Wimbo wa Isabela Kombo Mungu ni mmoja wazua gumzo

Wimbo wa Isabela Kombo Mungu ni mmoja wazua gumzo

Mkuu umeandika mkeka mrefu hapa cha msingi ni ukweli hata ukiwa ukweli mchungu kama ni Mungu apewe haki yake ya kuitwa Mungu lakini kama si Mungu basi pia ukweli usemwe hata kama alisema vitu vizuri kiasi gani ukweli usimame maana haufuti mafunzo mema aliyotuachia.

Hivi kumuita binadamu kama wewe Mungu unaona sawa?
Yule si binadamu soma maandiko Toka kuzaliwa kwake mpaka kufa na kufufuka

Labda kama huamini we endelea kuamimi mambo yenu ya kujitoa mhanga na ugaidi labda ndo dini ya kweli
 
Atheists 24:5

Mpumbavu amesema moyoni, Kuna Mungu maana hawezi kufikiria sawasawa na hawezi kuthibitisha uwepo wa huyo Mungu, Anaunda dhana za kufikirika tu.
Samahani "Atheists 24:5" n kitabu kilichopo kwenye msaafu au biblia
 
Kuiacha dunia hata wewe utaiacha na wala mimi sitakuwa wa kwanza wala wa mwisho kuiacha dunia.

Kama kwako Mungu huyo ni dhahiri, thibitisha udhahiri wake kwamba yupo.

Kama wewe huwezi kuthibitisha, Mwambie huyo Mungu wako ambaye ni dhahiri aje hapa ajidhihirishe mwenyewe uwepo wake.
Rafiki kwanza habari yako

Samahani naomba nikuelezee kitu

Mungu yupo kwa wanao mwamini na anajidhihurish kwao kupitia miujiza ya kiroho

Shetani pia yupo kwa wanao mwamini na anajidhihirish kwao kupitia miujiza ya kiroho

Tukumbuke hii vita ya wema na ubaya sio ya kimwili yaani kumwagana damu

Noo
Ni vita ya kiroho vita ambayo haionekani kwa macho ila nivita ambayo inaonekana kwa wanao mwamini Mungu tu

Tusimtafakar Mungu kwa kutumia mawazo yetu ,kwanza tuombe afu tujae ktk imani afu ndio tumtafakr Mungu

Tusitumie akili zetu maan hata maandiko yanasema
Akili za mwanadamu sio saw na mwenyezi Mungu,yaani hata nusu ya akili za Mungu hatuwezi kuzifikis
 
Ninachoamini ni Kwa Bella aliweka msisitizo wa Mungu ni Moja ila sio kwamba amekana nafsi tatu za Mungu
 
Rafiki kwanza habari yako

Samahani naomba nikuelezee kitu

Mungu yupo kwa wanao mwamini na anajidhihurish kwao kupitia miujiza ya kiroho
Mungu huyo Alishindwaje na anashindwaje kujidhihirisha kwa watu wote ili ajulikane yupo pasipo utata wa kiimani?

Kwa nini kila mtu anamwamini Mungu huyo kwa imani tofauti tofauti, zenye kupingana na kutofautiana mitazamo na maelezo ya kimaandiko?
Shetani pia yupo kwa wanao mwamini na anajidhihirish kwao kupitia miujiza ya kiroho
Mimi siamini shetani wala mungu. Na wote hawawezi kujidhihirisha kwangu kwa vile hawapo.
Tukumbuke hii vita ya wema na ubaya sio ya kimwili yaani kumwagana damu

Noo
Ni vita ya kiroho vita ambayo haionekani kwa macho ila nivita ambayo inaonekana kwa wanao mwamini Mungu tu

Tusimtafakar Mungu kwa kutumia mawazo yetu ,kwanza tuombe afu tujae ktk imani afu ndio tumtafakr Mungu
Kama hatuwezi kumtafakari Mungu kupitia mawazo yetu, Wewe ulijuaje na unathibitishaje Mungu huyo yupo?

Ulitumia nini kujua na kufahamu Mungu huyo yupo, Kama haiwezekani kumtafakari kwa mawazo yetu?
Tusitumie akili zetu maan hata maandiko yanasema
Akili za mwanadamu sio saw na mwenyezi Mungu,yaani hata nusu ya akili za Mungu hatuwezi kuzifikis
 
Saw saw

Kipo dini ya kiisilamu au kikristo
Dini sio hizo mbili tu unazozijua?

Maana ndizo ulizoletewa na mkoloni na zinazo pumbaza akili zenu.

Kuna dini nyingi sana ulimwenguni hapa.

Atheism sio dini..

Atheism ni kutokuwa na imani ya aina yeyote ile ya mungu, miungu, shetani na vishetani.
 
Yohana 1
1 Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

2 Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.

4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.

5 Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.

6 Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.

7 Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye.

8 Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru.

9 Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu.

10 Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua.

11 Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.

12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.

14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.

Yohana 1
17 Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.

