William Miller: Kama Yesu hakujua Hisabati au kutafsiri mambo bora angalikaa Kimya. Mbona siku ya mwisho wa dunia inakokotoleka kirahisi?

William Miller: Kama Yesu hakujua Hisabati au kutafsiri mambo bora angalikaa Kimya. Mbona siku ya mwisho wa dunia inakokotoleka kirahisi?

Umeandika kiushabiki sana. Lengo lako ni kuwaattack wasabato na wala si vinginevyo.

Mambo mengi uliyoeleza hapa si ya kweli, kama ifuatavyo.

1. Miller haukuwa msabato na hata kipindi akiwa anahubiri kurudi kwa Yesu, hapakuwa na dhehebu la kisabato.

2. Mama White pia hakuwa msabato kipindi hicho maana hapakuwa na hilo dhehebu, na wala hakuwa mwanzilishi wa hiyo kanuni ya kurudi Yesu unayoisema, isipokuwa alikuwa mfuasi wa Miller.

3. Papa hatawafumusha wasabato kusali jumamosi kama ulivyodai, badala yake atawalazimisha watu wote kusali siku ya kwanza ya juma (yaani Jumapili) badala ya siku ya saba ya juma (yaani Jumamosi).

4. Yesu yuko katika chumba cha patakatifu pa patakatifu mbinguni akifanya huduma ya uombezi, na si kwamba ameshaanza kushuka kuja duniani kama unavyodai. Maana patakatifu pa patakatifu ni mbinguni.

5. Wasabato hawaja set siku yoyote ya kuja kwa Yesu kama unavyotaka kuwaaminisha watu, badala yake wamaamini kwamba Yesu amekaribia sana maana dalili karibia zote zimeshatimia.

6. Pamoja na kukosoa mahesabu ya Miller kuhusiana na unabii wa Daniel wa siku 2,300, hujatoa tafsiri mbadala wa unabii huo kana k
kwamba unabii huo hauna maana yoyote kwa wanadamu wa leo.

7. Ukweli ni kwamba, mahesabu ya Miller yalikuwa sahihi, kwamba mwaka 1844 kulikuwa na tukio kubwa lilikuwa linaenda kutokea. Kosa la Miller ni kwamba, alitafasri vibaya kuwa hekalu ni dunia na kutakaswa kwa Hekalu ni dunia kusafishwa kwa moto (kama ulivyoelezea vizuri kabisa).

Ukitaka kujua tafasri ya huo unabii wa siku 2,300 unakaribishwa kuuliza.
Kulingana na namba saba,
Unamaana tafsiri ya Miller ni ya akili zake na hakuongozwa na Roho mtakatifu ambae wasabato wa sasa wanaamini alikuwa anamuongoza yy na Ellen,namba 1 na 2,kwa hyo baada ya wao kudanganya ndo wakaanzisha usabato na mkawafuata,
Kwa hiyo ninyi ni wafuasi wa waongo maarufu wawili kuwahi kutokea?
 
Kulingana na namba saba,
Unamaana tafsiri ya Miller ni ya akili zake na hakuongozwa na Roho mtakatifu ambae wasabato wa sasa wanaamini alikuwa anamuongoza yy na Ellen,namba 1 na 2,kwa hyo baada ya wao kudanganya ndo wakaanzisha usabato na mkawafuata,
Kwa hiyo ninyi ni wafuasi wa waongo maarufu wawili kuwahi kutokea?
Kukosea kutafsiri unabii siyo dhambi...hata wayahudi hawakuulewa unabii wa ujio wa Yesu, walikuwa wanamsubiri masihi mwingine. Hata wanafunzi wa Yesu walikuwa wanajua kuwa Yesu anakuja kusimika ufalme wake duniani, na ndiyo maana alivyowaambia anaenda zake mbinguni hawakumuelewa.

Pointi ni kwamba, huo unabii ulikuwa unalenga tukio fulani, lakini si kama yeye alivyoelewa, swali ni kwamba nyie mnaombeza Miller mnatoa tafasri gani ya huo unabii?
 
Wanazuoni:

Kichwa cha habari hapo juu sio kwamba ni cha uchochezi au kwamba kimelenga kupasukia watu kwa kashifa au kwamba ni kufuru kwa Mungu.La hasha, bali ni tafsiri ya kile alichomaanisha Mwanajeshi mmoja huko Marekani pale alipoibuka na Formula ya kukokotoa tarehe ya kurudi kwake Yesu duniani. Jamaa huyo anaitwa WILLIAM MILLER.

