Will a weakened America emerge victorious against communist China?

Will a weakened America emerge victorious against communist China?

Mbona covid 19 imemhenyesha hvyo Licha ya hizo decoration ulizozielezea hivyo unless Chinese ambao kwa mda mfupitu wameweza kuuzibiti ugonjwa
North Korea haina hata kesi moja ya covid19, kwa hiyo inazidi nchi zote duniani kiuchumi?
Tanzania haijaripoti kesi yoyote tangu April mwaka jana kwa hiyo utasema inazizidi nchi kama South Africa zenye maelfu ya vifo.

Umetumia kesi ya corona, hata hivo US ana chanjo yake na inakubalika duniani. Chanjo ya China wataitumia wenyewe na nchi zilizowekewa vikwazo ingawa WHO itazisaidia. Kwanza corona ulianzia China wakauficha badala watoe taarifa mapema dunia ijilinde. China wamerecover mapema hilo halipingiki, walifanya vizuri.
 
ukweli ni kwamba nguvu za kiuchumi zinahamia asia, marekani anajitahidi kuzuia hilo kwa kushirikiana na mataifa ya asia kama vile japan south korea! Hoa jamaa ni wajinga sana! Elon musk alishasema uchumu wa china utakua mara mbili au tatu zaidi ya wa marekani! kwa mara ya kwanza box office ya china ndo imeongoza kwa mauzo ya filamu mwaka huu kuipita marekani!
Uko Japan na South Korea Wamarekani wapo kule kabla hata Soviet Union haijawa superpower, leo hii haipo. US wapo kule tangu kuisha kwa WW2 na wamezisaidia hizo nchi kiuchumi. Linganisha North Korea yenye China dhidi ya South Korea yenye Marekani uone nani njaa kali.
 
North Korea haina hata kesi moja ya covid19, kwa hiyo inazidi nchi zote duniani kiuchumi?
Tanzania haijaripoti kesi yoyote tangu April mwaka jana kwa hiyo utasema inazizidi nchi kama South Africa zenye maelfu ya vifo.

Umetumia kesi ya corona, hata hivo US ana chanjo yake na inakubalika duniani. Chanjo ya China wataitumia wenyewe na nchi zilizowekewa vikwazo ingawa WHO itazisaidia. Kwanza corona ulianzia China wakauficha badala watoe taarifa mapema dunia ijilinde. China wamerecover mapema hilo halipingiki, walifanya vizuri.
Kwa nini na hao marekani wenye kila nyenzo wasirekave mapema Kama uchina
 
Amerikkkkka has been on a decline from the very moment she acquired an international hyperpower status.
America grew at an exponential rate within a span of 100 years only because she adopted Isolationism in 1789.
George Washington warned them of the perils of military adventurism plaguing the European Continent.
History teaches us global power campaigns never end well on the part of hegemons like the USA.

For the last 70 years, she has squandered all her resources and emptied her gold-coffers in a quest for a global empire.
British Empire, the greatest colonizer to ever appear on the face of earth during her zenith of power in 1922 had a control of almost 23% of the global landmass, stretching from the Canada to the peripheries of British India. But what happened ??? The global empire was a cause of her gradual decadence and the fall from grace.

Chancellor Otto Von Bismarck never wanted Prussia or Imperial Germany to have any colonial and territorial acquisitions out of Europe and Eurasian Landmass. He believed that, no matter how hard you nurture the colonies at some point they'll be a liability because people will tend to emancipate themselves and carry their future into their own hands. This is a curse of global empires: Even in places like Canada and Australia which were the cesspools for criminals and indentured laborers who are kith and kin of the British people, Independence was inevitable.

Not being able to focus on domestic issues is a quagmire that America is stuck in: When America is spending almost 2 Trillion US Dollars fighting in Iraq, China has been busy creating a foreign reserve fund special for Investment worth 3 Trillion US Dollars. They spend this money to purchase influence and resources all over the world including the forbidden territory "The Western Hemisphere" dubbed as "America's Own Backyard".

Look folks, while Obama and Trump were busy dealing with Iran: China just purchased a Mountain covered with Copper in Peru. The Toromocho Mountain is worth 3 Billion USD and China has just acquired it just as King Leopold acquired the Congo as his personal possession. And the list still goes on and on, I could spend almost three hours mentioning such brazen and grandiose projects, but my time is limited.

China overtaking America in terms of PPP is a real disaster enough to dread even a person with little knowledge of Economics. This means If America spends 50 million USD in building two fighter jets, China will spend the same 50 million USD in building three fighter jets of the same quality in China: This is what economists call The Big Mac Index. Now come to think of it, if with PPP the US is able to assemble an army of 1,000,000 active personnel, what advantages would China have against America militarily ???

