Will a weakened America emerge victorious against communist China?

Will a weakened America emerge victorious against communist China?

Mkuu umeongelea mambo mengi sana, lakini mimi ntajikita kwenye Uchumi tu.

China is the greatest exporter of merchandise in the world, and some of the merchandise are American owned. This is the single biggest advantage China has over America. Marekani anauza Uchina bidhaa za kiasi cha dola za kimarekani Billion 110, huku Uchina anauza Marekani bidhaa za kiasi cha dola za Kimarekani Billion 396.6 Billion. Nadhani hili litoshe tu kukuonesha kwamba Uchina yuko mbele ya Marekani.

Kwenye International Trade kuna kitu kinatwa The Corporate Inversion ambapo makampuni huamua kubadilisha urai wake na kwenda nchi nyingine ili kupata mazingira marahisi ya uwekezaji kama kodi na soko la ajira. Hayo makampuni ya Kimarekani uliyoyataja kama Nike, CocaCola, Boeing na Conglomorates nyingi ambazo ziko Patented America yamewekeza sana Uchina kwasababu nilizokutajia hapo awali. Unajua kwanini wanafanya hivi ?? The basic feature of Modern Capitalist Economy is the Export of Capital.

Chanzo kikubwa cha Trade War ya Donald Trump ilikuwa ni kuhakikisha kwamba anazuia Corporate Inversion ili ajira na nguvu ya uzalishaji virudi Marekani. Mwaka 2017 Ford Motors walitaka kuhamia Mexico wakapigwa mkwara kwamba bidhaa zao zitatozwa Tarrif kubwa pindi zinapoingia Marekani wakaogopa: Alichofanya ni kukimbilia kurekebisha mkataba wa NAFTA.
Bro Boeing imewekeza uchina??
 
Bro Boeing imewekeza uchina??
Ndiyo braza, wamefungua plant yao huko.
 
Hiyo ni Channel ya kimataifa. Bahati nzuri wewe mwenyewe unaitazama au kuisoma sana mpaka unajua mara nyingi inawazungumzia kina nani. US kuna Fox, Bloomberg, CNN, New York Times na mavyombo kibao yanajulikana. China ina nini kimataifa ukiachana na Xinhua na CCTV?

Ushawahi ona CCTV huwa zinamuonesha nani zaidi kwenye habari.
Hata ukiingia 5star huwez ikuta zaid ya cnn
 
Hudhani kwamba hii ni faida kwa Uchina hasa kwenye kumpunguzia gharama za uzalishaji, upatikanaji wa huduma bora kwa bei rahisi pamoja na kuongeza nguvu yake kijeshi. Au mpaka maisha yawe ya gharama kama Tokyo ndiyo tusema kwamba taifa ni tajiri ???
Juzi usiku nilisoma taarifa moja kuhusu online chains za vyakula. China na watu wake wote inahitaji uzalishaji mkubwa wa chakula ila ni sera ya serikali kuhakikisha wanajitoshelesha kwenye chakula. Serikali ya China iko vizuri sana kwenye kutoa incentives kwa raia.

Kwa vile hili soko ni jipya, giants kama Tencent na Alibaba wanapambana kujitanua uko.

Sasa kilichonishtua ni kusoma kwamba ndani ya miaka hii 10, wages na salaries za mashambani vijijini zimepanda ×3! Kwa rate hii miaka 20 ijayo sijui kama kutakuwa na cheap labour tunayoiona leo. Wamefikia hatua ya kufunga automated bracelets kwenye kila kuku ili kumfatilia. Hapa wanakwepa gharama za wafanyakazi na wanaongeza usahihi wa taarifa. Unakuta shamba la kuku 20,000 kila mmoja amevaa kidani cha electronic.

Gharama za kuzalisha zinapanda taratibu, kitakachoibeba China ni sera za kukaribisha uwekezaji ambazo ni nzuri sana kuliko Marekani yenye makodi makubwa na ukaguzi mwingi. Kwenye miundombinu na nishati wako sawa.

Wasiwasi wangu ni kuona giants wa tech wanawekeza kwenye kulima matunda na kufuga kuku, I think hawajiamini kushindana katika soko la teknolojia pekee. Itakuwa maajabu kuona Intel inaanzisha mradi wa kufuga ng'ombe au Apple inapambana kusaidia walima nganongano, kuna makampuni ya kufanya hizi kazi.
 
Kwangu naona US kaimarika zaidi kwenye systems zake za kidunia na kwa vile ndio muaisi wa Globalization bado anagusa kila sekta muhimu duniani na anahusika na kila kitu hata ambacho hakimuhusu. Sina rejea za wasomi ila nina sababu kama hizi:

Teknolojia zote.
US anaongoza kuwekeza kwenye tech mpya itakayoongoza dunia. Space inashindaniwa zaidi na makampuni ya Kimarekani kama SpaceX na Blue Origin. Nano technology na Artificial Intelligence bado US yuko mbele. Nchi zote zilizotawala au kuongoza dunia ziliongoza kiteknolojia, China bado.

