Who influenced Nyerere: His Ujamaa Philosophy and Azimio Principles?

Who influenced Nyerere: His Ujamaa Philosophy and Azimio Principles?

Na wakati wa Mwalimu tungeweza kuyasema haya hapo Diamond Jubilee bila kuwekwa kizuizini, au sielewi?

Jaribu kusoma huko juu kwanza ujue hio nimesema kwa sababu gani..mchangiaji alisema kuwa siku hizi tuko huru,yeye ndie aliyefananisha wakati wa sasa na ule wa wakati ule,sio mimi.Nilichojaribu hapa ni kutaka kuuelewa huo uhuru upo kweli au la? Na pia mazingira gani ambayo tunayo sasa ambayo wakati ule yalikuwa hayapo ndio yafanya mtu aseme kuwa tuko huru zaidi sasa hivi,moja ni internet
 
Rev.Kishoka,
Katika ramani ya mkoloni naona kuna barabara inayoitwa Great North Road hiyo barabara bado ipo kweli ama ndio imekufa kutokana na Usanii wa mwafrika, kisha huko upande wa Mbeya/Sumbawanga nimeona kuna Gold mine imeitwa Lupa hiyo ndio wapi?..

Mkandara,
Great North road ni barabara kuanzia Kenya hadi Zambia. Na mgodi wa Lupa ulikuwepo. Wakoloni walichimba dhahabu na kutuachia makorongo na historia inajirudia yenyewe.
 
Nawashukuru nyote mlionitetea dhidi ya makombora ya Kuhani. Pengine Kuhani aelewe tu kuwa pamoja na kwamba hivi sasa niko jikoni nampikia mjukuu wangu, mambo haya ya kuingia kwenye discussion forums mie sio wa kuja! Tulikuwepo tangu enzi za Nyenzi.com. Kwa ubishi katika jambo ambalo ninalijua ukweli wake mie ndio mwenyewe! Siwezi kujitapa kwamba najua kila kitu kuhusu Mwalimu lakini kidogo ninachojua kinaniwezesha kuchangia kwa kujiamini kabisaa!

Naamini wengi ama baadhi ya wanaojadili humu ni watu ambao wanaangalia mambo yanavyokwenda kisiasa na hawana mahali pa kuweza kutoa mchango wao ama madukuduku yao. La msingi ni kuchangia na kuvumiliana tu.

Mie siasa ninayoijua kwa dhati kabisa ni ya Nyerere maana siku ya Uhuru nilivaa gauni lenye rangi ya bendera ya Tanganyika. Enzi hizo siasa za Nyerere zilikuwa zimemuingia kila mtu kwa sababu moja kubwa - zilikuwa ni siasa zilizojali sana welfare ya wananchi ambao wote walikuwa wa hali ya chini, wa matawi ya juu hawakuwepo enzi hizo.

Naweza pia nikasema kutokana na kufahamu kwa kuona mwenyewe nchi ilikuwa katika hali gani wakati tunapata Uhuru na juhudi gani zilifanywa na Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya Mwalimu Nyerere ndani ya miaka 15 (awamu moja na nusu) baada ya Uhuru, yaliyofanywa yalikuwa ni mageuzi ya hali ya juu.

Ningeliweza kuorodhesha hapa mambo makubwa, moja baada ya jingine, yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya uongozi wa Mwalimu Nyerere kutokana na utu aliokuwanao Mwalimu ambao ndio uliozaa Ujamaa aliojaribu kuujenga na Azimio la Arusha. Pamoja na kuwepo makosa ya kiutendaji yanayotajwa, Taifa lilisonga mbele.

Kama Kuhani haamini hilo, akafanye 'utafiti' na atagundua kwamba baada ya Azimio la Arusha uchumi wa nchi ulikua mwaka hadi mwaka mpaka mwaka 1977. Kuvunjika kwa Jumuiya ya Mashariki kuliyumbisha uchumi wetu, Vita vya Kagera vya 1978, kupanda kwa bei ya mafuta na janga la njaa tangu mwaka 1979 - 1983; ukichanganya na watu kutamani utajiri bila kuuhenyea vilichangia kuzorotesha kukua kwa uchumi na kufanya tusiweze kusonga mbele zaidi. Mwalimu, Ujamaa ama Azimio si sababu.