William Miller alizaliwa tarehe 15 Februari1782, huko Jimboni Massachusetts, Marekani na kisha kulelewa katika familia ya Kikristu iliyokuwa na makazi yake Jimbo la New York ya Kaskazini.Familia ya William Miller ilikuwa ya Kibaptisti. Babu yake na wajomba zake wawili walikuwa ni wachungaji katika kanisa la Wabaptisti. Kanisa la Kibaptisti, ni mumeguko karne ya 17 BK kutoka Kanisa la England,yaani Kanisa la Serikali ya Uingereza (Anglikani) ambalo leo linaitwa Kanisa la Kianglikana.

Miller, katika ujana wake alipata kujiunga na jeshi laMarekani na kufikiaCheo cha Kapteini, wakati wa vita kati ya Marekani na Uingereza (Great Britain) mnamo mwaka 1812.Na inasemekana alikuwa na akili sana na kwamba alikuwa na kipaji cha kufafanua mambo.Bwana Miller baada ya kumaliza utumishi wake Jeshini na kurudi toka vitani (kati ya Marekani na Uingereza mwaka 1812), alianzisha makazi katika Shamba lake huko Low Hampton, New York, ambamo alikuwa amejenga nyumba na akawa akiishi hapo na wakati fulani akawa akienda kusali kwenye kanisa la Baptist la karibu yake.

Bwana Miller kwa kujishughulisha na mambo ya kiimani alipata kuwa mwana-DEIST,yaani alipata kuamini katika Falsafa ya Deism.

Deism ni Falsafa inayokazia kwamba Mungu hajihusishi moja kwa moja na mambo ya ulimwengu huu; kwamba yeye ndiye muumba wa vyote na kwamba ni mkamilifu lakini mungu huyo, hajiingizi katika mambo ya ulimwengu unaonekana kwa njia ya miujiza na kuwa ufunuo sio chimbuko pekee la maarifa juu ya imani na kwamba kufikiri tu kwa mwanadamu na kufanya utafiti juu ya maumbile kunatosha kufahamu na kubainisha kwamba kuna Mungu mmoja.

Kwa hiyo, tafsiri ya imani hii ya Deism ni kwamba Mungu baada ya kuumba ulimwengu alijiondokea zake na kuacha vitu vyote tuvirithi na tokea wakati huo hana mpango navyo tena na wala hajali yanayoendelea huku duniani.

SASA katika mkururu huo wa kutaka kuchimbua mambo magumu ndio William Miller alijikuta akivamia suala ambalo ndio kiini cha mjadala huu wa leo.Ni suala la tarehe ya kurudi kwa YESU KRISTU.

Ni hivi, kwa muda miaka miwili William Miller alipata kujichimbia ndani kwake “akibundi” au akibukua Biblia na ndipo katika kukisoma Kitabu cha Nabii Daniel, sura 8:13-19 ambacho kiliandikwa kabla hata Yesu hajazaliwa akagundua fomula ya kukotoa tarehe ya kurudi kwa Yesu duniani ambako inasomeka hivi:

“13.Ndipo nikamsikia mtakatifu mmoja akinena, na mtakatifu mwingine akamwuliza huyo aliyenena, Haya maono katika habari ya sadaka ya kuteketezwa ya daima, na lile kosa lifanyalo ukiwa, yataendelea hata lini, kukanyagisha patakatifu na jeshi? 14 Akamwambia, Hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa. 15 Ikawa mimi, naam, mimi Danieli, nilipoyaona maono hayo, nalitafuta kuyafahamu, na tazama, alisimama mbele yangu mmoja mfano wa mwanadamu.16 Nikasikia sauti ya mwanadamu katikati ya mto Ulai, iliyoita na kusema, Gabrieli, mfahamishe mtu huyu maono haya.17 Basi alipakaribia mahali niliposimama; nami naliogopa alipokaribia, nikaanguka kifudifudi; lakini aliniambia, Fahamu, Ee mwanadamu, kwa maana maono haya ni ya wakati wa mwisho.18 Basi alipokuwa akisema nami, nalishikwa na usingizi mzito na uso wangu uliielekea nchi; lakini alinigusa, akanisimamisha wima.19 Akaniambia, Tazama, nitakujulisha yatakayokuwa wakati wa mwisho wa ghadhabu; maana, ni ya wakati wa mwisho ulioamriwa.”

