Wimbi la watoto kutoa shuhuda za kutisha zinazohusu uchawi wa kuua na kula nyama za watu

Wimbi la watoto kutoa shuhuda za kutisha zinazohusu uchawi wa kuua na kula nyama za watu

Lady Mwali

Senior Member
Joined
Nov 15, 2018
Posts
147
Reaction score
333
Wanapendwa,
Watoto wadogo kuanzia umri wa miaka 6 mpaka 12 asilimia kubwa wasichana kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitoa shuhuda za kujishughulisha na uchawi katika kanisa maarufu lilipo Dar es Salaam.

Katika shuhuda hizo watoto hao hukiri kujihusisha katika vitendo vya kichawi vya kuua watu na kula nyama zao na kunywa damu zao.

Mchunguji umuhoji mtoto husika ameeingia vipi katika chama cha kichawi,wengi wanakiri bibi zao wamewapa uchawi, miongoni mwao hukiri kutaka kuwaua wazazi wao kwa uchawi.

Mtoto anahojiwa amekuja na nani na kumtaja mtu aliyekuja naye, mara nyingi mama na kuitwa kuja madhahabuni.

Mzazi huambiwa maisha yake yalikuwa hatarini kwa kuuawa na mwanae kishirikina.

Watoto hao huto shuhuda hizo muda wa usiku kuanzia saa tano mbele ya waumini wengi huku wakionesha kujiamini.

Mchungaji anawatoa katika chama cha kichawi na kuwa watoto wema.

Shuhuda iliyokuwa kubwa ni ile ya binti wa umri wa miaka 16 anayesoma kidato cha pili shule ya Kibasila kukiri kuua watu kwa kuwaaambukiza HIV kishirikina.

Amekiri kuua wanaume 600 kwa kuwaaambukiza HIV kishirikina.

Wasiwasi wangu ni vipi usalama wa hawa watoto baada ya kukiri kuua watu wengi kishirikina wakirudi mitaani? Maana kumekuwa na mauaji ya washirikina katika sehemu mbalimbali nchini.

Ikumbukwe shuhuda hizi zanarushwa kwenye tv na kuonwa na watu wengi ndani na nje ya nchi.


Sheria za mtoto zinasemaje kumlinda mtoto katika hali hii?
 
Niliwahi kushauri polisi wakamate hao watoto watiwe adabu, haiwezekani mtu anashuhudia eti ameua watu wengi mno na kunywa damu halafu anaachwa kisa dini…. eti hasa kwa njia ya ajali za magari.

Hawa watoto wanatumika vibaya, wakiminywa kidogo tu watasema ukweli.

Nakala kwa mama D.
 
Niliwahi kushauri polisi wakamate hao watoto watiwe adabu, haiwezekani mtu anashuhudia eti ameua watu wengi mno na kunywa damu halafu anaachwa kisa dini…. eti hasa kwa njia ya ajali za magari.

Hawa watoto wanatumika vibaya, wakiminywa kidogo tu watasema ukweli.

Nakala kwa mama D.
Police hawana uwezo wa kudhibitisha hilo.Mambo ya kiroho uthibishwa kiroho
 
Wanapendwa,
Watoto wadogo kuanzia umri wa miaka 6 mpaka 12 asilimia kubwa wasichana kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitoa shuhuda za kujishughulisha na uchawi katika kanisa maarufu lilipo Dar es Salaam.

Katika shuhuda hizo watoto hao hukiri kujihusisha katika vitendo vya kichawi vya kuua watu na kula nyama zao na kunywa damu zao.

Mchunguji umuhoji mtoto husika ameeingia vipi katika chama cha kichawi,wengi wanakiri bibi zao wamewapa uchawi, miongoni mwao hukiri kutaka kuwaua wazazi wao kwa uchawi.

Mtoto anahojiwa amekuja na nani na kumtaja mtu aliyekuja naye, mara nyingi mama na kuitwa kuja madhahabuni.

Mzazi huambiwa maisha yake yalikuwa hatarini kwa kuuawa na mwanae kishirikina.

Watoto hao huto shuhuda hizo muda wa usiku kuanzia saa tano mbele ya waumini wengi huku wakionesha kujiamini.

Mchungaji anawatoa katika chama cha kichawi na kuwa watoto wema.