'Siri' ama msingi wa mafanikio ya kukua kwa uchumi kwa miaka yote hiyo ilikuwa ni siasa ya Ujamaa iliyozaa Azimio la Arusha na kupelekea Serikali kuchukua hatua za makusudi kudhibiti njia kuu za uchumi.

Hata kama Kuhani hataki kukubali kwa sababu zake binafsi, Mwalimu alikuwa kiongozi aliyekubalika sana kwa sababu alijali wananchi aliokuwa akiwaongoza na mikakati yake yote ukiwemo Ujamaa na Azimio aliibuni kwa maslahi ya wananchi na si kwa maslahi yake binafsi, ama watoto wake, Wazanaki wenziwe ama marafiki. Kiongozi yoyote anayetaka kuiongoza nchi kwa mafanikio asijaribu kuvaa viatu vya Mwalimu maana vyaweza visimtoshe, lakini anaweza akafuata nyayo za Mwalimu katika misingi ya utu na kujali mustakabali wa wananchi wote, na kudhihirisha kwamba anajali zaidi wale wa hali ya chini ambao ndio majority.
 
Nyani....si nimeona umeweka jina lako hapa,au my eyes are doing tricks on me again.Au mods wame remove that post?
 
Mkandara,
Great North road ni barabara kuanzia Kenya hadi Zambia. Na mgodi wa Lupa ulikuwepo. Wakoloni walichimba dhahabu na kutuachia makorongo na historia inajirudia yenyewe.

Ni afadhari walichimba. Wasingeshimba hiyo Great North road isingekuwepo.
 
[/B]

Kama uko huru kwelikweli weka jina lako la kweli....muulize Invicible na mwenzake walivyokombwa na polisi....enzi hizo za Mwalimu kulikuwa na internet?

Au unamaanisha 'uhuru' unaousema tunao sasa hivi,tunaweza kukutana wote humu na kuongelea yoyote tunayoongelea humu kwenye threads tofauti bila woga lets say,pale Diamond jubilee? Trust me,wote tutajikuta tuko polisi!

Hata kama tunakutana kwenye neti lakini serikali yetu na powers that be hawatuzuii kufanya hivyo. Si uwezo wanao au?

Hivi vijiweni watu hawajadiliani yanayoendelea Tanzania? Na kama wanajadiliana ina maana wote wana mitazamo/ mawazo yanayofanana au kulingana? Au wewe unazungumzia majadiliano yanayo involve vipaza sauti na mispika....?
 
Nawashukuru nyote mlionitetea dhidi ya makombora ya Kuhani. Pengine Kuhani aelewe tu kuwa pamoja na kwamba hivi sasa niko jikoni nampikia mjukuu wangu, mambo haya ya kuingia kwenye discussion forums mie sio wa kuja! Tulikuwepo tangu enzi za Nyenzi.com. Kwa ubishi katika jambo ambalo ninalijua ukweli wake mie ndio mwenyewe! Siwezi kujitapa kwamba najua kila kitu kuhusu Mwalimu lakini kidogo ninachojua kinaniwezesha kuchangia kwa kujiamini kabisaa!

Naamini wengi ama baadhi ya wanaojadili humu ni watu ambao wanaangalia mambo yanavyokwenda kisiasa na hawana mahali pa kuweza kutoa mchango wao ama madukuduku yao. La msingi ni kuchangia na kuvumiliana tu.

Mie siasa ninayoijua kwa dhati kabisa ni ya Nyerere maana siku ya Uhuru nilivaa gauni lenye rangi ya bendera ya Tanganyika. Enzi hizo siasa za Nyerere zilikuwa zimemuingia kila mtu kwa sababu moja kubwa - zilikuwa ni siasa zilizojali sana welfare ya wananchi ambao wote walikuwa wa hali ya chini, wa matawi ya juu hawakuwepo enzi hizo.

Naweza pia nikasema kutokana na kufahamu kwa kuona mwenyewe nchi ilikuwa katika hali gani wakati tunapata Uhuru na juhudi gani zilifanywa na Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya Mwalimu Nyerere ndani ya miaka 15 (awamu moja na nusu) baada ya Uhuru, yaliyofanywa yalikuwa ni mageuzi ya hali ya juu.