Kanuni ya Miller inadai kwamba kinabii siku moja kwa Mungu ni sawa na mwaka mmoja wa Kalenda ya wakati huo na hata sasa. Kwa msingi hiyo, siku alizoziongelea Daniel kwa jicho la Miller ni sawa na miaka 2,300 kwa kutumia Kalenda ya wakati huo ambayo ilikuwa ni ya Gregori na ambayo inatumika hadi sasa. Kalenda ya Gregori ilianza kutumika nchini Marekani mwaka 1752. (Kalenda ya Gregori ilizinduliwa rasmimwaka 1582 na kuanza kutumiwa na nchi kama Ufaransa, Italia, Polandi, Ureno na Uhispania).

Katika Sadikifu(thesis) hiyo ya Miller, alikaza kudai kwamba wapo wasomi wengine kama yeye ambao tafiti zao zimeonyesha kuwa tarehe ya kurudi kwa Yesu INAKOKOTOLEKA KIRAHISI SANA. Miongoni mwa wanazuoni waliotajwa alikuwa ni Mwanasayansi Sir Issac Newton.Huyu kwa mjibu wa Miller anadai naye alipata kufanya hesabu kama zake (alipokuwa akitafiti juu ya Kanuni za asili zinazotawala mvutano kati ya Dunia na Jua, Laws of Gravity) na kupata majibu sawa na ya Miller juu ya unabii huo wa Biblia wa kurudi kwa Yesu, na kwamba Newton aliacha maandishi mengi sana juu ya jambo hilo!

Kwa maelezo ya Miller na kwa kadri ya “ufunuo wake” na kwa kanuni yake (ya Kitabu cha Daniel) na kwa kusoma historia, aliweza kwa hakika kwa madai yake kuona kuwa mwaka wa kuanza kuhesabika hizo siku 2,300 ambazo ni sawa na miaka 2,300 ilikuwa mwaka 457K.K. Kwa hiyo, kwa kutumia alichofanya ni kuchukua huo mwaka 457BK ns kutoa miaka 2,300 na hivi kupata jibu la 1843 kwamba ndiyo ingalikuwa ni muda wa kutakaswa “patakatifu pa patakatifu.” Hata hivyo baadaye tarehe ilisogezwa mbele hadi tarehe 22 Oktoba 1844.

Mathematically,Kanuni ya Miller ilikuwa ni hii:

2,300-457=1843 (siku ya kuingia Yesu duniani).

Vigezo alivyotumia Miller katika kuthibitisha Sadikifu yake

Kuna mambo mawili Miller aliyatumia katika kuthibitisha kwamba fomula yake ilikuwa sawa:

  • Miller alidai kuwa uelewa wa watu wa wakati wake ilikuwa kwamba patakatifu pa patakatifu kulimaanisha ulimwengu wetu tunamokaa.
  • Kutakaswaa kwa Ulimwengu tena kwa moto kulikuwa na maana ya kufikia mwisho na kufikia mwisho kwa dunia maana yake ni Yesu Kurudi?
Nini kilitokea baada ya Fomula ya kurudi Yesu kugunduliwa?

Baada ya Miller kuwa amechoropoka na fomula yake alianza kupita huko na huko akiwahubiria watu ili wachukue tahadhari kwa kujiandaa kumpokea Yesu.Miongoni mwao alikuwa mwanamama anayedaiwa kuwa “Nabii mahiri” sana kuwahi kutokea hapa duniani(kwa sababu aliwahi kupewa maono zaidi ya 2000) kusimika usabato duniani na ambaye anatajwa kuwa ndiye amepewa “maono” juu ya jinsi ambavyo Papa atawafumusha wasabato waanze kusali Jumamosi siku zijazo.

Msimamo wa yesu juu ya mwisho wa dunia

Utakumbuka kuwa Kitabu cha Daniel kiliandikwa miaka mingi sana kabla Yesu hajazaliwa.Na utaona kwamba hata Kanuni ya Miller juu ya kurudi kwake ilianza kuhesabiwa mwaka 457BK. Kwa hiyo, wakati Yesu anazaliwa kitabu cha Daniel kilikuwepo tayari na hizo habari za kutakaswa Patakatifu pa Patakatifu Yesu alikuwa amezisoma.

Pamoja na ukweli huo wote kwamba Yesu alikuwa amekisoma kitabu hicho bado alipoulizwa juu ya mwisho wa dunia alisema hivi kwa kadri ya Injili ya Matayo 24:35-38:

“35 Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.36 Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.37 Kwa maana kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.38 Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina.”