Kwenye electronics.
Tukiachana na uzalishaji ambao umegusia hasa tuje kwenye nani anamiliki hizo teknolojia za uzalishaji. Mwaka jana US alipoiwekea Huawei vikwazo nikashangaa kuona TSMC ya Taiwan inayoongoza kwenye foundry duniani nayo imelazimika kuendana na vikwazo kwa kigezo cha kutumia core American technology. Kampuni za processors, mifumo ya kompyuta, etc nyingi zaidi ziko US au ziko modeled kwenye mfumo wa US. Huawei na Samsung ziko vile kwa sababu ya kutumia American technology, wao ndio wanaruhusu competition wakiamua wanazuia.

Utulivu wa ndani.
CCP ndio inaongoza China tangu 1940s, hawa hawajakomaa lolote kisiasa bali wanatumia intimidation na nguvu nyingi. US wamekomaa sana hata hizi issue za BLM ni utoto mbele ya utengamano wao. China ina matatizo na Taiwan na Hong Kong, haina demokrasia wala mifumo imara na inategemea uwezo wa aliyepo madarakani. Nchi isiyo na utulivu haiwezi kuwa superpower.

Usafirishaji.
Magari ya umeme bado US anaongoza ingawa kwa China kama kina Nio wanakuja kasi. Usafirishaji kwa ujumla bado US ana edge, hakuna kampuni ya China inaweza kuipindua Boeing. Pale US kuna kampuni nyingi za kijeshi zinaweza tengeneza ndege za kiraia ila China hakuna hata moja.

Energy.
US anajitosheleza kwenye energy kuliko China. Japan ilipigwa WW2 sababu mojawapo ikiwa ni kuzuiwa kusafirisha mafuta. US ina teknolojia mbadala kama fracking kwenye mafuta na ina washirika wa kuiuzia mafuta kwa uhakika. Kwenye nuclear energy bado US anaongoza tena hapo China hajaifikia Japan.

Mifumo ya fedha.
PayPal, MasterCard, VISA, etc tunajua ni za wapi. Hizo kina Alipay zinatumika ukouko China. $ inaongoza kutumiwa, haitishiwi na yeyote kwa sasa sio crypto, gold wala fedha ya nchi nyingine. Mwaka 2008 uchumi wa dunia uliyumba kwa sababu ya taasisi za Marekani, hii inamaanisha nguvu waliyonayo. China itafanya nini mpaka uchumi wa dunia utetereke? Tukiachana na magonjwa ambayo hata shit country inaweza yatoa dunia ikatetereka.

Kijeshi.
Bado China haijakaribia hata kuifikia Marekani. Bado inajaribu kumfikia Russia ila sidhani kama ni within this 20 years. US ana makumi ya bases dunia nzima, ana allies wengi sana na silaha za kutosha. China ina maadui kama India, Japan, Taiwan, Vietnam, Philippines na hata Australia.

Kimataifa.
China haijawa na ushawishi wa kuikaribia Marekani kwenye EU, Asia-Pacific wala Middle East. Huu ushawishi kwa Africa ni mdogo duniani. Mashirika ya kimataifa kama WB, IMF na UN nzima yamekaa Kimarekani zaidi.

China inaizidi Marekani mbali kwenye population. Ni soko la uhakika na nguvukazi kubwa ya uzalishaji. Pia hii idadi kubwa inatoa mchujo mzuri sana wa vipaji kukiwepo elimu stahiki. Bado hatujaona vyuo vya China vikifanya breakthrough kubwa kama zinazofanyika kwenye vyuo vya Marekani.

Sioni dalili yoyote kubwa ya China kuipiku Marekani. Dalili chache kama PPP zote ni kutokana na population ya China wala sio mbinu, uwezo wala mikakati.
Wamarekani wana tabia ya kuishusha na kuitia hofu nchi yao, sio kama Warusi wenye brags na Wachina wenye historia ya kujipa moyo. Bado US ni strong

Fact check : Umekosea kusema kwamba USD haitishiwi na Gold mind you it is that any fiat currency you know (USD included) it is an artificial Gold
 
Juzi usiku nilisoma taarifa moja kuhusu online chains za vyakula. China na watu wake wote inahitaji uzalishaji mkubwa wa chakula ila ni sera ya serikali kuhakikisha wanajitoshelesha kwenye chakula. Serikali ya China iko vizuri sana kwenye kutoa incentives kwa raia.

Kwa vile hili soko ni jipya, giants kama Tencent na Alibaba wanapambana kujitanua uko.

Sasa kilichonishtua ni kusoma kwamba ndani ya miaka hii 10, wages na salaries za mashambani vijijini zimepanda ×3! Kwa rate hii miaka 20 ijayo sijui kama kutakuwa na cheap labour tunayoiona leo. Wamefikia hatua ya kufunga automated bracelets kwenye kila kuku ili kumfatilia. Hapa wanakwepa gharama za wafanyakazi na wanaongeza usahihi wa taarifa. Unakuta shamba la kuku 20,000 kila mmoja amevaa kidani cha electronic.

Gharama za kuzalisha zinapanda taratibu, kitakachoibeba China ni sera za kukaribisha uwekezaji ambazo ni nzuri sana kuliko Marekani yenye makodi makubwa na ukaguzi mwingi. Kwenye miundombinu na nishati wako sawa.

Wasiwasi wangu ni kuona giants wa tech wanawekeza kwenye kulima matunda na kufuga kuku, I think hawajiamini kushindana katika soko la teknolojia pekee. Itakuwa maajabu kuona Intel inaanzisha mradi wa kufuga ng'ombe au Apple inapambana kusaidia walima nganongano, kuna makampuni ya kufanya hizi kazi.
You are right my friend, this is indeed a predicament for China: But the good thing is that China can also export her capital to Latin America or the African continent where there's abundant cheap labor, natural resources and a vast market for her finished goods. How do you see this ???