And sometimes, I get appalled to the point of disgust and fury when people do not see PPP as a single biggest advantage one nation can have against the other nation. Or that despite the predictions of notorious pundits like Henry Kissinger the architect of China's Ascendancy and Paul Wolfowitz , that China will eventually collapse soon after the fall of communism did not come to pass and the CCP juggernaut is still rolling.

China achieved what the formidable USSR with all her might could not even come close to achieve: That is Economic Primacy over the USA in areas of International Trade and Manufacturing.
 
Uko Japan na South Korea Wamarekani wapo kule kabla hata Soviet Union haijawa superpower, leo hii haipo. US wapo kule tangu kuisha kwa WW2 na wamezisaidia hizo nchi kiuchumi. Linganisha North Korea yenye China dhidi ya South Korea yenye Marekani uone nani njaa kali.
ukweli ni kwamba china kwa sasa ni nightmare kwa marekani ukiingia www.msn.com habari nyingi ni za china kuliko hata za marekani yenyewe
 
Sasa hivi US imegawanyika vipande 538 🙂 So, Mrusi wako alikuwa muungwana sana (so generous) katika kutabiri kwake. Unaelewa hilo Engineer!??? 🙂
Kabla ya kuniuliza kama nimeelewa hoja yako, ingekuwa vyema zaidi endapo ungeanza wewe kuelewa kuhusu kile nilichokisema.
 
Nimeliona hilo bandiko la Huntington huko Foreign Policy amezungumzia ukuaji wa nchi kama Japan ukilinganisha na ukuji wa uchumi wa Marekani: Akasema uchumi wa Marekani haujatanuka tena wakati wenzake wanakuwa na kuanza kumfukuzia. Linaloongelewa na Joseph Nye na John Mearsheimer ni kwamba Relative Decline ya Marekani kwasasa ni kwamba hafukuziwi tena na Uchina tena bali ashapitwa tayari kwenye baadhi ya maeneo ya msingi kama Uchumi.

Narudia tena nilichokisema huko juu, Uchina ndiyo taifa pekee ambalo limemshinda Marekani kwenye nguvu ya soko in terms of Purchasing Power Parity (PPP) na Volume of International Trade. Ujerumani Magharibi, Japani na Umoja wa Kisovieti hawakuwahi kumshinda Marekani kwenye soko hata siku moja (Kama wamewahi nioneshe ushahidi), wao walikuwa wajaribu kumfikia Marekani lakini hawakufanikiwa.

Purchasing Power Parity and International Trade ndivyo viliifanya Marekani liwe taifa lenye nguvu kuliko yote duniani hadi kuyashinda mataifa tajiri kama dola la Ujerumani na Uingereza. Tokea mwaka 1872 hadi 2014 Uchina ndiyo taifa pekee lilifanikiwa kumshinda Marekani kwenye PPP kubwa na International Trade (Trade in Merchandise).
Awali ya yote, ulihoji kuhusu "Relative Decline of America" na kusema kuwa suala hilo halikuwahi kuzungumziwa hapo kabla na baadhi ya wanazuoni niliowatumia kama rejea hapo awali. Nafikiri mpaka hapa tulipofikia tutakubaliana sote kuwa suala hili limekwisha zungumzwa kwa miaka mingi kabla ya hili linaloendelea hivi sasa, hivyo si jambo geni. Huu umekuwa kama utamaduni wa muda mrefu sana wa Wamarekani wa kuujadili uchumi wao.

Tuundeleze mjadala!
Unasema kuwa Marekani kwa sasa imepitwa tayari kwenye baadhi ya maeneo na umetolea mfano uchumi. Mimi napingana na hoja hiyo. Si kweli kwamba China imeizidi Marekani kiuchumi. Pia, napingana na hoja hiyo kutokana na jinsi ambavyo unautafsiri 'uchumi'. Hilo ni la kwanza!

Jambo la pili: umetumia Purchasing Power Parity (PPP) na International Trade kama vigezo vya kusema kuwa China imeizidi Marekani kwenye soko. Hivi ni vigezo vichache tu katika suala la kuupima uchumi wa nchi. Purchasing Power Parity ni kigezo kimoja cha kulinganisha uchumi kati ya nchi mbalimbali lakini si kigezo pekee cha kukitumia kwenye masuala ya uchumi na kuhitimisha kuwa China imeizidi Marekani kiuchumi. Maana, hata Nigeria ina higher PPP kuliko Scandinavian countries. Iraq pia imezizidi PPP nchi zaidi ya kumi za bara la Ulaya. Mifano ni mingi!