Analysis ya Sadikifu ya “Mwanahisabati” Miller

Kwa kuisoma Sadikifu (thesis) ya Miller na msimamo wa Yesu juu ya mwisho wa dunia,yafuatayo yanajitokeza:

1. Miller na wenzie walikosea wapi katika fomula yao kiasi kwamba Yesu hajawahi kuonekana toka mwaka 1843?

2. Je, wanahisabati wanaweza kuendeleza pale Miller na wenzie walipoishia katika kukokotoa mwisho wa dunia kwa kuihakiki hiyo fomula ya Kisabato juu ya kurudi kwa Yesu?

3. Je, Miller na wenzie hawakuwa wamefanikiwa kulisoma Agano Jipya ambamo msimamo wa Yesu juu ya tarehe ya mwisho wa dunia unawekwa wazi wazi kuwa tarehe husika haijulikani?

4. Je, ikiwa Miller na wafuasi wake akiwemo Mama wa “maono”,Ellen White, walikuwa wamelisoma Agano Jipya ni kwa nini wao waliamua kuasisi Fomula ya jambo ambalo Yesu alikwisha kusema hana uwezo nalo?

5. Je, kwa Yesu kusema haijui tarehe halafu Miller na Ellen White wakaja wakasema wanaifahamu tarehe ina maana Wasabato hao na wa leo mbingu ni yao kiasi kwamba wanaingia na kutoka hata wameweza kushirikishwa yanayoendelea huko Mbinguni?

6. Je, kwa Miller na Ellen kukubaliana kwamba wao walikuwa wameipata fomula ya kurudi kwa Yesu walimaanisha kwamba wao walikuwa ni wasomi sana na kwamba Yesu kusema haijui tarehe kulimaanisha Yesu alikisoma Kitabu cha Daniel na kutokikielewa au kwamba Yesu alikuwa anasoma mambo kwa kurukaruka?

7. Je, hadi sasa tumsikilize nani kati ya Yesu na wasabato juu ya mwisho wa dunia kwa sababu Ellen White ameshapewa maono yanayoonyesha kwamba Yesu ameshaanza kushuka na kwamba kwa sasa yuko katika chumba cha patakatifu pa patakatifu sana ambako anapitia majina ya wasabato na akitoka hapo moja kwa moja anatia timu hapa duniani?


Kwa yote hayo,sasa KARIBUNI kwa mjadala.
Kwa Wasabato, dhambi wanayoichukia sana kuliko zote ni '' kufanya ibada siku ambayo siyo Jumamosi''! Kusema uongo si kitu kwao!
 
Ilishaandikwa "Hakuna ajuaye siku wala saa ya kurudi kwa mwana wa Adam" ikimaanisha kurudi kwa Yesu Kristo ni siri ya Mungu mwenyewe, kwahiyo huyo Miller na wapuuzi wenzie waondolee huko upuuzi wao


Mkuu:

Tusipuuze hiyo formula ya Miller.Inawezekana labda kuna jambo la maana kizazi cha leo na vijavyo vinaweza kujifunza .

Yawezekana labda wataalamu wa Hisabati wakikaza macho na akili kunaweza siku za mbele kutokea kugundua fomula sahihi.Ninasema hivyo kwa sababu wafuasi wa Miller, Ellen White na wenzie, walisema Miller alikosea padogo tu katika kufikiri kwamba siku ile ya 22 Oktoba Yesu angaliwasili kabisa duniani kumbe Yesu aliamua kupumzika katika "chumba" fulani kinaitwa "patakatifu pa patakatifu.Na yuko hapo hadi leo akikagua daftari wa wafuasi wa Usabato.Hirum Edson, mwanzilishi mmoja wapo wa usabato alimuona Yesu akiingia hapo "chumbani" na hata wafuasi wake kama Ellen White ambaye alibahatika kupewa maono 2000 alimuona Yesu sehemu hiyo na ndiyo maana aliandika machapisho lukuki juu ya namna hukumu ya kipelelezi inavyoendeshwa sehemu hiyo na Yesu.

Na ndio maana sasa tunawaalilka wanahisabati wasiuweke pembeni huo mchakato wa Miller wa kutumia fomula ili kufahamu lini Yesu anaingia hapa maskani. Inawezekana siku moja dunia ikaja kuokota kitu cha maana sana huko mbeleni.