Ningeliweza kuorodhesha hapa mambo makubwa, moja baada ya jingine, yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya uongozi wa Mwalimu Nyerere kutokana na utu aliokuwanao Mwalimu ambao ndio uliozaa Ujamaa aliojaribu kuujenga na Azimio la Arusha. Pamoja na kuwepo makosa ya kiutendaji yanayotajwa, Taifa lilisonga mbele.

Kama Kuhani haamini hilo, akafanye 'utafiti' na atagundua kwamba baada ya Azimio la Arusha uchumi wa nchi ulikua mwaka hadi mwaka mpaka mwaka 1977. Kuvunjika kwa Jumuiya ya Mashariki kuliyumbisha uchumi wetu, Vita vya Kagera vya 1978, kupanda kwa bei ya mafuta na janga la njaa tangu mwaka 1979 - 1983; ukichanganya na watu kutamani utajiri bila kuuhenyea vilichangia kuzorotesha kukua kwa uchumi na kufanya tusiweze kusonga mbele zaidi. Mwalimu, Ujamaa ama Azimio si sababu.

'Siri' ama msingi wa mafanikio ya kukua kwa uchumi kwa miaka yote hiyo ilikuwa ni siasa ya Ujamaa iliyozaa Azimio la Arusha na kupelekea Serikali kuchukua hatua za makusudi kudhibiti njia kuu za uchumi.

Hata kama Kuhani hataki kukubali kwa sababu zake binafsi, Mwalimu alikuwa kiongozi aliyekubalika sana kwa sababu alijali wananchi aliokuwa akiwaongoza na mikakati yake yote ukiwemo Ujamaa na Azimio aliibuni kwa maslahi ya wananchi na si kwa maslahi yake binafsi, ama watoto wake, Wazanaki wenziwe ama marafiki. Kiongozi yoyote anayetaka kuiongoza nchi kwa mafanikio asijaribu kuvaa viatu vya Mwalimu maana vyaweza visimtoshe, lakini anaweza akafuata nyayo za Mwalimu katika misingi ya utu na kujali mustakabali wa wananchi wote, na kudhihirisha kwamba anajali zaidi wale wa hali ya chini ambao ndio majority.

Duh! kumbe ulikuwepo hata siku ya uhuru.....wewe kweli umekula chumvi.....
 
Jasusi,

..inaelekea wewe umevaa 'miwani ya mbao,' na 'kumimina zege 'kwenye masikio.

..kuna postings ambazo zinawataja wabunge waliochukuliwa hatua na Nyerere/TANU kwa kuikosoa serikali bungeni.

..hatua hizo ilikuwa ni pamoja na kufukuzwa ktk chama na wengine kuwekwa kizuizini.

..wakati huo kulikuwa hakuna kinga kwa wabunge kwa yale watakayoongea ndani ya bunge.

..mimi naamini Nyerere alikuwa akiipenda hii sheria ya kusweka watu kizuizini. nasema hivyo kwa sababu aliitumia kwa wapinzani wake. hii ni tofauti na mtazamo wake kuhusu sheria ya kunyonga, ambayo tunaelewa kabisa hakuipenda na aliitumia kwa nadra kabisa kabisa.

NB:

..halafu napenda niulize kuhusu suala la Sheikh Khassim Hanga. alifariki katika mazingira gani? alifariki mikononi mwa serikali ya Karume, au serikali ya Nyerere?

..inasemekana mara ya mwisho Hanga kuonekana hadharani ilikuwa ni ktk mkutano wa hadhara ambapo Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alimsema vibaya.
 
Hata kama tunakutana kwenye neti lakini serikali yetu na powers that be hawatuzuii kufanya hivyo. Si uwezo wanao au?

Hivi vijiweni watu hawajadiliani yanayoendelea Tanzania? Na kama wanajadiliana ina maana wote wana mitazamo/ mawazo yanayofanana au kulingana? Au wewe unazungumzia majadiliano yanayo involve vipaza sauti na mispika....?

Serikali ingekuwa na powers hizo basi Utamu Blog ingekuwa imefungwa siku nyingi,unajua kwa nini,kama hujui kaipitie.