Kwenye suala la mauzo ya nje hali kadhalika, pia si kigezo pekee hata kama utakitumia pamoja na PPP kama hitimisho la kusema kuwa China imeizidi Marekani kiuchumi. Bado kuna masuala mengine mengi yanayohusika katika kuupima uchumi wa nchi, hasa pale unapofanya ulinganisho kati ya mataifa hayo mawili. Chukulia mfano: nominal GDP pamoja na per capita income (nominal & PPP) kati ya mataifa hayo mawili, ni wazi kuwa hoja yako kwamba China imeipita Marekani kiuchumi inahitaji masahihisho.

Wataalamu mbalimbali wa masuala ya kiuchumi wamekuwa wakitoa makisio kuhusu China kuja kuipiku Marekani kiuchumi kwa miongo kadhaa sasa na imekuwa ni tabia ya miaka nenda rudi kuhusiana na uchumi wa Marekani dhidi ya mataifa mengine yenye kuleta ushindani. Miaka takribani 10 iliyopita (2010), wataalamu mbalimbali wa masuala ya kiuchumi walituambia kuwa China itaipiku Marekani kuwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi pale itakapofika mwaka 2020, yaani mwaka jana. Pia, miaka michache iliyopita, kulikuwa na makisio mapya kuhusiana na ukuaji wa uchumi kati ya hizi nchi mbili; baadhi ya wataalamu wakidai kuwa China itauzidi uchumi wa Marekani panapo mwaka 2030 huku wengine wakiongeza kiwango cha muda zaidi ya huo.

Hivi sasa, yameibuka makisio mapya kuwa China itaipiku Marekani kuwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi duniani panapo mwaka 2028. Lakini, kiwango hiki cha muda ni katika kuzingatia janga lililopo hivi sasa la virusi vya corona ambalo limetajwa kuiathiri Marekani. Vilevile hii ni estimation ambayo haikuzingatia mwenendo wa China katika masuala mengineyo yenye kuweza kuleta athari katika ukuaji wa uchumi wake tofauti na janga la COVID-19. Kuna masuala ya kisera, kiutawala, kidiplomasia n.k. ambayo hayakuzingatiwa katika tafiti mbalimbali mpya.

Nilisema hapo awali kuwa, tujipe muda kuhusiana na makisio na tabiri hizi. Mijadala hii imekuwepo muda mrefu sana sambamba na makisio mbalimbali kuhusiana na mwenendo wa kiuchumi wa Marekani dhidi ya mataifa mengine ambayo yalionekana kuwa na ushindani mkubwa katika masuala mbalimbali hasa kiuchumi.
 
ukweli ni kwamba china kwa sasa ni nightmare kwa marekani ukiingia www.msn.com habari nyingi ni za china kuliko hata za marekani yenyewe
Hiyo ni Channel ya kimataifa. Bahati nzuri wewe mwenyewe unaitazama au kuisoma sana mpaka unajua mara nyingi inawazungumzia kina nani. US kuna Fox, Bloomberg, CNN, New York Times na mavyombo kibao yanajulikana. China ina nini kimataifa ukiachana na Xinhua na CCTV?

Ushawahi ona CCTV huwa zinamuonesha nani zaidi kwenye habari.
 
Hiyo ni Channel ya kimataifa. Bahati nzuri wewe mwenyewe unaitazama au kuisoma sana mpaka unajua mara nyingi inawazungumzia kina nani. US kuna Fox, Bloomberg, CNN, New York Times na mavyombo kibao yanajulikana. China ina nini kimataifa ukiachana na Xinhua na CCTV?

Ushawahi ona CCTV huwa zinamuonesha nani zaidi kwenye habari.
imf imesema china ndo nchi yenye uchumi mkubwa duniani kwa sasa China Is Now the World’s Largest Economy. We Shouldn’t Be Shocked.
 
Awali ya yote, ulihoji kuhusu "Relative Decline of America" na kusema kuwa suala hilo halikuwahi kuzungumziwa hapo kabla na baadhi ya wanazuoni niliowatumia kama rejea hapo awali. Nafikiri mpaka hapa tulipofikia tutakubaliana sote kuwa suala hili limekwisha zungumzwa kwa miaka mingi kabla ya hili linaloendelea hivi sasa, hivyo si jambo geni. Huu umekuwa kama utamaduni wa muda mrefu sana wa Wamarekani wa kuujadili uchumi wao.

Tuundeleze mjadala!
Unasema kuwa Marekani kwa sasa imepitwa tayari kwenye baadhi ya maeneo na umetolea mfano uchumi. Mimi napingana na hoja hiyo. Si kweli kwamba China imeizidi Marekani kiuchumi. Pia, napingana na hoja hiyo kutokana na jinsi ambavyo unautafsiri 'uchumi'. Hilo ni la kwanza!