Shuhuda iliyokuwa kubwa ni ile ya binti wa umri wa miaka 16 anayesoma kidato cha pili shule ya Kibasila kukiri kuua watu kwa kuwaaambukiza HIV kishirikina.

Amekiri kuua wanaume 600 kwa kuwaaambukiza HIV kishirikina.

Wasiwasi wangu ni vipi usalama wa hawa watoto baada ya kukiri kuua watu wengi kishirikina wakirudi mitaani? Maana kumekuwa na mauaji ya washirikina katika sehemu mbalimbali nchini.

Ikumbukwe shuhuda hizi zanarushwa kwenye tv na kuonwa na watu wengi ndani na nje ya nchi.


Sheria za mtoto zinasemaje kumlinda mtoto katika hali hii?

Zamani wakati naolewa nilienda kijijini kwa somo wangu (bibi yangu). Akaniuliza unaolewa wapi? Nikamwambia....

Alishtuka!
Akaniambia mbali kote huko? Hilo kabila unalijua? Huo ukoo je? Mwisho kabisa akaniambia mambo ya kisomo yanasababisha mnaenda kwenye miji ya watu wa mbali ila mimi nakuombea usiingie kwa watu wanaokula nyama za watu

Sikua naelewa kama alikua anamaanisha. Ila nimekua sasa naelewa nguvu za uchawi na nguvu zote za giza zinategemea sana maiti, wafu na makaburi

Ukiona mchawi mzee alianzia utotoni
 
Niliwahi kushauri polisi wakamate hao watoto watiwe adabu, haiwezekani mtu anashuhudia eti ameua watu wengi mno na kunywa damu halafu anaachwa kisa dini…. eti hasa kwa njia ya ajali za magari.

Hawa watoto wanatumika vibaya, wakiminywa kidogo tu watasema ukweli.

Nakala kwa mama D.


Si tunasemaga uchawi hauna ushahidi? Sasa unamshughulikiaje mtu kisheria bila kuwa na ushahidi??

Tunahitaji nguvu za rohoni zile za Mungu kupambana na nguvu za rohoni za shetani
 
MIKA 3: 3
3 Naam, mnakula nyama ya watu wangu, na kuwachuna ngozi zao, na kuivunja mifupa yao; naam, kuwakata vipande vipande kama kwa kutiwa chunguni, na kama nyama sufuriani.
 
Wanapendwa,
Watoto wadogo kuanzia umri wa miaka 6 mpaka 12 asilimia kubwa wasichana kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitoa shuhuda za kujishughulisha na uchawi katika kanisa maarufu lilipo Dar es Salaam.
 
Wanapendwa,
Watoto wadogo kuanzia umri wa miaka 6 mpaka 12 asilimia kubwa wasichana kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitoa shuhuda za kujishughulisha na uchawi katika kanisa maarufu lilipo Dar es Salaam.

Katika shuhuda hizo watoto hao hukiri kujihusisha katika vitendo vya kichawi vya kuua watu na kula nyama zao na kunywa damu zao.

Mchunguji umuhoji mtoto husika ameeingia vipi katika chama cha kichawi,wengi wanakiri bibi zao wamewapa uchawi, miongoni mwao hukiri kutaka kuwaua wazazi wao kwa uchawi.

Mtoto anahojiwa amekuja na nani na kumtaja mtu aliyekuja naye, mara nyingi mama na kuitwa kuja madhahabuni.

Mzazi huambiwa maisha yake yalikuwa hatarini kwa kuuawa na mwanae kishirikina.

Watoto hao huto shuhuda hizo muda wa usiku kuanzia saa tano mbele ya waumini wengi huku wakionesha kujiamini.

Mchungaji anawatoa katika chama cha kichawi na kuwa watoto wema.

Shuhuda iliyokuwa kubwa ni ile ya binti wa umri wa miaka 16 anayesoma kidato cha pili shule ya Kibasila kukiri kuua watu kwa kuwaaambukiza HIV kishirikina.

Amekiri kuua wanaume 600 kwa kuwaaambukiza HIV kishirikina.

Wasiwasi wangu ni vipi usalama wa hawa watoto baada ya kukiri kuua watu wengi kishirikina wakirudi mitaani? Maana kumekuwa na mauaji ya washirikina katika sehemu mbalimbali nchini.

Ikumbukwe shuhuda hizi zanarushwa kwenye tv na kuonwa na watu wengi ndani na nje ya nchi.