Nani kakwambia vijiwe zamani havikuwepo? Kwani vilianzia wapi? Tofauti ni kwamba siku hizi access ya news ni rahisi kutokana na mitandao,tv,mobile phones n.k.Zamani walikuwa wanongelea Yanga na Simba tu.Enzi zile 'Cool Stuff'(Ile email ya Chavda iliyoibua EPA) ungeitoa wapi? Hata kama ungekuwa nayo,ingebidi uingie gharama kubwa ya kutoa copies nyingi then utume kama barua kwa members wote wa JF,ambao sijui ungewakusanya kivipi.Technology ndio imetufanya tuwe 'huru' kama unavyosema wewe,sio serikali.
Umetoa jina lako hapo,sawa...je unakaa Tanzania? Maana sio unatutolea jina kumbe uko Saskatchewan,thats the advantage we have thru tekelinalokujia,hujulikani uko wapi,and yet unaona huo ni uhuru
 
Ni afadhari walichimba. Wasingeshimba hiyo Great North road isingekuwepo.
Zakumi,
Great north road haikujengwa kutokana na dhahabu hiyo. Hiyo barabara ilijengwa na wakoloni kuunganisha koloni lao la Kenya na Southern and Northen Rhodesia. My point ni kwamba dhahabu ya Lupa haikuwanufaisha wakazi wa eneo hilo. That's all
 
Serikali ingekuwa na powers hizo basi Utamu Blog ingekuwa imefungwa siku nyingi,unajua kwa nini,kama hujui kaipitie.

Nani kakwambia vijiwe zamani havikuwepo? Kwani vilianzia wapi? Tofauti ni kwamba siku hizi access ya news ni rahisi kutokana na mitandao,tv,mobile phones n.k.Zamani walikuwa wanongelea Yanga na Simba tu.Enzi zile 'Cool Stuff'(Ile email ya Chavda iliyoibua EPA) ungeitoa wapi? Hata kama ungekuwa nayo,ingebidi uingie gharama kubwa ya kutoa copies nyingi then utume kama barua kwa members wote wa JF,ambao sijui ungewakusanya kivipi.Technology ndio imetufanya tuwe 'huru' kama unavyosema wewe,sio serikali.
Umetoa jina lako hapo,sawa...je unakaa Tanzania? Maana sio unatutolea jina kumbe uko Saskatchewan,thats the advantage we have thru tekelinalokujia,hujulikani uko wapi,and yet unaona huo ni uhuru

Ndio teknolojia imechangia kwa kiasi kikubwa kutufanya tuwe huru lakini mchango wa serikali na wenyewe huwezi kuupuuza. Hivi unadhani North Korea wana ma forum kama haya yanayoendeshwa ndani ya nchi? Ni mara ngapi umesikia crack down na monitoring ya matumizi ya computer China.

Haijalishi ninakaa Tanzania au Saskatchewan au Winona, Minnesota, au Dixie land Georgia. Advancement ya technology ni advantegous kwangu mimi ninayeweza kutoa jina langu hapa na wao (powers that be) kwa sababu wanazo resources za kutosha wakitaka kukupata. Therefore, it cuts in a multiple of ways.
 
Bibi Ntilie said:
Kama Kuhani haamini hilo, akafanye 'utafiti' na atagundua kwamba baada ya Azimio la Arusha uchumi wa nchi ulikua mwaka hadi mwaka mpaka mwaka 1977. Kuvunjika kwa Jumuiya ya Mashariki kuliyumbisha uchumi wetu, Vita vya Kagera vya 1978, kupanda kwa bei ya mafuta na janga la njaa tangu mwaka 1979 - 1983; ukichanganya na watu kutamani utajiri bila kuuhenyea vilichangia kuzorotesha kukua kwa uchumi na kufanya tusiweze kusonga mbele zaidi. Mwalimu, Ujamaa ama Azimio si sababu.

'Siri' ama msingi wa mafanikio ya kukua kwa uchumi kwa miaka yote hiyo ilikuwa ni siasa ya Ujamaa iliyozaa Azimio la Arusha na kupelekea Serikali kuchukua hatua za makusudi kudhibiti njia kuu za uchumi.

Bibi Ntilie,

..baada ya azimio la arusha tulianza harakati za kujenga viwanda, which i believe was a good decision.

..lakini azimio hilo hilo, utaifishaji wa mashamba makubwa, na operesheni vijiji, vilisababisha mazao ya katani, na korosho kuanguka.

..hasara za matukio hayo zinafichwa na mafanikio ya muda mfupi ya ujenzi wa viwanda, na kupanda kwa bei ya kahawa[coffee boom] ya miaka ile.

