mkuu 'Masopa'; hakika CCM ya miaka mitano iliyopita, hiyo ilikuwa ni CCM ya aina yake kabisa, sitarajii kuwa itatokea tena katika miaka ya hivi karibuni. Hiyo ilikuwa ni CCM "iliyotekwa" na mtu mmoja mwenye mabavu mengi.
Lakini, hata hivyo, hii "CCM ya majadiliano" unayosema tumeiona, hii kweli ndiyo CCM itakayodumu chini ya mama?
Kuna watu humo walishaonja nyama za watu, miaka mitano iliyopita, hawa nao je, mtawafanyaje?
Phew, hivi "principles na imani ya misingi ya CCM ya siku hizi (nina maana ile ya Kikwete, na hii tunayoikaribisha kwa furaha, ya mama) ni ipi vile? unaweza kutukumbusha mkuu Masopakyindi?
Hivi pacha wako 'Jidu' kapotelea wapi, maana yapo mengi ambayo angekuwa ameyachangamkia sana wiki hizi chache zilizopita.
Una uhuru wa kutokwenda mkuu.Tutaanza kutembeza vibaba tena, hayo ndio waliyoyataka baada ya kuwekwa kapuni na chinga pamoja na jiwe,sasa wote hawapo kila mtu anatoka shimoni, tunakoenda siko.
Katibu Mkuu alikuwa mtu wa CUF yule hakijui chama kabisa.Chama kilitekwa haswa, na wenye chama hata muelekeo na itikadi tulikuwa hatujui kinaelekea wapi.
Cha kukera ni kuwekewa Katibu Mkuu ambaye hakijui chama.
OOOooh My!IMANI YA CCM
- Binadamu wote ni Sawa
- Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake
- Ujamaa na kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru
AHADI ZA WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI
(1) Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja
(2) Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote
(3) Nitajitolera nafsi yangu kuondosha umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
(4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.
(5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
(6) Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote.
(7) Nitashjirikiana na wenzangu wote kujenga nchi yetu.
(8) Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
(9) Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika.
Mkuu nimekuwekea Imani na misingi ya ya CCM , misingi ambayo imetumika miaka yote kukiendesha chama.
Haijalishi nani yupo katika uongozi wa juu, lakini misingi hiyo na uendeshaji wake ndiyo roho ya chama.
Mama Samia alipopata tu Urais aliweka mbele misingi hiyo, hasa kwenye haki za mtu binafsi, kutoonewa na kuondoa dhulma(wasiojulikana), kuwa na uhuru wa habari, kutoa mawazo yako kwa uhuru, kujitegemea na kutobugudhiwa isivyo halali katika kipato na serikali(TRA).
Kimsingi kwa kusema tu hayo, Mama Samia alirudisha imani kubwa ya wanachama kwa CCM.
Na hapo ndio wazoefu kama JM Kikwete wamafanya kazi kubwa kumsaidia Mama kuweka imani hiyo kwa vitendo na kwa uzoefu wao.
Mtu yoyote akienda kinyume na imani hizo na principles zake, hana chama.
Kuhusu Jidu, mtafute , yumo mtandaoni namwona , ingawaje anaikwepa mada.
Si ajabu naye yuko kwenye lile genge la kanda, na linamsuta.
Nitapambana hapa hapa siendi kokoteUna uhuru wa kutokwenda mkuu.
Hamia nchi nyengine tuache Sisi Watanzania tumuunge mkono mama
Hilo pia ni chaguo Bora ila ili liwe Bora zaidi nakushauri tumuunge mkono mama.Nitapambana hapa hapa siendi kokote