Mkuu T14 Armata you are too calm, observant and versatile: And for this you have my deepest respect !!!
Please keep up this good vibe,......
 
Fact check : Umekosea kusema kwamba USD haitishiwi na Gold mind you it is that any fiat currency you know (USD included) it is an artificial Gold
Mkuu hujadadavua vizuri: Fiat Money ina faida au hasara kwa uchumi wa Marekani ???
 
This is a very generous description from purposefully blind individual.
Slander.jpg
 
Kuhusu kuhamisha mtaji hii hatua bado sana kwa sasa.
China ina miundombinu mizuri sana na nishati ya uhakika kuliko nchi nyingine ambazo ni possible candidates. Kama zingekuwepo makampuni ya Marekani yangehama China kwa vile sera za US juu ya China zinasumbua baadhi ya biashara.

China ina watu wengi sana wenye elimu. Human capital yake ni educated na wana nidhamu ya kazi kama ilivyo kwa Japan. Afrika wengi ni wajinga and not suitable for large scale industrial output. Latin America nchi kama Mexico na Brazil bado hazijafikia kuwa mbadala wa China. Vietnam nayo bado, ingekuwa ni jimbo la China ingekuwa ya 13 kiuchumi.

Sasa kwa vile China ni kubwa na ina watu wengi bado. Haiwezi hamisha uzalishaji kwenda kwingine, itakuja uku kutafuta malighafi na uwekezaji wake mwingi ukifatilia ndio huu. Inawekeza kwenye bandari ili isafirishe malighafi zake na kuleta bidhaa zake, inawekeza kwenye uchimbaji. Hizo elimu na afya ni ufadhiri wala sio uwekezaji, hata Norway wanatupatia.

Pia kwenye soko. Sisi hapa Afrika tunanunua takataka nyingi kutoka China ambazo hazina thamani kubwa, Latin America nayo sio sana. Exchange baina ya US na China au US na Europe ni kubwa sana. Kuwekeza nchi maskini utakosa advantage ya kuuza kwa soko la ndani, mfano iPhone zinatengenezwa China na pia zina soko kuu uko.

Ikitokea China ikafikia level sawa za mazingira ya kazi ya Ulaya Mashariki bidhaa zake zitapanda bei. Njia rahisi ni kutumia AI na robotics kwenye production kuliko kuwekeza kwingine.

NB: Hapo mwisho mimi mwenyewe nakukubali sana humu ila umebadilisha avatar.
Napata shida kwenda na speed ya thread, sometimes napata interruptions kama sasa nimeitwa kufanya group discussion.
 
kwa hiyo tuseme ww unataka kutuaminisha IMF wanatudanganya sio juu ya uchumi wa china??? China is the worlds largest economy now China Is Now the World’s Largest Economy. We Shouldn’t Be Shocked. na xi jinping anataka kudouble uchumi wa nchi yake ndani ya miaka 30 ijayo
Nikufahamishe tu kuwa, hii imekuwa ni tabia ya Wamarekani kwa miaka mingi for some reason! Miaka ya 80 hadi 90, wanahabari na vyombo vya habari kwa ujumla vilikuwa vikiitangaza Japan wakati fulani katika namna ifananayo na hii ambayo vinaitangaza China hivi sasa.

By the way, kinachozungumziwa hapo ni Purchasing Power Parity. Hicho ni kipimo kimoja tu cha uchumi. Si sahihi kukitumia kama kigezo pekee cha nchi kuwa na uchumi mkubwa kuliko nchi nyingine. Unapotumia PPP kama kigezo pekee cha nchi kuwa na uchumi mkubwa kuliko nchi nyingine, unaweza kuulizwa swali: je, Nigeria ina uchumi mkubwa kuliko Sweden sababu tu ina PPP kubwa kuliko Sweden?

Hali ya kimaisha nchini Nigeria inaweza kuwawezesha kufanya manunuzi makubwa ya fungu la bidhaa kuliko Sweden kwa kiasi cha fedha kinachofanana. Let's say, nchini Nigeria, kwa dola 100 unaweza kununua pair 6 za viatu, lakini kwa dola 100 hizohizo ukiwa Sweden, unaweza kujikuta unanunua pair 2 pekee. Maana yake ni kuwa nchini Nigeria, pesa yake ya ndani ina higher purchasing power kuliko pesa ya Sweden nchini Sweden. Lakini, vipi kuhusu ubora wa viatu hivyo na kiwango cha matumizi ya bidhaa hiyo ukilinganisha nchi hizo mbili? Pia, vipi kuhusu ubora wa maisha na vipato vya raia kati ya nchi hizo mbili? Vipi kuhusu mapato yanayoingizwa kwa mwaka kitaifa kati ya nchi hizo mbili?
 
Ukiniwekea andiko la Huntington ambalo limezungumzia The Decline of America kabla ya hilo la kutoka Foreign Policy. Tena la miaka ya 50 kama ulivyosema mwanzoni ntakushukuru sana.


Vipimo vikubwa vya uchumi ni PPP, GNP na GDP. Kinachoaminika na taasisi kubwa za kimataifa kama IMF ni PPP.
GNP wamarekani wameacha kukitumia kwasababu kina madhaifu.