Na katika kufanya hivyo ni vizuri tukashirikiana na wasabato kwa sababu hawa jamaa walibahatika kumuona Yesu akiingia humo chumbani na wanamuona kila mara akiendelea na kazi yake ya kupitia daftari la wateule wa kisabato.
 
1. Tueleze hilo tukio ni lipi ambalo unabii ulikuwa unalenga?

2. Hivi unaelewa maana ya unabii?

3. Kwa maelezo yako anayeweza kukosa kuelewa unabii ni mpokea Unabii au mtoa unabii?

4. Unapowatolea mfano Wayahudi, je, wayahudi ndio waliokuwa wametoa unabii au wao walikuwa wapokea unabii?

5. Unapotolea mfano wa wanafunzi wa Yesu kutoelewa kupaa kwake Mbinguni unamaanisha wanafunzi ndio waliotoa huo unabii au wao walikuwa wapokeaji wa unabii husika tu?

6.Je,historia inaonyesha kwamba manabii mbalimbali walipewa unabii au ufunuo fulani na Mungu.Je,unapojitetea kwamba hutokea unabii usiende sawa unaweza kutupatia mifano isiyoacha shaka ya manabii ambao waliwahi kutoa unabii na ukashindwa kwenda sawa sawa?

7.Ellen White aliwaachia wasabato unabii kibao ikiwemo wa Kanisa Katoliki kupitia Papa kuja kuwatesa wasabato, je kwa kutumia utetezi wako wa kwamba hutokea unabii uka-deviate from the reality,unaupa ufunuo au unabii huo wa Ellen White asilimia ngapi kutimia?
 
Mkuu:

Hii yote inatokana na uelewa mdogo wa maandiko matakatifu.Yesu alikuja kufafanua zile Amri kumi kwamba zote ni UPENDO.Kwamba ni upendo kwa Mungu na kwa binadamu wenzetu na mazingira yanayotuzunguka.Kwa hiyo, ukikosa kipengele kimoja unakuwa umekosa upendo wote na Mungu atakuhukumu kwa kukosa upendo na wala si kwa sababu ulikuwa hukosi sabato Jumamosi pamoja na kuongopa na kupotosha watu wake!

Hawa jamaa wanawapotosha sana wafuasi wao kwa kuwajengea chuki dhidi ya wanadamu wenzao wasiokutana nao huko Kanisani kwao Jumamosi.Wanawajengea matumaini makubwa kwamba kwa vile ni wasabato tayari wanayo tiketi ya kuingia Mbinguni na kwamba majina yao yalishaandikwa tayari na ndio maana Yesu alishaanza kushuka kutoka Mbinguni na yuko mahali fulani kwa kazi moja tu ya kupitia majina hayo.Unaweza kuona Ellen White kwa uelewa finyu wa maandiko aliwahi kuwaambia wasabato wenzie wauze mali zao ili wachangie kazi za utume ikiwa ni maandalizi ya kumpokea Yesu mwaka 1885 baada ya ile 1844 kubuma.Utashangaa wakati alikuwa akiwaeleza wenzie juu ya kuuza mali ili wachangie utume katika kujiandaa kumpokea Yesu mwaka 1885 yeye hakuuza hata kijiko chake!
 
1. Tueleze hilo tukio ni lipi ambalo unabii ulikuwa unalenga?

2. Hivi unaelewa maana ya unabii?

3. Kwa maelezo yako anayeweza kukosa kuelewa unabii ni mpokea Unabii au mtoa unabii?

4. Unapowatolea mfano Wayahudi, je, wayahudi ndio waliokuwa wametoa unabii au wao walikuwa wapokea unabii?

5. Unapotolea mfano wa wanafunzi wa Yesu kutoelewa kupaa kwake Mbinguni unamaanisha wanafunzi ndio waliotoa huo unabii au wao walikuwa wapokeaji wa unabii husika tu?

6.Je,historia inaonyesha kwamba manabii mbalimbali walipewa unabii au ufunuo fulani na Mungu.Je,unapojitetea kwamba hutokea unabii usiende sawa unaweza kutupatia mifano isiyoacha shaka ya manabii ambao waliwahi kutoa unabii na ukashindwa kwenda sawa sawa?

7.Ellen White aliwaachia wasabato unabii kibao ikiwemo wa Kanisa Katoliki kupitia Papa kuja kuwatesa wasabato, je kwa kutumia utetezi wako wa kwamba hutokea unabii uka-deviate from the reality,unaupa ufunuo au unabii huo wa Ellen White asilimia ngapi kutimia?
Maswali yote la 1-7, hayana mantiki, kwa sababu unabii tunaoungelea ni unabii wa Daniel, siyo wa Miller. Miller hakutoa unabii, bali alitafasri vibaya unabii, kwahiyo Miller hakuwa nabii bali alikuwa mhubiri. Kwahiyo unabii wa Daniel 8:14, hukufail, bali umeshatimia, kama vile mama White alivyoonyeshwa katika maono yake.