Jambo la pili: umetumia Purchasing Power Parity (PPP) na International Trade kama vigezo vya kusema kuwa China imeizidi Marekani kwenye soko. Hivi ni vigezo vichache tu katika suala la kuupima uchumi wa nchi. Purchasing Power Parity ni kigezo kimoja cha kulinganisha uchumi kati ya nchi mbalimbali lakini si kigezo pekee cha kukitumia kwenye masuala ya uchumi na kuhitimisha kuwa China imeizidi Marekani kiuchumi. Maana, hata Nigeria ina higher PPP kuliko Scandinavian countries. Iraq pia imezizidi PPP nchi zaidi ya kumi za bara la Ulaya. Mifano ni mingi!

Kwenye suala la mauzo ya nje hali kadhalika, pia si kigezo pekee hata kama utakitumia pamoja na PPP kama hitimisho la kusema kuwa China imeizidi Marekani kiuchumi. Bado kuna masuala mengine mengi yanayohusika katika kuupima uchumi wa nchi, hasa pale unapofanya ulinganisho kati ya mataifa hayo mawili. Chukulia mfano: nominal GDP pamoja na per capita income (nominal & PPP) kati ya mataifa hayo mawili, ni wazi kuwa hoja yako kwamba China imeipita Marekani kiuchumi inahitaji masahihisho.

Wataalamu mbalimbali wa masuala ya kiuchumi wamekuwa wakitoa makisio kuhusu China kuja kuipiku Marekani kiuchumi kwa miongo kadhaa sasa na imekuwa ni tabia ya miaka nenda rudi kuhusiana na uchumi wa Marekani dhidi ya mataifa mengine yenye kuleta ushindani. Miaka takribani 10 iliyopita (2010), wataalamu mbalimbali wa masuala ya kiuchumi walituambia kuwa China itaipiku Marekani kuwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi pale itakapofika mwaka 2020, yaani mwaka jana. Pia, miaka michache iliyopita, kulikuwa na makisio mapya kuhusiana na ukuaji wa uchumi kati ya hizi nchi mbili; baadhi ya wataalamu wakidai kuwa China itauzidi uchumi wa Marekani panapo mwaka 2030 huku wengine wakiongeza kiwango cha muda zaidi ya huo.

Hivi sasa, yameibuka makisio mapya kuwa China itaipiku Marekani kuwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi duniani panapo mwaka 2028. Lakini, kiwango hiki cha muda ni katika kuzingatia janga lililopo hivi sasa la virusi vya corona ambalo limetajwa kuiathiri Marekani. Vilevile hii ni estimation ambayo haikuzingatia mwenendo wa China katika masuala mengineyo yenye kuweza kuleta athari katika ukuaji wa uchumi wake tofauti na janga la COVID-19. Kuna masuala ya kisera, kiutawala, kidiplomasia n.k. ambayo hayakuzingatiwa katika tafiti mbalimbali mpya.

Nilisema hapo awali kuwa, tujipe muda kuhusiana na makisio na tabiri hizi. Mijadala hii imekuwepo muda mrefu sana sambamba na makisio mbalimbali kuhusiana na mwenendo wa kiuchumi wa Marekani dhidi ya mataifa mengine ambayo yalionekana kuwa na ushindani mkubwa katika masuala mbalimbali hasa kiuchumi.
kwa hiyo tuseme ww unataka kutuaminisha IMF wanatudanganya sio juu ya uchumi wa china??? China is the worlds largest economy now China Is Now the World’s Largest Economy. We Shouldn’t Be Shocked. na xi jinping anataka kudouble uchumi wa nchi yake ndani ya miaka 30 ijayo
 
imf imesema china ndo nchi yenye uchumi mkubwa duniani kwa sasa China Is Now the World’s Largest Economy. We Shouldn’t Be Shocked.
I think hiihii ndio niliisoma day one ilipotolewa. PPP nishaizungumzia comment yangu ya kwanza uzi huu.
China for the first time imeongoza kwa PPP ila inawekewa vikwazo na Marekani na vinaiathiri. Haiwezi iwekea US vikwazo vya kiuchumi.

PPP kubwa hutokana na gharama za uzalishaji kuwa ndogo na kama member mmoja alivyosema, China haijafikia kuwa na labour ya kulipwa viwango sawa na Japan, South Korea, US, UK, Germany au Switzerland. Ikifikia hatua hii basi labour itakuwa expensive na ile advantage ya uzalishaji kwa gharama nafuu itapotea. Hapo ndio bidhaa zitakuwa juu na PPP itapungua.
 