Kwani ili tuweze kokotoa PPP na kufanya ulinganifu wa Country's Output tunazingatia vigezo gani ???
Pia, ukiangalia The Big Mac Index 2020 ya PPP, Nigeria na Iraq zimezipita nchi kama Sweden na Norway kweli ???


Turudi kidogo kwa Adam Smith kidogo, taifa ambalo linauza sana bidhaa kuliko mataifa mengine kwenye soko la dunia ndiyo litakuwa na mirija mingi ya kufyonza pesa kutoka mataifa mengi duniani, hivyo ndilo ambalo litakuwa ni tajiri. Marekani amekuwa taifa kubwa kiuchumi duniani kwasababu ndiye aliyekuwa muuzaji mkuba wa bidhaa kwenye soko la dunia. Hili nalo lina ubishi ???


Tuachane na mikisio na tufanye rejea ya takwimu kutoka taasisi kubwa za kiuchumi duniani kama IMF. Wao wamesema kabisa kwamba kipimo bora na kinachoaminika na wao ni PPP kuliko GDP kwasababu GDP inategemea Market Rates which are not stable for a long time and only relevant to internationally traded goods. Non-traded goods are left out of the periphery. Unadhani ni sahihi kusema Marekani ina Uchumi mkubwa kuliko Uchina kwa kuzingatia Market Rates peke yake mkuu ???


Hebu tuache makisio ya wanazuoni na twende kwenye takwimu maana zile huwa hazidanganyi. IMF wanasema PPP ndiyo kikokotoo bora kabisa cha uchumi kuliko GDP kwasababu kinazingatia mambo mengi. Lakini nadhani itakuwa vizuri zaidi kama tusaidie kufahamu kwanza jinsi ambavyo PPP inakokotolewa halafu tufanye rejea ya The Big Max Index 2020 kisha mwisho kabisa turudi kwenye takwimu za IMF na WB.

NB: Maswala ya kisera na kidiplomasia ni muhimu lakini ni Subjective sana katika kuangalia mwenendo wa Uchumi wa nchi. Kuna nchi ambazo hazifanyi vizuri kidiplomasia, haki za binadamu na kisera lakini zinafanya vizuri kwenye soko la dunia. Au hapa ulikuwa unamaanisha nini mkuu ???

Karibu tuendeleze mjadala......
Kwanza kabisa, nimeshangazwa na ombi lako kuhusu andiko la Huntington la miaka ya 50 ambalo limezungumzia "decline of America". Nimeshangazwa kwa sababu sijapata kufahamu sababu juu ya ombi hilo. Je, ni kwa sababu hautaki kukubaliana na hoja yangu kwamba mjadala huu na mingine ya namna hii imekwisha jadiliwa toka miaka ya 50 ama ni kwa sababu nyingine tofauti?

Huntington, kwa maneno yake mwenyewe na katika maandiko na machapisho yake (kama umemfuatilia kwa makini) ameeleza kuhusu chimbuko la huo mjadala wa "decline of America". Kama umemfuatilia kwa makini, amezungumza kwamba alikuwa akiufuatilia huo mjadala tangu miaka ya 50 mwishoni na aliushuhudia huo mjadala ukishamiri katika vipindi tofauti-tofauti ama kwa lugha nyingine "waves". Wave ya kwanza ni kipindi ambacho USSR ilifanikiwa kurusha satellite ya Sputnik 1 mwaka 1957. Mafanikio ya USSR ya Sputnik 1 yaliamsha mjadala kwamba Marekani inaelekea kwenye "decline" na kwamba tayari kuna uwezekano kuwa imekwisha achwa nyuma na USSR katika masuala mbalimbali ambayo yamekuwa yakiiwezesha Marekani kuwa taifa lenye nguvu zaidi duniani. Hiyo ni miaka ya 50 mwishoni.

Kipindi kingine maarufu kilicho shamirisha mjadala huo ni miaka ya 70 mwishoni. Mafanikio ya kiuchumi ya Japan yalipelekea kuamsha mjadala wa namna hiyohiyo nchini Marekani kwamba uchumi wa Marekani inakabiliwa na tishio la ukuaji na Japan inakaribia kuizidi Marekani na huenda imekwisha izidi katika masuala mbalimbali muhimu ya kiuchumi. Pia, ukisoma machapisho ya karne hii ama ya hivi karibuni kuhusiana na hoja hii ya "decline of America", wasomi mbalimbali wanadai kuwa Marekani ipo katika "wave ya 5 ya declinism", na wanafuatisha trend ileile ya kina Huntington ya kuanzia miaka ya 50 mwishoni kuanzia USSR na Sputnik 1, kuelekea Vietnam war, kisha Japan, Ulaya na mpaka hivi sasa, China.

Tuendelee na mjadala!

Umetoa hoja kwamba tuachane na makisio na tuzitumie data zilizopo. Kwanza kabisa, hizo data unazozisema ndizo ambazo zimekuwa zikitumika kufanya makadirio au makisio mbalimbali ya kiuchumi ambayo yamekuwa yakitolewa mara kwa mara. Wataalamu wa masuala ya kiuchumi hutoa makadirio ya ukuaji wa uchumi kwa kuhusisha taarifa mbalimbali zilizopo za kiuchumi kutoka katika mashirika mbalimbali hususani haya tunayoyafahamu sana. Kuna taarifa kuhusu mapato ya nchi na uzalishaji katika kipindi cha muda maalumu, mapato ya raia kutokana na mapato ya nchi zao (per capita income), taarifa za ukuaji wa kiuchumi (GDP growth), na masuala mengineyo.

