Hiyo chanjo sijui kama warundi watakuja kupewa.
 


ni wiki kadhaa zmepita toka magufuli alitoa ushauri kwa wananchi kuhusu janga hili la corona na alisisitiza kwamba inabidi tuizoee corona, kama kawa kulikua na kejeli nyingi lakini leo maneno yake yametimia tena! hii ni baada ya DKT MIKE RYAN nae kukubali kwamba hakuna namna imebaki zaidi ya kuizoea corona kama magonjwa mengine ambapo awali magufuli alifafanua mwanzoni kwanini anaamini hivi

Corona itaendelea kuwepo, yasema WHO
 
Mfumo wa magufuli mtauelewa tu! Hii kitu tutaishinayo kama watu wanavyoishi na magonjwa mengine na yanaambukizika kirahisi mfano homa ya ini.

jamaa aliona mbali sna kweli magufuli genius
 
Leo nimemsikiliza mweshimiwa MAKONDA nimependa uchapaji kazi wake, TANZANIA namini tunaenda kumaliza awo mabeberu tuwapuze tule vuzuri na mazoezi huku tukichukua hatua zinazotolewa na wizara ya afya .

CCM DAMUDAMU!!!,CHAMA CHA MAMA &BABA

ebu agiza pepsi apo ntalipa
 
Kwa hiyo watakaa lockdown mpaka dunia iishe?
Lockdown haikuwekwa mpaka virus waishe. Lockdown iliwekwa ili kupunguza watu wengi wasiugue kwa wakati mmoja na hospital zikaelemewa. Na lililo muhimu ni kuwa lockdown imewekwa ili wataalam wapate muda wa kuwa-study vizuri virus na kutengeneza chanjo au tiba au vyote kwa pamoja.
 
WHO yakubali msimamo wa Tanzania kuhusu ‘lockdown’

Na Mwandishi Wetu

GENEVA, Mjumbe Maalum wa Shirika la Afya Duniani (WHO) na Mkurugenzi Mkuu wa Convid-19, Dkt. David Nabarro amependekeza kuwe na jamii ambayo watu watakuwa tayari kuuzoea na kuishi na ugonjwa wa virusi vya Corona (COVID-19) badala ya kuendelea kuwekewa zuio la kukaa ndani (lockdown) au kutoka kwa mashariti, kwani hatua za awali zinaonyesha hakuna chanjo au tiba ya virusi hivyo.

Wachambuzi wa masuala ya afya wameueleza mtandao wa TimesMajira Online kuwa, hatua hiyo ni ushindi mkubwa kwa misimamo ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo tangu awali ilikataa kuweka zuio la watu kukaa ndani, ikiwa ni agizo la Rais Dkt. John Magufuli huku akiwasisitiza wananchi kuzingatia miongozo yote inayotolewa na Serikali ikiwemo kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni, kuvaa barakoa, matumizi ya vitakasa mikono na kuepuka mikusanyiko isiyokuwa ya lazima.

Dkt.Nabarro ametoa taarifa hiyo kupitia akaunti yake ya Twitter akisema kwamba kuendelea kuwawekea watu zuio, kunaweza kuwaumiza zaidi kutokana na athari zake kwa watu na uchumi wa mataifa kwa jumla.

“Virusi hivi vitakuwa na sisi kwa siku za usoni inayoonekana na hakuna mtu anayetaka kuwa katika zuio,kama tulivyo na wakati huu,”amesema.

Fuata link ifuatayo for more information.

WHO yakubali msimamo wa Tanzania kuhusu 'lockdown' - TimesMajira
 

Attachments

  • IMG-20200514-WA0002.jpg
    60.9 KB · Views: 1
  • VID-20200514-WA0000.mp4
    4.9 MB
Areafiftyone,
Hivyo huyu Dr. Nabarro mtazamo wake ni kusifia kila msimamo wa nchi yoyote kuhusu namna ya kukabiliana na COVID -19 iwe lockdown au hakuna lockdown. Kwa mahojiano lukuki aliyofanya Dr. Nabarro na kulinganisha na uzi huu nakataa msomi na afisa wa juu wa WHO Dr. Nabarro kuwa amekunwa na msimamo wa Tanzania.

7 May 2020
WHO's Special Envoy On COVID-19 Dr David Nabarro Lauds The Steps Taken by India To Deal With Corona


Source : India Today
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…