Wengi hawajaielewa kauli ya Dkt. Ally Bashiru kuhusu CCM kutumia faida ya kuwa na dola kuendelea kubaki madarakani

Nigrastratatract, Anajifanya bingwa wa misemo ya akili lakini hebu mumuulize ikiwa kutumia dola kubaki madarakani ndio utaratibu wa katiba unavyoelekeza.

Katiba iko wazi haikusema dola katika kupokezana madaraka bali watu watapiga kura na mshindi atatangazwa kwa mujibu wa sheria dola haina wajibu katika b
Hilo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesikiliza kwa umakini alichosema katibu mkuun CCM juu ya matumizi ya dola kuhakikisha chama kilicho shika dola, nimegundua kuna upotoshaji.

Alicho maanisha ni kutumia dola kwa maslahi ya chama dola ili kilinde maslahi umma.

Mfano kudhibiti rushwa, ufisadi, kuleta nidhamu kazini n.k . Na sio kukandamiza upinzani.
 
Acheni kutetea wapuuzi na wahujumu uchumi
 
... weka video clip wacha taarabu.
 
Mpaka mifano ya KANU na Zambia ameisema sasa tusichoelewa ni nini?
Sikiliza mpaka mwisho
 

Umechelewa Kumtetea na acha Kuwafanya Watanzania wote Wewe pekee ndiyo mwenye Akili Kubwa. Ukitaka kujua kuwa alidhamiria na hata alichokisema alikuwa akikimaanisha angalia hata Body Language yake utapata jibu kamili.

Halafu nilitegemea baada ya Kuona amechemka na hata Kueleweka hivi vibaya na Watanzania (Neutral) Kisiasa kama Mimi Mzukulu na wengineo basi ama pale pale au hata Kesho yake tu angeomba Radhi na Kuirekebisha hiyo Kauli lakini kwa Kunyamaza Kwake na hata Chama cha CCM pia kupitia Mwenezi wake Kitaifa Polepole Kunyamaza kwa wenye Akili tumeshajua kuwa alikuwa akimaanisha na wala hakukosea.

Tuacheni Unafiki tafadhali!
 

Kwa hiyo yeye anaona kaongea sawa, ila wewe ndio unaona kanukuliwa vibaya? Wapi amekanusha alichoongea?
Hapa ndio unajua nini maana ya kuwa mnafiki.
 
chagu wa malunde, Hivi kanukuliwaje vibaya? Kwamba aliongea Kihaya sisi tuka tafsiri kiswahili au?
Maana alitumia lugha inayo eleweka na Watanzania wote tukamuelewa. Nyie mnao jaribu kumsemea ni kina nani?
Ajitokeze hadharani aseme alimaanisha nini..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
chagu wa malunde,
Aliyetoa hiyo kauli amenyamaza kimya hajakanusha. Sasa wewe sijui umetoka wapi kukanusha wakati aliyetamka hajakanusha? Au umetumwa kuja kupima upepo.

Mwache aje kwenye media akanushe na si wewe ukanushe kwa niaba yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…