Awali ya yote, ulihoji kuhusu "Relative Decline of America" na kusema kuwa suala hilo halikuwahi kuzungumziwa hapo kabla na baadhi ya wanazuoni niliowatumia kama rejea hapo awali. Nafikiri mpaka hapa tulipofikia tutakubaliana sote kuwa suala hili limekwisha zungumzwa kwa miaka mingi kabla ya hili linaloendelea hivi sasa, hivyo si jambo geni. Huu umekuwa kama utamaduni wa muda mrefu sana wa Wamarekani wa kuujadili uchumi wao.
Ukiniwekea andiko la Huntington ambalo limezungumzia The Decline of America kabla ya hilo la kutoka Foreign Policy. Tena la miaka ya 50 kama ulivyosema mwanzoni ntakushukuru sana.

Tuundeleze mjadala!
Unasema kuwa Marekani kwa sasa imepitwa tayari kwenye baadhi ya maeneo na umetolea mfano uchumi. Mimi napingana na hoja hiyo. Si kweli kwamba China imeizidi Marekani kiuchumi. Pia, napingana na hoja hiyo kutokana na jinsi ambavyo unautafsiri 'uchumi'. Hilo ni la kwanza!
Vipimo vikubwa vya uchumi ni PPP, GNP na GDP. Kinachoaminika na taasisi kubwa za kimataifa kama IMF ni PPP.
GNP wamarekani wameacha kukitumia kwasababu kina madhaifu.

Jambo la pili: umetumia Purchasing Power Parity (PPP) na International Trade kama vigezo vya kusema kuwa China imeizidi Marekani kwenye soko. Hivi ni vigezo vichache tu katika suala la kuupima uchumi wa nchi. Purchasing Power Parity ni kigezo kimoja cha kulinganisha uchumi kati ya nchi mbalimbali lakini si kigezo pekee cha kukitumia kwenye masuala ya uchumi na kuhitimisha kuwa China imeizidi Marekani kiuchumi. Maana, hata Nigeria ina higher PPP kuliko Scandinavian countries. Iraq pia imezizidi PPP nchi zaidi ya kumi za bara la Ulaya. Mifano ni mingi!
Kwani ili tuweze kokotoa PPP na kufanya ulinganifu wa Country's Output tunazingatia vigezo gani ???
Pia, ukiangalia The Big Mac Index 2020 ya PPP, Nigeria na Iraq zimezipita nchi kama Sweden na Norway kweli ???

Kwenye suala la mauzo ya nje hali kadhalika, pia si kigezo pekee hata kama utakitumia pamoja na PPP kama hitimisho la kusema kuwa China imeizidi Marekani kiuchumi. Bado kuna masuala mengine mengi yanayohusika katika kuupima uchumi wa nchi, hasa pale unapofanya ulinganisho kati ya mataifa hayo mawili. Chukulia mfano: nominal GDP pamoja na per capita income (nominal & PPP) kati ya mataifa hayo mawili, ni wazi kuwa hoja yako kwamba China imeipita Marekani kiuchumi inahitaji masahihisho.
Turudi kidogo kwa Adam Smith kidogo, taifa ambalo linauza sana bidhaa kuliko mataifa mengine kwenye soko la dunia ndiyo litakuwa na mirija mingi ya kufyonza pesa kutoka mataifa mengi duniani, hivyo ndilo ambalo litakuwa ni tajiri. Marekani amekuwa taifa kubwa kiuchumi duniani kwasababu ndiye aliyekuwa muuzaji mkuba wa bidhaa kwenye soko la dunia. Hili nalo lina ubishi ???

Wataalamu mbalimbali wa masuala ya kiuchumi wamekuwa wakitoa makisio kuhusu China kuja kuipiku Marekani kiuchumi kwa miongo kadhaa sasa na imekuwa ni tabia ya miaka nenda rudi kuhusiana na uchumi wa Marekani dhidi ya mataifa mengine yenye kuleta ushindani. Miaka takribani 10 iliyopita (2010), wataalamu mbalimbali wa masuala ya kiuchumi walituambia kuwa China itaipiku Marekani kuwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi pale itakapofika mwaka 2020, yaani mwaka jana. Pia, miaka michache iliyopita, kulikuwa na makisio mapya kuhusiana na ukuaji wa uchumi kati ya hizi nchi mbili; baadhi ya wataalamu wakidai kuwa China itauzidi uchumi wa Marekani panapo mwaka 2030 huku wengine wakiongeza kiwango cha muda zaidi ya huo.
Tuachane na mikisio na tufanye rejea ya takwimu kutoka taasisi kubwa za kiuchumi duniani kama IMF. Wao wamesema kabisa kwamba kipimo bora na kinachoaminika na wao ni PPP kuliko GDP kwasababu GDP inategemea Market Rates which are not stable for a long time and only relevant to internationally traded goods. Non-traded goods are left out of the periphery. Unadhani ni sahihi kusema Marekani ina Uchumi mkubwa kuliko Uchina kwa kuzingatia Market Rates peke yake mkuu ???

