Kama umemfuatilia Samuel P. Huntington vizuri kuna ugumu gani kuniwekea rejea ???
Kuhusu PPP umeongea mambo mengi sana lakini bado maswali yangu hayapatiwa majibu ambayo niliuliza awali.
Nimekwisha weka reference kuhusiana na suala la Samuel Huntington. Haujaiona?
The Big Mac Index ni kipimo kinachotumika katika kulinganisha thamani ya sarafu ya nchi moja dhidi ya zingine kwa kutumia bidhaa ya aina moja pekee ambayo ni Big Mac. Hiyo Big Mac kama bado hujapata kuifahamu ni chakula kinachofahamika kama 'hamburger' ambacho huuzwa katika nchi mbalimbali duniani kupitia migahawa maarafu ya McDonald's.
Kipimo kinahusika katika kuonesha utofauti wa nguvu ya sarafu ya nchi moja dhidi ya nchi nyingine pale sarafu hizo zinapotumika kufanya manunuzi ya hamburger hizo katika nchi zao. Kwa mfano; gharama ya Big Mac moja nchini Marekani ni dola za Kimarekani zipatazo 5. Lakini, katika wakati huohuo gharama ya Big Mac moja nchini Tanzania ni dola 2. Maana yake ni kuwa, sarafu ya Tanzania inaweza kutumika kufanya manunuzi ya hamburger nyingi zaidi za Big Mac kuliko ambavyo sarafu ya Marekani ikitumika katika manunuzi ya bidhaa hiyo nchini Marekani.
Katika mfano huo, unaweza kukokotoa Purchasing Power Parity kama ifuatavyo:
Kanuni ya PPP inasema; Purchasing Power Parity = Cost of good in currency 1 / Cost of the same good in currency 2
Maana yake ni kuwa, ili upate PPP ya nchi moja ukilinganisha na nyingine, yakupasa kuchukuwa bei ya kiasi cha bidhaa (basket of goods) katika nchi husika yenye sarafu yake mahususi, kisha kuigawa (divide) kwa bei ya kiasi cha bidhaa hizohizo katika nchi nyingine yenye sarafu yake mahususi.
Kwa kuzingatia mfano wa Big Mac nilioutoa, yakupasa kuanza kwa kutafuta exchange rate ya nchi hizo mbili.
Exchage rate: dola 1 ya Kimarekani = shilingi 2300 za Kitanzania.
Umepewa bei ya baga moja ya Big Mac ukiwa 'Bongo' in terms of USD ambayo ni dola 2 sawa na shilingi 4600 za Kitanzania. Nafikiri unafahamu jinsi ambavyo hiyo 4600 imepatikana!
Bei ya Big Mac moja nchini Marekani in terms of USD umekwisha pewa pia ambayo ni dola 5.
Mpaka hapo una 'costs' za aina tatu (3) tofauti:
1) Cost of Big Mac in US in US Dollars ambayo ni 5.
2) Cost of Big Mac in Tanzania in US Dollars ambayo ni 2.
3) Cost of Big Mac in Tanzania in Tanzanian Shillings ambayo ni 4600.
Kumbuka kanuni ya PPP kuwa; Purchasing Power Parity = Cost of good in currency 1 / Cost of the same good in currency 2
Hivyo basi, ili kupata PPP ya Tanzania ukilinganisha na Marekani, yakupasa kuchukua cost aina ya 3 kisha kuigawa kwa cost aina ya 1.
Yaani, Purchasing Power Parity = Shilingi 4600 / Dola 5 = 920
Therefore, Purchasing Power Parity = Shilingi 920 kwa Dola 1.
Mpaka hapa nafikiri nimejibu swali lako kuhusu jinsi ya kukokotoa PPP, tena kwa urahisi kabisa.
Sasa, nilisema kuwa Nigeria imezizidi PPP nchi za Scandinavia. Pia, nilisema kuwa Iraq imezizidi PPP nchi zaidi ya kumi (10) za bara la Ulaya. Hapa namaanisha GDP katika kipimo cha Purchasing Power Parity.
Tafuta data za hivi karibuni kutoka IMF ama World Bank kuhusiana na GDP (PPP) za mataifa yote duniani kisha fanya ulinganisho kwa kuzingatia kile nilichokisema. Katika hiyo link uliyoiweka hapa, kuna orodha ya nchi 15 pekee. Kuna nchi kama Indonesia humo ambayo imeorodhesha juu ya mataifa ambayo ni more developed kama Uingereza, Ufaransa, Italia, Spain, South Korea n.k.
Ukitafuta orodha kamili, utakutana na Nigeria ikiwazidi kina Norway, Denmark, Finland, Sweden n.k. Pia utakutana na Iraq nayo ikizizidi nchi zaidi ya kumi (10) za bara la Ulaya zikiwemo Norway, Denmark, Ureno, Ugiriki n.k.
Nami naweka link:
Free and open access to global development data
data.worldbank.org
Pia, umesema kwamba Nigeria haimo kwenye The Big Mac Index ya mwaka 2020. Kumbuka kuwa BMI huzingatia mauzo ya hamburger ya Big Mac katika mataifa mbalimbali. Lakini, kuna nchi ambazo bidhaa hii haipatikani kabisa. Hapa ndipo mapungufu ya hicho kipimo yanapoanza kujionesha. Pia, kuna nchi ambazo bidhaa hii imetengenezwa kuendana na soko la nchi husika lakini in theory, bidhaa hiyo inatambulika kuwa ni sawa (the same) dunia nzima. Inconsistency!
Swali jingine; je, ni sahihi kutegemea kikokotoo cha nominal GDP?
Swali la namna hii nimekwisha kulijibu katika post yangu iliyopita kama ulinisoma kwa makini. Nilisema, kila kipimo huwa na nguvu pale kinapotumika kwa kuzingatia masuala kadhaa ama vipengele fulani pekee au maalumu. Hakuna kipimo cha uchumi ambacho kinaweza ku-stand alone kama kipimo bora cha uchumi katika masuala ama vipengele vyote bila kuzingatia vipimo vingine.
Pia, nilisema kuwa hivi sasa kuna mjadala mkubwa kuhusiana na hivi vipimo. Hapo baadaye, kuna uwezekano mkubwa sana wa baadhi ya vipimo vinavyotumika hivi sasa kuwekwa kando baada ya vipimo vipya kuvumbuliwa. Umezungumzia The Ease of Doing Business Index kwamba ni theoretical. In fact, Purchasing Power Parity pia ni theoretical.
Pia, si kweli kwamba Ease of Doing Business Index haina methodology. Tembelea link ifuatayo (World Bank), utakutana na maelekezo [zikiwemo PDF] kuhusiana na methodologies mbalimbali.
Link:
Methodology for Doing Business
Jambo la mwisho; nilisema kwamba Marekani inafanya vizuri zaidi kiuchumi katika kipimo cha GDP (PPP) per capita ukilinganisha na China. Nadhani umeninukuu tofauti. Ni vyema ukarejea katika hiyo post, nimezungumzia GDP per capita (PPP) ama GDP (PPP) per capita.
Takwimu zipo katika link ifuatayo (World Bank):
Free and open access to global development data
data.worldbank.org
Mpaka kufikia hapa, nafikiri nitakuwa nimeyajibu maswali yote ambayo hayakujibiwa hapo awali. Asante!