Hebu sasa tuangazie hizo data za kiuchumi. Nitauzungumzia uchumi wa Marekani kwa data za kiuchumi za hivi sasa ili ku-justify hoja yangu ya awali kuwa China bado haijaizidi Marekani kiuchumi. Fuatana nami!

1) Nominal GDP. Pato la taifa kwa mwaka. Mashirika mbalimbali duniani hasa yale tunayoyafahamu kama vile IMF, World Bank pamoja na UN yanatuambia kwamba, Marekani ni nchi yenye uchumi mkubwa zaidi duniani kwa kipimo cha nominal GDP ikifuatiwa na China. Kuna haja ya kuziweka takwimu hapa?

2) Net wealth ama national net worth. Thamani ya mali zote za nchi ukitoa madeni (assets minus liabilities), ikiwemo thamani ya mali zinazomilikiwa na raia wote kwa ujumla. Marekani ni kinara katika hili pia kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za kiuchumi.

3) GDP per capita. Pato la raia kutokana na pato la taifa zima kwa mwaka. Marekani inafanya vizuri zaidi hapa ukiilinganisha na China. Kulingana na data za hivi karibuni za kina IMF, WB na wenzake, Marekani imeorodheshwa katika nafasi kumi za juu ikishindana na nchi za Scandinavia, Luxembourg, Qatar n.k.

4) GDP per capita (PPP). Pato la raia katika kipimo cha Purchasing Power Parity kutokana na thamani ya bidhaa zote na huduma zinazozalishwa kwa mwaka. Pia, Marekani inafanya vizuri zaidi kuliko China kulingana na data zilizopo za hivi karibuni.

Sambamba na masuala hayo, kuna vipimo vingine ambavyo hutumiwa na wataalamu wa masuala ya uchumi kuonesha uwezo wa kiuchumi wa nchi kwa kuzingatia masuala mbalimbali muhimu. Kuna vipimo vya uchumi kama vile: Ease of Doing Business Index, Indices of Economic Freedom, Global Competitiveness Index n.k.

Ease of Doing Business Index. Hutumika kuonesha, pia kulinganisha nchi zenye urahisi katika kufanya shughuli za kiuchumi ama kibiashara. Hapa kuna masuala ya masharti rafiki ama rahisi ya kibiashara, ulinzi madhubuti na usalama wa mali, hakimiliki ama property rights hususani intellectual property n.k. Kwa mujibu wa ripoti za hivi karibuni, Marekani inatajwa miongoni mwa nchi zenye urahisi zaidi duniani katika kufanya biashara ikishindana na nchi kama vile Korea Kusini, Denmark, Singapore n.k.

Pia, kuna kipimo kingine kinachofahamika kama Global Competitiveness Index.
Watafiti wa masuala ya kiuchumi huangalia uwezo wa nchi kuweza kuufanya uchumi wake uwe na ustawi kwa jinsi ambavyo nchi hiyo inavyoweza kuzitumia ama inavyozitumia rasilimali ilizonazo.

Hapa kuna masuala kadhaa muhimu sana katika ukuaji na ustawi wa uchumi ambayo huangaliwa ama huzingatiwa:
a) Institutions ama taasisi za umma na zile za binafsi ambazo ni well-functioning.
b) Elimu bora (primary & higher education).
c) Afya bora.
d) Miundombinu mahususi.
e) Market size. Ukubwa wa soko la nje na lile la ndani.
f) Innovation. Uwezo katika uvumbuzi wa kisayansi na kiteknolojia.
g) Matumizi ya teknolojia zilizopo na mbinu za kisasa katika uzalishaji. Na kadhalika!

Marekani inafanya vizuri katika hili pia kuliko China. Kwenye ripoti kadhaa za GCI hasa za miaka ya hivi karibuni za World Economic Forum, Marekani imekuwa ikitajwa katika nafasi bora na za juu (ya kwanza ama ya pili) ikishindana na nchi za Scandinavia pia na nchi kama vile Singapore.

Marekani inafanya vizuri kuliko China katika studies nyinginezo muhimu kama vile Global Innovation Index (capacity for, and success in innovation) pia hata katika HDI yaani Human Development Index. Katika HDI kuna masuala kadha wa kadha ambayo huzingatiwa ikiwemo life expectancy ya watu, literacy rate n.k.

Kuna hoja umeiwasilisha kuhusiana na Purchasing Power Parity kwamba ni kipimo "kinachoaminika zaidi kuliko GDP", hapa nafikiri unamaanisha nominal GDP. Nafikiri hoja yako hapa haiko sawa!

Iko hivi,
Kila kipimo cha uchumi kinachotumika na mashirika makubwa kama vile IMF, World Bank na UN kina mipaka yake ya matumizi ama limitations. Wataalamu wa masuala ya uchumi kwa ujumla wanaposema kuwa kipimo fulani ni bora kuliko kingine, ni katika kuzingatia baadhi ya masuala pekee. Kuhusu PPP, ni kipimo kizuri hasa pale unapolinganisha bei ya bidhaa kati ya nchi moja na nyingine kulingana na masoko ya nchi hizo lakini kina mapungufu yake mengi ambayo kwayo hakiwezi kusimama kama kipimo pekee sahihi cha uchumi. Hivi sasa kuna mjadala mkubwa sana kuhusiana na hicho kipimo na baadhi ya vipimo vingine hali ambayo itapelekea wataalamu kuja na vipimio vipya hapo baadaye.