18 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.
From hiyo Yohana 1: 14 means yesu ni neno aliye umba vyote.
Tuongeze mengine Kidgo.

Yohana 8:58
[58]Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Jesus said unto them, Verily, verily, I say unto you, Before Abraham was, I am.

Yohana 10:30
[30]Mimi na Baba tu umoja.
I and my Father are one.

Matendo ya Mitume 20:28
[28]Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.
Take heed therefore unto yourselves, and to all the flock, over the which the Holy Ghost hath made you overseers, to feed the church of God, which he hath purchased with his own blood.

[ Kanisa MUNGU alilo linunua kwa Damu yake mwenyewe, Means someone alimwaga damu, wew jibu wajua ]

Tito 2:13
[13]tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;
Looking for that blessed hope, and the glorious appearing of the great God and our Saviour Jesus Christ;

Mathayo 2:11
[11]Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.
And when they were come into the house, they saw the young child with Mary his mother, and fell down, and worshipped him: and when they had opened their treasures, they presented unto him gifts; gold, and frankincense, and myrrh.

[ Kuna settings nyingi sanaa, watu wa rohon, wachaw,mama jusi wanaofaham mambo ya rohon walikuw wakisujudia mbele ya Yesu]

Ufunuo wa Yohana 22:13-16
[13]Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
I am Alpha and Omega, the beginning and the end, the first and the last.
[14]Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.
Blessed are they that do his commandments, that they may have right to the tree of life, and may enter in through the gates into the city.
[15]Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.
For without are dogs, and sorcerers, and whoremongers, and murderers, and idolaters, and whosoever loveth and maketh a lie.
[16]Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi.
I Jesus have sent mine angel to testify unto you these things in the churches. I am the root and the offspring of David, and the bright and morning star.
 
Ninachoamini ni Kwa Bella aliweka msisitizo wa Mungu ni Moja ila sio kwamba amekana nafsi tatu za Mungu
Kama haku kana kuwa mungu hana nafsi tatu basi jua tu huyo naye ni mpumbavu na muhuni tu kama ccm
 
Maswala ya Imani yapo complicated sana Yani yanajifunga yenyewe Kwa yenyewe Hawa wanasema mkiri yesu kama bwana na mwokozi wako na Hawa wanasema uislam ni dini ya haki ya mwenyezi MUNGU. Pia ukristo una madhehebu yanayokinzana katka mafundisho Yao wasabato ,walokole , wakatoliki , mashahidi wa yehova , walutheran nk mfano wasabato wanasema ikumbuke sabato siku ya bwana jumamosi usifanye kazi . Kwa wakatoliki ni shika kitakatifu siku ya MUNGU badala ya ikumbuke sabato . Biblia zenyewe zinatofautiana🤔 Aya mambo ni mengi ya kiimani yanayofungamana wengi mnayafahamu . Nikiuliza wapi nifate kla mtu atanijibu kulingana na Imani yake , yule aliyezaliwa na kukulia katika ukristo atanambia nimkiri bwana kama mwokozi wa maisha yangu. Na yule aliyelelewa na kuzaliwa katka jamii na familia ya kiislam atanishauri uislam ndio dini ya haki mara uku msabato atanambia wakatoliki wanaabudu sanamu . Yani shaghalabaghala tafrani sasa apa unashindwa uamini wp unaishia kuwa upande ulioikuta hiyo imani ,kama familia ya kisabato utakuwa msabato kama kiislamu utakuwa muislam sasa je ntakua nna kosa Gani nisipoamini upande wowote mi nkaishi tu maisha yangu ,nkaishi kibinadamu tu siwatendei mabaya binadamu wenzangu je MUNGU atanihukumu Kwa kuwa sikuiamini dini yake ya haki uislam au atanihukumu kutomkiri bwana yesu Kristu kama mwokozi wa maisha yangu🤔🤔 sasa MUNGU mwnyw amenifanya nibaki njia panda nishindwe wapi pa kuamini. Ukijiuliza maswal haya utagundua tu dini ni za wanàdamu tu ni utaratibu wao wamejiwekea tu wa kumuabudu MUNGU ko wakamua wajiite waislam ,wakristo nk . Kama dini ya haki ni uislam ko wakristo wote moton?🤔. Ukristo ndo dini yenye wafuasi wengi ko wote wataenda motoni🤔😌. Wakuu ishi maisha Yako tu saka pesa tafuta ugali ule na familia Yako maisha yaende tu vitu vya kiroho vpo complicated sana huwezi kuvielewa . Ishi tu vizuri ña watu usiwatendee maovu binadamu wenzako tu maisha yaendelee Yani ni Bora kuishi neutral tu saka pesa ishi . Acha mambo za kutukana dini za watu Kila mtu aamini anachoamini . Anayeamini MUNGU yupo sawa na asiyeamini MUNGU yupo sawa tu mana apa manake MUNGU atakuwa kampa Kila mtu ufahamu wake sijui 🤔 Yani uyu kampa ufaham wa kumwamini na huyu kampa ufahamu wa kutokumuamini 🤔😌 so complicated. Kama MUNGU yupo ni yupo tu kama hayupo ni hayupo tu mi naona Bora niwe neutral tu kama yupo ntaenda kujieleza uko kwake kwamba duniani sikuelewa nifate dini Gani pia ww ndo ulinipa huu ufahamu wa kuwa na mashaka juu ya uwepo wako. Mfano zumaridi alisema yeye ni MUNGU lakini watu walimponda hakuna aliyemwamini je VP kama ni kwel MUNGU alikuja kupitia yeye🤔 kama swala la Imani ni gumu kiasi hichi huyu anaamini hv na uyu ana amini ichi inatatanisha kidogo. Kama binadamu sio wakamilifu basi ni sawa tu mtu kutokumuamini uwepo wa dini na MUNGU mana ufahamu wake ndo umemfanya aone kama maswala ya MUNGU ni stori za kufikirika mana ana mashaka juu ya uwepo wa MUNGU . Tena mtu uyu ni Bora kuliko yule anayeamini MUNGU yupo afu anamkaidi. Mtu ambaye haamini MUNGU yupo naona ni sawa na watu wengi walivokuwa hawajaamini kuwa zumaridi ni MUNGU. So complicated 😌😥🤔🤔
 