Hivi sasa, yameibuka makisio mapya kuwa China itaipiku Marekani kuwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi duniani panapo mwaka 2028. Lakini, kiwango hiki cha muda ni katika kuzingatia janga lililopo hivi sasa la virusi vya corona ambalo limetajwa kuiathiri Marekani.
Hebu tuache makisio ya wanazuoni na twende kwenye takwimu maana zile huwa hazidanganyi. IMF wanasema PPP ndiyo kikokotoo bora kabisa cha uchumi kuliko GDP kwasababu kinazingatia mambo mengi. Lakini nadhani itakuwa vizuri zaidi kama tusaidie kufahamu kwanza jinsi ambavyo PPP inakokotolewa halafu tufanye rejea ya The Big Max Index 2020 kisha mwisho kabisa turudi kwenye takwimu za IMF na WB.

NB: Maswala ya kisera na kidiplomasia ni muhimu lakini ni Subjective sana katika kuangalia mwenendo wa Uchumi wa nchi. Kuna nchi ambazo hazifanyi vizuri kidiplomasia, haki za binadamu na kisera lakini zinafanya vizuri kwenye soko la dunia. Au hapa ulikuwa unamaanisha nini mkuu ???

Karibu tuendeleze mjadala......
 
PPP kubwa hutokana na gharama za uzalishaji kuwa ndogo na kama member mmoja alivyosema, China haijafikia kuwa na labour ya kulipwa viwango sawa na Japan, South Korea, US, UK, Germany au Switzerland. Ikifikia hatua hii basi labour itakuwa expensive na ile advantage ya uzalishaji kwa gharama nafuu itapotea. Hapo ndio bidhaa zitakuwa juu na PPP itapungua.
Hudhani kwamba hii ni faida kwa Uchina hasa kwenye kumpunguzia gharama za uzalishaji, upatikanaji wa huduma bora kwa bei rahisi pamoja na kuongeza nguvu yake kijeshi. Au mpaka maisha yawe ya gharama kama Tokyo ndiyo tusema kwamba taifa ni tajiri ???
 
Mimi nachagua democracy na personal freedoms

Sichagui suppression na authoritaniasm,matako mmoja aliepo Beijing anaamua ufungwe au unyongwe popote ulipo duniani bila hata kupita mahakamani

Heri hata America ni lazima upite mahakamani u urgue your case na kuna real rule of law

China akiwa boss we are all subject to a stupid dictatorial rulling.

America aendelee tu kua boss,japo ana mapungufu yake ni heri kabisa..tutavumilia kama tulivyokwisha vumilia kwa miaka 100 so far.

Fvck China
Hivi taifa ambalo Raisi wao ashawahi kumiliki watumwa zaidi ya 300 utasema kuna personal freedoms kweli ???
Au taifa ambalo limeruhusu watu weusi waanza kuanza kupiga kura mwaka 1965 utasema ni la kidemokrasia ??
Kiufupi hakuna ambacho Uchina anafanya leo dhidi ya raia wake, Marekani hajawahi kufanya dhidi ya raia wake.

NB: Marekani imefanya haya wakati wana The Rule of Law, Parliamentary Supremacy na The Independent Judiciary.!
 
Naona hujui

USA ni democratic since inception yake kutoka kwa founding fathers wake 1777
Sasa ndugu yangu wewe unayejua kuliko mimi unakoseaje kufahamu kwamba Marekani ilizaliwa mwaka 1776 siyo 1777.
Pili, watu (minorities) wasiporuhusiwa kupiga kura bila sababu za msingi, hapo utasema kuna demokrasia kweli ???
 
Unafeli eti pale ninapokosea mwaka kwa margin error ya 1 year unaona basi umenishiika?
Siyo naona nimekushika, ni kweli ulikuwa hujui. Hebu thibitisha kwa kusoma ulichoandika hapa chini:
Na kumbuka actual year ya implementation ya declaration ni mwaka unaofuata,usijitie eti umenishika sana
Legally, a Declaration of Independence is a political statement issued by a governing entity affirming sovereignty , political independence and birth of a nation state. And for your information dummy, once issued they immediately become effective because they are not subjected to any legal procedure. Once a nation has declared it's independence, it's independent indeed.

Kiufupi, AZIMIO LA UHURU ndiyo UHURU wenyewe wa nchi, ni mtu ambaye hajaelimika pekee ndiyo anaweza kusema kwamba Marekani ilijitangazia UHURU mwaka 1776 lakini ikaamua kutimiza adhma ya kuwa huru mwaka 1777. Nadhani kama uliamua kuchangamsha genge, waungwana tunaweza kukuelewa lakini kama ulikuwa unamaanisha basi uko na shida kubwa sehemu.

