Tatizo ni kwamba unasema na kujijibu mwenyewe, sasa kuna ubaya gani Tanzania ikileta mshauri wa Kijapan?
Dar es salaam.
Read between the line. Digest. Filtrate the meanining.
Tatizo si huyo mjapan tatizo ni ninyi SISIEMU.
Katika suala la ujenzi wa Technolojia Viwanda na Biashara ninyi SISIEMU Vision yenu ni Zero,mmeshindwa na hamsaidiki.
You belong to a Dumpstar.
Fikra zenu na dhamira zinawasukuma kuweka uchumi wa nchi mikononi mwa wageni kwa sababu mnaamini kwa dhati kwamba wananchi wa Tanzania kamwe hawawezi kuongoza mashirika yao wenyewe na kuyapeleka katika ufanisi.
Mmeshindwa kuwapa nafasi wananchi kuyanunua na kuyaongoza mashirika ambayo serikali ya chama cha SISIEMU imebuma kuyaongoza kwa sababu ya Uroho, Ubinafsi, Upofu wa maono na hamu na nia yenu chafu kutajirika kwa KIFISADI.
Ukweli kwamba Mashirika ya Umma yamekufa mbele ya Usimamizi wenu na mbele ya utaratibu usio wa kisayansi wa kuendesha mashirika mlioujenga kwa miaka 47, utaratibu ambao umefanya SISIEMU kukosa kabisa mwelekeo katika ujenzi na uendeshaji wa viwanda; si FREE TICKET ya kuuza kila Shirika kwa wageni na kuja kutamba Ki Umsloopagas hapa JF, kwamba kuweka viwanda mikononi mwa wageni ni jambo la msingi na jambo la maendeleo kwa wanchi wote wa Tanzania, na watanzania wote tunatakiwa kujivunia.
Watanzania hawajashindwa kumiriki na kuyaendesha mashirika yao ndani ya nchi yao.
Ninyi SISIEMU na serikali yenu ndiyo meshindwa na kulegea katika uongozi wa Mashirika na viwanda.
Uongozi wenu wa miaka 47 umeshindwa, umebuma umelegea kabisa kiasi cha kuamini kwamba mkipigwa Fobe na Wazungu Mashirika yenu yatadumu na uchumi wa nchi utafufuka.
Tanzania imeuza Dhahabu ya thamani ya $3,000,000,000.00 katika soko la dunia kwa muda wa miaka 6 tangu wazungu waanze kuichimba, hayo ndo maendeleo ambayo SISIEMU inaweza kujivunia Duniani kote, wakati ni 0.03% ndo imeingia kwenye mfuko wa serikali na ninyi SISIEMU kugawana 120% ya hiyo 0.03%.
Maendeleo na ndege upaa katika duru za SISIEMuni kujijaza manoti mifukoni mwenu na kwenye mifukio ya vimada wenu.
Watanzania wakiomba kununua mashirika ya umma ninyi SISIEMU macho yanawatoka midomo inatoa mapovu mikono inakinga ngumi na kupiga Ukelele mkuu kama radi za masika kule Morogoro na upiga kura ya turufu ya hapana. Hapna kwa wananchi ndiyo kwa wageni.
Yote hayo ni kwa sababu moja tu mnaweka kwenye mzani Rushwa kutoka kwa wageni dhidi ya kuwamirikisha mashirika wananchi ili wayaendeshe kwa nguvu zao wenyewe.
SISIEMU mmeshindwa katika Uongozi na Utawala wa kisiasa na kiuchumi sasa mnataka kwenda kuzimu na kila Mtanzania.
Jambo hilo la kutupeleka Watanzania wote kuzimu mimi Madela Wa Madilu nimelikata na nina uhakika wenzangu wengi tu hapa JF na Tanzania kwa ujumla wanalikataa.
Siku ya kwenda kuzimu ikifika Wewe Dar na wenzio wa SISIEMU mtaenda pekee yenu, amani iwe nanyi.
Ndugu yangu Dar, SISIEMU ikishindwa imeshindwa SISIEMU siyo Tanzania.
SISIEMU ni sehemu ndogo ya Watanzania.
SISIEMU si Tanzania wala haitakuwa.
Kumleta Mjapan ni tatizo lakini si Tatizo la msingi .
Tatizo la msingi ni Vision ya chama chenu cha SISIEMU ya kuamini kwamba ni wageni tu ndiyo wenye uwezo wa kushauri na kujenga uchumi.
Tatizo kubwa si mjapan tatizo ni ufinyu wa Mtazamo na wepesi wa kurukia ushauri wa nje kutoka kwa watu wageni kuliko kuweka umakini na upembuzi na kutumia ushauri wa ndani ulio jaa tele.
Hata kama mngeita Wjapani wote vipnga waje Tanzania kushauri na kuongoza mashirka kama SISIEMU bado iko madarakani uchumi utaendelea kubuma tu. Kuna utamaduni unaoendana na ukuzaji wa Teknolojia biashara na viwanda ambao ninyi SISIEMu mmeupa makalio.
Si hivyo tu hata kama Chama cha SISIEMU ,mashabiki na wapenzi w wake wote watapewa waingoze Japan baada ya miaka 3 Japan itakuwa ni moja kati wadaiwa wakubwa Duniani,na kwa mara ya kwanza tajiri mkubwa kuliko wote duniani atakuwa Mtanzania mwana SISIEMU Kwa nini?
Kwa sababu SISIEMU ni Bomu hakuna hirizi wala mzizi wa kuwaponya na jinamizi hili zaidi ya kifo chenu wenyewe.
SISIEMU mnatakiwa kufa ili mjiponye!!!?!!!
Wajapan wana interest na South Corridor ndiyo maana wamekuwa wepesi kuikubali Post hiyo ya ushauri.
Wajapan wanataka kuwapiga South na ninyi kwa tamaa ya pesa mmekubali kwii!! kwii!! kwii!! kwii!!
Wanataka Bandari ya Mtwara na Madini ya Chuma na makaa ya mawe yote yapatikanayo kule South.
Ndugu Dar kwa kuwaita Wajapan kuwa washauri wa Serikali ya SISIEMU mmepingwa kazu na kufungwa goli la fobe.
Dar es salaam Read my lips.
By the way where is your causin Mchambuzi????