Kuhusu kutimia kwa unabii unaohusu mateso kwa kanisa la Mungu, huo lazima utatimia, maana si unabii wa Mama White bali ni unabii wa Mungu mwenyewe, inaweza isiwe katika wakati wangu mimi na wewe lakini lazima utimie maana neno la Mungu haliendi bure.
 
Kukosea kutafsiri unabii siyo dhambi...hata wayahudi hawakuulewa unabii wa ujio wa Yesu, walikuwa wanamsubiri masihi mwingine. Hata wanafunzi wa Yesu walikuwa wanajua kuwa Yesu anakuja kusimika ufalme wake duniani, na ndiyo maana alivyowaambia anaenda zake mbinguni hawakumuelewa.

Pointi ni kwamba, huo unabii ulikuwa unalenga tukio fulani, lakini si kama yeye alivyoelewa, swali ni kwamba nyie mnaombeza Miller mnatoa tafasri gani ya huo unabii?

1. Tueleze hilo tukio ni lipi ambalo unabii ulikuwa unalenga?

2. Hivi unaelewa maana ya unabii?

3. Kwa maelezo yako anayeweza kukosa kuelewa unabii ni mpokea Unabii au mtoa unabii?

4. Unapowatolea mfano Wayahudi, je, wayahudi ndio waliokuwa wametoa unabii au wao walikuwa wapokea unabii?

5. Unapotolea mfano wa wanafunzi wa Yesu kutoelewa kupaa kwake Mbinguni unamaanisha wanafunzi ndio waliotoa huo unabii au wao walikuwa wapokeaji wa unabii husika tu?

6.Je,historia inaonyesha kwamba manabii mbalimbali walipewa unabii au ufunuo fulani na Mungu.Je,unapojitetea kwamba hutokea unabii usiende sawa unaweza kutupatia mifano isiyoacha shaka ya manabii ambao waliwahi kutoa unabii na ukashindwa kwenda sawa sawa?

7.Ellen White aliwaachia wasabato unabii kibao ikiwemo wa Kanisa Katoliki kupitia Papa kuja kuwatesa wasabato, je kwa kutumia utetezi wako wa kwamba hutokea unabii uka-deviate from the reality,unaupa ufunuo au unabii huo wa Ellen White asilimia ngapi kutimia?
 
Kwa Wasabato, dhambi wanayoichukia sana kuliko zote ni '' kufanya ibada siku ambayo siyo Jumamosi''! Kusema uongo si kitu kwao!

Mkuu:

Hii yote inatokana na uelewa mdogo wa maandiko matakatifu.Yesu alikuja kufafanua zile Amri kumi kwamba zote ni UPENDO.Kwamba ni upendo kwa Mungu na kwa binadamu wenzetu na mazingira yanayotuzunguka.Kwa hiyo, ukikosa kipengele kimoja unakuwa umekosa upendo wote na Mungu atakuhukumu kwa kukosa upendo na wala si kwa sababu ulikuwa hukosi sabato Jumamosi pamoja na kuongopa na kupotosha watu wake!

Hawa jamaa wanawapotosha sana wafuasi wao kwa kuwajengea chuki dhidi ya wanadamu wenzao wasiokutana nao huko Kanisani kwao Jumamosi.Wanawajengea matumaini makubwa kwamba kwa vile ni wasabato tayari wanayo tiketi ya kuingia Mbinguni na kwamba majina yao yalishaandikwa tayari na ndio maana Yesu alishaanza kushuka kutoka Mbinguni na yuko mahali fulani kwa kazi moja tu ya kupitia majina hayo.Unaweza kuona Ellen White kwa uelewa finyu wa maandiko aliwahi kuwaambia wasabato wenzie wauze mali zao ili wachangie kazi za utume ikiwa ni maandalizi ya kumpokea Yesu mwaka 1885 baada ya ile 1844 kubuma.Utashangaa wakati alikuwa akiwaeleza wenzie juu ya kuuza mali ili wachangie utume katika kujiandaa kumpokea Yesu mwaka 1885 yeye hakuuza hata kijiko chake!
 
zamani nilikuwa nkisikia mwisho wa dunia nawaza watu wote twafaaa....kumbe sio....KILA NAFSI itaonja mauti kwa miaka, miezi, wiki, siku na mida tofauti!