Mkuu Malcolm unajitia kama unajua sana kumbe nashangaa hata hujui maana ya demokrasia

Demokrasia ni kuhusu walio wengi,hua haijali minorities..hiyo ndio weakness ya demokrasia...Demokrasia ni wengi wape na wala sio kinyume chake

Marekani imejitahidi sana ku-broden demokrasia yake ina include hadi minorities now,kumbuka ni work in progress
Haya sasa hebu twende kwenye hoja yako ya mwisho ya mimi kujifanya Najua kumbe Sijui. Hebu tuiangalie na kuichambua kwa mapana yake haya chini ya mwamvuli wa dhana nzima ya demokrasia.

Wagiriki wa Athens ndiyo wanasemekana walituletea neno demokrasia na maana yake: Hivyo huwezi kusema demokrasia ilianzia nchini Marekani na ina madhaifu. Wagiriki wa Athens walisema kwamba Demokrasia ni mfumo wa utawala ambao unamhusisha kila mtu ndani ya jiji (Polity): Hivyo wakaunda mfumo wa DIRECT DEMOCRACY ambapo mji mzima walifanya kikao ili kusikiliza maoni na matakwa ya kila raia na kila kaya, bila kubagua mtu.

Hawakumwacha mtu yeyote nyuma na wala hawakuamini katika wengi wape: Kifalsafa hili la WENGI WAPE kwasababu wamelitaka limeanzia Uingereza na jina lake sahihi ni THE PRINCIPLE OF UTILITARIANISM ambayo iliasisiwa na mwanafalsafa nguli wa kiingereza aitwaye JEREMY BENTHAM. Sorry to burst your bubble, but your understanding of democracy is lackadaisical.

Wanafalsafa wakubwa wa karne ya 19 kama Freidrich Nietzsche walikataa na kusema kwamba hii ya wengi wapeni siyo demokrasia kwasababu husababisha kitu kiitwacho THE TYRANNY OF NUMBERS ambayo huweza kupelekea NIHILISM hasa kwa wale ambao wanaachwa (Minorities).
 
Kwenye hoja ya pili, service market ndio ukomavu wa biashara na uzalishaji. Ndio maana kina Apple wanauza devices ila bado wanawekeza kwenye huduma kama Apple Tv na iOS za kuendeshea hizo products. China bado inazalisha tu ila kwa kasi sana inakuja. Marekani ina patents nyingi sana zinazotumika duniani na inaendelea kusajiri nyingine. Uzalishaji wa China hata Vietnam na India wanaweza jaribu kuweka mazingira rafiki wakavuta kiasi kidogo cha uwekezaji, US ana biashara ambazo huzikuti kwingineko kirahisi. Hatujaona China ikija na conglomerates kama CocaCola, Pepsi, Microsoft, McDonald's, Nike, Ford au Boeing.

Hatuoni dunia ikikimbilia kuwekeza kwenye soko la hisa la China, Wachina wenyewe makampuni yao makubwa wanayasajiri kwenye soko la Kimarekani. Hatuoni cream za dunia zikikimbilia China, Wachina wanaenda kusoma na kufanya kazi Marekani na sio kinyume chake.

Hatuoni fedha ya China ikifanya manunuzi, hata China yenyewe haijiamini ina-devaluate Yuan yao ili kuzuia matumizi yake kwenye exchange duniani. USD inazunguka dunia nzima bila kuathiri uchumi wa US.

Hapo namba tatu kwenye jeshi. Marekani ina jeshi kubwa mno na lenye nguvu. Dunia haijalishuhudia jeshi la US likiitetea mipaka yake, huwa tunaona vita za kujitakia ambazo wakishindwa simply wanaondoka. China haina silaha za aina yoyote kutishia Marekani, ukiachana na makombora kama DF-41 vita ya China vs US hakuna Mchina atakanyaga kwenye shores za mainland US. China doctrine zake ni kuizuia US isifike Southern China sea, hata ikitaka kufikisha majeshi yake eneo kama Maryland itaanzaje? Tangu WW2 tunajua madhara ya kupigia vita kwako yalivyo, US kaingia vita zote za karne ya 20 na 21 bila kupigana nyumbani.

Hizi Norinco na Shenyang haziwezi tengeneza silaha za kuzishinda Raytheon, General Dynamics, Boeing, Lockheed Martin, Huntington Ingalls, Northrop Grumman na nyingine nyingi za US.