Wataalamu wa masuala ya uchumi wanaeleza kuwa, comparisons kwa kutumia kipimo cha Purchasing Power Parity are more useful than those using nominal GDP. Lakini, Purchasing Power Parity is limited when measuring financial flows kati ya mataifa mbalimbali. Pia huleta shida katika kulinganisha ubora wa bidhaa zinazofanana kati ya mataifa mbalimbali (kuna mfano nimeutoa katika post yangu iliyopita wakati nikijibu hoja ya mchangiaji fulani). Purchasing Power Parity pia inahitaji makisio zaidi ama estimations katika mahesabu yake kuliko nominal GDP. Yote hayo ni kwa mujibu wa IMF. Kwa logic ya kawaida tu, kipimo kinachohitaji makisio zaidi kuliko kipimo kingine sidhani kama kinaweza kusimama pekee kama kipimo bora zaidi ama cha kuaminiwa zaidi kuliko vipimo vingine vyote na katika masuala yote muhimu.

Asante!
 
Kwenye hoja ya pili, service market ndio ukomavu wa biashara na uzalishaji. Ndio maana kina Apple wanauza devices ila bado wanawekeza kwenye huduma kama Apple Tv na iOS za kuendeshea hizo products. China bado inazalisha tu ila kwa kasi sana inakuja. Marekani ina patents nyingi sana zinazotumika duniani na inaendelea kusajiri nyingine. Uzalishaji wa China hata Vietnam na India wanaweza jaribu kuweka mazingira rafiki wakavuta kiasi kidogo cha uwekezaji, US ana biashara ambazo huzikuti kwingineko kirahisi. Hatujaona China ikija na conglomerates kama CocaCola, Pepsi, Microsoft, McDonald's, Nike, Ford au Boeing.

Hatuoni dunia ikikimbilia kuwekeza kwenye soko la hisa la China, Wachina wenyewe makampuni yao makubwa wanayasajiri kwenye soko la Kimarekani. Hatuoni cream za dunia zikikimbilia China, Wachina wanaenda kusoma na kufanya kazi Marekani na sio kinyume chake.

Hatuoni fedha ya China ikifanya manunuzi, hata China yenyewe haijiamini ina-devaluate Yuan yao ili kuzuia matumizi yake kwenye exchange duniani. USD inazunguka dunia nzima bila kuathiri uchumi wa US.

Hapo namba tatu kwenye jeshi. Marekani ina jeshi kubwa mno na lenye nguvu. Dunia haijalishuhudia jeshi la US likiitetea mipaka yake, huwa tunaona vita za kujitakia ambazo wakishindwa simply wanaondoka. China haina silaha za aina yoyote kutishia Marekani, ukiachana na makombora kama DF-41 vita ya China vs US hakuna Mchina atakanyaga kwenye shores za mainland US. China doctrine zake ni kuizuia US isifike Southern China sea, hata ikitaka kufikisha majeshi yake eneo kama Maryland itaanzaje? Tangu WW2 tunajua madhara ya kupigia vita kwako yalivyo, US kaingia vita zote za karne ya 20 na 21 bila kupigana nyumbani.

Hizi Norinco na Shenyang haziwezi tengeneza silaha za kuzishinda Raytheon, General Dynamics, Boeing, Lockheed Martin, Huntington Ingalls, Northrop Grumman na nyingine nyingi za US.

China hakuna derivative ya DARPA yenye miradi mikubwa ya kimapinduzi kwenye ulinzi. Elimu ya China nayo sio supportive sana kwenye ulinzi kama US. Hata uuzaji wa silaha US anaongoza kuwauzia superpowers ila China bado ananunua silaha muhimu kwa Russia. China anauza silaha kwa kina Nigeria, Pakistan, Sri Lanka ambao wanakwepa masharti na kutafuta bei nafuu ila hawana budget ya kuchukua kwa wingi.

Bila hata allies US vs China lazima China isiishinde US kimapigano. US inaweza shinda au kutoka suruhu ila sio kushindwa. Kwanza experience aliyonayo US ni kubwa mno na yuko kila mahala duniani.

Kwenye ujasusi, cyber warfare na cyber security bado US anamzidi China. Hapa China hajaifikia Israel au Russia.

Tukiachana na ulinzi ambao ni muhimu kuhakikisha usalama wa biashara zote za nchi na ustawi wa sera zake. Maendeleo yajayo tumekubaliana yanatokana na nani anafanya nini na anamiliki nini kwa sasa katika teknolojia.

China ina kina Huawei, ZTE na CSMC ambao hawajazishinda Intel, AMD au Apple.

Kampuni kubwa za magari duniani haziko China. Hata kampuni za EV zinazoibuka US inaongoza ila China iko karibu sana.
5G China anaongoza ila wapo kina Ericsson na Nokia walikuwa wanakuja (hawana fedha). Ikumbukwe Nokia na Ericsson waliitoa 4G, Japan walishatoa 3G kupitia Docomo. Leo hii wako wapi?
Tutakuja kupata 6G wakitokea watu ambitious kama Elon Musk.