WACHAGGA walishaambiwaga mwisho wa duniaa....hahaaaa...WAZEE wakachinja mbuzi wakanywa supu na mashoraaa, wengine wapo hai adi leo
 
Umeandika kiushabiki sana. Lengo lako ni kuwaattack wasabato na wala si vinginevyo.

Mambo mengi uliyoeleza hapa si ya kweli, kama ifuatavyo.

1. Miller haukuwa msabato na hata kipindi akiwa anahubiri kurudi kwa Yesu, hapakuwa na dhehebu la kisabato.

2. Mama White pia hakuwa msabato kipindi hicho maana hapakuwa na hilo dhehebu, na wala hakuwa mwanzilishi wa hiyo kanuni ya kurudi Yesu unayoisema, isipokuwa alikuwa mfuasi wa Miller.

3. Papa hatawafumusha wasabato kusali jumamosi kama ulivyodai, badala yake atawalazimisha watu wote kusali siku ya kwanza ya juma (yaani Jumapili) badala ya siku ya saba ya juma (yaani Jumamosi).

4. Yesu yuko katika chumba cha patakatifu pa patakatifu mbinguni akifanya huduma ya uombezi, na si kwamba ameshaanza kushuka kuja duniani kama unavyodai. Maana patakatifu pa patakatifu ni mbinguni.

5. Wasabato hawaja set siku yoyote ya kuja kwa Yesu kama unavyotaka kuwaaminisha watu, badala yake wamaamini kwamba Yesu amekaribia sana maana dalili karibia zote zimeshatimia.

6. Pamoja na kukosoa mahesabu ya Miller kuhusiana na unabii wa Daniel wa siku 2,300, hujatoa tafsiri mbadala wa unabii huo kana k
kwamba unabii huo hauna maana yoyote kwa wanadamu wa leo.

7. Ukweli ni kwamba, mahesabu ya Miller yalikuwa sahihi, kwamba mwaka 1844 kulikuwa na tukio kubwa lilikuwa linaenda kutokea. Kosa la Miller ni kwamba, alitafasri vibaya kuwa hekalu ni dunia na kutakaswa kwa Hekalu ni dunia kusafishwa kwa moto (kama ulivyoelezea vizuri kabisa).

Ukitaka kujua tafasri ya huo unabii wa siku 2,300 unakaribishwa kuuliza.
Hivi bado kuna mkirisito mwenye akili anaamini kusali jumosi au jumapili ndo kigezo cha kwenda mbinguni??
 
Mkuu:

Hii yote inatokana na uelewa mdogo wa maandiko matakatifu.Yesu alikuja kufafanua zile Amri kumi kwamba zote ni UPENDO.Kwamba ni upendo kwa Mungu na kwa binadamu wenzetu na mazingira yanayotuzunguka.Kwa hiyo, ukikosa kipengele kimoja unakuwa umekosa upendo wote na Mungu atakuhukumu kwa kukosa upendo na wala si kwa sababu ulikuwa hukosi sabato Jumamosi pamoja na kuongopa na kupotosha watu wake!

Hawa jamaa wanawapotosha sana wafuasi wao kwa kuwajengea chuki dhidi ya wanadamu wenzao wasiokutana nao huko Kanisani kwao Jumamosi.Wanawajengea matumaini makubwa kwamba kwa vile ni wasabato tayari wanayo tiketi ya kuingia Mbinguni na kwamba majina yao yalishaandikwa tayari na ndio maana Yesu alishaanza kushuka kutoka Mbinguni na yuko mahali fulani kwa kazi moja tu ya kupitia majina hayo.Unaweza kuona Ellen White kwa uelewa finyu wa maandiko aliwahi kuwaambia wasabato wenzie wauze mali zao ili wachangie kazi za utume ikiwa ni maandalizi ya kumpokea Yesu mwaka 1885 baada ya ile 1844 kubuma.Utashangaa wakati alikuwa akiwaeleza wenzie juu ya kuuza mali ili wachangie utume katika kujiandaa kumpokea Yesu mwaka 1885 yeye hakuuza hata kijiko chake!
Hujui unalolisema...Namwomba Mungu akusamehe tu!
 
Hujui unalolisema...Namwomba Mungu akusamehe tu!

1.Ni jambo jema kuniombea msamaha kwa Mungu.

