Wezi walichonifanyia usiku wa kuamka leo

Wezi walichonifanyia usiku wa kuamka leo

Mkuu utakuwa unalala kama pono au labda wapulize dawa, sababu kwa kishindo cha kuvunja mlango lazima ungekurupuka.
Alafu mlango hautakiwi kuwa na kakitasa kamoja tu bali funga na makomeo mazito sio chini ya matano unless unaishi masaki na sio uswahilini

Komeo la chini, komeo la juu, komeo la kati, kitasa, komeo la kati kutoka chini, hapo mwizi atasanda tu.
 
Pole!.

Angalau wamekuachia remote. Mgeni akija utapata hata ushawishi wa kuvalidate kuwa umeibiwa.

Kanunue betri mpya kabisa.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] ushahidi upo au sio
 
Mkuu jipange upya uvute flat nyingine ...lakini pia hapo hama kama umepanga, km ni kwako ongeza usalama
 
Swali wakati unangalia
Je kuna watu ulikuwa nao?

Ova
 
Pole mkuu, na huo mlango ulimeguliwa na chuma chenye ncha haukuvunjwa kwa sauti. Inaonekana walikuwa karibu wakati unakaribia kulala.
 
Kuna mtu Twitter anajiita DC wa twitter amepost picha hizo hizo na caption hyo hyo. Ni wewe? Ni yeye? au ni nyinyi?
 
Huyu
_20220403_214820.JPG
 
Baada ya kumaliza kuangalia tuzo za muziki, nikalala naamka asubuhi hii nakuta wezi wametembea na Tv yangu.

Hapa natafuta nauli niende Bagamoyo au Pangani au Kwamsisi Tanga. Wezi wanarudishabsana maendeleo nyuma.

View attachment 2174025

View attachment 2174026
Pole ila sijaelewa picha ya mlango wako.je ni kweli mlango ni wa playwood? kama ni kweli nadhani watairudia hiyo subwoofer leo
 
Nenda kwa msisi tanga mkuu kapige tarawea watarudi nayo wamebeba kichwani kukuletea we kataa tu sio yako watabaki maisha yote wanatembea nayo kumtafuta mwenyewe.
Ukitaka kusamehe pokea ila walipe fidia
 
Kwa akili hizo za kila ukipata changamoto ukimbilie Tanga au Bagamoyo utakuwa looser kila siku.
Hivi hujui kuwa siku hizi hayo madude ya wachawi tulishayavunja na yamebaki hayana nguvu?
 
Mlikuwa mnaangalia wote, nenda hapo msikiti wa jirani kasome alubadili ila uwe na uhakika kuwa pesa uliyonunulia uliipata kihalali.

Vinginevyo mtachizika wote
 
Back
Top Bottom