"Will Powers!", "Faith Healing!"-Nguvu za Kufanya Miujiza ya Uponyaji kwa Imani. Kila Mtu Anazo!

Kwanza mimi sio mchungaji!.
Yes nimefanya meditation kidogo tuu kwa kujisomea not in class!, sifanyi zile za class kuepuka masharti, mimi pombe natumia, kujirusha najirusha, na ile starehe number moja duniani kwa viumbe vyote pia natumia, vitu ambavyo meditation inapiga marufuku kabisa!.

Pasco
 
,Mada yako iko poa. Watu wamejiimarisha kiuchumi Kwa kutumia utapeli huu Kwa namna ya pekee. Je serikali inapata kodi kwao? Wachungaji wa uponyaji ukiwahoji kuhusu kipato chao wanakuwa wakali sana
 
imenivutia sana hii, ahsante kwa kutupatia ujuzi huu :nod:
 
Mungu ajlie usiwe na affiliation na shetani Pasco:shocked:
 

Du, yaani Pasco unakuwa broader kuliko Yesu? Kweli nimeamini "Kufanikiwa kwa m.p.u.m.ba.v.u kutamuangamiza".
 
Nasoma huu uzi wote bila kuruka hata kipengele kimoja
 
sio bure naona unaendelea kusisitiza kuwa YESU haponyi au ndo mambo ya NWO ,umetumwa kuja kuiangamiza jamii yetu
mim napata shida kweli...anasema kinachoponya ni power aliyonayo mtu anaeponywa,sas yesu alipomfufua lazaro...teyari lazaro alishakufa sas hiyo power ilitoka wapi kwa lazaro
 
tomjelly natumai utapitia hapa

hakika nimewasili. nimesoma, nimeelewa na akili inafunguka zaidi. Point ya kushikilia ni "The power within" nshaanza mazoez ya kusogeza vitu kwa macho (nkifanikiwa ntawaambia). kwani tayari nina uwezo wa kujua kitakachotokea kabla hakijatokea, only kwa kuiskiliza nafsi yangu ya ndani bila kuhusisha imani a Ya dini yoyote. naamini tu naweza kwa kutumia nguvu iliyopo ndani yangu.
 
Last edited by a moderator:
"Belief is a positive word and therefore creative. Everything positive is alive and works. Everything negative is dead and has no creative power." nimenukuu kutoka kitabu cha Bring out the magic in your mind Page 9 - by Al Koran.
 
hv mkuu Pasco hauna blog? kama unayo tuambie inaitwaje ili tujifunze zaidi.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Pasco umesema ukweli kuwa kuna watu wana nguvu ya Uponyaji pasipo na wao kujijuwa lakini wengine wana nguvu za uponyaji kwa kutumia njia ya Shetani hawana Nguvu za uponyaji Nature. Mimi ninazo nguvu za Uponyaji ninapo mshika mgonjwa kwa kutumia Mikono yangu kisha nikamuombea mgonjwa dua basi ataweza kupona kwa asilimia 99% nimesha jaribu sana na wengi niliowafanyia uponyaji kutokana na mikono yangu wamepona. Ninajijuwa kuwa ninao uwezo wa kumponya mtu kwa kutumia mikono yangu.


 
Last edited by a moderator:

Nguvu zako wewe ni za nature au unatumia njia ya shetani? Hongera kwa kuwa na nguvu hizo
 
Last edited by a moderator:
Bravo mkuu MziziMkavu nguvu hizo ndo zinazofaa
 
Last edited by a moderator:
Pasco tupo pamoja na unazidi kunipa nguvu zaidi. Naomba unisaidie ktk hili. Nikiwa mdogo nilikua nikiwaza kitu kinatokea. Mfano tulikua na jiran yetu ambe tangu nikae hapo sikuwai kumuona. Siku moja huyo jiran alitoka nje bibi yangu akamsalimia. Nikamuuliza bibi mbana huyu simjui akasema ni.jiran yetu.na yupo hapa siku zote nikamjibu hata angekufa jana ningejiuza sana yukoje. Ajabu usiku ule alikufa. Nilishangaa sana. Tukio lingine kuna kaka mmoja nilikutana nae akiwa amelewa sana nikawaza huyu anaweza akagongwa na gari na maiti yake isijulike ona anavoyumba. Baada ya mda nikasikia kagongwa na tren. Matukio hayo. Na mengine mengi yalikua yakitokea. Sasa mimi.mtu mzima, bado.najihisi.nina nguvu za miujiza ila sijajua jinsi ya kuzitumia vizuri. Mf lilibahatika kuwa na watoto wa kike tu. Baada ya miaka 8 bila kupata mtoto nilitaman tena kupata mtoto wa kiume.ile hali ilinisukuma sana na ikapelekea kuanza kununua nguo za kiume, viatu. Nk vyote vihusuvo mtt wa kiume nikiwa sina hata mimba. Miezi 7 badae nilipata ujauzito rohon niliamin.kabisa ajae ni mtoto wa kiume. Na jina nililokua nalo rohon ni.gudluck. sikuwahi kujadili na baba ake lolote juu ya mtt ajae. Baada ya miez 9 Nilipikea mtt wa kiume nilipomjulisha baba ake akanoambia asante huyo ataitwa gudluck. Shuhuda mwingine ni huu ndani kwangu kulikua na mende wengi wasioisha hata upulize dawa vip. Siku moja nikachukua maji nikayaombea kisha nikanyunyiza ndan nikaondoka huku nikisema nikirudi mende wote watakua wamekufa. Niliporudi nilishangaa kuona mende wate wamekufa na ni miaka 3 sasa wale mende hawapo. Naweza nikakaa nikawaza ghafla kuwa mume wangu ana mwanamke nashika simu.nampigia halafu namuomba anipe huyo alie nae nimsalimie atakata simu atazima akiamin huwenda nimemuona ajabu sijamuona ila alimudithia mdogo wake kuwa anajiuliza sana nina nini kwani kila ninachomwambia huwa ni.kweli na wakati mwingine huwa mikoan. Alimwambia mdogo wake imefika mahali ananigopa kwani kila ninachamtahadharisha asipozingatia hutokea. Naomba no.ya simu ili unipe ushauri zaid..binafs mimi ni.mkristo ila siamin kabisa kuombewa naamini.kujiombea, siamin mch, padri, askofu, nabii, mitume nk. Yaan siamin kabisa kabisa. Naamin sana mimi kama mimi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…