Artificial Intelligence na robotics wapo US, Japan na Russia wanakuja vizuri. Tumeona baadhi ya demo za robots kutoka US na Russia ila hatujaona demo za China. AI iko integrated sana kwenye teknolojia za magari kama Tesla na kwenye smartphone. Kwenye AI kompyuta na robots zitafidia watu na uzalishaji utapungua gharama uku kasi ikiwa ileils hakuna likizo wala kuchoka. China sioni kama anaongoza hapa, atategemea idadi yake ya watu na gharama zake ndogo za uzalishaji.

Nilitazama production site ya F-35, wanatumia laser beam kuelekeza mfanyakazi wapi pa kufunga nati, wapi pa kuchomeka hiki. China hana precision hii kwenye uzalishaji na hivo faults kwenye systems muhimu kama kompyuta hazikwepeki wakati huo speed ya kuzalisha hana ila atategemea wingi wa watu.

Teknolojia nyingine za zamani kidogo kwa US bado China hajazifikia. China hana true stealth technology ambayo US anayo tangu 1980s, hana uwezo wa kutengeneza injini za ndege kama P&W pale US, aircraft carrier ndio anayo moja ya kwake ikiwa diesel powered wakati US anazo zaidi ya kumi nuclear powered, nuclear submarines bado sana. Yani nuclear technology bado hajafikia US, mpaka majuzi hapa China ilikuwa inatumia coal wakati wenzake walishahama muda sana uko.

Katika ustaarabu na kutegemeana kwa mifumo na taasisi China haijaongoza. Benki, mashirika ya bima, mifuko ya uwekezaji popote duniani na taasisi zinazojitegemea viko zaidi wazi na endelevu kwa US. Utasikia FDA imezuia Monsanto kuuza dawa flani, FAA imezi-ground Boeing Max mpaka izichunguze, FBI imechunguza Russiagate na kukuta rais Trump hana hatia. Ingekuwa China ungesikia CPP wamefanya hivi, serikali imefanya kile, serikali ime...
Nchi haina hata mgawanyo wa mamlaka itaanzaje kuongoza ulimwengu.

Naamini ili nchi iipite Marekani lazima kwanza iifikie, hata Britain kabla haijapitwa na Marekani kwanza zililingana kisha Marekani akaipita. Sasa China hajaweza kulingana na Marekani, hayuko mzimamzima kuna vitu yuko mbele vingine nyuma kabisa uko
kwanza mimi ntaweka na refence kabisa, cha kwanza unatakiwa ujue China ndio nchi yenye uchumi mkubwa kwa sasa kwa mujibu wa IMF (IMF Admits China Has Overtaken The US As The World’s Largest Economy; But Why Is The Media Silent? )
kumvimbia marekani usifikiri ni ishu ya kitoto ni lazima uwe nae sawa au umemzidi

si kweli kwamba china haina conglomerates kubwa duniani, sema sio maarufu kama za west na nyingine ni kubwa kuliko hata za west, Alibaba, Huwawei hizo ni kampuni ndogondogo China, katika makampuni 10 makubwa zaidi duniani , matano yametoka china manne us na moja saudi arabia, kampuni la kwanza na la pili kwa ukubwa duniani yote yametoka china (https://www.forbes.com/global2000/#142b81a9335d )

soko la hisa halimaanishi kwamba uchumi wako ndio mkubwa kuliko mwingine, na wala soko la hisa sio kigezo cha uchumi wa nchi ndio maana China hilo jambo sio ishu sana, Makampuni mengi ya china wanaorodheshwa marekani lakini mwisho wa siku faida kubwa inaenda kwenye makampuni ya china na sio marekani! ndio maana kuna baadhi ya makampuni trump aliyatoa sokola hisa marekani

Suala ya yuan kutokutumika kimataifa huu ni mfumo ambao china wanautaka wenyewe na yuan hawataki ipande thamani kuliko dola kwasababu ya kuvutia uwekezaji wa moja kwa moja! ukiwa na dola mia ni rahisi kuwekeza China kuliko marekani! dola 100 kwa marekani ni hela ya maji ya kunywa tu lakini ukiwa china hiyo hela unaweza fanyia mengi sana! Ndio maana mpaka kesho china hawezi pandisha thamani ya yuan ili kuvutia watu na marekani hua analalamika sana kila siku juu ya hili lakini hawez fanya lolote,mpaka kampuni kama telsa na apple kuwekeza china ndo ujiulize

China ni mtengeneza silaha mzuri tu, ila sio muuzaji silaha kila nchi na strategy yake, china, india na urusi ndo nchi pekee zina hypersonic missiles mpaka sasa hata hao marekani na israeli hawana ! china ina jeshi kubwa kuliko nchi yoyote duniani (29 Largest Armies In The World) , China ndo nchi yenye jeshi la majini kubwa kuliko nchi yoyote
(China Has The World’s Largest Navy. And It’s Getting Better, Pentagon Warns )

china ndo nchi inaoongoza kwa matumizi ya artificial intelligence duniani (China Leads in Practical AI | Enterprise IT News) na kampuni zinazojihusisha na AI ni nyingi China kuliko marekani