China hakuna derivative ya DARPA yenye miradi mikubwa ya kimapinduzi kwenye ulinzi. Elimu ya China nayo sio supportive sana kwenye ulinzi kama US. Hata uuzaji wa silaha US anaongoza kuwauzia superpowers ila China bado ananunua silaha muhimu kwa Russia. China anauza silaha kwa kina Nigeria, Pakistan, Sri Lanka ambao wanakwepa masharti na kutafuta bei nafuu ila hawana budget ya kuchukua kwa wingi.

Bila hata allies US vs China lazima China isiishinde US kimapigano. US inaweza shinda au kutoka suruhu ila sio kushindwa. Kwanza experience aliyonayo US ni kubwa mno na yuko kila mahala duniani.

Kwenye ujasusi, cyber warfare na cyber security bado US anamzidi China. Hapa China hajaifikia Israel au Russia.

Tukiachana na ulinzi ambao ni muhimu kuhakikisha usalama wa biashara zote za nchi na ustawi wa sera zake. Maendeleo yajayo tumekubaliana yanatokana na nani anafanya nini na anamiliki nini kwa sasa katika teknolojia.

China ina kina Huawei, ZTE na CSMC ambao hawajazishinda Intel, AMD au Apple.

Kampuni kubwa za magari duniani haziko China. Hata kampuni za EV zinazoibuka US inaongoza ila China iko karibu sana.
5G China anaongoza ila wapo kina Ericsson na Nokia walikuwa wanakuja (hawana fedha). Ikumbukwe Nokia na Ericsson waliitoa 4G, Japan walishatoa 3G kupitia Docomo. Leo hii wako wapi?
Tutakuja kupata 6G wakitokea watu ambitious kama Elon Musk.

Artificial Intelligence na robotics wapo US, Japan na Russia wanakuja vizuri. Tumeona baadhi ya demo za robots kutoka US na Russia ila hatujaona demo za China. AI iko integrated sana kwenye teknolojia za magari kama Tesla na kwenye smartphone. Kwenye AI kompyuta na robots zitafidia watu na uzalishaji utapungua gharama uku kasi ikiwa ileils hakuna likizo wala kuchoka. China sioni kama anaongoza hapa, atategemea idadi yake ya watu na gharama zake ndogo za uzalishaji.

Nilitazama production site ya F-35, wanatumia laser beam kuelekeza mfanyakazi wapi pa kufunga nati, wapi pa kuchomeka hiki. China hana precision hii kwenye uzalishaji na hivo faults kwenye systems muhimu kama kompyuta hazikwepeki wakati huo speed ya kuzalisha hana ila atategemea wingi wa watu.

Teknolojia nyingine za zamani kidogo kwa US bado China hajazifikia. China hana true stealth technology ambayo US anayo tangu 1980s, hana uwezo wa kutengeneza injini za ndege kama P&W pale US, aircraft carrier ndio anayo moja ya kwake ikiwa diesel powered wakati US anazo zaidi ya kumi nuclear powered, nuclear submarines bado sana. Yani nuclear technology bado hajafikia US, mpaka majuzi hapa China ilikuwa inatumia coal wakati wenzake walishahama muda sana uko.

Katika ustaarabu na kutegemeana kwa mifumo na taasisi China haijaongoza. Benki, mashirika ya bima, mifuko ya uwekezaji popote duniani na taasisi zinazojitegemea viko zaidi wazi na endelevu kwa US. Utasikia FDA imezuia Monsanto kuuza dawa flani, FAA imezi-ground Boeing Max mpaka izichunguze, FBI imechunguza Russiagate na kukuta rais Trump hana hatia. Ingekuwa China ungesikia CPP wamefanya hivi, serikali imefanya kile, serikali ime...
Nchi haina hata mgawanyo wa mamlaka itaanzaje kuongoza ulimwengu.

Naamini ili nchi iipite Marekani lazima kwanza iifikie, hata Britain kabla haijapitwa na Marekani kwanza zililingana kisha Marekani akaipita. Sasa China hajaweza kulingana na Marekani, hayuko mzimamzima kuna vitu yuko mbele vingine nyuma kabisa uko
Katika uchambuzi hai ni huu, we have another 80yrs to go china apite
 
ofcoz China is now a threat to USA, however not possible to suppress USA. Ni kweli China anaspidi Kali ya ku kutaka ku undertake marekani Ila kwa bahati mbaya China hajajua madhaifu ya amerika ,na kwa bahati mbaya amerika anayajua madhaifu ya China,na anajua wakati upi wa kuanza ku deel na madhaifu ya China,na mlango wa Siri wa kutekelezwa anaujua na Alisha ufanyia analysis yakutosha.

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
China bado saaana juzi mkwala mmoja tu wa trump huawei wameanza fuga nguruwe
 
Back
Top Bottom