..unajua tatizo lingine la Mwalimu lilikuwa ni kuvuruga hata pale ambapo things were working fine ilimradi tu atekeleze itikadi zake.

..alichopaswa kufanya Mwalimu ni kuanzisha mashamba mapya ya mkonge, siyo kutaifisha yale yaliyokuwa yakizalisha na kuchangia ktk pato la taifa.

..Mwalimu pia hakupaswa kwenda kuswaga watu na kupeleka kwenye vijiji vya ujamaa, huku wakiacha mazao na ardhi zao un-attended.

..Mwalimu hakupaswa kuvunja vyama vya ushirika. mimi nilifikiri ushirika ni moja kati ya misingi ya ujamaa. kuna vyama vya ushirika vilivyovunjwa vilikuwa na umri wa zaidi ya miaka 30.

NB:

..Mwalimu aliondoka wakati nchi ina hali mbaya kabisa kiuchumi. inflation ilikuwa ktk double-digits, viwanda vilikuwa vimesimama, hazina ilikuwa haina akiba ya fedha kulipia bidhaa muhimu kama mafuta.

..kitu cha ajabu kabisa Mwalimu hakujiuzulu kutokana na makosa yake ktk kuongoza nchi na kuendesha uchumi. wakati anaondoka alipaswa kueleza bayana kwamba alikuwa ameharibu na ameshindwa, badala yake akasema anangatuka kwasababu ametawala kwa muda mrefu.

..Mwalimu angetuangalia machoni wa-Tanzania na kutueleza kwamba amekosea, na angeachana na propaganda zake na visingizio, tusingekuwa na mjadala huu. vilevile angeisaidia nchi hii kusonga mbele, na kuepukana na makosa yake.
 
Ndio teknolojia imechangia kwa kiasi kikubwa kutufanya tuwe huru lakini mchango wa serikali na wenyewe huwezi kuupuuza. Hivi unadhani North Korea wana ma forum kama haya yanayoendeshwa ndani ya nchi? Ni mara ngapi umesikia crack down na monitoring ya matumizi ya computer China.

Haijalishi ninakaa Tanzania au Saskatchewan au Winona, Minnesota, au Dixie land Georgia. Advancement ya technology ni advantegous kwangu mimi ninayeweza kutoa jina langu hapa na wao (powers that be) kwa sababu wanazo resources za kutosha wakitaka kukupata. Therefore, it cuts in a multiple of ways.

Trust me brother,inajalisha sana.Nimeshakaa na polisi mmoja wanaoshughulika na mambo IT fraud sikumoja na akaniambia jinsi wanavyojaribu kuipata identity ya jamaa wa Utamu Blog ili wamkamate,kwa sababu wamepata complaints kutoka kwa watu wengi sana,na akasema wamegundua hayupo hapa.
You would have or use that advantage to publish your name kwa sababu hauko Tanzania
 
Bibi Ntilie,

..baada ya azimio la arusha tulianza harakati za kujenga viwanda, which i believe was a good decision.

..lakini azimio hilo hilo, utaifishaji wa mashamba makubwa, na operesheni vijiji, vilisababisha mazao ya katani, na korosho kuanguka.

..hasara za matukio hayo zinafichwa na mafanikio ya muda mfupi ya ujenzi wa viwanda, na kupanda kwa bei ya kahawa[coffee boom] ya miaka ile.

..unajua tatizo lingine la Mwalimu lilikuwa ni kuvuruga hata pale ambapo things were working fine ilimradi tu atekeleze itikadi zake.

..alichopaswa kufanya Mwalimu ni kuanzisha mashamba mapya ya mkonge, siyo kutaifisha yale yaliyokuwa yakizalisha na kuchangia ktk pato la taifa.

..Mwalimu pia hakupaswa kwenda kuswaga watu na kupeleka kwenye vijiji vya ujamaa, huku wakiacha mazao na ardhi zao un-attended.

..Mwalimu hakupaswa kuvunja vyama vya ushirika. mimi nilifikiri ushirika ni moja kati ya misingi ya ujamaa. kuna vyama vya ushirika vilivyovunjwa vilikuwa na umri wa zaidi ya miaka 30.

NB:

..Mwalimu aliondoka wakati nchi ina hali mbaya kabisa kiuchumi. inflation ilikuwa ktk double-digits, viwanda vilikuwa vimesimama, hazina ilikuwa haina akiba ya fedha kulipia bidhaa muhimu kama mafuta.

