Wewe ndio chanzo cha umasikini katika familia yenu

Wewe ndio chanzo cha umasikini katika familia yenu

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Katika familia, gharama hazipo kwenye kuzaa tu; bali gharama zipo kwenye malezi.

Na kwa mazingira ya sasa, unaweza kuta kijana ana miaka zaidi ya 30, lakini bado anaishi kwao, huku akiendelea kuwapa mzigo mzito wazazi wake.

Kwa nini nasema wewe ndio chanzo cha umasikini wa kwenu; ni kwa sababu gharama zilizotumia kukuza au kukulea wewe, ni gharama kubwa ambazo wazazi wako wangewekeza kwenye ujenzi wa viwanda, tungekuwa na bidhaa nyingi huko nje ya nchi na tungepata fedha za kigeni.

Mfano:-

Chukulia kwa siku unatumia 10,000/=

Mwaka una siku 365

Kukaa kwa wazazi mpaka kujitegemea, chukulia miaka 30


Fedha/nguvu zilizotumika kwa wazazi = 10,000 x siku 365 x miaka 30

=109, 500,000/=

Hii ina maana, mtu mmoja mpaka aje aondoke kwa wazazi wake, atakuwa ametumia kiasi kisichopungua Tsh. 109,500, 000/=

Kama mmezaliwa saba (7), ina maana wazazi wenu mmewabebesha mzigo wenye thamani ya Tsh. 766,500,000/=; kwa hiyo kama wanaishi kwenye mazingira mabovu, kaa ukijua, chanzo chao cha umasikini ni wewe.

Ndio maana matajiri hawazai watoto wengi, sio kwamba wana akili sana, bali wanaepuka gharama hizo nilizoziainisha hapo juu.

Kwa hiyo, usiwalaumu wazazi wako, kwa sababu chanzo chao cha umasikini ni wewe.

Karibuni kwa hoja.​
 
Kama wewe umeweza kutoka kwenu mapema na kwenda kujitegemea ni jambo la kumshukuru mungu lakini kamwe usitumia hiyo fursa uliyoipata kama fimbo ya kuwatandikia ambao bado wapo makwao .

Watu kubaki kwao siyo kama wanapenda ila ni changamoto tu za kimaisha ndyo zimepekekea wawe hapo walipo , mfano katika umri huo wapo waliomaliza vyuo lakini mungu hajawafungulia milango ya wao kupata kazi , wapo waliojaribu kuanzisha biashara lkn kutokana na mazingira kutokuwa rafiki biashara zimeanguka hivyo sababu ni nyingi ..

Mwisho unapofanya kitu na kikafanikiwa siyo kwamba wewe ndyo umefanya vizuri kuliko wengine hapana bali ni baraka za mungu zimekuwa upande wako hivyo jitahidi kuombea na wengine waipite hyo changamoto na siyo kuwasengenya ...
 
Katika familia, gharama hazipo kwenye kuzaa tu; bali gharama zipo kwenye malezi.

Na kwa mazingira ya sasa, unaweza kuta kijana ana miaka zaidi ya 30, lakini bado anaishi kwao, huku akiendelea kuwapa mzigo mzito wazazi wake...​
Watu wanawez kukaa mpka zaidi ya miaka 30 hata pengne kuzeekea nyumbna Kwa juu 2 ambazo nazifaham


1. Pengne huyo ndo chanzo wazazi wake kula na kupta baadi ya matumiz japokuwa yuko home

2. Tunatofautiana maisha Kuna mwingne ametoka maisha flan ya hadhi ya juu kidogo amejengewa nyumba yake ndani ya uzio mmoja lakin chakula wanakula pamoja.

Ko unaposema hvyo jalibu kuangalia na utofauti WA maisha Kwa Kila mmoja usiseme chanzo ni ww katika kufeli maisha
 
Mtu mmoja ndani ya familia awe anatumia 10,000 kwa siku?

Familia yenye uwezo huo mbona sio hata ya kuionea huruma kabisa.

Kama wenzangu wote hali ipo hivi basi mi nimetokea kwenye familia ya kimasikini sana.

Na kama hii hali ipo kweli kwa watu wengi basi zile kelele za kulia lia tozo ambazo kimsingi ni mia mia za juu zilizoongezwa ni unafiki wa kiwango chake.
 
Back
Top Bottom