Kwa mara ya kwanza china imeipita marekani kwa mauzo ya filamu duniani (In 2020, China Surpassed America In Box Office Revenue ) china haiitaji hollywood tena bali hollywood ndo inahitaji china kwa sasa

kwenye cyber security china wapo vizuri sanaaa, waliwaibia NSA pentagon silaha ya kufanyia hacking (Chinese spies stole NSA hacking tools, report finds) na wakaitumia kuwa hack wao wenyewe kwa miaka kadhaa bila kushtukiwa, kwenye cyber securty China na Urusi wapo vizuri sana kuliko unavyofikiri

suala la vita , experience na vifaa kwenye vita vina advantage ndogo sana, marekani alipigwa na kataifa kadogo sana ( vietnam)lenye silaha duni sana na bila experience yoyote mpaka akakimbia akarudi kwako! vita ni teknik bana sio silaha wala experience! unaweza pigana vita miaka 20 mfululizo lakini ukaja kupigwa na mtu ambae hakuwahi kunyanyua hata jiwe maishani mwake! hakuna siku marekani atamvamia na kumpiga mchina, america hana uwezo huo hata china hawezi piga marekani! hizi nchi kamwe haziwez kuingia vitani kwasababu hakutakua na mshindi kati yao
 
kwanza mimi ntaweka na refence kabisa, cha kwanza unatakiwa ujue China ndio nchi yenye uchumi mkubwa kwa sasa kwa mujibu wa IMF (IMF Admits China Has Overtaken The US As The World’s Largest Economy; But Why Is The Media Silent? )
kumvimbia marekani usifikiri ni ishu ya kitoto ni lazima uwe nae sawa au umemzidi

si kweli kwamba china haina conglomerates kubwa duniani, sema sio maarufu kama za west na nyingine ni kubwa kuliko hata za west, Alibaba, Huwawei hizo ni kampuni ndogondogo China, katika makampuni 10 makubwa zaidi duniani , matano yametoka china manne us na moja saudi arabia, kampuni la kwanza na la pili kwa ukubwa duniani yote yametoka china (https://www.forbes.com/global2000/#142b81a9335d )

soko la hisa halimaanishi kwamba uchumi wako ndio mkubwa kuliko mwingine, na wala soko la hisa sio kigezo cha uchumi wa nchi ndio maana China hilo jambo sio ishu sana, Makampuni mengi ya china wanaorodheshwa marekani lakini mwisho wa siku faida kubwa inaenda kwenye makampuni ya china na sio marekani! ndio maana kuna baadhi ya makampuni trump aliyatoa sokola hisa marekani

Suala ya yuan kutokutumika kimataifa huu ni mfumo ambao china wanautaka wenyewe na yuan hawataki ipande thamani kuliko dola kwasababu ya kuvutia uwekezaji wa moja kwa moja! ukiwa na dola mia ni rahisi kuwekeza China kuliko marekani! dola 100 kwa marekani ni hela ya maji ya kunywa tu lakini ukiwa china hiyo hela unaweza fanyia mengi sana! Ndio maana mpaka kesho china hawezi pandisha thamani ya yuan ili kuvutia watu na marekani hua analalamika sana kila siku juu ya hili lakini hawez fanya lolote,mpaka kampuni kama telsa na apple kuwekeza china ndo ujiulize

China ni mtengeneza silaha mzuri tu, ila sio muuzaji silaha kila nchi na strategy yake, china, india na urusi ndo nchi pekee zina hypersonic missiles mpaka sasa hata hao marekani na israeli hawana ! china ina jeshi kubwa kuliko nchi yoyote duniani (29 Largest Armies In The World) , China ndo nchi yenye jeshi la majini kubwa kuliko nchi yoyote
(China Has The World’s Largest Navy. And It’s Getting Better, Pentagon Warns )

china ndo nchi inaoongoza kwa matumizi ya artificial intelligence duniani (China Has The World’s Largest Navy. And It’s Getting Better, Pentagon Warns) na kampuni zinazojihusisha na AI ni nyingi China kuliko marekani

Kwa mara ya kwanza china imeipita marekani kwa mauzo ya filamu duniani (In 2020, China Surpassed America In Box Office Revenue ) china haiitaji hollywood tena bali hollywood ndo inahitaji china kwa sasa

kwenye cyber security china wapo vizuri sanaaa, waliwaibia NSA pentagon silaha ya kufanyia hacking (Chinese spies stole NSA hacking tools, report finds) na wakaitumia kuwa hack wao wenyewe kwa miaka kadhaa bila kushtukiwa, kwenye cyber securty China na Urusi wapo vizuri sana kuliko unavyofikiri

suala la vita , experience na vifaa kwenye vita vina advantage ndogo sana, marekani alipigwa na kataifa kadogo sana ( vietnam)lenye silaha duni sana na bila experience yoyote mpaka akakimbia akarudi kwako! vita ni teknik bana sio silaha wala experience! unaweza pigana vita miaka 20 mfululizo lakini ukaja kupigwa na mtu ambae hakuwahi kunyanyua hata jiwe maishani mwake! hakuna siku marekani atamvamia na kumpiga mchina, america hana uwezo huo hata china hawezi piga marekani! hizi nchi kamwe haziwez kuingia vitani kwasababu hakutakua na mshindi kati yao
Hivi technology Kama ya cocacola ina nafasi gani Kwenye uchumi kwa Karne ya 21
 
Back
Top Bottom