Sheria za mtoto zinasemaje kumlinda mtoto katika hali hii?
Kamata mchungaji, Kamata watoto na wazazi wao. weka ndani siku tatu tu watatajana usanii wao, tunaharibu jamii na watoto wa Tanzania ya kesho for an expense ya upuuzi
 
Kamata mchungaji, Kamata watoto na wazazi wao. weka ndani siku tatu tu watatajana usanii wao, tunaharibu jamii na watoto wa Tanzania ya kesho for an expense ya upuuzi

Upuuzi ni upi hapo?

Ni matendo ya uchawi na wachawi wenyewe kuweka mambo hadharani au ni watoto kujihusisha na mambo hayo ya nguvu za giza?

Kutetea na kukataa kuongelea nguvu za kichawi ambazo zipo ni hofu watu wanayotiwa na wachawi ili waendelee kufanya mambo yao ya kuiharibu jamii kwa siri

Mungu atusaidie kusimama kiimani ili tuweze kupambana katika ulimwengu wa roho

 
Mind over matter, ukianza kuutafuta kuufikiria na kuuwaza kila dakika uchawi utauona tu.., kila paka utakayemuona au kila ugonjwa utaona uchawi...

Solution ni kuyapuuzia haya mambo unless otherwise tutaanza kuchomana moto na kuuana kwa kuitana wachawi
 
Mind over matter, ukianza kuutafuta kuufikiria na kuuwaza kila dakika uchawi utauona tu.., kila paka utakayemuona au kila ugonjwa utaona uchawi...

Solution ni kuyapuuzia haya mambo unless otherwise tutaanza kuchomana moto na kuuana kwa kuitana wachawi

Acha woga😅😅😅😅

Tuuongelee uchawi kwa maana ya madhara yake na jinsi ya kuumaliza. Kunyamaza ni woga.

Na ujue kabisa uchawi ni sanaa kwa baadhi ya jamii
Kama ambavyo jamii zina ngoma zao, vyakula vyao, vinywaji vyao pia zina uchawi wao ambao hurithishana kizazi baada ya kizazi
 
Acha woga😅😅😅😅

Tuuongelee uchawi kwa maana ya madhara yake na jinsi ya kuumaliza. Kunyamaza ni woga.
Shida ya kujikita kwenye vitu abstract especially kwa watoto ni kujitafutia majibu rahisi na kudumaa..., kila kitu kitakuwa jibu ni either uchawi, majini au kazi ya Mungu..., badala ya kutafuta suluhisho na kuchimba ni kitu gani, kwahio badala ya kuamini kwamba unachanganya madawa unapaa kwenye ungo ni vema kuchunguza inawezekanaje mtu akapaa na ku-defy gravity kwa nishati ipi na inapatikana vipi..., In short tabia hii ni ya easy answers from complicated questions
a ujue kabisa uchawi ni sanaa kwa baadhi ya jamii
Kama ambavyo jamii zina ngoma zao, vyakula vyao, vinywaji vyao pia zina uchawi wao ambao hurithishana kizazi baada ya kizazi
uchawi sanaa in what terms (yaani mazingaombwe kama kiburudisho au tricks za hapa na pale)..., unless otherwise anatumia hii sanaa kuboresha maisha yake na ya jamii zake na sio kuleta ugomvi na kusingiziana kwamba shangazi kamuua babu yangu au jirani fulani anafanya nisipate pesa au nisipokee pesa sababu ya chuma ulete..., sioni faida ya hii Sanaa
 
mama D

Nyongeza....

Kuna baadhi ya watu nawajua kwa ku-implant hii mentality kwa watoto kwamba wana majini watoto wao wameshindwa hata kusoma kila siku kwa waganga kuondoa mapepo kuna kijana mmoja anapitia humo humo kufanya usanii yeye kila siku za mtihani sikija anapata mapepo hence hafanyi mtihani au akifanya anafeli.., na kisingizio ni mapepo..., na culprit ni jirani yake, jambo lililopelekea hadi mzazi kuuza hio nyumba na kuhama kwenda kupanga....

Now tell me si bora kutokuamini haya mambo na kujihusisha nayo ? (Ignorance a Bliss wanasema); Kumbuka mind over matter ukiamini tu kweli utaugua hata fulani akikuangalia vibaya
 
Back
Top Bottom