..kitu cha ajabu kabisa Mwalimu hakujiuzulu kutokana na makosa yake ktk kuongoza nchi na kuendesha uchumi. wakati anaondoka alipaswa kueleza bayana kwamba alikuwa ameharibu na ameshindwa, badala yake akasema anangatuka kwasababu ametawala kwa muda mrefu.

..Mwalimu angetuangalia machoni wa-Tanzania na kutueleza kwamba amekosea, na angeachana na propaganda zake na visingizio, tusingekuwa na mjadala huu. vilevile angeisaidia nchi hii kusonga mbele, na kuepukana na makosa yake.

Can we let go of Mwalimu shoulda, woulda, coulda done this and just move on? Some of you are so hung up on the past that you can't move forward with your lives. It's getting kinda old now...
 
Trust me brother,inajalisha sana.Nimeshakaa na polisi mmoja wanaoshughulika na mambo IT fraud sikumoja na akaniambia jinsi wanavyojaribu kuipata identity ya jamaa wa Utamu Blog ili wamkamate,kwa sababu wamepata complaints kutoka kwa watu wengi sana,na akasema wamegundua hayupo hapa.
You would have or use that advantage to publish your name kwa sababu hauko Tanzania

Kwani huyo jamaa anahatarisha usalama wa taifa? Na hao watu wanaolalamika si waache tu kutembelea hiyo bulogu, ugumu uko wapi hapo? Jaribu ku-plot kwenye mtandao kuipindua serikali uone....
 
Bibi Ntilie,

..baada ya azimio la arusha tulianza harakati za kujenga viwanda, which i believe was a good decision.

..lakini azimio hilo hilo, utaifishaji wa mashamba makubwa, na operesheni vijiji, vilisababisha mazao ya katani, na korosho kuanguka.

..hasara za matukio hayo zinafichwa na mafanikio ya muda mfupi ya ujenzi wa viwanda, na kupanda kwa bei ya kahawa[coffee boom] ya miaka ile.

..unajua tatizo lingine la Mwalimu lilikuwa ni kuvuruga hata pale ambapo things were working fine ilimradi tu atekeleze itikadi zake.

..alichopaswa kufanya Mwalimu ni kuanzisha mashamba mapya ya mkonge, siyo kutaifisha yale yaliyokuwa yakizalisha na kuchangia ktk pato la taifa.

..Mwalimu pia hakupaswa kwenda kuswaga watu na kupeleka kwenye vijiji vya ujamaa, huku wakiacha mazao na ardhi zao un-attended.

..Mwalimu hakupaswa kuvunja vyama vya ushirika. mimi nilifikiri ushirika ni moja kati ya misingi ya ujamaa. kuna vyama vya ushirika vilivyovunjwa vilikuwa na umri wa zaidi ya miaka 30.


Mwalimu alitoa jibu lake hapa:

IB: What were your main mistakes as Tanzanian leader? What should you have done differently?

MJN: There are things that I would have done more firmly or not at all. For example, I would not nationalize the sisal plantations. This was a mistake. I did not realize how difficult it would be for the state to manage agriculture. Agriculture is difficult to socialize. I tried to tell my government that what was traditionally the family's in the village social organization should be left with the family, while what was new could be communalized at the village level. The land issue and family holdings were very sensitive. I saw this intellectually but it was hard to translate it into policy implementation. But I still think that in the end Tanzania will return to the values and basic principles of the Arusha Declaration.
 
Mwalimu alitoa jibu lake hapa:

IB: What were your main mistakes as Tanzanian leader? What should you have done differently?

MJN: There are things that I would have done more firmly or not at all. For example, I would not nationalize the sisal plantations. This was a mistake. I did not realize how difficult it would be for the state to manage agriculture. Agriculture is difficult to socialize. I tried to tell my government that what was traditionally the family's in the village social organization should be left with the family, while what was new could be communalized at the village level. The land issue and family holdings were very sensitive. I saw this intellectually but it was hard to translate it into policy implementation. But I still think that in the end Tanzania will return to the values and basic principles of the Arusha Declaration.

Nadhani swali lilikuwa "mistakes" ila yeye katoa "mistake". Ina maana alikosea kitu kimoja tu?
 
Back
Top Bottom