Ninachoamini ni Kwa Bella aliweka msisitizo wa Mungu ni Moja ila sio kwamba amekana nafsi tatu za Mungu
Nami nina amini hivyo na ndiyo maana kamtofautisha na miungu mingine yani dagoni, asheli na baali. Sidhani kama alikuwa anaongelea nafsi za Mungu
 
Mmisionari alipokuja alikuambia Yesu ni Mungu na ukakubali bila kuhoji, una uhakika gani na hizo imani za wazungu? Ukaambiwa "fumbo la imani na ukakubali " anaepinga ninaona ana akili na anaekaa kimya hana akili.
 
Nyimbo nyingi za injili anaembwa na shetani wakimaanisha mungu.
Ni hadi uwe na uelewa
Wimbo kama You rise me up,
Umbrella wa Rihanna.
Strength of women wa shaggy
Jerulasema nk
Hapa anaeitukuzwa ni shetani
 
Kuna nabii ametokea anadai wimbo huu mdada kauimba kwa kutumiwa na shetani bila yeye kujua, labda kwasababu amekuja wakati wa trend shetani anaagiza manabii na mitume wa uongo hao wauza mafuta waufute uungu wa Yesu. what I think about it;

1. Mungu ni mmoja tu, ila amejidhihirisha kwa nafsi tatu.
2. Yesu ni nafsi ya Mungu, hivyo ni Mungu yule yule.
3. Mzee wa ngome ya temboni ambaye namjua ni ajenti, mzee wa kibangu a.k.a Konyagi bapa, manabii mbalimbali wa uongo bongo wameibuka kwa pamoja wanadai Hakuna utatu mtakatifu na kwamba Yesu alikuwa mwanadamu wa kawaida tu, sio Mungu. wakati Biblia inasema hata kabla ya Agano JIpya (kitabu cha Isaya) kwamba Yesu ni Mungu mwenye Nguvu.

4. Wimbo huu ukiusikiliza vizuri, unaweza kuamini kwamba ni mojawapo ya shughuli za adui kuingiza ajenda zake kidogokidogo hadi aufute kabisa Uungu wa Yesu.

5. Kwa msiojua, ukijifanya wewe unamtumikia Mungu hakikisha upo vizuri kiroho, haufungui milango kama uzinzi, ugomvi, na uchafu mwingine. ukifanay hivyo hata kama wewe unajifanya kumtumikia Mungu shetani anaweza kuingia kwako akajifanya malaika wa nuru, akakupa mahubiri ya uongo, akakupa maono ya uongo, akakupa kunena kwa lugha ya uongo, akakupa nyimbo za uongo akakufanay ajenti wake bila wewe kujua kwasababu umeshafungua milango na yupo ndani yako. anaweza hata kufanya miujiza ya ajabu kabisa na watu wakakuona kama ni mtumishi au mwimbaji, kumbe shetani ameingia ndani ya kanisa anapigana kutokea ndani.

Hii ndio imewafanay wahubiri wengi wa Mungu ambao walikuwa wazuri kubadilika, walitumiwa na Mungu, wakateleza na kufungua milango, shetani akaingia akawabadilisha kabisa namna ya utendaji. hao wanaouza mafuta, maji, na keki usifikiri hawajawahi kuokoka. Majority yao wametokea kanisa la TAG, EAGT, FPCT na mengine ya kiroho. walikuwa walokole, ila walifungua mlango shetani akaingia, akabadilisha theologia yao kabisa na wanamtumikia shetani na shetani anawapa pesa.
Ungeweka na wimbo wenyewe hapa. Ili nasi tuweze kuusikiliza
 
Back
Top Bottom