2.Lakini toka lini wasabato mnaaamini katika fundisho la mtu mmoja kumuombea mwenzie msamaha kwa Mungu na kweli Mungu akapokea msamaha kama huo? Ni kwa nini usionyeshe tu dhambi yangu halafu mimi nijiombee msamaha mwenyewe maana bado niko hai sijafa.Kama Mungu anaweza kupokea ombi lako kwa dhambi zangu wakati mimi mwenyewe bado niko hai ni kwa nini basi akatae maombi ya msamaha wa dhambi kwa ajili ya waliokwisha kufa?
 
Hivi bado kuna mkirisito mwenye akili anaamini kusali jumosi au jumapili ndo kigezo cha kwenda mbinguni??

Waulize wenye sabato yao kwa maana wanasema Agizo hilo halina mjadala.Na ndio maana katika nyimbo zao mara zote wanaimba Mungu aje awachukue haraka na nyingine wanaimba kwa madaha kuonyesha jinsi watakavyokuwa wakipokelewa na Mungu siku hiyo.Hii yote ni kuonyesha kwamba tayari wanayo ASSURANCE la sivyo wangaliimba nyimbo za kuomba HURUMA ya Mungu.
 
Ndugu yangu haya mambo ni makubwa sana...kama husomi biblia huwezi kujua...nakushauri soma vizuri kitabu cha Daniel chote na Ufunuo...humo ndiyo mambo yote utayapata. Ila inatakiwa umuombe sana Mungu akupe roho wake uelewe vinginevyo utatoka kapa.

Kuhusu watu kulazimishwa kusali siku ya Jumapili ipo inakuja...Soma Ufunuo 13, utaipata, na kama ni mfutiliaji wa mambo, kuna kitu kinaitwa One World Religion, ambacho kimeshaanza kufanyiwa kazi.

Mwaka 1999, viongozi wa makanisa yote ya Kiprotestant na Roman Catholic walisaini makubaliano ya kuondoa tofauti zao, ili kuwa kitu kimoja. Na Octoba mwaka jana, katika kuazimisha miaka 500 ya uprotestant, ulioanzishwa na Martin Luther alipoandika mambo 93 ambayo alikuwa anapingana na kanisa la Roman Catholic, kanisa la Lutheran lilisaini declaration ya kumalizika kwa uprotestant. Kama unafuatialia mambo utakuwa unajua hili. Hii ni mwanzo wa One World Religion.
Upo vizuri mkuu! Heshima kwako.
 
Mwaka 1999, viongozi wa makanisa yote ya Kiprotestant na Roman Catholic walisaini makubaliano ya kuondoa tofauti zao, ili kuwa kitu kimoja. Na Octoba mwaka jana, katika kuazimisha miaka 500 ya uprotestant, ulioanzishwa na Martin Luther alipoandika mambo 93 ambayo alikuwa anapingana na kanisa la Roman Catholic, kanisa la Lutheran lilisaini declaration ya kumalizika kwa uprotestant. Kama unafuatialia mambo utakuwa unajua hili. Hii ni mwanzo wa One World Religion.
Mkuu! Hivi ni kweli kanisa la wasabato lipo kwenye muungano wa makanisa?
 
Maswali yote la 1-7, hayana mantiki, kwa sababu unabii tunaoungelea ni unabii wa Daniel, siyo wa Miller. Miller hakutoa unabii, bali alitafasri vibaya unabii, kwahiyo Miller hakuwa nabii bali alikuwa mhubiri. Kwahiyo unabii wa Daniel 8:14, hukufail, bali umeshatimia, kama vile mama White alivyoonyeshwa katika maono yake.

Kuhusu kutimia kwa unabii unaohusu mateso kwa kanisa la Mungu, huo lazima utatimia, maana si unabii wa Mama White bali ni unabii wa Mungu mwenyewe, inaweza isiwe katika wakati wangu mimi na wewe lakini lazima utimie maana neno la Mungu haliendi bure.

Unasema William Miller hakutoa unabii? Umeshindwa kuangalia hata maana ya neno Unabii katika Kamusi? Unaka tuamini kwamba William Miller kusema Yesu angalirudi tarehe 22 Oktoba 1844 siyo Unabii bali mahubiri tu,siyo? Kusema kwamba jambo fulani linalohusiana na imani litatokea namna hii au tarehe fulani au sehemu fulani siyo unabii bali ni mahubiri tu,siyo?
 
Back
Top Bottom